Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

*ANGA LA WASHENZI – 19*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

“Ni kweli kabisa!” kisha akauliza: “Na vipi Brokoli? – alichukuliaje hii taarifa?”

Mudy akapandisha mabega juu.

“Sijui! Ila nakumbuka walikaa vikao viwili kama si vitatu mfululizo. Hatukuambiwa wanaongelea nini. Wala hatukupashwa habari kama kuna mabadiliko ama mazingatio yoyote kutokana na vikao hivyo!”

ENDELEA…

Kinoo akaguna kisha akauliza:

“Unajua wapi Brokoli anaishi?”

“Yah! Najua,” Mudy akajibu akitikisa kichwa.

“Na ulishawahi kuiftuatilia hiyo kampuni ya umeme wa jua?”

“Hapana. Sikufanya hilo kwa kutegemea polisi watalivalia njuga.”

“Sawa, na vipi kama hili jambo likabuma tena huko polisi, upo radhi kwenda umbali gani kutafuta haki ya Bite?”

Kidogo Mudy akasita.

“Una maanisha nini?”

“Unajua Mudy, si kila muda mambo yanaenda kama vile tunavyotarajia ama tunavyotaka. Nadhani uliona namna polisi walivyokuangusha ulivyowapelekea hili jambo. Sasa mimi nataka kujua unaweza kwenda kilomita ngapi kutafuta haki ya Bite?”

“Kadiri ya uwezo wangu.”

“Ahsante sana, hicho ndicho nilikuwa nataka. Njia hii inaweza ikawa ngumu na ndefu, inabidi tujiandae. Aidha kupita njia kuu ama nyinginezo ilimradi haki ipatikane.”

Kinoo akasafisha kwanza koo, akaendelea:

“Kikubwa ninachohitaji toka kwao ni taarifa tu, hayo mengine mimi nitayasimamia. Nitahitaji taarifa mbalimbali toka ofisini mwenu kama hutojali, yote kwa ajili ya Bite.”

“Nitajitahidi kadiri ninavyoweza.”

Wakapeana mikono. Kinoo akaaga.

“Ina maana mgeni unaondoka pasipo kupata chochote kitu?”

“Nashukuru sana, usijali. Leo si mwisho wa dunia. Anyway, unaishi mwenyewe?”

“Yah! Nipo mwenyewe.”

“Nyumba yote hii?”

Mudy akatabasamu. “Ndio, nipo mwenyewe.”

“Aisee!” Kinoo akatahamaki akiangaza huku na huko. Akapandisha mabega yake na kupinda mdomo.

“Haya mzee. Ningependa unipatie hizi nyaraka zako nikajaribu kufuatilia baadhi ya mambo. Pengine naweza nikaibuka na jambo.”

Mudy akamkabidhi.

“Kuwa makini, bado zinahitajika na ni muhimu ofisini.”

Kinoo akaitikia kabla hajaenda zake. Cha kwanza alichokifanya ni kumtafuta na kukutana na Miranda. Alikuwa yupo nyumbani kwake akijipatia kinywaji laini na kutazama televisheni. Alikuwa amevalia bukta ya timberland na blauzi nyeusi.

Akamweleza yale yote aliyoyapata huko kwa Mudy.

“Umefanya kazi nzuri!” Miranda akampongeza akipitisha pitisha macho yake kwenye nyaraka alizokuja nazo Kinoo.

“Lakini … Kinoo, kama vile naijua hii kampuni.”

“Serious?”

“Yah! Serious.”

“Ipo wapi?”

“Kama sijakosea, nilishawahi kuiona ikitangazwa kwenye TV. Tena si zamani, jana tu! … ngoja!” Miranda akanyaka rimoti na kubadili alichokuwa anakitazama toka kwenye movie mpaka chaneli ya kawaida.

“Bila shaka niliona hilo tangazo hapa.”

Alipoweka hiyo chaneli, wakaendelea na maongezi mengine. Wakagusia swala la picha ya Bite iliyopo kwa Jona.

