Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tivie.....utakapo anza nyengine....Umeme haupo huku Mbezi beach tangu asubuhi!
Acha kuendekeza dezo jiongeze nduguAsante kamanda , Hatimae tumehitimisha safari, nabuku nafasi ingine kwa hiyo ijayo na kama hutojali tuwekee pia huo mzigo ujao hapa Jf ,usisahau kunitag
nimefika epsode ya 50
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] siunajua tenaHahahaaaaaa
Mkuu naona unaweka kumbu kumbu kiaina
Mkuu umetisha*ANGA LA WASHENZI (MWISHO)*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
“Do I know you, madam?” Kamanda akauliza.
“Yes, you do!” akajibu Glady akirembua. “Would you mind a dance?”
“Off course!”
Glady akamkwapua Kamanda na kusonga naye kando kucheza wimbo wa taratibu uliokuwa unapiga. Sikioni mwake sauti ya mbali ikamwambia, “Hakikisha unamuua.”
ENDELEA
Kamanda alimtazama Glady machoni akamwona mwanamke mrembo haswa. Mwanaume huyu hakuwa mtu wa kupenda rangi nyeusi, ila hapa kwa Glady akachina haswa. Hakuwahi kumwona mwanamke mrembo kama huyu. Kwenye mikono yake alikuwa anampatia joto fulani analolihitaji.
Na zaidi ya yote Glady alikuwa na kitu ambacho wanawake wote wa kizungu aliokuwa nao hawakubahatika kuwa nacho - shepu! Kiuno kinajulikana kipo wapi, na baada ya kiuno basi nini kinafuatia.
Hakika hapa bwana Kamanda alikuwa ameshikwa. Ugumu na ukatili wake wote ukawa ni sponji chakavu mbele ya mwanamke kubuhu. Mtambo. Bibie Glady.
Kwa kujiamini kabisa mwanamke huyo alikuwa anamtazama mwanaume huyo machoni. Lakini siyo kumtazama kama ujuavyo wewe, lah! Kumtazama kiuanamke. Kumtazama kwa macho yanayoomba huba. Macho yanayolilia mapenzi ya ndani!
Ama kwa hakika chunusi ilipata kucha ndefu. Kiuno cha Glady kilichokuwa kimeshikiliwa na mkono mpana wa Kamanda kilikuwa kinaenda kutoka na midundo ya muziki. Nyonga yake iliaga kila melodi.
“Who are you?” Kamanda akajikuta anauliza. Alishindwa kuvumilia zaidi. Hakutaka muziki ukome. Hakutaka mwanamke huyu atoke mikononi mwake. Na hii ndiyo ilikuwa sababu ya Glady kulipiwa kila kitu aje Uingereza. Hata wale waliokuwa wanatilia shaka, sasa walianza kusadiki. Kila kazi na mkono wake.
“My name is Rebentha…” akasema Glady pasipo kutumia nguvu. Lips zake zilizokuwa zimechovya ‘lipstick’ hazikuwa zikihangaika bali ulimi.
“Rebentha?” Kamanda akaguna. “Rebentha from?”
Glady akatabasamu. Kamanda akahisi amepigwa shoti, kwa muda kidogo akasahau hata alichouliza, akasema, “You are so beautiful, Rebentha!”
“Thanks,” Glady akaipokea kwa madaha na kusema, “I am from Caribbean.”
“Caribbean! Wow! I have never been there. How did you know me?”
“How long does it take to see a handsome lonely man in the party?”
Kamanda akatabasamu pasipo kutia neno.
“Honestly I don’t know you. But my eyes just fell on you. Is it wrong?”
Kabla Kamanda hajatia tena neno, Glady akatazama kushoto kwake kwa mbali na kusema alikuwapo kule akinywa kinywaji kabla hajamtia machoni mwanaume huyo aliyependeza akiwa mpweke, aongea tu na wazee hapa na pale.
“You are so confident!” akasema Kamanda.
“Doesn’t that turn you on?” Glady akauliza. Basi Kamanda akaishia kutabasamu, akamkumbatia kwanguvu mwanamke huyo na kucheza naye kwa muda kabla hajamwomba wakapumzike kidogo na kufanya maongezi zaidi.
Lakini kabla ya kwenda huko, Glady akamlaghai wacheze zaidi kwani bado ana hamu ya kufanya vivyo. Akiwa nyumbani huwa hapati huo muda na yeye kucheza ndicho kitu anapenda zaidi.
Basi Kamanda hakuona tabu. Hakutaka kumghafirisha mwanamke huyo mrembo, akampatia dakika tatu za ziada. Wakacheza na akiwa anamuuliza maswali ya hapa na pale, wapi ametokea na amekuja na nani?
