Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Mbona saa tatu inachelewa kufika? [emoji57][emoji57][emoji57][emoji57]
 
*ANGA LA WASHENZI --- 33*


*Simulizi za series*




ILIPOISHIA



Dakika kama kumi mwanaume huyo akatoka nje akiwa amevalia taulo na mswaki upo mdomoni. Kuna kitu alikuwa anaenda kuchukua kwenye gari lake, VX la grey.


Lakini wasaa huo ukawa wa mwisho kwake! Akajikuta amekabwa na mkono mzito. Pua na mdomo vikabanwa na kitambaa kizito chenye malighafi kama taulo.


Kuvuta kwake hewa kukawa kosa. Alivuta mara moja tu na mara mapigo yake ya moyo yakasimama! Habari yake ikaishia papo hapo!


Kinoo akayoyoma zake akifunga mahesabu...


ENDELEA



****


Kwa mbali sauti za majogoo ungeweza kuzisikia zikitangaza asubuhi. Kama ilivyo ada, ndani ya jiji la Dar es salaam, magari yalikuwa yamesongamana barabarani watu wakienda makazini. Wale walioamka na kujiandaa saa kumi na moja, wao walikuwa wameshafika na huenda wameshaanza na kazi.


Lakini kwa Jona haikuwa hivyo. Yeye alikuwa yupo ndani, tofauti kabisa na desturi yake ya kudamka asubuhi na kuwahi kazini. ni siku kadhaa sasa amekuwa akifanya hivyo, na sababu kubwa ikiwa ni kazi za hapa na pale ambazo zimekuwa zikitokea na kumuibia muda. Kuna muda anajikuta amerejea kwenye kazi yake ya upelelezi, maana amekuwa akiumiza kichwa kweli.


Anachofanya akiamka, ni ‘kumchek’ Jumanne na kumjulia hali, kisha anaendelea na kazi zake zingine alizozikubalia kuzivulia nguo. Kazi ambazo anajitahidi kuzikimbia na kuziepuka pasipo mafanikio.


Akiwa ameketi na tarakilishi yake, mwenyewe sebule nzima, kwenye majira ya saa mbili asubuhi, akasikia hodi inabishwa getini. Akachungulia kupitia dirisha lake, akaona uso wa mtu mmoja anayemfahamu.


Alikuwa ni Inspekta Norbert Mlanje, mwanaume polisi aliyeonana na Jona miezi kadhaa iliyopita. Mwanaume huyu akiwa ametumwa na uongozi kwa dhumuni la kumshawishi Jona arejee kazini.


Kwahiyo Jona akawa ameshabashiri kinachofuatia. Ila si vema kumwacha mgeni mlangoni, basi akaenda kuwafungulia na kuwakaribisha ndani. Walikuwa wamevalia makoti marefu ya kaki na suti za kaunda kwa ndani.
Kama kawaida uso wa Inspekta Norbert ulikuwa umekatwa na mustachi mpana mweusi. Macho yake ya kijanja yalikuwa yanapekuapekua eneo la nyumba ya Jona akiwa anasonga ndani.


Wakajitambulisha, yule mpya machoni mwa Jona alikuwa anaitwa Bwire. Ni afisa wa polisi kwa cheo cha koplo.
“Karibuni, bila shaka mtakuwa mna jipya.”


Norbert akasema hana jipya bali ni lile lile, ila kwa sasa ameagizwa na Kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam. Anahitaji kumwona haraka iwezekanavyo, ana maongezi nyeti naye.


Jona akasema ana kazi za kufanya kwa muda huo. Bwana Norbert akamsihi sana aende kuonana na mkuu muda huo kwani wametumwa kuja kumchukua. Hakukuwa na muda wa kutafakari.
Kwa ustaarabu Jona akaridhia. Akajiandaa na kwenda ofisini kwa kamanda baada ya kumuaga Panky ambaye alikuwa amefungiwa ndani ya chumba. Akajipaki kwenye gari la maafisa hao na kuanza safari.


Wakiwa njiani, Norbert akawa anampeleleza Jona juu ya maisha yake. Alikuwa anataka kujua ni kwanini Jona aliamua kuachana na kazi hiyo aliyokuwa akiitenda vema, ila Jona akawa mfinyu wa taarifa. Hakutaka kujiweka bayana kiasi hicho.


