Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Steve wewe ni maasai upande wa Kenya uko kwenye kupiga kura ?
 
[emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]
 
ANGA LA WASHENZI --- 06

*Simulizi za series inc.*


Mwanamke akatazama nyuma, akaona pikipiki. Alijitahidi kuing'amua sura ya Jona lakini akashindwa, kofia ilimkinga.

Alisonya kisha akauliza; "Ni nani huyu?" Hakukuwa na mwenye majibu. Ila walijua tu hawapo salama, na ni lazima jambo lifanyike.

Dereva akadaka njia zingine za kuchepukia, ndani ya muda mfupi wakatokea baharini, wakasimamisha gari.

Jona naye akasimamisha pikipiki na kuwatazama. Mpaka hapo alikuwa amehisi huenda akawa ameshtukiwa.

Alijifanya anatazama maji ya bahari kwa muda kidogo kisha akakwea tena pikipiki na kupotea.

Pande lile la mtu na mwanamke aliyeongozana naye wakamtazama mpaka alipoyoyoma. Walishindwa kujua nini haswa lengo la huyo mtu, ambaye ni Jona sasa.

Walikaa hapo eneo la bahari kwa muda wa dakika kumi kusoma mambo. Walipojihisi wapo salama, wakaondoka zao, lakini wakiwa waangalifu sana.

Walisogeza chombo mpaka kwenye nyumba namba 89. Nyumba kubwa yenye uzio mrefu. Wakazama ndani na geti kufungwa nyuma yao.

Walijua sasa wapo salama. Waliketi sebuleni wakajadili kuhusu pikipiki ile iliyokuwa inawafuata. "Kuna haja ya kumfikishia taarifa, mkuu?" Akauliza pande la mtu ambaye ndani ya maongezi haya jina lake lilijiweka wazi, Kinoo.

Na la mwanamke lilikuwa Miranda. "Hapana, ni mapema sana," alijibu Miranda akiliza mifupa ya vidole vyake. Macho yake yalionyesha yupo mbali kifikra.
"Tunahitaji kujua kwanza ni nani anayetufuatilia na anahitaji nini," akaendelea kueleza Miranda. "Endapo tukimwambia mkuu kwa taarifa hizi robo robo, hatatuelewa, atatuona wazembe." Kukawa kimya kidogo. "Shida ni kwamba tuna maadui wengi, ni ngumu kubashiri," alisema Miranda. "Ni kweli," akaitikia Kinoo. "Ila tuna jukumu la kujua ni adui gani ameanza kunyoosha mkono tusije tukawaamsha wengine usingizini." Miranda akaitikia kwa kutikisa kichwa. Alinyanyuka akaendea chupa ya kinywaji, wiski, akaiweka mezani pamoja na glasi mbili. "Sasa yule mshenzi ameshaenda, nini sasa kinafuata?" Akauliza Kinoo akijinyoosha kuiteka glas ajipatie kinywaji. "Hali inakuwa ngumu zaidi," akajibu Miranda. Alimimina kinywaji akanywa kwanza fundo moja kupoza koo. "Nani kammaliza Bite? Unajua hilo swali linanitatiza sana," alisema Miranda akimtazama Kinoo. "Na kamuua kwasababu gani? Amekufa kabla hajatusaidia kupata ile picha na kutufafanulia." "Picha si ipo kwa yule mchoraji?!" Akasema Kinoo. "Umeipata?" "Hapana, ila angalau tuna uhakika ipo." Miranda akanywa fundo mbili. "Hata nguvu za kuitafuta hiyo picha zinaniisha," akasema akitikisa kichwa. "Hapana!" Kinoo akawaka. "Mimi naamini yule mchoraji atakuwa anajua jambo. Sema wewe ndiyo unazingua?" "Mimi?" "Ndio!" "Kivipi nazingua?" "Unamremba sana yule boya, tunajikuta watakatifu sana yani."
"Kwani wewe ulikuwa unatakaje, Kinoo? Tutengeneze kesi zingine? ... Si kila kitu chaendeshwa na mdomo wa risasi!" "Sasa kwa hiyo system tutapatia wapi hiyo picha? Tumekagua nyumba nzima hamna kitu! Ukimwomba akupe, hata kwa fedha, hataki! Sasa?" Miranda akashusha pumzi ndefu. Akanywa tena mafundo mawili. "Tujaribu tena," akashauri. "Unajua nini Kinoo, tatizo ni kwamba nataka kuepuka vyombo vya habari kabisa.
Nataka tufanye mambo haya kwa siri, tumalize kwa siri. Unajua mwenyewe namna gani hii ishu ilivyo ngumu." "Una maanisha nini?" "Endapo hili jambo la huyu mchoraji likivuma, basi wale wabaya wetu watalifahamu, watajua kuna jambo na watalifuatilia.

