KikulachoChako
JF-Expert Member
- Jul 21, 2013
- 19,185
- 37,239
- Thread starter
- #41
Yaani mtu ananunua dawa 1,000/= anakwenda kuuza 10,000/= hiyo nayo unataka CCM ilaumiwe....??Kama ambavyo ccm hawana huruma na wauza madawa nao hivyo hivyo.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Yaani mtu ananunua dawa 1,000/= anakwenda kuuza 10,000/= hiyo nayo unataka CCM ilaumiwe....??Kama ambavyo ccm hawana huruma na wauza madawa nao hivyo hivyo.
Mfano wako hauna Uhalisia....kutoka2500 hadi 30000?Uchinga haupo kwenye mitumba tu ndugu zangu hata kwenye dawa,mfano ukiwa kinondoni studio nguo zilizotundikwa kwenye boutique za mtumba unaambiwa 30 ila nguo hiyohiyo ukiikuta karume 2500 unabeba hata famacy nazo kuna sehemu huwa wanachukulia kwa jumla lakini wanakuja kuuza kama duka la dawa,tofauti yao na duka la dawa wao wanaleseni ya kuuza dawa zaidi ya zile mhimu
Ndugu.....Kabisa Sasa hivi Kuna upandaji holela wa Dawa
Mfano Kuna Dawa moja Wanaita Erythromycin Nilikuwa nikinunua 10 kwa Tsh 1000
Ajabu Ndani ya muda mfupi Imekuwa 2000
Sasa Inapandaje Ghafla kwa ×2
Sijui nchi hii tunakwemda wapi
Mtu hajachangia hata mia na anafisadi hadi mabilioni unataka kulaum aliyechukua elfu 10?Yaani mtu ananunua dawa 1,000/= anakwenda kuuza 10,000/= hiyo nayo unataka CCM ilaumiwe....??
Kwa niliyoyaona au kunitokea yanawezekana ndugu.....hawa jamaa hawana haya wala soni usoni mwaoMfano wako hauna Uhalisia....kutoka2500 hadi 30000?
Kwa hiyo kwako ndugu ni sawa tu...??Mtu hajachangia hata mia na anafisadi hadi mabilioni unataka kulaum aliyechukua elfu 10?
Ndugu yangu tunakubali kweli haya mambo yameshaingia kwenye DNA zetu lakini huku kwenye afya ndio kunatia mashaka na hofu zaidiKupigwa kupo sana na muasisi wa upigaji katika taifa hili anajulikana. Ni mboga mboga fc na kansa hio imesambaa kila kona ya nchi.
Uhalisia wangu kama upo dar basi tembelea hizo sehemu mbili nilizozitaja kwa hitaji moja hilo hilo harafu njoo na mrejesho.Mfano wako hauna Uhalisia....kutoka2500 hadi 30000?
Tunajua ni huria ndugu na ndio maana nikaja kuwastua ndugu zangu ili tuangalie penye unafuu maana kuna watu tamaa zao zimepitilizaHiiii ni dunia ya kibepariiiiii,,,,,,
Na ni biashara huria
Na huko hali hii ipo sana, ikishamiri ndio tutaangamia.Ndugu yangu tunakubali kweli haya mambo yameshaingia kwenye DNA zetu lakini huku kwenye afya ndio kunatia mashaka na hofu zaidi
Huyu jamaa kwa namna anavyotetea nina mashaka atakuwa mmiliki wa hizi pharmacy za mtaaniUhalisia wangu kama upo dar basi tembelea hizo sehemu mbili nilizozitaja kwa hitaji moja hilo hilo harafu njoo na mrejesho.
NduguNa huko hali hii ipo sana, ikishamiri ndio tutaangamia.