Akasema ni maamuzi, na maisha aliyoyachagua.


“Bila shaka utakuwa unafanya vema huko kwenye mambo mengine. Ni wapi ulipojishkiza?” Norbert aliuliza.
“Kwenye kazi mbalimbali,” akajibu Jona kisha akafunga mdomo wake. Mpaka wanafika Norbert hakuwa amekipata anachokitaka. Moja kwa moja, Jona akaingizwa ofisini kwa kamanda na kuketi, kamanda alikuwa akiongea na simu ya mezani.


Alipomaliza akamkaribisha Jona na kumjuia hali ya muda mrefu. Akamwambia amemuita hapo kwasababu kuu moja, ya kumtaka arejee kazini kwani wanamhitaji kuliko muda mwingine wowote.


“Jona, unajua serikali ilitoa pesa yake ukapate mafunzo ili uje kusaidia taifa. Tunaomba urejee na uendelee kutimiza majukumu yako. Huu ni muda ambao Taifa linahitaji ujuzi, juhudi na nguvu yako.”


Jona akaendelea kushikilia msimamo wake, hapana. Kamanda akashindwa kumshawishi kabisa, na sasa ikabidi ahamie upande wa pili wa kumpa vitisho Jona. Uso wake ulibadilika akiwa anasisitizia kile anachosema.


“Jona, maisha yako kamwe hayatakuwa sawa ukiwa nje ya jeshi. Huu ndiyo wito wako na hauwezi kuukwepa. Na sisi tutakukumbusha hilo kila uchwao.”


“Ahsante, Kamanda,” akasema Jona, na kuongezea: “Nitarejea jeshini siku n’takapopata maelezo ya kutosha toka jeshi la polisi juu ya kifo cha mke wangu na mtoto wangu. Siku n’takayopewa maelezo ya kina kwanini biashara yangu ilifungiwa kwasababu sizizo na mantiki. Siku ntakapopewa majibu ya kueleweka, pengine ntashawishika kulamba matapishi yangu.”


Kamanda akaangua kicheko kabla hajaanza kukohoa mara kadhaa. Akatulia na kumwambia tena Jona kauli yake aliyoisema hapo awali ya kwamba maisha yake hayawezi yakawa sawa akiwa nje ya jeshi.


Hakutoa maelezo zaidi, akamwambia Jona amehitimisha na siku moja atakuja kukumbuka hicho anachokisema. Jona akaaga na kwenda zake. Lakini kauli ya Kamanda juu ya maisha yake haikumwacha upesi.


Akawa anaifikiria akiwa garini na mpaka alipofika nyumbani. Kuna mawazo mabovu yalimjia kichwani, ila akayapuuzia kwa kuona muda utaongea.


Akajikuta anamkumbuka sana mkewe na mwanae kana kwamba wamefariki jana.
Alipofika nyumbani, akaendea karatasi zile ambazo amemchora mkewe na mwanae. Akazitazama sana akikumbuka ‘memory’ kadhaa. Machozi yakasonga machoni. Panky akamkuta hapo, na asimsumbue akaachana naye akienda kuketi na kutumia tarakilishi.


Punde Panky akamshtua na kumwambia kuna jambo la kulisikiliza. Kuna sauti ilikuwa inasikika toka eneo la tukio, kule ambapo Nade alikuwa amefungiwa.



***



“Haloo!” Mh. Eliakimu aliongea na simu akiwa amekunja sura. “Nade?”
Mara akasikia sauti ya kiume.
“Malaya wako uliyemtuma, tunaye hapa.”
“Wewe nani?” Mheshimiwa akawahi kuuliza.


“Mimi ni yule uliyedhani ni fala kwa kumtuma Malaya wako aje kunimaliza.”
Mheshimiwa akapandwa na hasira. Maneno mabovu na makali yakamtoka.


Ila aliyeongea naye akiwa ametulia, akamngojea amalize, kisha akamuuliza:
“Unamtaka malaya wako hai ama lah?”
Mheshimiwa akanyamaza kwanza. Swali likarudiwa. Akatishishia kummaliza mwanaume huyo endapo akifanya lolote kwa Nade. Vitisho ambavyo havikusaidia lolote lile, kwani mwishowe alinywea na kwenda sawia na mtekaji.
Hakuwa na namna.


