DOKEZO Angalizo: Utapeli na wizi kwenye maduka ya Pharmacy/ biashara ya dawa za binadamu

DOKEZO Angalizo: Utapeli na wizi kwenye maduka ya Pharmacy/ biashara ya dawa za binadamu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

KikulachoChako

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2013
Posts
19,185
Reaction score
37,239
Habari za wakati huu ndugu zanguni.

Kama ilivyo ada na kawaida kuhabarishana habari mbali mbali zenye manufaa kwa ajili ya kuepushana na mambo yanayoonekana kutuathiri kwenye jamii na familia hii kwa ujumla wake.

Nimepata bahati mbaya ya kumuuguza mgonjwa hapa nyumbani kwangu mwenye ugonjwa wa muda mrefu anayelazimika kutumia dawa fulani kwa kila wiki.

Hali hiyo ilipelekea kuwa na bajeti ya kiasi cha Elfu 20 kila wiki ili kukidhi mahitaji ya mgonjwa wangu kimatibabu kwa maelekezo ya Daktari wake.

Nilikuwa navichukua kwenye pharmacy za mitaani wakinihakikishia kuwa dawa za namna hiyo ni adimu sana na hivyo ni ghali.

Walikuwa wananiuzia kila kidonge kiasi cha Elfu mbili.

Kuna siku ikatokezea pale wakawa hawana zile dawa, nikaona anamuita kijana wa boda boda ingawa walitaka kufanya siri lakini niliibahatika kunasa maongezi yao na kujua anapomuelekeza kwenda kuchukua.

Nikasikia jina la duka kubwa la pharmacy kubwa hapa Dar es salaam ambapo mimi mwenyewe nalijua lilipo.

Nikafanya maamuzi ya kwenda kununua huko nikamwambia basi siku nyingine nikamuona akawa mbishi kidogo lakini nikakomaa.

Kufika kule( huko kwenye hilo duka kubwa maarufu) nikakuta kule vile vidonge vinauzwa 6,000/= vyote kumi nilishtuka sana kutoka 20,000/= mpaka 6,000/= lakini ndio basi tena ikawa nimeshapigwa, yule binti mpaka leo ananionea haya.

NB: Nawasihi ndugu zanguni kama una uhitaji au matumizi ya dawa fulani wa muda mrefu jitahidi walau uzungukie maduka matano makubwa kujiridhisha maana hawa ndugu zetu wanaouza madawa wamepanga kuwa matajiri kupitia afya zetu na wapendwa wetu tunao wauguza.
 
Habari za wakati huu ndugu zanguni.........

Kama ilivyo ada na kawaida kuhabarishana habari mbali mbali zenye manufaa kwa ajili ya kuepushana na mambo yanayoonekana kutuathiri kwenye jamii na familia hii kwa ujumla wake.......

Nimepata bahati mbaya ya kumuuguza mgonjwa hapa nyumbani kwangu mwenye ugonjwa wa muda mrefu anayelazimika kutumia dawa fulani kwa kila wiki......

Hali hiyo ilipelekea kuwa na bajeti ya kiasi cha Elfu 20 kila wiki ili kukidhi mahitaji ya mgonjwa wangu kimatibabu kwa maelekezo ya Daktari wake.........

Nilikuwa navichukua kwenye pharmacy za mitaani wakinihakikishia kuwa dawa za namna hiyo ni adimu sana na hivyo ni ghali......

Walikuwa wananiuzia kila kidonge kiasi cha Elfu mbili.......

Kuna siku ikatokezea pale wakawa hawana zile dawa....nikaona anamuita kijana wa boda boda ingawa walitaka kufanya siri lakini niliibahatika kunasa maongezi yao na kujua anapomuelekeza kwenda kuchukua........

Nikasikia jina la duka kubwa la pharmacy kubwa hapa Dar es salaam.....ambapo mimi mwenyewe nalijua lilipo......

Nikafanya maamuzi ya kwenda kununua huko nikamwambia basi siku nyingine.....nikamuona akawa mbishi kidogo lakini nikakomaa......

Kufika kule( huko kwenye hilo duka kubwa maarufu)....nikakuta kule vile vidonge vinauzwa 6,000/= vyote kumi....nilishtuka sana....kutoka 20,000/= mpaka 6,000/= lakinj ndio basi tena ikawa nimeshapigwa.....yule binti mpaka leo ananionea haya......

NB;
Nawasihi ndugu zanguni kama una uhitaji au matumizi ya dawa fulani wa muda mrefu jitahidi walau uzungukie maduka matano makubwa kujiridhisha maana hawa ndugu zetu wanaouza madawa wamepanga kuwa matajiri kupitia afya zetu na wapendwa wetu tunao wauguza.......
Ni kweli kabisa mimi ilishanikuta kwenye kumuuguza ndugu pia, na ilikuwa ni dawa za moyo, nilibahatika kumpata jirani yangu anayefanya kusambaza dawa na masoko kwenye hizo pharmacy, dawa za laki na 20 nilinunua kwa elfu 60/80 hivi ni takribani miaka minne iliyopita nadhani.
 
