*ANGA LA WASHENZI II -- 76*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
“Yes, you bitch!” akafoka komandoo mwenye radio call. Uso wake mweusi ulijawa na ndita na kona za mdomo wake zilishuka chini. “If you are a man, show yourself up!” akatema mate kwa kufoka.
“Then come down where you heard shots. I will be waiting!” sauti ikamjibu.
ENDELEA
Bwana yule komandoo akasonya na kukata mawasiliano kisha akawatazama wenzake na kuwaambia kile alichoambiwa ya kuwa watu hao, waliowamaliza wenzao, wanataka washuke kufuata sauti ya mlio wa risasi ilipotokea.
Ila wakakabwa na tahadhari. Kama wakienda huko, wanajuaje namna ambavyo watu hao wamejipanga? Ilibidi waibuke na namna ya kukabiliana nao kwanza kabla ya kwenda. Kama inawezekana wajue pia na idadi na hata silaha walizo nazo.
Ila yote hayo watayafanyaje? Basi wakakubaliana kumtuma mmoja kama chambo, yeye aende kwa siri huko ambapo wanahisi hao watu wapo kisha atoe taarifa na basi wenzao wataenda kutimiza kazi.
Mtu huyo akateuliwa, na pasipo kuuliza akaenda kutekeleza kazi yake. Wakati akienenda akawa anawasiliana na wenzake barabara juu ya wapi alipofikia.
Basi wakiwa wanafanya hilo na wakitaraji matunda ya kazi yao, hawakujua ya kwamba tayari walikuwa ndani ya mpango kabambe wa kumalizwa.
Watu wale, wauaji, ambao walikuwa wameongea nao kwenye mawasiliano walikuwa na vifaa bora kabisa vya mawasiliano. Kwa kupitia vifaa hivyo wakatambua makomandoo wale wapo pande gani ya dunia, na hata mipango ya kuwamaliza ikasukwa na sasa inatekelezwa.
Wanaume hao wauaji wakajigawa kwenda kila pande kuwazunguka makomandoo. Walikuwa wananyata kiasi cha kutokutoa sauti yoyote. Watu hawa walikuwa wataalamu haswa. Kila nyendo yao ilikuwa ni ‘professional’. mikononi mwao walikuwa wamebebelea bunduki na masikioni mwao walikuwa wamechomelea waya za mawasiliano.
Waya hizo zilikuwa hazionekani kwa haraka kwasababu ya barakoa walizokuwa wamezivaa. Ila ungetazama vema upande wa masikioni mpaka kinywani, basi ungepata kuziona.
Basi watu hawa wakiwa wananyata, wakawa wanazungumza kwa sauti ya kunong’ona. Na baada ya kama robo saa, wakawa tayari wamewazunguka walengwa wao. Lakini kwa namna walivyotenda kazi yao, hakuna komandoo hata mmoja aliyebaini hilo!
Hali ilikuwa tulivu sana. Baridi bado lilikuwa linatawala. Usiku huu ulikuwa mrefu sana. Na kabla haujakoma, wazi kulikuwa kuna mambo mengi yanakuja.
“... Hakuna mtu, over… hakuna mtu, over!” sauti ya komandoo aliyetumwa ilivuma.
Mwanaume huyo alikuwa tayari kwenye eneo ambalo wenzao wameuawa. Aliiona miili yote ya wenzao ila hakuona watu wengine wa ziada. Miili hiyo ambayo tayari ilikuwa imeanza kuvutia wadudu, ilikuwa inatisha. Japo komando huyu alikuwa amefundwa kuzoeza mambo haya, hili jambo lilimsisimua.
Namna ambavyo miili ile ilikuwa imetifuliwa pasi na huruma kulimfanya akajita na hofu.
Mara akasikia sauti ya kitu kikitembea. Haraka akageuza uso wake kutazama. Hakuona jambo. Akawasha kurunzi kuangaza akiwa amekodoa macho haswa. Napo hakuona kitu. Ila pale alipotazama juu, mara akavamiwa na mtu mzito aliyemwangusha chini. Mtu huyo alikuwa amebebelea kisu chenye mpini mdogo na ncha ndefu.
Kwenye makali ya kisu hicho kulikuwa na mawimbimawimbi yaliyochongoka. Upande wake wa pili kulikuwa kumenyooka kisha kukajipindia kama upinde wa mshale kuelekea kwenye ncha. Kilikuwa ni kisu kizito na cha kutisha.
Yule mvamizi akajitahidi akitaka kumchoma komandoo kichwani. Komandoo akakidaka na kumzuiza. Wakapambania nguvu, mwishowe komandoo akamzidi na kumtupia kando kisha akanyanyuka upesi. Akatazama kando na kando kutafuta silaha yake, akaiona! Kabla hajainyanyua, kisu kikarushwa kwanguvu kumchoma mkono. Akalalama kwa maumivu makali!
Hajakaa vema, akakitwa teke la kifua na kujikuta chini kama kifusi. Hakukaa hapo, akachomoa kisu mkononi akiugulia maumivu, akakitupa kikaenda kombo, akasimama na kujipanga kwa ajili ya kupambana. Mkono wake wa kulia ulikuwa unamwaga damu, alikuwa anahisi maumivu makali sana, lakini hakuwa na wa kumdekea hapa la sivyo atatolewa uhai!
Basi yule bwana mwenye barakoa nyeusi akaguna kwa cheko. Akatazama mkono wa yule komando unaovuja damu kisha akatikisa kichwa chake akiigiza masikitiko. Alipokaa tenge, akamkaribisha komandoo aje kupambana.