Huoni kama hapo itakuwa nongwa? Wakifuatilia wakajua ni kuhusu picha, basi watatusumbua zaidi. Watataka kujua kilicho kwenye picha.

Kama waliweza kummaliza Bite kuficha siri, vipi wakisikia kuna jambo litakalovujisha neno?" Kukawa kimya. Kinoo alimalizia kinywaji chake glasini kisha akalaza mgongo kitini. "Miranda," akaita. "Mimi bana nakuachia hili jambo mwenyewe. Wewe utakavyoona, sawa. Utantaarifu." "Usijali," alisema Miranda kisha akanyanyuka. "Leo hatuendi?" Aliuliza. "Wapi?" Kinoo akatoa macho. "Nawe acha uoga, unadhani ni wapi?" Akaangua kicheko. "Ni klabu tu hapo!" "Siendi," Kinoo akajibu na kuongezea: "Hivi wewe hujachoka enh? Siku nzima msibani na bado unataka kwenda klabu! We kiboko."
Miranda akatabasamu. Akanyanyua chupa kubwa ya wiski na kumiminia mdomoni. "Tena usinikumbushe huo msiba wa kis*nge. Nimekaa hapo kutwa nzima na wala sijapata chochote. Nimepoteza muda tu!" Kinoo akatabasamu. Akanyanyuka na kujinyoosha. "Maisha ndivyo yalivyo. Si kila mara wapata, la hasha! Kuna muda wakosa na kuna muda wapata. Cha msingi ni kutokata tamaa. Tuendelee kupambana." "Ila roho inaniuma sana, Kinoo," akasema Miranda akipiga kifua chake ngumi. "Kwanini?" "Kila mara tunazidiwa hatua, kwanini? Ina maana sisi ni wajinga na wazembe kiasi gani?" "Hapana, Miranda. Kila mbwa ana siku yake. Kuna siku wataingia kwenye anga letu. Anga la washenzi. Hakika watajuta!" Kinoo aliposema hivyo akapiga mihayo. Miranda alitabasamu na kumtaka aende akapumzike. "Usiku tuna kazi ya kufanya, bila shaka unakumbuka," akasema Miranda. "Tena?" "Ndio, kwani iliisha?" "Poa, mida!" Kinoo akatoka ndani, Miranda akaingia chumbani.

Kinoo akaelekea nyuma ya nyumba ambapo kulikuwa kuna chumba kikubwa kilichojitenga ambacho kilifungwa na mlango wa bati.

Akafungua mlango huo kwa kutumia funguo aliyoitwaa dirishani. Akatoa pikipiki moja matata, Ducati Monster nyekundu modeli ya 2016 aliyotia moto na kuhepa nayo.

Alivalia kofia ngumu na uso wake ukazibwa na kioo cheusi cha kofia hivyo ikawa ngumu kumng'amua uso.
Lakini Jona alimjua mwanaume huyo upesi. Alikuwa amejibanza kwenye jengo moja karibu sana na jengo alimotoka huyo mwanaume, yaani Kinoo.

Lakini pia na nguo alizovaa Kinoo zilimfanya Jona, mwanaume mwenye macho mabovu ndani ya miwani, amkumbuke na kumtambua kwa usahihi.

