Angekuwa ndio Magufuli kapokea report ya CAG leo, naamini angefanya maamuzi haya ya kishujaa...

ATCL Nako Hasara Ya Billions 60 Angesemaje
 
Mkuchika mara ya mwisho kumuona lini au unaongea tu.na kuhusu eitisielo angejitumbua sio
 
Maamuzi bila uchunguzi sio wa uhakika ni uonevu
Umemjibu vyema kabisa.kaa pembeni pisha uchunguzi...yawezekana alikuwa antekeleza amri za wanene..nitampa mama credit kwa jinsi atakavyoshughulikia ripoti ya uchunguzi...
 
Kuna watu wengine nimegundua hawajui historian za watu,Kakoko na Magufuli ni marafiki na MTU pekee hapa Tanzania alikuwa na uwezo wa kumgomea Magufuli ni Kakoko.
Je Charles kitwanga si alikuepo ni best yake na akatenguliwa na je makonda ilikuwaje
 
🤣🤣
 
Hio ripoti ilishakua tayari toka magufuli akiwepo kilichokua kimebaki ni kui submit tu kwa Rais ndio mzee akaanza kuumwa.sio kwamba ni vitu vya juzi baada ya magufuli kuondoka.
Reports zote hupitiwa na Rais kabla ya kuwa public. Magufuli asingeruhusu udhaifu wa ATCL na bandari kuanikwa hadharani kama alivofanya samia suluhu. Kwa sababu tumeona akifumbia macho hayo yote yaliyohojiwa na CAG
 
Angefanya maamuzi gani ya ATC kwa mfano wa kupata hasara miaka 5 mfululizo?
 
Umesema "Magufuli angekuwa hai" acha kuishi kwenye ndoto ndugu yangu ! Kwani unadhani ile tumbua tumbua ya Magufuli imeleta tija kiasi gani? Na hao wanajeshi unaosema maeneo waliyowekwa yameonyesha ufanisi gani so far?
Kumbuka pia kwamba kama hiyo report ingepelekwa kwa Magufuli isingesomeka kama ilivyokuwa leo

Sent from my vivo 1904 using JamiiForums mobile app
 
Maamuzi bila uchunguzi sio wa uhakika ni uonevu
Ripoti ya CAG siyo uchunguzi? Hata kama wezi ni watu wengine wa ngazi za chini sana, uwajibikaji hufanyika juu kwa walioshindwa kuzuia wizi huo!
 

Nadhani na wewe unaongeza chumvi kwenye post hii. Ripoti ya CAG huwa haiandikwi ndani ya siku moja kiasi kuwa imeandikwa jana tu baada ya Magufuli kufa; hii imeakuwa inaandaliwa kwa muda mrefu sana wakati Magufuli angali hai.

Kuhusu Tumbua tumbua huelta nidhamu sana kwenye utendaji; ni lazi mazingira ya tumbuatuma yaendelee ili kuendeleza nidhamu kwenye utendaji wa taasisis za umma.
 
Kwan kumteua ndo kungemzuia kumtengeua? Kwani Kichere alimtumbua mara ngap na akampa nafasi tena? Lugola alimteua mwenyewe na akamtengua, Mwigulu pia.. tuache unafiki Magu hakuwa na masiala na watu wazembe na wabadhilifu...!! Kuna hotuba moja akiwa anaongea hapohapo TPA aliwah kusema unaweza ukamtoa mtu huko akiwa safi lakini akifika hapa akalaa wiki mpaka mwezi tayar ashakuwa mwizi... sijui kuna mdudu gani hapa Bandarini.... kwaiyo Magu angemla kichwa huyo jamaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…