Wakiwa hapo wanacheza kutafuna hizo dakika tatu za ziada, ndipo Glady akawa anapanga namna ya kufika kwenye kilele cha kazi yake. Wigi lake refu lilikuwa linamziba masikio yaliyokuwa yana ‘earphone’ za mawasiliano na pia hereni zake zenye ncha kali.
Baada ya kutazama huku na kule, akiwa anapiga mahesabu kichwani, akatengeua mguu wake wa kuume, kisigino cha kiatu kikameguka, akaangushia kichwa chake kwenye bega la Kamanda. Mara Kamanda akaguna kutoa sauti ya maumivu akiwa amekunja sura.
“I am sorry! … shit! Its my earring!” Glady akasema akitoa kichwa chake akijitahidi kusimama. Shingo ya Kamanda ilikuwa imechanjwa kidogo. Kwa mbali kulikuwa kuna kamstari kekundu. Na punde, damu ikaanza kuchuruza.
“It’s okay, never mind!” Kamanda akasema akishika eneo lenye maumivu. Kutazama vidole vyake akaona alikuwa anavuja damu, basi akamwomba mrembo muda mchache akapate kujiosha, atarejea.
“Its ok. I will be waiting,” akasema Glady akiwa na sura ya taharuki na huzuni. Mwanamke huyu aliigiza haswa. Basi Kamanda akaenda zake ‘washroom’ Glady akimtazama mwanaume huyo akiishia, kisha akaweka kidole chake sikioni na kusema,
“Nimemaliza kazi!”
Ama kweli vitamu ndivyo venye sumu.
**
Alijihakikisha kama yupo sawa. Anhaa akaridhika. Damu ilikuwa haitoki tena hata tone. Basi akajifuta kwa mara ya mwisho na kitambaa chake kilicholowana maji alafu akajitengenezea vema. Bado alikuwa amependeza na suti yake toka Italia.
Kamanda akajirekebisha nywele zake kabla ya kwenda kukutana tena na mrembo. Alipojihakikishia kuwa yuko sawia kwa kila kitu, akatoka kuuendea mlango. Ila kabla hajaufikia, akahisi kichwa chake kinagonga. Alisimama na kuskizia, akajiona bado yu vema, basi akaendelea na safari yake.
Alipofika kwenye uwanja akaangaza huku na kule, hakumwona Rebentha! Lakini punde , si Rebentha tu, hata watu wengine akawa hawaoni. Walianza kuwa maruweruwe, asione cha kueleweka! Kichwa kikamgonga sana, na damu zikaanza kummiminika toka puani kwa fujo.
Hakudumu kwa muda mrefu akiwa amesimama, akajikuta chini!
Watu wakamtazama na kumsogelea. Damu hazikukatika, zikaendelea kummiminika zaidi na zaidi kuchafua suti yake aghali. Kwa muda kidogo shughuli ikawa imesimama. Mwili wa Kamanda ukanyanyuliwa na upesi ukatiwa kwenye gari la wagonjwa lililokuwapo eneoni kuwahishwa hospitali, huku nyuma tukio hilo likiwa limeacha zogo.
Gari hilo la wagonjwa likatimka haswa, ving’ora vikitawala barabarani. Lakini kumbe waliopo humo ndani si wahudumu bali ni Jona na wenzake. Walikuwa wamevalia sare na vichwa vyao vimemezwa na kofia zenye chapa ya huduma.
Sasa watu hawa walikuwa wamempata Kamanda. Tena kwa ulaini kabisa. Gari hilo la wagonjwa baada ya kutembea kwa takribani dakika kumi na tano, likazima ving’ora na kutoka kwenye barabara kuu.
Likapotelea huko kusikojulikana.
**
Baada ya juma moja … Dar es salaam, kituo kikuu cha polisi.
Sauti ya kishindo cha miguu yenye buti ilikomea mbele ya lango la nondo za chuma, hapo akasimama Askari mnene mweusi mkononi akiwa amebebelea bunduki na kiunoni mwake amening’iza pingu.
Akatazama ndani ya chumba cha mahabusu, macho yake makubwa yakaangukia kwa mtu mmoja aliyekaa nyuma kabisa. Jona. Akampa ishara ya kichwa kumtaka asonge karibu. Jona akafanya hivyo. Akashika nondo na kumuuliza askari,
“Mmefanya nilichokiomba?”
Askari hakumsemeza jambo, akachojoa ufunguo na kufungua lango, Jona akatoka. Akaongozana naye mpaka kaunta ambapo huko alikutana na Makamu wa Raisi, ambaye kwa sasa ndiye alikuwa amekaimu kiti cha Raisi.