Alimtazama Kinoo anavyoyoyoma, kisha akaurudisha uso wake getini mwa jengo. Akatazama kwa muda pasipo kuona jambo.

Akaamua kuondoka, ila akiapa kurudi na kufanyia jengo hilo upelelezi zaidi. Alitaka kujua uhusiano wa hao watu na kifo cha Bite,na picha pia.

Ilimradi sasa alishajua makazi yao, kwake hii ni hatua muhimu kuelekea kupata majibu yake. Hivyo hakupoteza muda.

Akajirudisha nyumbani asiende kazini. Alikoga na kula kisha akapumzika kidogo kabla ya kuanza kuchora picha kadhaa kwenyw makaratasi yake marefu.

Leo hii hakuchorea chumbani, bali sebuleni. Alijivika earphone masikioni akisikiza muziki laini huku akitenda.

Macho yalitazama katatasi, mkono wake ukienda kwa ustadi. Alikuwa anarejelea kwenye kumbukumbu zake, na baada ya muda picha ya mtu sasa ikaonekana vizuri.

Alikuwa ni mwanaume mrefu mwenye mwili mpana. Alikuwa amevalia shati lililobana mwili. Kichwa chake hakikuwa na nywele, ila ndevu lukuki. Alikuwa ni Kinoo! Hata mtoto mdogo angekueleza hivyo kwa kutazama tu mara moja.
Kama haitoshi, akachora pia na picha ya Bite vilevile kama alivyoichora awali. Alipomaliza akaketi na kuanza kuitazama picha hiyo kwa umakini kama fumbo.
Hakudumu hapo muda mrefu, simu ikamshtua. Akaichomoa mfukoni na kutazama. Ulikuwa ni ujumbe toka kwa Nade.

Kabla hajaujibu ujumbe huo, akajiuliza ni namba ngapi zilizotunzwa ndani ya simu hiyo. Ni mara ya pili sasa amekuwa akiona majina yanatokea katika njia ya kumrahisishia kufahamu.

Ina maana namba hizo zilitunzwa kwa ajili ya matumizi yake? Ndio, akili yake ikamjibu.

Ile simu alikuwa ameandaliwa, na hata watu wa kuwasiliana naye walishaainishwa. Alitumia muda wake kuperuzi majina yaliyotunzwa simuni, akayakuta manne tu.
1. Mh. Eliakimu Mtaja
2. Mama Mdogo (Kinondoni)
3. Nade
4. Shangazi (Kimara)

Ikamshangaza kidogo. Alipewa simu hiyo akiwa hamjui yeyote kati ya hao, labda tu Mheshimiwa.
Ina maana watu hao waliwekwa simuni kabla hata hajaipokea? - Hadi Mama Mdogo na Shangazi wa mke wa mheshimiwa!

Alipuuzia maswali hayo akauendea ujumbe wa Nade na kuufungua. "Habari?" Ujumbe uliuliza. "Njema," Jona akajibu. Hata salio lilikuwa kedekede kwenye simu. "Kuna kitu umepata?" Ujumbe ukaingia. "Ndio," Jona akaandika, ila kabla hajajibu akasita. Akaufuta ujumbe huo na kuuandika mwingine. "Hapana, bado." "Kweli?" "Ndio." Kimya kidogo. "Haya sawa. Naomba unishirikishe utakapopata jambo. Hata kama kidogo. Sawa?" "Sawa." Jona akaweka simu chini. Alistaajabishwa na namna alivyoulizwa kuhusu upelelezi wake ndani ya masaa machache tu.
Alijiuliza ni hofu ama hamu iliyosukuma maswali hayo.
Hakutaka kuumiza kichwa chake zaidi. Alifunga zile picha alizokuwa amechora kisha akazipeleka chumbani.

Baadae kwenye majira ya usiku akiwa yupo kitandani, na tayari amejishindilia kilevi, akazama kwenye mtandao wa Facebook na kuanza kuperuzi akaunti ya mke wa mheshimiwa.