“Tutabadilishana na Miriam. Utamleta Miriam, nawe utampata mtu wako. Deal?”


Hapa pakawa pagumu kwa Mheshimiwa. Ila akajikuta hana machaguzi mengine zaidi ya kuridhia, japo kwa shingo upande. Simu ikakata.


Akabakia akiwaza haswa juu ya namna ya kufanya. Akabakia akiwaza namna gani ya kumkomboa mwanamke pekee anayemuamini.


Kazi haikwenda kabisa, na kichwa kiligoma. Akaaga na kurudi zake nyumbani. Akamkuta Miriam akiwa ameketi sebuleni anatazama televisheni. Ulinzi ulikuwa mkubwa kuhakikisha mwanamke huyo haendi popote pale.


Mwanamke huyo alikuwa amechafuka kwa majeraha. Uso wake ulikuwa umevimba, macho yake yakiwa mekundu usijue kama analia ama ameumia.


Akamuuliza juu ya yule mwanaume ambaye amemteka Nade. Miriam asiseme kitu, akamtazama na kunyamaza akiangalia televisheni. Baada ya Mh. Kurudia swali mara kadhaa akiambatanisha na vitisho, Miriam akamwambia kwa ufupi, akihangaika kuongea:
“Eli, umeingia kwenye anga la wenyewe.”


Baada ya hapo hakusema tena lolote.



***



Kang! Kang! Kang!


Sauti ya chuma kilichopo mlangoni ilisikika ikilia. Mara sauti ya kichina ikatoa ruhusa na mtu akazama ndani, alikuwa Panky. Akasimama kiukakamavu akimtazama mkuu wake aliyekuwa amejaa kwenye kiti kirefu cheusi nyamanyama.


Juu mezani kulikuwa tarakilishi kubwa iliyokuwa ipo on na kunguruma. Panky aliposalimu akakaribishwa kuketi na kisha mwenyeji wake akampatia atensheni yote. Akamtazama na macho yake nyuma ya miwani.


“Nimemaliza kazi,” akasema Panky. Mkuu huyu alikuwa hawezi kuongea Kiswahili vema ila alikuwa anakisikia na kukielewa. Aliposikia kauli ya Panky, akapandisha nyusi zake kwa mshangao. Kisha akauliza kazi hiyo imemalizwa lini akitumia lugha ya kichina.


Uzuri Panky alikuwa anaelewa lugha hiyo, japokuwa naye matamshi yalikuwa yanamshinda. Ana kichwa chepesi cha kujifunza ila lugha ya kichina iligoma kunasa mdomoni.


Akaweka bahasha ya kaki mezani alafu akamsogezea mkuu wake kwa kuiburuza. Mkuu akaipokea na kufungua kutazama yaliyomo ndani.


Akaona picha tatu alizozitoa na kuziangaza kwa macho yake. Akamwona Jona akiwa amelala chini akielea kwenye dimbwi la damu. Paji lake la uso lilikuwa linachuruza damu na macho yake yakiwa yametoka nje!


Picha zilikuwa zinatisha na kusisimua kutazama.


Mkuu akatabasamu na kisha akamtazama Panky. Akampongeza kwa kazi aliyoifanya huku akiweka bayana kwamba hakutegemea kama angefanikisha hilo. Panky akamwambia alijitahidi ili kufuta makosa aliyoyafanya.


Mkuu akampongeza tena na kisha akampatia kibali cha kwenda kuendelea na kazi akimsihi Panky abakize picha zile palepale na yeye. Panky akaridhia na kwenda. Mkuu akamwita Nigaa na kumpatia kazi.


Akamwonyesha picha zile ambazo Panky alimpatia, akamwambia neno moja alilolisema kwa lafudhi ya kichina:
“Hakikisha.”


Nigaa akajua nini cha kufanya na pasipo kuuliza akatoka zake nje. Mkuu akalalia kiti na kushusha pumzi. Akatafakari zile picha, ila kwa macho yake zilikuwa sahihi na si za kubandikwa kiteknolojia. Ila hakuamini uwezo wa Panky kiasi hicho.
Amewezaje kitu ambacho Bigo ameshindwa?