“Nimeona ni vema nikaonana naye binafsi,” alisema Bite akikuna kichwa. “Nadhani nikimwelezea vizuri anaweza akanielewa. Hata kama asiponipa hiyo picha basi anipe wasaa mdogo wa kuitazama.”

“Unadhani atakukubalia?” Kinoo akauliza.

“Hayo yote ni matokeo: kunikubalia ama kunikatalia. Ila angalau nimejaribu. Lakini najua sitashindwa.”

Kinoo akaguna.

“Labda … sijui.”

“Kuna utofauti kati yangu na wewe,” Miranda akasema akimtazama Kinoo. “Tofauti moja kubwa mimi ni mwanamke na wewe ni mwanaume.”

Mara simu ya Miranda ikanguruma na kukatisha maongezi. Miranda akaitazama kujua ni nani kabla hajaiweka sikioni. Alikuwa ni waziri wa michezo; Mheshimiwa Eliakimu Mtaja.

“Tunaweza tukaonana, binti?” sauti ya Eliakimu iliuliza.

“Muda gani mheshimiwa?”

“Kesho majira ya jioni hapa nyumbani kwangu.”

“Sawa.”

Simu ikakata. Lakini ilimkumbusha jambo, kuwasiliana na bwana Boka, waziri wa Afya. Alienda chumbani kwake akarejea na kadi ya biashara aliyopewa na mwanaume huyo, akapiga namba iliyokuwa imeanishwa.

Bahati haikuwa kwake, simu haikupokelewa. Alipiga mara tatu kabla hajaamua kusitisha zoezi hilo.


***


“Kesho atakuja,” alisema bwana Eliakimu akimwambia Nade. Wote walikuwa sebuleni peke yao. Sauti ya televisheni ilikuwa inanguruma kwa mbali ikikosa shabiki wa kuitazama.

Eliakimu alikuwa amevalia suti ya traki ya michezo rangi ya bluu, Nade akiwa amejivalia suruali nyeusi ya kitambaa iliyoendana na koti lake fupi jeusi lenye kola rangi ya pinki.

“Nadhani mipango yetu imeenda kama tulivyotarajia,” alisema bwana Eliakimu. Nade akatikisa kichwa.

“Ndiyo, mkuu. Lakini kuna kajitatizo kadogo kametokea.”

“Wapi huko?”

“Ni kumhusu Maxwell Ndoja. Ameapa kutoshirikiana nasi tena. Amesema inatosha kwa yale yote tuliyoyafanya. Kwa sasa anataka kufungua ukurasa mpya.”

“Ukurasa mpya! Bloody fool!” bwana Eliakimu alifoka. “Anamaanisha nini kusema inatosha?”

Nade akapandisha mabega yake juu.

“Tangu lini pesa ikatosha?” Aliuliza Eliakimu. “Maxwell anataka kunipanda kichwani sasa. inabidi ajue hichi ni kitabu, hakuna ukurasa mpya kama haupo wa zamani, na ukitoa karatasi moja kwenye riwaya basi riwaya nzima inapoteza maana.”

Aliposema hayo akaulaza mgongo wake kwenye kiti akizama fikirani. Kwa dakika kama moja kukawa kimya kabla Nade hajamuuliza:

“Kwahiyo tunafanya nini, mkuu?”

Bwana Eliakimu akanyaka simu yake, akatafuta jina la Max, akaliita. Baada ya muda mchache ikapokelewa.

“Max, tunaweza tukaonana?” bwana Eliakimu aliuliza. Mzee huyu huwa haongei na mtu kwenye simu kuhusu mambo yake. Kuficha taarifa zake huwa anamwomba mtu wake wakutane. Na hupendelea zaidi nyumba yake kama mahali pa makutano.

“Hapana, hatuwezi kukutana,” ikajibu sauti ndani ya simu.

“Kwanini?”

“Kwasababu sina tena sababu ya kukutana na wewe mheshimiwa. Nadhani kibaraka wako ameshakwambia.”

“Max!”