Ni kweli kabisa mimi ilishanikuta kwenye kumuuguza ndugu pia, na ilikuwa ni dawa za moyo, nilibahatika kumpata jirani yangu anayefanya kusambaza dawa na masoko kwenye hizo pharmacy, dawa za laki na 20 nilinunua kwa elfu 60/80 hivi ni takribani miaka minne iliyopita nadhani.
Dah!!
Pole sana ndugu.....

Watanzania tunaumizana sana....
 
Hio ipo kwenye biashara zote. Hawa wauzaji hawafikirii mbali. Angesema 8,000 wala usingejali ungeona 2,000 yake ya usumbufu ila wana tamaa sana. Matokeo yake anapoteza mteja.
Anapoteza mteja na wakati mwingine kujenga uadui..... imagine unamuumiza mtu unayemfahamu karibia eflu 14 yote kwa zaidi ya miezi mitatu......
 
Uchinga haupo kwenye mitumba tu ndugu zangu hata kwenye dawa,mfano ukiwa kinondoni studio nguo zilizotundikwa kwenye boutique za mtumba unaambiwa 30 ila nguo hiyohiyo ukiikuta karume 2500 unabeba hata famacy nazo kuna sehemu huwa wanachukulia kwa jumla lakini wanakuja kuuza kama duka la dawa,tofauti yao na duka la dawa wao wanaleseni ya kuuza dawa zaidi ya zile mhimu
 
Uchinga haupo kwenye mitumba tu ndugu zangu hata kwenye dawa,mfano ukiwa kinondoni studio nguo zilizotundikwa kwenye boutique za mtumba unaambiwa 30 ila nguo hiyohiyo ukiikuta karume 2500 unabeba hata famacy nazo kuna sehemu huwa wanachukulia kwa jumla lakini wanakuja kuuza kama duka la dawa,tofauti yao na duka la dawa wao wanaleseni ya kuuza dawa zaidi ya zile mhimu
Kabisa mkuu. Wala siyo jambo la kushangaza. Nmemuambia kuwa bei ya dawa kwenye duka la dawa ni tofauti na phamacy..kwa mfano mtaani kwangu duka la dawa wanauza drip la maji kwa sh elf 5...lakin phamacy wao wanauza elf 1.

Ni mambo ya kawaida tu kwenye biashara nyingi
 
Mimi pia niliwahi kuuziwa kidonge kimoja elfu 2, ilikuwa dose ya mwezi mmoja. Nikasema ngoja nowe nachukua vya wiki wiki. Baade nikapata wazo la kuwasiliana na mdogo wangu yuko kwenye field hii ya afya. Akanielekeza sehem ambapo nilipata vile vidonge kwa 350 kwa kila kimoja.
 
Habari za wakati huu ndugu zanguni.........

Kama ilivyo ada na kawaida kuhabarishana habari mbali mbali zenye manufaa kwa ajili ya kuepushana na mambo yanayoonekana kutuathiri kwenye jamii na familia hii kwa ujumla wake.......

Nimepata bahati mbaya ya kumuuguza mgonjwa hapa nyumbani kwangu mwenye ugonjwa wa muda mrefu anayelazimika kutumia dawa fulani kwa kila wiki......

Hali hiyo ilipelekea kuwa na bajeti ya kiasi cha Elfu 20 kila wiki ili kukidhi mahitaji ya mgonjwa wangu kimatibabu kwa maelekezo ya Daktari wake.........

Nilikuwa navichukua kwenye pharmacy za mitaani wakinihakikishia kuwa dawa za namna hiyo ni adimu sana na hivyo ni ghali......

Walikuwa wananiuzia kila kidonge kiasi cha Elfu mbili.......

Kuna siku ikatokezea pale wakawa hawana zile dawa....nikaona anamuita kijana wa boda boda ingawa walitaka kufanya siri lakini niliibahatika kunasa maongezi yao na kujua anapomuelekeza kwenda kuchukua........

Nikasikia jina la duka kubwa la pharmacy kubwa hapa Dar es salaam.....ambapo mimi mwenyewe nalijua lilipo......

Nikafanya maamuzi ya kwenda kununua huko nikamwambia basi siku nyingine.....nikamuona akawa mbishi kidogo lakini nikakomaa......

Kufika kule( huko kwenye hilo duka kubwa maarufu)....nikakuta kule vile vidonge vinauzwa 6,000/= vyote kumi....nilishtuka sana....kutoka 20,000/= mpaka 6,000/= lakinj ndio basi tena ikawa nimeshapigwa.....yule binti mpaka leo ananionea haya......

NB;
Nawasihi ndugu zanguni kama una uhitaji au matumizi ya dawa fulani wa muda mrefu jitahidi walau uzungukie maduka matano makubwa kujiridhisha maana hawa ndugu zetu wanaouza madawa wamepanga kuwa matajiri kupitia afya zetu na wapendwa wetu tunao wauguza.......
Usiwasahau na hawa wenye butcheries, hizi mizani digital wanaibia sana wateja. Mfano nyama kilo ni 10,000 yeye kwenye mzani anaandika 12,000 so utaambulia nyama pungufu maana mzani ukifika kwa 10,000 anakupa nyama yako. Muweni makini.
 
Back
Top Bottom