Alitamani kujua.
 
*ANGA LA WASHENZI --- 34*


*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

“Hakikisha.”

Nigaa akajua nini cha kufanya na pasipo kuuliza akatoka zake nje. Mkuu akalalia kiti na kushusha pumzi. Akatafakari zile picha, ila kwa macho yake zilikuwa sahihi na si za kubandikwa kiteknolojia. Ila hakuamini uwezo wa Panky kiasi hicho.

Amewezaje kitu ambacho Bigo ameshindwa?

Alitamani kujua.

ENDELEA

“Tayari, nimefanikiwa.” Ujumbe ulifika kwenye simu ya Jona toka kwa Panky. Jona akaupokea na tabasamu alafu akaujibu ujumbe huo.

“Basi fanya kama vile tulivyopanga.”

Panky akaupokea ujumbe huo, na kisha akaujibu:

“Hamna shida,” huku akielekea eneo lao la kazi. Mbele yake kulikuwa kuna mlango mkubwa wa chuma ukiwa umepachikwa bandiko jeupe lililosomeka ‘SPACE BUTTON’. Pembezoni mwa mlango huo kulikuwa kuna kifaa cha kuandikia ‘password’.

Panky akabofya hapo mara kadhaa na mara mlango ukafunguka. Akazama ndani na kupokelewa na wenzake ambao walimkumbatia na kumkaribisha kwa bashasha. Hawakutegemea kama Panky angerejea salama.

Baada ya muda kidogo, na hali kutulia, Panky akamtafuta Marwa ndani ya eneo lao. Eneo lilikuwa kubwa lililotapakaa mashine na tarakilishi. Kwa mbali kwenye kona akamwona mlengwa wake.

Ndani ya ofisi hiyo kuna vitengo kadhaa: ukarani, graphics, hacking na coding, na Marwa alikuwa kwenye kitengo cha graphics. Yeye na jamaa wawili.

Marwa alikuwa ni mwanaume mweusi mwenye nywele nyingi na chunusi kadha wa kadha usoni. Vidole vyake vilikuwa katika keyboard akichapa jambo. Macho yake yalikuwa yamezama kwenye kioo cha tarakilishi.

Kwa kumtazama tu, alionekana yupo bize. Panky akamjongea na kumsalimu. Akajibiwa pasipo kutazamwa. Marwa alikuwa anafanyia kazi picha fulani ambayo Panky aliona inapendeza sana ikikaa ukutani.

Marwa akasimamisha shughuli yake na kumtazama Panky. Alikuwa anamwona anampotezea muda ingali ana kazi lukuki za kufanya. Akauliza:

“Una shida gani?”

Panky akatabasamu. Kisha akamwambia Marwa kuna picha fulani aliiona akiifanyia kazi, ilimvutia na angependa kuiona.

“Nafanyia kazi picha nyingi Panky, unamaanisha ipi?”

Panky akajitahidi kuielezea picha yake iliyokichwani. Marwa akamwelewa, ila akamuuliza pasipo kumtazama:

“Unajua miiko ya kazi?”

“Najua, Marwa. Usijali, Moderator hatajua,” Panky akajibu.

Moderator ni msimamizi wa mule ndani. Ni mchina kwa utaifa na kazi yake ni kuhakikisha kila mtu anafanya kazi yake pasipo kuingiliana. Kuhakikisha wafanyakazi hawapangi jambo lolote kwa pamoja mule ndani, aidha kugoma, kuharibu mashine kwa kudhamiria, ama kupanga jambo la kitaaluma likaathiri kampuni.

Macho ya Moderator yanakuwa yanaambaa muda kwa muda, mahali kwa mahali, na masikio yake yanasikiza muda wote. Ujuzi wake pia kwenye mambo ya tarakilishi na mifumo yake yote, upo juu.

Kabla Marwa hajasema jambo, akasikia vishindo vya miguu. Na mara vikakoma na sauti ikauliza:

“Kuna tatizo hapa?” sauti nyembamba yenye lafudhi ya ki-mandarin. Alikuwa ni Moderator, mwanaume mfupi mwenye nywele za wastani. Macho yake yakisaidiwa na miwani maana yameshaharibiwa na mwanga wa tarakilishi kupitiliza.