Akafungua akaunti yake upesi akiipa jina la Giovanni Lacatte. Akaweka taarifa bandia akijinadi anaishi Italia na anahusika na mitindo mavazi.

Akarusha picha kadhaa za wanawake wanamitindo. Baada ya hapo akadukua akaunti mifumo na mara punde akawa ana wafuasi wengi waliomfuata.

Wafuasi laki tatu! Wafuasi hawa wote walikuwa feki. Ila usingeweza kutambua mpaka uanze kuwatazama.

Alikuwa ni mtu mmoja tu aliyezidishwa mara elfu!

Jona alipoona kila kitu kipo sawa, akamuomba urafiki Mariam Jullian, mke wa Mheshimiwa.

Haikupita muda mrefu, kabla hajaanza kusinzia, ombi lake likakubaliwa. Akiwa amefungua jicho moja, akamtumia Mariam ujumbe.

Waliwasiliana wakitumia lugha ya kiingereza wakijuliana hali. Jona akamlaghai amempemda na angependa kumtumia kutangazia mavazi yake.

Jambo hilo likamvutia sana Mariam. Akaingia mkenge akitaka kufanya kazi hiyo. Ila alishikwa tahadhari, akauliza kama kutakuwa kuna malipo yoyote anayotakiwa kufanya.

Jona akamtoa shaka. Lakini pia kutengeneza mazingira ya 'kiprofesheno' hakutaka kuzoeana ghafla na 'mteja' wake, akamwambia atamtafuta tena siku za usoni.
Mariam akiwa mwenye furaha, akaridhia na kuaga.

Jona alikuwa sasa anasinzia mno. Akaiweka simu kando na kulala. Dakika tano kupita, akashtuka. Alisikia sauti ya mlango wa geti.

Akakurupuka na kusimamisha masikio.
.
.
.
.
. ***
LAKO JICHO!
***
 
ANGA LA WASHENZI --- 07*

*Simulizi za series inc.*



Hakusikia kitu. Akaamua kunyanyuka na kwenda mpaka jikoni alipochungulia nje. Hakuona jambo.

Hakuridhika, akatoka nje. Aliangaza kila pande ya nyumba, hamna kitu. Sasa ni nini? Akajiuliza.

Alitulia hapo nje kwa dakika kama tano kama atasikia ama kuona jambo lolote. Hola! Akaamua kujirejesha kitandani na kujilaza.

Haya sasa ni mawenge, si bure. Aliongea na nafsi yake.
Kabla hajalala akawaza kuhusu mambo yake anayoyafanyia kazi. Alikumbuka yale yote aliyoyatenda, akagundua siku ilikuwa ndefu sana.

Ndani ya siku hiyo yalitukia mengi. Aliwaza nini kitajiri siku inayofuata. Akiwa dimbwini mwa fikra, usingizi ukambeba sasa pasipo taarifa. -- Ndani ya usiku huo huo. Majira ya saa tisa usiku, pembezoni mwa klabu ya usiku ya Masai.

Nje ya uzio ilikuwa imepaki Range Rover sport, ile wanayoitumia Miranda na Kinoo. Gari hiyo ilikuwa imezimwa na haikuwa na mtu ndani yake.

Muda kidogo mbele, Miranda anatoka ndani ya klabu. Alikuwa amevalia gauni fupi jeusi linalobana mwili. Viatu virefu vyekundu.

Nywele zake ndefu za bandia alikuwa amezichana na kuzilazia pembeni. Kwenye mkono wake wa kushoto alikuwa ana kapochi kadogo chekundu. Wa kulia ana funguo ya gari.

Alitazama kushoto na kulia kisha akaminya funguo, gari ikalia na kuwaka taa. Akafungua mlango na kuzama ndani.