Simu ikakata. Bwana Eliakimu akaitazama kana kwamba haamini.

“Amekata!” akasema akimtazama Nade. “Hivi huyu ananijua ama ananisikia?”

Akashusha pumzi ndefu … akakuna kidevu … akakuna kichwa.

“Hatuwezi tukamwacha huyu mtu hai,” akasema Bwana Eliakimu. “Anajua siri zetu nyingi mno. Hawezi akatoka tu kienyeji namna hii. Tutapataje uhakiki wa taarifa zetu kwake?”

“Hilo ndiyo jambo kubwa. Siri ziko mashakani sasa. hatuwezi jua nini kimemsukuma akajitoa kwenye duara.”

“Kwanini hukummaliza?”

“Nisingeweza kummaliza pasipo idhini yako.”

Eliakimu akanyanyuka akiweka mikono yake nyuma ya mgongo.

“Hakikisha kesho unammaliza huyu punguani. Usibakize ushahidi wowote nyuma!” alisema bwana Eliakimu kwa macho ya kumaanisha.

“Sawa, mkuu. Nitajitahidi,” Nade akapokea kauli.

Eliakimu akaenda zake chumbani. Alikuwa amekunja uso akibinua mdomo.


***


“Kwanini ulimuua Fakiri?” Jona alimuuliza Bigo aliyekuwa hapo kitini kwa masaa ya kutosha sasa. Bigo hakuwa amekula wala kunywa chochote. Tangu alipofungiwa kwenye kiti hakuwa amesogea wala kwenda popote.

Kuepusha asije akapiga makelele na kuzua tafrani, Jona huwa anamfunga mdomo pale anapotaka kulala ama kuondoka.

Bigo alitabasamu akimtazama Jona kwa kebehi.

“Sijui nini unaongelea,” akajibu kisha akalaza kichwa chake kutazama chini.

“Bigo, unapenda kuhangaika na kuteseka namna hii?” Jona aliuliza. “Mimi sina shida na wewe, najua wewe ni kibaraka tu unayetumwa. Mimi nina shida na bosi wako. Na shida yangu ni kujua kwanini anataka kuniua. Kwanini mnataka kuniua?”

Bigo akatabasamu.

“Ngoja nikwambie kitu kimoja, msanii. Sisi huwa hatumfuati wala kusumbuka na mtu asiye na faida kwetu, tunamfuata yule aliye na chetu, yule ambaye ana kitu tunachokitaka.”

“Mimi nina kipi chenu?”

Bigo akatikisa kichwa kichovu.

“Sina haja ya kukwambia, utakuja kujua mwenyewe. Kwa sasa mimi ni wa kufa tu, aidha nifie kwako ama kwa mkuu wangu. Najua hataniacha hai. Kwahiyo sina cha kupoteza, fanya upendacho.”

“Sina haja ya kukuua. Nipe taarifa ninazozitaka.”

“Alafu?”

“OK
 
*JOANA ANAONA KITU USIKU -- 16*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Alikuwa ana usingizi mzito ila alikuwa na hofu huenda akakabwa tena.

Kwa upande wa Joana yeye alikuwa amekabwa na maswali. Akili yake ilikuwa inawaza huyo mkabaji ni nani? Na je anahusiana na yule mhanga wa ukabwaji kwenye hoteli ya kwanza?

Vipi kama Rosie asingempiga teke? Alikuwa anakufa?

Mawazo ambayo alikuwa ameanza kuyasahau, sasa yanaanza kumrejea.

ENDELEA

Alikosa raha kabisa. Mpaka usiku unaisha hakulala kabisa. Walienda kunywa chai asubuhi na mapema lakini bado akiendelea kuwaza.

Walikula na kurejea mapumziko, baadae majira ya jioni wakatoka kwenda mazoezini kupasha viungo.

Ilikuwa imebakia siku mbili tu ili mashindano yaanze rasmi. Mkufunzi wao aliwapa maelekezo ya kuzingatia na kuwataka waanze kujenga picha ya shindano vichwani mwao.