Alikuwa amevalia shati jeusi kama vile sweta likimbana mpaka koo. Pamoja na suruali pana ya kitambaa cha rangi ya fedha, na mokasin nyeusi.

“Hamna tatizo,” Panky akawahi kujibu akitabasamu. “Nilikuwa namuuliza kama angeweza kuhudhuria sherehe ya mdogo wangu.” Akasema kwa haraka akijua fika Moderator hakuwa mzuri kwenye lugha hiyo.

Kisha akanyanyuka na kurejea tarakilishi yake. Kuna kazi akawa anazifanya ila akifikiria ni kwa namna gani anaweza kumuingia Marwa.


***


Baada ya maongezi yaliyokuwa yanafanyika kwa sauti ya chini chini, Mkuu, ama Sheng’ kama aitwavyo na wachache, akiwa anaongea na mwaname fulani mweusi mwenye nywele ndefu na macho madogo akiwa amevalia suti, akatikisa kichwa na kusema:

“This must be a plot.” (Huu lazima utakuwa ni mpango.) alisema kwa sauti yake ya kichina kiasi usijue kama ameongea lugha ya kiingereza. Mwanamke naye akatikisa kichwa kwa kukubali.

Watu hawa walikuwa wanaongelea mauaji ya kushtukuza ya Brokoli. Nani aliyeshiriki, na pia sababu iliyopelekea tukio hilo.

Mwanamke huyu mweusi ambaye yupo hapa, alikuwa ndiye yule ambaye Brokoli alikuwa akiwasiliana naye wakati akifanya tukio la mauaji ya Mudy na hata akiwa njia kumtafuta yule ambaye Mudy amemkabidhi nyaraka, yaani Kinoo.

“The document should be fetched! Otherwise we may awake the dead demon.” (Nyaraka lazima ipatikane! La sivyo tunaweza tukaamsha jinni lililolala.) alisema Sheng’ kwa msisitizo akimwambia yule mwanamke.

Punde mwanamke huyu akasimama na kuinamisha kichwa chake. Alafu akaondoka akitembea kikakamavu. Chini alikuwa amevalia viatu vya visigino virefu lakini akitembea kana kwamba amevaa raba.

Mwanamke huyu akaendea gari lake alilolipaki nje, IST nyeupe new Model, akazama ndani na kuondoa chombo.

Kwa jina waweza kumwita Gee.


***


Saa moja usiku …


Simu ilinguruma … ggrrrrrmmmm! Mara mbili kabla Glady hajaipokea na kuweka sikioni. Alikuwa amejilaza kitandani akiwa na mashoga zake wawili wote wakiwa wamevalia nguo za ndani tu.

“Vipi?” akauliza .

“Njoo hapa nje,” sauti ya kiume ikamjibu na mara simu ikakata. Wenzake wakawahi kumuuliza kama ni mteja, Glady akatikisa kichwa chake na kusema ni fala fulani aitwaye Mustapha.

Akajiveka khanga na kutoka nje. Akamkuta huko mwanaume aliyevalia ‘form six’ ya bluu na suruali nyeusi ya kadeti. Mkono wake wa kulia ulikuwa upo ndani ya POP, ameuning’iniza ukibembeshwa na kamba uliyodaka shingo.

Mwanaume huyu alikuwa ndiye yule aliyezama matatizoni na Lee kwa kushikilia nyaraka isiyo ya kwake. Glady akamtazama mkono wake uliovunjwa, alafu akamuuliza:

“Unataka nini?”

Mustapha akamwambia yupo pale kwa ajili ya kupata taarifa za yule mchina, Lee. Kwa alimchofanyia, kamwe hawezi kumwacha salama!

“Vita aliyoianzisha, kamwe haitaisha. Nitahakikisha ananijua mimi ni nani, na si kila mtu ni wa kumchezea!”

Glady akaangua kicheko.

“Mustapa, ulishindwa siku ile. Au unataka uuawe kabisa?”

Mustapha akamsisitizia apewe taarifa za huyo mchina alafu atakuja kumpatia taarifa baadae juu ya nini alichomfanyia. Glady akamwambia hana taarifa yoyote ya Lee. Alikutana naye klabuni na kuachana huko huko.