Alichoropoa simu ndani ya kipochi, akatuma ujumbe kwa Kinoo.
"Fanya fasta, usiuweke usiku."
.
.
Ndani ya muda mfupi, ujumbe ukaingia kumjibu;
.
.
"Poa najitahidi. Tunaelewana bei."
.
.
Haikupita muda mrefu, kama dakika tano, Kinoo akatoka naye ndani ya klabu akiwa ameongozana na mwanamke mweupe mrefu mwembamba.

Alikuwa amenyoa upande mmoja, upande mwingine akiwa na nywele ndefu rangi ya bluu. Alitoga kila sikio mara tano na kuvisha hereni.

Alivalia sidiria nyekundu na sketi fupi ya kuchanua rangi ya pinki aliyofananisha na mkoba wake aliouweka begani.

Alikuwa na uso mwembamba usiovutia, ila aliupamba ukawa angalau. Akiwa ameshikwa kiuno na Kinoo, wakaelekea kwenye gari na kupanda, gari likaondoka.

Usingejiumiza kichwa kujua mwanamke huyu alikuwa anajiuza, yani malaya ama tuseme changudoa.
.
.
"Hukunambia kama mtakuwa wawili!" Alisema malaya akimtazama Miranda aliyekuwa anaendesha gari. "Unajua mkiwa wawili bei yake ni tofauti."
.
.
"Nipo peke yangu tu," akasema Kinoo. "Huyo ahusiki na mambo yetu."
.
.
Malaya akaitikia kwa kutikisa kichwa akibinua mdomo. Akachoropoa sigara kwenye mkoba.
.
.
"Unataka ufanye nini?" Kinoo aliwahi kumuuliza. Hakungoja jibu, akammarufuku: "Ah! Ah! Huwezi ukavuta sigara humu. Rudisha!"
.
.
Malaya akarudisha sigara akibinua mdomo.
.
. "Isiwe kesi."
.
.
.
Baada ya muda kidogo wa safari, Miranda akawashusha maeneo ya Kijitonyama Sayansi mbele ya nyumba ndogo yenye uzio.
Wakateta kidogo na Kinoo.
.
.
"Hakikisha kila kitu kinaenda sawa," alisema Miranda akikaza macho. "Si kila kitu unacho?"
.
.
"Ndio, kila kitu kipo," akajibu Kinoo.
.
.
"Sasa usije ukanogewa ukasahau kazi." "Haiwezi ikatokea. Kama lini?"
.
.
"Poa. Kesho! Kama kuna lolote, utanchek kwa phone."
.
.
"Usikonde."
.
.
"Enjoy!"
.
.
Gari likahepa. Kinoo akatazama kushoto na kulia. Kulikuwa kimya hamna mtu. Akazama na malaya ndani baada ya kufungua geti.

Wakaekea moja kwa moja ndani ya chumba, milango ikifungwa. Wakapata maji na kujilaza kitandani kwa ajili ya kupeana raha.

Walifanya tendo kwa muda wa lisaa. Kila mtu akawa hoi na mwenye kuhitaji kupumzika.
Mwanamke akalala usingizi mzito akiwa tayari ameshapokea chake na kukiweka begini. Ila Kinoo alijitahidi sana kuepuka hilo swahibu. Akakaza macho.

Alijua fika akilala itakula kwake. Hawa malaya huwa wanaondoka majira ya saa kumi na moja asubuhi na sasa ilikuwa saa kumi na madakika yake.

Alipohakikisha mwanamke amelala vizuri, akatoka kitandani na kwenda kabatini.

Kulikuwa kuna makabati mawili moja lilikaa karibu na kitanda na lingine karibu na mlango. Lililo karibu na mlango lilikuwa la ukubwa wa kati lenye milango miwili.

Ila lililokaribu na kitanda lilikuwa kubwa na pana. Milango mitatu na kioo kikubwa. Lilikuwa ni la nguo.

Kinoo alifuata hili la mlangoni akapenyeza mkono wake kwa nyuma, akatoka na ufunguo. Akalifungua kabati.
Lilikuwa limegawanyika katika vipengele vitano. Cha kwanza kilikuwa kina vitu vilivyokuwa vimefunikwa na makaratasi magumu meusi.