Mimi kaka yangu alikufa 2001 kwa kukosekana buku 5 ya sindano ya pumu. Zahanati ya mtaani kabisa ambapo tunajulikana ila mtu na roho yake mbaya alishindwa kufanya tendo la kibinadamu na kupelekea mapafu kubana hatimaye kukata moto. Ni story ambayo haiwez futika akilini mwangu.Ndugu
Tumeshaangamia kwani wapo wengi wanaojifia kwa kukatishwa tamaa na bei za kubumba Hali ya kuwa ni bei za kitapeli
Ni kawaida hiyo mkuu mbona. Wale ni machinga hivyo bei watakupga mara kadhaa. Hii ni kwa biashara zote si duka la dawa tu.Mimi pia niliwahi kuuziwa kidonge kimoja elfu 2, ilikuwa dose ya mwezi mmoja. Nikasema ngoja nowe nachukua vya wiki wiki. Baade nikapata wazo la kuwasiliana na mdogo wangu yuko kwenye field hii ya afya. Akanielekeza sehem ambapo nilipata vile vidonge kwa 350 kwa kila kimoja.
Ni kweli kabisa, inashangaza sana sikuhizi Wauza madawa mpaka wanajitangaza sana kupitia WhatsApp, Tiktok, Instagram na kwingineko kama wauza nguo na bidhaa zingineHabari za wakati huu ndugu zanguni.........
Kama ilivyo ada na kawaida kuhabarishana habari mbali mbali zenye manufaa kwa ajili ya kuepushana na mambo yanayoonekana kutuathiri kwenye jamii na familia hii kwa ujumla wake.......
Nimepata bahati mbaya ya kumuuguza mgonjwa hapa nyumbani kwangu mwenye ugonjwa wa muda mrefu anayelazimika kutumia dawa fulani kwa kila wiki......
Hali hiyo ilipelekea kuwa na bajeti ya kiasi cha Elfu 20 kila wiki ili kukidhi mahitaji ya mgonjwa wangu kimatibabu kwa maelekezo ya Daktari wake.........
Nilikuwa navichukua kwenye pharmacy za mitaani wakinihakikishia kuwa dawa za namna hiyo ni adimu sana na hivyo ni ghali......
Walikuwa wananiuzia kila kidonge kiasi cha Elfu mbili.......
Kuna siku ikatokezea pale wakawa hawana zile dawa....nikaona anamuita kijana wa boda boda ingawa walitaka kufanya siri lakini niliibahatika kunasa maongezi yao na kujua anapomuelekeza kwenda kuchukua........
Nikasikia jina la duka kubwa la pharmacy kubwa hapa Dar es salaam.....ambapo mimi mwenyewe nalijua lilipo......
Nikafanya maamuzi ya kwenda kununua huko nikamwambia basi siku nyingine.....nikamuona akawa mbishi kidogo lakini nikakomaa......
Kufika kule( huko kwenye hilo duka kubwa maarufu)....nikakuta kule vile vidonge vinauzwa 6,000/= vyote kumi....nilishtuka sana....kutoka 20,000/= mpaka 6,000/= lakinj ndio basi tena ikawa nimeshapigwa.....yule binti mpaka leo ananionea haya......
NB;
Nawasihi ndugu zanguni kama una uhitaji au matumizi ya dawa fulani wa muda mrefu jitahidi walau uzungukie maduka matano makubwa kujiridhisha maana hawa ndugu zetu wanaouza madawa wamepanga kuwa matajiri kupitia afya zetu na wapendwa wetu tunao wauguza.......
Utapeli na wizi ndio wamueweka mbele ndio maana wanajitangazaNi kweli kabisa, inashangaza sana sikuhizi Wauza madawa mpaka wanajitangaza sana kupitia WhatsApp, Tiktok, Instagram na kwingineko kama wauza nguo na bidhaa zingine
Pole sana ndugu yangu......Mimi kaka yangu alikufa 2001 kwa kukosekana buku 5 ya sindano ya pumu. Zahanati ya mtaani kabisa ambapo tunajulikana ila mtu na roho yake mbaya alishindwa kufanya tendo la kibinadamu na kupelekea mapafu kubana hatimaye kukata moto. Ni story ambayo haiwez futika akilini mwangu.