Akamsalimu na Makamu akamuuliza, “Ndiyo wewe Jona?”
“Ndio, mheshimiwa.”
“Hata kama usingeliomba kuonana na mimi, ningekuja kuteta nawe maana nahisi nina mengi ya kusikia toka kwako.”
Basi Jona akapatiwa nafasi ya kuteta pamoja na Makamu wa Raisi kwa faragha. Akamweleza yote toka herufi A mpaka Ze. Na kama haitoshi, akamkutanisha mheshimiwa huyo na wenzake: Miranda, Lee na Marwa. Nao kila mmoja kwa nafasi yake akaeleza yote yale ya kweli, na hata kuthibitisha wayasemayo kwa nyaraka na shahidi mbalimbali zilizokuwa mikononi.
Makamu wa Raisi akapigwa na butwaa na yale yote aliyoyasikia. Ilikuwa ni ngumu kuyakataa kwani hata matukio yaliyokuwa yanatukia ndani ya nchi pasipo na majibu ya uhakika, yaliungana mkono na maelezo na shahidi zilizotolewa.
Akaamuru wale wachimba madini, wakina Nyokaa, watiwe nguvuni upesi. Pia akatoa agizo wakina Jona waachiwe huru, lakini akamtaka Jona aonane naye faragha baada ya majuma mawili. Zaidi akawapatia kiasi fulani cha fedha kama motisha kwa kupigania nchi yao kwa dhati.
Siku hiyo Jona na wenzake wakafanya tafrija nyumbani kwa kujipongeza. Wakamwalika pia Glady na Miriam ambaye hakusita kuja upesi. Tafrija ikafana sana na kila mtu akafurahia isipokuwa kwa Sheng ambaye alikuwa mlemavu wa kudumu kwa kupooza.
Yeye alikuwa kwenye ‘wheelchair’ akitokwa na machozi. Hakuwa anaweza kusogeza mwili wake hata kidole. Alikuwa ni wa kufanyiwa kila kitu, na kwakuwa hakukuwa na mtu mwenye muda huo, wote walishakubaliana kuwa mwanaume huyo atatumwa kwenda kwao China kukutana na familia yake.
Kwa mujibu wa daktari hakuwa anaweza kudumu hai zaidi ya miezi miwili tangu sasa.
“Samahani sana, Sheng,” alisema Lee. “Sitaweza kuwa nawe tena kwa sasa maana nimepata familia mpya. Nasikitika maana utakuwa mpweke sana, na mikono yako iliyozoea kuua haiwezi tena kufanya kazi hiyo.
Ila nina furaha pia maana kwa sasa hatimaye utakuwa huru kuwa na familia yako. Hautakuwa na haja ya kujificha tena maana wote wameshamalizana wenyewe kwa wenyewe. Pengine kwa muda kidogo tutaiona dunia ikiwa tofauti.
Kwaheri Sheng.”
Lee aliposema hayo, akambusu Sheng kwenye paji la uso na kurudi tafrijani alipokutana na Glady na kukumbatiana kwa huba. Ila muda si mrefu, Jona akamwita na kumtaka faragha.
“Kuna lolote?” akauliza.
“Ndio, lipo,” Jona akajibu na kisha akatazama kushoto na kulia kuhakikisha kama wapo wenyewe. Akamnong’oneza jambo Lee, Lee akatabasamu. Ghafla, Lee akamshika mkono Jona na kumvutia tafrijani kisha akapaza sauti,
“Naomba tuskizane tafadhali!” muziki ukazimwa. Watu wote wakawatazama. “Jona hapa ana kitu cha kuwaambia…”
“Mimi?” Jona akatahamaki.
“Oooh basi nitakusaidia kusema …” Lee akapayuka. “Jona wants to marry Miranda!”
Watu wakalipuka kwa shangwe, ila Miranda akaziba mdomo wake akiwa ametoa macho kwa kutoamini. “Serious?” akauliza akitahamaki. Basi Jona akamtazama na kujikaza akimwambia, “Yes, serious!”
Mara Miriam akadondoka chini na kuzirai.
***
NASHUKURU SANA KWA KUWA NAMI MPAKA MWISHO. KWA WALE WATAKAOHITAJI KUWA PAMOJA KWENYE SIMULIZI YETU MPYA YA MWEZI WA TANO, ROHO YAKE INADAI, TUTUMIANE UJUMBE WHATSAPP KWA NAMBA 0685 758 123.
NAWAPENDA! MAMBO MAZURI HAYAKOMI KUJA.