Komandoo akatupa mitupo yake mizito, bwana yule akakwepa. Naye bwana yule alipotuma mashambulizi yake, komandoo ‘akazitoa’ kwa ustadi. Ila sasa shida ilikuwa ni mkono wake. Alikuwa anahisi maumivu makali. Kisu kilitoboa kabisa mkono wake na kutokezea upande wa pili.
Alijituma kukwepa, kukinga na hata kushambulia lakini kasi yake ilikuwa inazorota. Kuna muda pia alikuwa anashindwa kujikinga kwa mashambulizi ya upesi kwasababu alikuwa anahisi maumivu makali mkononi hivyo akawa anabaki ‘uchi’ mbele ya adui.
Na bwana yule, mwenye barakoa, akiwa ametambua udhaifu huo, akautumia ipasavyo na mwishowe akamdhibiti komandoo na kumlaza chini. Akamtwanga risasi tatu za kummalizia kabla hajauacha mwili hapo na kuondoka zake.
***
“Don’t fire!” sauti ya kunong’ona ilisikika kwenye vipokea sauti. “I think we need them.”
Wanaume hawa, saba kwa idadi, walikuwa wamelala chini wakifunikwa na majani yaliyojawa na umande. Hawakuwa wanaonekana kabisa kwa kumezwa na majani pia ukiongeza na rangi zao za nguo.
Macho yao yalikuwa yamezama kwenye tundu za hadubini za bunduki wakiwa tayari wameshawaweka walengwa wao kwenye rada kwa ajili ya shambulizi, na tayari walishawazingira makomandoo.
Basi baada ya amri ile kutoka, wakasimama na punde, “Hands up!” amri ikapazwa. Makomandoo kutazama, walikuwa wamezingirwa na watu saba kwa idadi. Kila pande ya dunia ilikuwa ina matundu ya bunduki!
Wakaamriwa watupie bunduki kando ya mbali na kisha walale chini upesi, wakatii! Wakafungwa kamba mikononi na safari ikaanza kwenda kule ufukweni kukuta boti yao wapate kwenda.
Wakatembea kwa muda wa dakika kadhaa, kama dakika kumi na hivi, wakafika fukweni. Huko wakawatweka makomandoo wale kwenye boti na kutaka kuondoka.
“There are still more!” akasema Wales punde baada ya kuwaona wale makomandoo wakiingizwa botini, na akaendelea kwa kusema kuwa watu hao bado watakuwa huko kisiwani, ndiyo waliokuwako kabla ya hawa wengine kufika.
“Those are more dangerous,” akatahadharisha akimtazama yule kamanda wa kikosi kilichokuja kumwokoa.
“Worry out,” akasema kamanda kisha akauliza, “How many are they?”
“Three!” akajibu Wales. Basi kamanda wa kile kikosi akateua watu wake sita na kurudi nao kisiwani kwenda kuwatafuta hao waliobakia, hivyo basi hapa botini wakabakia wawili, mbali na Wales wa tatu.
**
“You go to this side! … you two go over that one!” alisema kamanda wa kikosi akiwagawa watu wake. Wawili wakaenda upande wa mashariki wa kisiwa, wawili wakaenda upande wa magharibi wa kisiwa na yeye pamoja na mmoja wakazama katikati ya kisiwa.
Msako ukaanza.
Wakati huo majira yalikuwa bado ni ya usiku. Mwezi ulikuwa unaangaza lakini kwa ufifu sana ndani ya kisiwa kwani miti iliyofungamana matawi yalikuwa yanazuia mwanga usipenye.
Hivyo kwa humu ndani, kulikuwa kuna kagiza katotoro, isipokuwa tu kwenye sehemu moja moja hapa na pale palipokuwa hapajazongwa na matawi magumu ya miti.
Wanaume wakasonga kwa tahadhari na huku wakijiweka kwenye mawasiliano. Kwa kama mwendo wa dakika kumi, wakawa bado hawajaambulia jambo. Kulikuwa patupu. Ni kiza na ndege, matawi na popo.
**
“How long will this take?” akuliza mwanaume mmoja aliyekuwa amevalia barakoa kule botini, akiwa ni miongoni mwa wale wawili walioachwa pamoja na Wales. Hata kwa sasa walikuwa wamevulia barakoa zao, ila tutawaita kwa majina hayo tupate kuwatambua vema.
“No one knows!” akajibu mwingine mwenye barakoa. Alikuwa amejegemeza akiwa anavuta sigara yake aliyoichoropoa kwenye droo moja ndani ya boti.
“You know we have to be at the bay before the dawn,” akasema tena yule mwanaume wa kwanza. Ni yeye ndiye alikuwa karibu na usukani wa boti, bila shaka ni dereva. “We must be on time, otherwise we may miss the plane.”
“I know that story, pal,” akajibu mwenzake. “But do you think we can do anything about this?”
“Perhaps there was no need to go back for the others. If we leave them here, they will just die! Was there a need?” akang’aka yule mwanaume karibu na usukani kisha akamtazama Wales aliyekuwa amelala chini kwa uchovu, akamuuliza, “was there?”
“Yes, it was,” akajibu Wales. “It is better we finish what we’ve started. If we leave these punks alive, I surely tell you they will come back knocking at our door.”
Alipomaliza kusema hayo, wakahisi boti inapepesuka. Wakatazamana pasipo kusema jambo. Pengine wakahisi ni pepo ama maji ya bahari. Ila hapana, boti ikapepesuka zaidi na zaidi! Mmoja akalazimika kwenda kutazama.
Ila alipoenda hakurejea ndani ya muda. Mwenzake, yule aliyekuwa karibu na usukani, akapata shaka. Kabla hajaenda kutazama huko nje, Wales akamsimamisha na kumwambia, “Be careful.”
***