Vingine vilikuwa vina umbo la mstatili, vingine pembe tatu na hata zisizoeleweka.
Kwenye makaratasi kulikuwa kuna maandishi madogo ya lugha ya kirusi. Maandishi hayakuwa mengi, yaliandikwa na kupigiwa mstari.

Kipengele cha pili cha kabati kilikuwa kina matambara ya rangi mbalimbali. Hakikuonekana kama kina zaidi ya hapo, labda kama kingepekuliwa.

Cha tatu kilikuwa kina kitambaa kimoja kikubwa cheusi pamoja na chupa moja kubwa ya plastiki yenye kifuniko kama cha pafyumu.

Cha nne hakikuwa na kitu. Kitupu. Vichengachenga tu vya tembe za vidonge ndivyo vilizagaa.

Cha tano kilikuwa kina chupa tatu za kioo. Chupa moja ilikuwa na shingo nyembamba, umbo la pembe tatu na kalio flat.
Chupa nyingine ilikuwa na umbo la mstatili na shingo nyembamba kama ile ya kwanza. Na ya tatu vilevile kama hii ya pili.

Zote zilikuwa zina vifuniko vya vyupa.

Chupa hizi zilikuwa zimebandikwa vikaratasi vya rangi visivyo na maneno. Chupa ya kwanza ilikuwa na karatasi ya rangi ya nyeupe. Ya pili rangi ya chungwa. Na ya tatu rangi nyekundu.

Lakini kile kilichomo ndani ya chupa zote hizi, kilikuwa cheupe kama maji. Kwa macho usingeona utofauti.

Kinoo alinyanyua chupa moja baada ya moja, akaitikisa na kuitazama. Baada ya hapo akachukua kitambaa kilichopo kwenye kipengele cha tatu.
Akafungua chupa yenye kikaratasi chekundu na kumiminia kwenye kitambaa kimiminika kidogo kilichomo ndani.

Akarudisha chupa na kufunga kabati. Akazima taa na kwenda kitandani. "Hicho kitambaa cha nini?" Akashtuka kusikia hilo swali. Kumbe mwanamke alikuwa macho na alimuona.

Hakuwa sasa na cha kueleza wala muda wa kupoteza, akamdaka mwanamke na kumziba mdomo na pua kwa kitambaa.

Mwanamke akatapatapa kutafuta hewa. Alijaribu kujichoropoa, lakini hakufanikiwa abadani. Hakuweza kupambana na nguvu za mwanaume Kinoo.

Baada ya dakika tatu akawa kimya tuli akiwa amefumba macho. Kinoo akammwagia pembeni. "Shenzi!" Akasonya. Alirudisha kitambaa kabatini na kulifunga. Akaunyanyua mwili wa malaya yule na kuupeleka kwenye chumba fulani kidogo alipoulaza chini kisha akatoka.

Chumba hichi kilikuwa cheupe kisafi. Hakikuwa na kitu chochote kile. Kilikuwa kina dirisha dogo lililokuwa juu kabisa.

Kinoo alirejea akiwa amebebelea kamera yenye miguu mirefu mitatu. Akaisimamisha na kuiwasha, akaielekezea kwa mwanamke yule chini.

Alipoona inamchukua vema, akatoka na kwenda zake chumbani alipozima taa na kujifunika shuka akalala.

Asubuhi, kwenye majira ya saa nne, akaamshwa na honi kali huko nje. Akakurupuka. Macho yake yalikuwa mekundu kwa kulewa usingizi.

Alijinyanyua akaenda nje. Alijua atakuwa Miranda, na kweli. Akafungua geti Miranda akaingia ndani.
"Vipi? Kila kitu kipo shwari?" Aliuliza Miranda wakitembea kuelekea ndani ya sebule.
.
.
"Kila kitu kipo poa. Nimefanya kama maagizo yanavyosema," akaeleza Kinoo.
.
.
"Enhe, ikawaje?" Miranda akauliza kwa shauku. Walishafika sasa sebuleni wakaketi kwenye sofa.
.
.
"Sijatazama imekuaje. Unajua nilikuwa nimechoka sana. Hapa unavyoniona ndiyo umeniamsha wewe. Nimelala saa kumi na mbili kasoro!" Miranda akanyanyuka.
.
.
"Twende ukanionyeshe," akaamuru. Akaongozana na Kinoo mpaka kwenye kile chumba kutazama.

Walifungua wakapokelewa na harufu kali. Walikunja nyuso wakaziba pua.
.
. "Imefanya kazi." Alisema Miranda akitikisa kichwa. Sauti yake haikusikika vema kwasababu ya kujiziba.

Mbele yao kulikuwa kuna kitu cheusi kisichoeleweka. Ni palepale alipowekwa yule malaya masaa kadhaa nyuma, sasa hivi palikuwa pana chembechembe nyeusi nyingi mno.

Huwezi ukadhani kama binadamu alikuwa hivyo. Ni ngumu kuamini.

Chembechembe hizo zilikuwa zinatoa harufu mithili ya pafyumu kali iliyooza ama kuchacha. Harufu hiyo ilikuwa nyepesi na kali kiasi cha kukutoa machozi ukiivuta mara mbili tu.

Kinoo aliitwaa kamera wakatoka ndani ya chumba kwenda sebuleni. Wakaketi, Miranda akaanza kutazama nini kilichotukia.
Kinoo alijitahidi kutazama, ila usingizi ulimmeza ndani ya muda mfupi. Hakuweza kudumu kuendelea kukodoa.
Alikuwa na usingizi mzito. Aliachama mdomo wakati Miranda akifuatilia video kwa umakini. Mara nyingine akiipeleka mbele ama kuirudisha nyuma asipitwe na mambo muhimu.

Alipomaliza kuitazama akajikuta anatabasamu.
.
.
"Kinoo, hii ni kabambe!" Akasema akitikisa kichwa. "Imechukua dakika kumi tu, mwili wote umebadilika na kusahaulika! Hakika mkuu ataifurahia."
.
.
Kimya.
Alitazama akamuona Kinoo amelala. Akasonya akisimama. Akaaga kana kwamba Kinoo anamsikia kisha akaenda zake.

Alijiweka kwenye gari akarudi kwenye makazi yake, Kawe. Alikuwa amebebelea kamera aliyokuwa anaitumia kutazamia video.

Alipoingia ndani akanyanyua simu ya mezani akatia namba na kupiga.
.
.
.
"Hello, I've got good news to tell!" (Helo, nimepata taarifa nzuri za kuongelea)
.
.
Alisema kisha akatabasamu.
.
.
"Yes, it's about the chemical. The red one's proved its worth." (Ndio, ni kuhusu kemikali. Nyekundu imethibithisha thamani yake.)
.
.
"Really. I am going to write a report about it. Expect my email at night." (Kweli. Naenda kuiandikia taarifa. Tegemea barua pepe yangu usiku.)
.
.
"Ok, later then." (Sawa, baadae basi.)
.
.
.
Akakata simu kisha akashusha pumzi ndefu. Akaenda chumbani akiacha kila kitu sebuleni. Hakukaa muda mrefu chumbani akarejea akiwa amevalia bukta nyeusi na blauzi nyeupe.
Akaangaza mezani, hakuona kamera. Moyo ukamlipuka! Hakukaa vizuri akaona mlango wa sebuleni upo wazi. Akili ikamtonya, nimevamiwa!

Haraka akakimbia kufuata meza ya kulia chakula, chiniye akanyofoa bunduki ndogo.
Macho yake yakaanza kuambaa ambaa huku masikio yake yakifanya kazi ya kushurutisha sauti ya kila kitu.

Taratibu alikuwa anaufuta mlango wa sebule kwa tahadhari ya kiwango cha juu.
.
.
.
.
.
- *NANI KAIBA KAMERA?* *YUPO WAPI?* *AMETUMWA NA NANI?*
.
 
Back
Top Bottom