Angekuwa Magufuli kesho tungeamka na Breaking News ya Waziri wa michezo kutumbuliwa

Abby Newton

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2017
Posts
1,252
Reaction score
2,253
Asilani abadani Magufuli asingeweza kuvumilia huu upuuzi uliotokea leo uwanja wa Mkapa. Kesho asubuhi mapemaaa! kuna mtu angetumbuliwa. Huu si uzembe tu bali dharau iliyopindukia kwa familia ya wanamichezo.

Kiungwana tu Waziri wa michezo atoke hadharani kutuomba msamaha. Na namshauri Mh. Rais nafasi km hii achague watu wa michezo kweli kweli sio kumteua mbumbumbu asiyejua sheria na kanuni za michezo. Ona sasa jinsi soka letu lilivyodhalilika,Hii haivumiliki hata kidogo!
 
Mama can do it either! Nauona utenguzi wake wa kwanza kwa ngazi hii...
 

 
Mama yuko anagawa benzi huko
πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Vipi kama kamtuma yeye ...wewe kwa akili yako ya kawaida unadhani Waziri anapata wapi nguvu ya kusogeza mechi mbele...Na baadooo nchi imeshachukuliwa na mdebwedo ...watu wa Pwani...mbona tutanyooka mwaka huu...Kwani hiyo mechi haiwezi kusogezwa mbele shehe ahaa..Mimi ni Rais Mwanamke
 
Kuna mtu ameshauri Serikali vibaya kimazoea!,bila kujali maslahi ya wapenda soka.
Raia wanapaswa kuwa huru kwenda watakapo,kusikiliza watakacho,kuona watakacho ili mradi hawavunji sheria.

Serikali imezoea kupora uhuru wa raia kuamua wakitakacho,sasa leo maelekezo ya Serikali kwenda chama cha mpira imeleta madhara(Mechi imeahirishwa huku washabiki wakipata hasara ya fedha waliotoa baada ya mechi kuvunjika).
Watendaji,wamezoea kutoa ushauri wa kujipendekeza bila kufanya tathimini yenye kujali maslahi ya wengi.
BORA RAIS AFANYE MABADILIKO ZAIDI KWA WATENDAJI,KUNA MAMBO WANAYOYAFANYA HAYAENDANI NA MTAZAMO WA SERIKALI YA AWAMU YA 6.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…