Mustapha hakuamini. Na kwa kutaka taarifa hiyo ya Lee, akamwambia Glady kwamba ile nyaraka ambayo Lee alikuwa anaitaka na kuichukua, wanayo. Na muda si mrefu watajua kuna nini ndani yake.

Glady akaagua tena kicheko. Alijua Mustapha anaongopa.

“Unatolea wapi na uliitoa?” akauliza. Mustapha akatoa simu yake kubwa na kumwonyesha Glady picha. Kumbe mwanaume huyo alikuwa amepiga picha ile nyaraka ya Lee, picha zimetunzwa kwenye gallery!

Glady akashangazwa.

“Ila we Mustapha una hatari!”

“Hii lazima itakuwa dili. Kwa namna alivyokuwa anaitafuta vile, itakuwa dili tu!”

“Sasa utaelewa nini humo na kimeandikwa kichina?”

“Aaaggh! Unadhani hakuna watu wanaojua kichina? Wachina wapo wangapi Kariakoo?”

Mustapha akamtaka sasa Glady amsaidie kupata taarifa za Lee, ili na yeye aweze kunufaika na chochote kitu kitakachopatikana humo. Taarifa hizo za Lee si tu kwamba zitamsaidia Mustapha kulipiza kisasi, bali pia zitawasaidia kujua namna gani watanufaika na nyaraka ile endapo wakiona kuna mhitaji wa yule ‘mchina’.

“Mustapha, kweli sina!” Glady akajibu. “Lakini naahidi kukutafutia. Nipe muda kidogo.”

Wakaachana kwa ahadi hiyo.


***


Saa tatu usiku…

Jona amesimama mbele ya karatasi zake za kuchorea, anatazama jambo.

Anafungua karatasi ya kwanza na kisha ya pili. karatasi hizo zina picha ya mkewe na mwanae. Anazitazama kwa muda kabla hajapindua karatasi nyingine mpya na kuanza kuchora mchoro mpya akitengeneza msingi kwa penseli ya kawaida.

Ilikuwa ni picha ya mtoto anachora. Na hakuwa anarejelea popote pale isipokuwa kichwani kwake.

Akiwa anaendelea kuchora mchoro huo, akili yake ipo kwenye amani na macho yake yakizingatia kazi anayoifanya, mara anasikia sauti ya honi huko nje. Anasita na kujiuliza ni nani huyo. Hakuwa na miadi na yoyote, na ule ulikuwa ni muda wa usiku.

Akaendea dirisha na kuchungulia. Akaona gari kubwa, VX rangi ya fedha. Akiwa hapo hapo anatathmini, akaona kuna mtu mmoja ameshuka toka kwenye gari hilo. Macho yake nyuma ya miwani yakatambuo umbo la mgeni huyo.

Alikuwa ni Mh. Eliakimu!

Muda huo! Akastaajabu. Akateka bunduki ndogo na kuikobeka nyuma ya kiuno, alafu akaendea geti na kumkarimu mgeni. Alikuwa amebeba tahadhari zote akiwa tayari kwa lolote linaloweza kutokea.

Mheshimiwa alikuwa ameongozana na bodyguard, mwanaume mrefu mweusi mwenye misuli mipana. Bodyguard huyo akaamriwa abakie nje wakati Mheshimiwa akiingia ndani na kuketi kochini.

“Sikutegemea ujio wako, vipi mheshimiwa?”

Mh. Eliakimu akashusha kwanza pumzi ndefu. Hakuwa anajua wapi pa kuanzia. Kujileta kwake kwa Jona kulikuwa hatari kwake na kwa siri zake, ila ndiyo hivyo hakuwa na namna! Maji yalikuwa yamemfika shingoni.

“Jona,” Mheshimiwa akaita. “Achana na yote yaliyopita. Najua kuna mambo ambayo yalitokea hapa kati, nisingependa kuyaongelea kwa sasa maana si muda muafaka. Nimekuja hapa maana nina shida na ninahitaji tena msaada wako.”

Jona alikuwa kimya akimtazama. Mheshimiwa akameza kwanza mate, alafu akasema:

“Nade ametekwa, naomba unisaidie kumuokoa.”


***
 
Back
Top Bottom