"Hatujaja hapa kushiriki bali kupambana. Kumbukeni lengo letu ni kufika robo fainali."

Pengine lengo hilo waweza liona ni la chini, ila kwa hiyo klabu lilikuwa ni lengo mujarab tu ukilinganisha na uchanga wao.

Pale kwenye mashindao watakutana na klabu kubwa, zoefu na zenye ujuzi mkudufu. Hivyo kuchomoza na kufika hatua ya robo fainali, kwao itakuwa hatua kubwa mno.

Wakapeana motisha wakiamini kila kitu kinawezekana pakiwa na nia.

"Tule vizuri. Tupumzike na tuzingatie," mkufunzi alisisitiza.

Ila kabla watu hawajatawanyika kwenda kujiandaa ili warudi kambini, huko hotelini, mkufunzi akamwomba Joana waonane.

"Nina maongezi nawe."

Wakawa wanatembea wakiteta. Mkufunzi alikuwa anata kuulizia hali ya Joana kwani hakuonekana kama yupo sawa mazoezini.

"Ulikuwa unamis sana mipira. Hata energy na passion ilikuwa chini. Kuna tatizo?"

Joana akamwomgopea Mkufunzi kwamba alikuwa sawa, pengine ni siku tu haikuwa njema kwake.

Alihofia kama angesema ukweli kuwa hakulala basi mkufunzi angeng'aka kumgombeza.

Kwa shingo upande, mkufunzi akakubali ila akamtaka azingatie kazi kubwa iliyopo mbeleni.

"Tunakutegemea kwa kiasi kikubwa. Usije ukatuangusha."

Basi wakarudi hotelini. Baadae majira ya usiku, Joana akiwa amejitenga mwenyewe akachukua picha zake na kurudia kuzitazama.

Alizitazama kwa umakini sana. Alitazama kile kivuli alichokuwa anakiona na hakutaka hata kujiuliza maswali.

Alipapasa papasa na vidole vyake kabla hajafunga hizo picha na kubakia akiwanda wanda.

Hakutaka kulala. Aliogopa kulala japokuwa kwa muda ni kama vile hakuwa anajua kwanini anaogopa kufanya hivyo.

Alimtazama Rosie akamwona tayari ameshalala. Amejifunika shuka akikoroma kabisa. Akatamani angelikuwa yeye.

Basi kwasababu hakuwa na usingizi na usiku ni mrefu, akaamua kutafuta jambo litakalomsogezea muda. Asingeliweza kukaa macho muda wote vile.

Akili yake ikampatia wazo. Ila wazo hatarishi. La kwenda mojawapo ya klabu ndani ya jiji la Paris akaukatie usiku huko.

Swala la pesa halikuwa na shida kwani alikuwa ana kiasi cha maana tu alichopewa na mamaye.

Ila akasita ... akawaza ... akaamua kukata shauri kwenda. Abaki pale hotelini kufanya nini na wakati amekuwa bundi?

Akavaa na kutoka, akachukua taksi iliyompeleka moja kwa moja mpaka kwenye klabu moja ya usiku inayoitwa ROGUE. Humo akazama ndani na kushawishika kunywa vileo.

Akaagiza whisky moja kali ya kumsahaulisha mawazo. Taratibu akawa anapiga tarumbeta akitazama watu wakicheza muziki kwenye mwanga hafifu unaong'arishwa na vijitaa vya rangi rangi.

Alipokuwa amekaa palikuwa ni kochi kubwa gizani. Mwanga ulikuwa unamulika mara moja moja na Joana alitokea kupenda hayo mazingira.

Akatulia hapo akinywa na kunywa. Muda si mwingi akapata kampani ya mwanaume fulani mnene aliyejitambulisha kwa jina la Rabiot.

Mwanaume huyo alikuwa amebebelea glasi ya mvinyo na alikuwa anapata shida kuongea kiingereza kuelewana na Joana.

Ni mtu mwenye asili ya Ufaransa. Kiingereza chake kilikuwa kimemezwa na lafudhi ya kifaransa akiongea maneno utadhani anayameza.

Joana alifurahia kampani hiyo kwani ilimwondolea upweke. Lakini pia ilikuwa imamsogezea muda.

"Unahitaji nyingine?" Akauliza Rabiot baada ya kuona Joana anatikisa chupa ya whisky. Kabla Joana hajajibu, Rabiot akamuita mhudumu na kumpatia chupa ya Joana.

"Leta kama hiyo!" Akasema kwa kifaransa. Mhudumu akaleta nyingine, Joana akaendelea kujimiminia.

Kwenye majira ya saa tisa usiku, Rabiot akatoka na Joana. Joana alikuwa amelewa na maamuzi anayoyafanya yakisukumwa na kileo kichwani.

Aliridhia kwenda kulala na Rabiot nyumbani kwake. Jambo ambalo kama angelikuwa mzima asingelifanya.

Rabiot yeye hakuwa amelewa. Alikuwa mzima na anayejitambua. Na alikuwa anajua kile anachokifanya.

Alimpakia Joana kwenye gari lake, Volkswagen ndogo rangi ya kijivu, wakaelekea mpaka nyumbani kwake.

Ilikuwa ni apartment moja nzuri inayopatikana pembezoni mwa jiji. Ndani yake kulikuwa kumepangiliwa vizuri, na rangi za kupendeza.

Rabiot akampeleka Joana chumbani kumlaza, kisha akaenda kuoga. Aliporudi akamvua nguo Joana na kuanza kumkagua kwa macho ya uchu.

Alitimiza haja yake pasipo shaka kisha akajilaza pembeni hoi. Alijiona mwenye bahati siku hiyo tangu aanze mtindo wake wa kwenda klabu za usiku.

Alipitiwa na usingizi mzito akalala kama mfu. Yalikuwa ni majira ya saa kumi na dakika kadhaa.

Usichukue muda mrefu, Rabiot akajikuta anakabwa na mikono migumu yenye nguvu. Alifurukuta kwa namna zote ila hakufanikiwa kabisa. Alidakwa shingo mpaka akakata moto.

Aliachama mdomo ulimi ukienda kando. Kisha kama hakuna kilichofanyika muda ukasonga kukiwa kimya.

Yalipofika majira ya saa tatu asubuhi, Joana akashtuka. Alijikuta uchi amelala kando mwanaume. Akaangaza huku na huko kabla hajampiga kofi Rabiot na kufoka kwanini kamfanyia tendo lile pasipo ridhaa yake.

Alifoka akiendelea kumpiga Rabiot, akagundua Rabiot hakuwa hai. Hakuwa anahema wala kutikisika.

Nani kamuua? Akajikuta anajiuliza upesi.

Alipomtazama Rabiot shingoni akagundua alikuwa ana michubuko, na mivilio ya damu. Ndani hakukuwa na mtu mwingine yoyote bali wao, sasa nani kamuua?

Ni yeye!

Aligundua ana alama za meno kwenye mkono wake wa kuume. Maana yake nini? Ina maana aling'atwa wakati anamkaba Rabiot?

Mbali na hayo ilibidi kwanza atoke eneo hilo upesi kabla mambo hayajaharibika, ila huko napo anapoenda ataeleza nini? Mpaka muda ule itakuwa tayari imeshajulikana kambini kuwa hayupo!

Alivaa akaangaza usalama nje. Alichukua kila kilicho chake. Akafanikiwa kuchoropoka ila maeneo ya getini ndipo akakutana na mwanamke fulani ambaye hata hakumsalimia, akaenda na zake.
.
.
.
USIKOSE SEHEMU IJAYO.

Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
 
*JOANA ANAONA KITU USIKU --- 17*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Alivaa akaangaza usalama nje. Alichukua kila kilicho chake. Akafanikiwa kuchoropoka ila maeneo ya getini ndipo akakutana na mwanamke fulani ambaye hata hakumsalimia, akaenda zake.

ENDELEA

Alijikagua kama ana pesa, akapanda taksi mpaka hotelini ilipo kambi yao, akanyookea moja kwa moja chumbani kwake ambapo hakumkuta mtu. Watu wote walikuwa wameondoka asijue wameenda wapi.

Alikaa mwenyewe akapitiwa na usingizi. Alikuja kuamshwa na Rosie majira ya mchana wa saa nane. Rosie akamwambia walikuwa walienda kufanya mazoezi na matembezi kidogo.

Pia mkufunzi alikuwa anamuulizia kupita kiasi.

“Amekasirika sana,” Rosie alisema. “Amenigombeza kwa kutokujua umeenda wapi akiamini nimekufichia siri.”

Joana akamtuliza Rosie na kumpa pole, ataenda kuonana naye mwenyewe na kumweleza yaliyomsibu.

“Kwani ulienda wapi, Joana?” Rosie akauliza.

Joana akamzungusha zungusha asimpatie jibu. Punde kidogo akatoka kwenda kuonana na mkufunzi.

Mkufunzi alikuwa amefura kwa hasira, hakuona mantiki kwenye maneno ya Joana akawaka na kumtaka aondoke kwani awamuhitaji tena kwenye timu.

“Hatuwezi kuongea na wewe ilhali umegoma kuelewa. Tunakuomba uondoke!”

Haikujalisha namna gani Joana aliongea, mkufunzi hakutaka kumwelewa. Kutoroka kambini na kwenda klabu nyakati za usiku, ni kosa kubwa kwa mazingira ya kambi ya michezo.

Mkufunzi akampatia nauli Joana na kumtaka arudi kwao Ubelgiji. Joana akaumia sana kwani hakutaka kurudi. Ile ndiyo ilikuwa fursa pekee kwake kubadilisha maisha yake.

Akalia sana, mkufunzi asimjali akaondoka zake na kumwacha peke yake. Akajinyanyua na kwenda chumbani ambapo akampasha habari Rosie.

“Sasa inakuaje, Joana?” Rosie akauliza.

“Siwezi nikaondoka, Rosie. Siwezi!”

Joana akaendelea kulia. Baadae akanyamaza na kumwambia Rosie kwamba hataondoka kwenda popote pale.

Basi zikapita siku mbili Joana akiwa bado yupo pale kambini ila hashiriki kwenye mazoezi ya pamoja na wenzake. Wenzake wakienda mazoezini basi naye anaenda kufanya mazoezi yake binafsi kwenye gym.

Rosie akamwambia mkufunzi kuhusu hayo mambo, ikiwa imebakia masaa tu kabla mashindano hayajaanza rasmi, mkufunzi akaonana na Joana. Akamsikiliza na kumsamehe.

“Natumai hili jambo halitajirudia tena, Joana,” mkufunzi alimalizia kwa kusema hivyo.

Joana akafurahi sana. Akamshukuru sana Rosie kwa kumsaidia, amefurahi na hana cha kumlipa kumtosheleza.

“Wewe ni rafiki wa kweli, Rosie!”

Joana akapangwa kwenye kikosi cha kwanza kwa ajili ya mechi ya kwanza kabisa ya ufunguzi. Kwa jitihada zote, akacheza na wakafanikiwa kuibuka na ushindi. Wenzake wakampongenza sana kwa kazi yake.

Wakiwa wanatoka uwanjani kurejea kwenye basi kurudi kambini, miongoni mwa watu waliokuwa wamesongamana kupiga picha na kuomba sahihi za wachezaji, Joana akamwona mtu yule mfanana na Moa.

Mtu huyu alikuwa amesimama mbali, ng’ambo ya barabara, akiwa amefunikwa na koti la mvua lenye kofia iliyoziba uso wake. Ni mdomo tu na kidevu ndivyo ambavyo vilionekana.

Mikono yake alikuwa ameitumbukiza ndani ya mifuko ya koti. Akiwa ametanua miguu kusimama kama vile mnara wa Eiffel.

Joana alimtazama na kuzubaa kabla hajashtuliwa asije angushwa na ngazi za gari. Alipopanda garini na kuangaza, mtu yule hakuwepo. Alitazama kila pande, lakini hakumwona yeyote.

Basi likaondoka, bado Joana akimtafakari yule mtu kiasi kwamba hakujua hata wapi basi lilipo na linapoelekea mbali na kujua tu ya kwamba wanaelekea kambini.

Furaha yake ya mchezo ilipotea kwa muda akizamia mawazoni. Alikuja kushtuliwa na makelele makali ya wenzake ndnai ya basi. Kutazama akaona basi likienda mrama, likiparamia watu na magari mengine.

Kufumba na kufumbua, basi likabiduka na kugaragara mara tatu!

Baada ya hapo Joana hakujua kilichoendelea kwani alikuwa gizani. Alipokuja kupata fahamu, alikuwa juu ya kitanda cha hospitali. Kwa nje, kupitia dirisha la kioo, wazazi wake walikuwa wanaongea na daktari.

Punde tu taarifa ya habari iliporushwa kuhusu ajali mbaya iliyowakumba, wazazi wake wakapanda ndege kwenda kumtazama. Baba alitokea Korea, mama akitokea Ubelgiji wakakutania Paris, Ufaransa.

Joana alikuwa anasikia maumivu makali ya kichwa na mbavu. Mkono wake wa kushoto ulikuwa umefungwa na bandeji ngumu. Usoni alikuwa amewekewa mashine ya kumsaidia kuhema.

Haikupita muda mrefu akaonana na mamaye ambaye alifurahi sana kumwona binti yake akiwa hai. Kitu cha kwanza Joana kuuliza, ikawa ni wenzake. Wanaendeleaje na wapo wapi.

“Wamebakia watatu tu basi zima, wamewekwa vyumba vya watu mahututi,” mama akamweleza.

Joana akaumia sana. Alianza kulia hali ambayo ikampelekea apate maumivu maradufu ya mbavu. Daktari alikuja kumtoa mama ndani ya chumba cha mgonjwa na kumtaka amwache mgonjwa apumzike.

“Anahitaji muda zaidi wa kupumzika. Naomba umpatie nafasi hiyo.”

Joana akakaa hospitalini kwa juma moja kabla hajaruhusiwa kurudi nyumbani. Ndoto zake za furaha akawa ameziacha huko Paris. Alirudi mwenyewe ingali walienda wengi.

Hata mkufu aliokuwa nao, ule aliompatia Moa, nao alikuwa ameuacha huko. Hakuuona tangu alipopata fahamu.

Basi maisha yakaendelea. Na kama ulidhani Joana alikuwa ameacha mabalaa yote baada ya kuuondoa mkufu wa Moa kifuani, basi umekosea tena sana.

Majaribu yalikuwa na njia yake yapekee kumfikia Joana.

Zikapita wiki tatu akiwa nyumbani. Wiki hizo hakuona kitu wala chochote cha kumuogofya. Ilipowadia wiki ya nne, Joana akaanza kusumbuliwa na ndoto za ajabu. Ndoto za watu waliokufa.

Ndoto za wale wote aliowaua!

Joana akawa anaona kitu usiku. Watu wakimjia toka makaburini. Wakiwa wamevalia sanda zilizochakaa na kuoza. Wakiwa na nyuso zilizoliwa na wadudu. Wakiwa na viungo vilivyokatika katika.

Usiku kwake ukawa mtihani mkubwa. Alikuwa anakurupuka mara kwa mara na kuangaza. Akawa anaona vitu vinacheza. Sauti za watu zinateta zikiyoyoma. Mlango na madirisha yakiwa wazi.

Siku nyingine alikuwa anasikia sauti za vishindo vya miguu na watu hawaoni. Ama anakuta ujumbe mezani!


KWANINI MABALAA YANAMUANDAMA JOANA? NINI MWISHO WAKE? USIKOSE SEHEMU IJAYO.


Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom