Anguko la Ndugai: Somo la Katiba, viongozi na nchi

Anguko la Ndugai: Somo la Katiba, viongozi na nchi

Ni kosa kubwa sana! Katiba ni makubaliano na mwongozo wa jamii. Kwamba , kuna taratibu zinapaswa kufuatwa ili tuishi kama jamii. Katiba imetoa nafasi 'kukiukwa' katika msingi ya kikatiba. Mfano, Rais akapewa haki ya kumsamehe muuaji aliyethibitishwa na mahakama
Rais kapewa haki ya kuingiza nchi vitani kwanza lakini pia kuna utaratibu wa kufanya hivyo
Katiba imempa haki Rais juu ya umiliki wa ardhi ya MTU anaweza ku revoke hati ya mali ya mtu

Kwahiyo mfumo mzima wa katiba unatoa taratibu ikiwemo 'ukiukwaji wake'' lakini siyo open season kwamba anaibuka mwendawazimu anakiuka katiba tunajenga uhalali.
Uhalali wa ukiakwaji wa katiba upo ndani ya katiba siyo

Hata Simba na Tembo wanaishi kama jamii, tofauti baina yao na sisi ni weledi! Sisi tunaishi kwa taratibu ili kuepuka 'rule of the jungle'' . Kutofuata taratibu tulizojipangia kwa njia ya katiba ni kufuata mfumo wa rule of the jungle ambao 'tumeujaribu'' hivi karibuni na tunajua matokeo yake.

Siyo tuhuma hewa, tuhuma zilikuwepo na utawala wa JPM unajua hilo. Kilichotakiwa ni kueleza zipo wapi pesa za walipa kodi, hadi anaingia kaburini hakuwahi kujibu. Wasaidizi wake akiwemo mtoto wa Dada yake hakuna anayesema 'ni tuhuma za uongo'' . Kwavile hakuna anayekanusha basi aliyesema anabaki kuwa mkweli, hazijulikani zilipo 1.5T, CAG Assad
Ni sawa na anachosema Zitto hakuna maelezo ya 70B zilizokwenda Mwanza! CAG Kichere

Kumstaafisha kwa lazima ilikuwa kuondoa ''udhia'' ili asije ibua tena madudu mengine
Kumuondoa hakujibu hoja wapi zilipo 1.5T . Kabla ya jibu wapo wanaouliza 70 Bilioni zilikuwa za nini. Chuki haikuwahi kujibu tuhuma ndio maana siku za karibuni rekodi ya Magufuli inawekwa wazi na wapo wasiotaka kama wewe kwa kujua yapo mengi katika rekodi!!!

Kuna aina mbili za usomaji, kusoma maandiko kwasababu tunaziona herufi na kusoma maandiko kwa kuyaelewa. Nina shaka sijui upo wapi katika makundi hayo

Katiba haielengi kueleza usahihi wa taarifa za CAG. Katiba inalenga kuzuia upuuzi kama ule wa kumstaafisha CAG ili kuendelea kufanya watakavyo.
Tuliishi kwa mazoea ya viongozi waliotangulia wakiogopa taratibu tu kwa uadilifu
Tumejifunza kuwa kila 'kiingacho si dhahabu' . Tuipitie katiba ili kuzuia ubazazi usijitokeze tena

Ndio maana nasema maoni ya watu hayawezi kuwa chuki na siwezi kukubaliana nawe eti nisiwe na chuki. Kwani shutuma nizitoa dhidi ya Magufuli ni zipi? Mbona huelezi ili tuweke ushahidi!
Siwezi kuweka ushahidi bila tuhuma, weka tuhuma mezani kwanza !

Rekodi ya Magufuli ndicho kitu pekee kitakachosaidia legacy yake.

Watetezi wake wajikite kuieleza rekodi yake, wasiokubaliana naye wanajenga hoja zenye mantiki, zijibiwe kwa mantiki

Hakuna mtu mwenye mamlaka ya ustawi wa umma. Ustawi wa Umma ni jukumu la Umma na ni wajibu wa Umma na haki ya Umma. Kilichotokea kwa watu kujivika joho la Tanzania ulikuwa uzuzu 'imbecile'' . Tukatae uzuzu huo na hapa ndipo tunahitaji rekodi .
Rekodi ya kudhani Tanzania ni mtu na rasilimali za nchi za kikundi ni mbaya ndiyo inajadiliwa!

Kudhani ustawi wa jamii unahitaji kuigawa jamii katika misingi ya udini, ukabila na ukanda ni jambo la kulaaniwa na wenye akili timamu. Hilo haliondoi haki ya ' collective imbecilisation'

Kwamba Marehemu anasemwa kwa flyover, JNHP , SGR tu! hatusemi rekodi nyingine kwa kisingizo cha Marehemu hasemwi ili kuficha lundo la uchafu na uvundo linalonuka
Uvundo haupuuliziwi ubani unaondolewa na huwezi kuuondoa kama husemi upo wapi

Kuna watu wamedhulumiwa wanadai haki zao japo kuombwa radhi. Kuna watu hatujui wapo wapi, hakuna wa kuwasema isipokuwa tunaamini marehemu hasemwi.


Naam ni jukwaa la wote na tuwaache wenye nyongo zao wateme.
Wanotetea nyongo nao wana haki lakini tusijifiche chini ya kapeti linalovunda kwa kisingizio cha Marehemu hasemwi! Ni marehemu gani huyo ? Nyerere ? Mkapa? au Magufuli?
Kwanini Magufuli? nini kinafichwa !
1. Kukiuka Katiba si sawa na Rule of Jungle. Hakuna Katiba Kamilifu, zote zina mipaka ya muda na mazingira. Hilo linahalalisha Ukiukwaji wake pale inaposhindwa Kulinda Maslahi ya Umma kutoka na Udhaifu wake.

2. Wewe lete Ushahidi kwamba 1.5t zilikuwepo kweli, na si kwamba ni Tuhuma hewa kama uwezekano mwingine. TUPE USHAHIDI HAPA.

Kwamba "Kumstafisha ni kuondoa udhia, asije kusema madudu mengine."
Nadhani umekuwa mpiga ramli sasa. MATAMANIO yako zao la Hisia zako hayatoshi kutetea hoja yako. Hata Mimi naweza sema kama hizo, mfano, Assad alinunuliwa kumchafua Magufuli, kwa busara Magufuli alimstaafisha bila kumfunga. (huo ni mfano sawa na hoja yako)

3. Tuhuma zisizo na Ushahidi, Ni Chuki. Ulitaja kwa kuunga mkono tuhuma za Udini, Ukanda, Ukabila, Ufisadi, nk... Je, ulileta ushahidi?

4. Acha kujidanganya, Ustawi wa Umma u mikononi mwa kila RAIA kulingana na nafasi yake. Nafasi ya Rais haiwezi kuwa sawa na mjumbe wa nyumba kumi. Hekima ni kutambua na Kuheshimu wajibu wa kila RAIA kulingana na nafasi yake.
Uzuzu ni kujaribu kukataa nafasi yako na kujilinganisha na wengine. Na hicho ndicho cha kupigwa vita. (Kwa bahati mbaya wasomi Wetu, wastaafu, WanaCCM, Wapinzani, Watu wa Dini, nk...mmechagua upande wa kupigwa vita) Magufuli ametufundisha kutowaonea aibu tena. Tutawapiga Vita.

5. Humu ndani hakuna anayekupangia cha kusema juu ya marehemu. Hivyo usiirudierudie manung'uniko yako. TEMA NYONGO NDUGU. Nasi tupo tutakusikiliza na kujibia zile utakazopotosha au kuhitaji hoja za upande mwingine. Usilielie.

6. "Kwanini Magufuli?"
JIBU: Ni Mtu wenye Matunda. Na werevu ni wachache sana kuliko wapumbavu!


Hotep!
 
6. "Kwanini Magufuli?"
JIBU: Ni Mtu wenye Matunda. Na werevu ni wachache sana kuliko wapumbavu!


Hotep!
Hoja zako 1 hadi 6 hakuna hata moja inayotetea yale anayotuhumiwa nayo magufuli
Kama JPM ni mti wenye matunda basi uachwe watu wapopoe! kitendo cha kutuambia eti ni marehemu asisemwe ni kutaka kuficha rekodi yake katika haya
Utu
Ubinadamu
Haki na ustawi
Demokrasia
Ubadhirifu unajitokeza. Wewe unaweza kutueleza Mayanga construction!
Rekodi mbaya ya mahusiano ya kitaifa na kimataifa
Kujenga mgawanyiko katika jamii kwa ukanda udini , ukabila. Kasema Rais SSH
 
Hoja zako 1 hadi 6 hakuna hata moja inayotetea yale anayotuhumiwa nayo magufuli
Kama JPM ni mti wenye matunda basi uachwe watu wapopoe! kitendo cha kutuambia eti ni marehemu asisemwe ni kutaka kuficha rekodi yake katika haya
Utu
Ubinadamu
Haki na ustawi
Demokrasia
Ubadhirifu unajitokeza. Wewe unaweza kutueleza Mayanga construction!
Rekodi mbaya ya mahusiano ya kitaifa na kimataifa
Kujenga mgawanyiko katika jamii kwa ukanda udini , ukabila. Kasema Rais SSH
Chutama, ulinde walau Utu uzima wako.

Kauli za "Si Kasema Fulani" ni za kitotototo, zinakutia aibu. Na hizo ndizo unazodai facts eti. Pole sana.

Yes, upopoeni mpendavyo. Kama Rais anarusha mawe ni nani wa kuzuiliwa kurusha mawe? UPOPOENI TU, RUKSA.

Kama hoja zako ni za Fulani Kasema basi usitupotezee muda kuanzisha Shutuma nyingine. Umeshindwa la udini, ukabila, 1.5t na ukanda, sasa unaleta la Mayanga. Usitufanye watoto.

*UTU:
Usisemee Kitu usichokijua wala usichopenda kukitafakari. UTU haupikiki chungu kimoja na huo upuuzi ulioitaja wa Haki na Demokrasia. UTU si zao la Mihemko ya watu.

Kuwa kifupi huwa natilia shaka uwezo wa kufikiri kila mtu anayejaribu kutetea Demokrasia na Haki za Binadamu. Mbaya zaidi ninapoona anajivunia uzamivu wake katika hivyo Viini Macho. Pole sana.
 
3. Tuhuma zisizo na Ushahidi, Ni Chuki. Ulitaja kwa kuunga mkono tuhuma za Udini, Ukanda, Ukabila, Ufisadi, nk... Je, ulileta ushahidi?
JPM ni kiongozi aliyewahi kutamka hadharani 'Kanda ya kasakazini itusubiri''
Kwamba Rais wa nchi anaeleza umma kuhusu kanda moja ya nchi anayotawala.

Rais JPM alikuwa na mamlaka ya kuinyima kanda hiyo anachodhani anataka bila kutangaza
Kutangaza ililenga kujenga chuki kati ya wananchi wa kanda nyingine na ile ya kaskazini

Wakati huo huo Magufuli
1. Kukiuka Katiba si sawa na Rule of Jungle. Hakuna Katiba Kamilifu, zote zina mipaka ya muda na mazingira. Hilo linahalalisha Ukiukwaji wake pale inaposhindwa Kulinda Maslahi ya Umma kutoka na Udhaifu wake.
Well said, Magufuli kama aliona hilo hakutaka kulirekebisha. Watu wanaodai katiba mpya hoja yao ni hiyo uliyoitoa, kwamba, katiba iliyopo inashindwa kulinda masilahi ya Umma kutokana na udhaifu wake. Pamoja na udhaifu wa katiba ya 1977 JPM haikuiheshimu hata pale ilipokuwa takwa.
2. Wewe lete Ushahidi kwamba 1.5t zilikuwepo kweli, na si kwamba ni Tuhuma hewa kama uwezekano mwingine. TUPE USHAHIDI HAPA.
Hakuna mtu akiwemo JPM aliyewahi kukataa uwepo wake. Maana yake ni moja uwepo wake upo kama alivyosema CAG lakini haijulikani upo wapi. Alichokataa JPM ni kuibwa!
Kwahiyo dhima ya ushahidi si yangu ni ya wanaotuhumiwa
Kwamba "Kumstafisha ni kuondoa udhia, asije kusema madudu mengine."
Assad alinunuliwa kumchafua Magufuli, kwa busara Magufuli alimstaafisha bila kumfunga. (huo ni mfano sawa na hoja yako)
Alimstaafisha kwasababu hakuweza kufanya jingine lolote lakini huenda alifikiri hata kumfunga. Kuna wakati CAG alielezwa kuwa katika wakati usio wa kawaida, hilo linabaki kitendawili.
Ikiwa Assad alitumika kumchafua ni jukumu la mhusika kuonyesha hilo si wewe kuja na nadharia
Wananchi wanauliza 1.5T ipo wapi? Wanataka jibu wala hawasemi imeibwa !
3. Tuhuma zisizo na Ushahidi, Ni Chuki. Ulitaja kwa kuunga mkono tuhuma za Udini, Ukanda, Ukabila, Ufisadi, nk... Je, ulileta ushahidi?
OK tuangalie tuhuma

1. Akiwa Iringa, na imesemwa Bungeni na hadi leo kuna magazeti yana nukuu yake, JPM alisema ''Watu wa kasakazini watusubiri''. Kwamba anajenga chuki ya eneo moja la nchi dhidi ya jingine. Kulikuwa na sababu yoyote?

2. Ubaguzi: JPM alisema hatapeleka maendeleo walipochagua Wapinzani
Kwamba anakusanya kodi za Wananchi halafu anaamua matumizi kwa njia ya ubaguzi
Hili nalo unalionaje mheshimiwa!

3. Ukanda: Ni neno wakati wa utawala wa JPM na watu husema ni zamu ya kanda..
Hatujawahi kuzungumzia ukanda kama wakati wa wa JPM , teuzi zake tu zinatueleza
Ukisikia wanaosema ''gang' kuna hoja ! Unakumbuka tumbua majipu? Ilianzaje na iliishaje?

Kwanini Tumbua majipu ilikwenda kasi mwanzoni mwa utawala wake kisha kufa kabisa?

3. Udini : Aliyendekeza udini akipita maeneo ya ibada kueleza siasa.
Kuna mtu aliweka ushahidi wa teuzi zake na hilo halikupingwa na yoyote.

Aliifanya nchi kuwa na'' imani'' na kuwatenga wasioamini, wasio na imani, dini nyingine zilizopo nchini. Abadilisha salamu na kuzifanya katika misingi ya dini kitu kilichochoea udini.
Salamu za Waislam na Wakristi akitenga makundi mengine ya jamii

Akatumia imani yake kupambana na COVID-19 akilazimisha Taifa kuamini, kazi isiyo ya Rais

Akawanyima wenye dini , wasio na dini au imani fursa ya ''kupambana' na COVID kwa kukataa chanjo na kulazamisha watu watumie majani na MAOMBI. Kazi ya Rais si kusimamia IMANI

3.Ufisadi: Matumizi ya pesa nje ya bajeti!
Ndege ziliidhinishwa kununuliwa bajeti gani kwa cash?
Kwanini kuna mafungu yalipitishiwa Ikulu?

Pesa za EU kwa ajili ya COVID-19 hazikutmika ilipokusudiwa!

Zitto wa ACT kauliza Bilioni 70 zilizokuwa zinakwenda Mwanza bila maelezo ni za nini?

Uwanja wa Chato ulikuwa katika bajeti ya mwaka gani na unaletea nchi faida gani?

Mayanga construction ni kampuni ya nani?

Tanroad wanajenga vipi viwanda vya sukari?

Labda tuangalie rekodi ya ripoti ya CAG Kichere kwa undani
 
Chutama, ulinde walau Utu uzima wako.
Utu uzima haujengwi kwa kuchutama! unajengwa kwa ukweli.
Sitachutama nitakuwa sawa na wale wanaosema '' Marehemu asisemwe' ili kuficha rekodi

Sema kadri utakavyojaliwa!
Kama hoja zako ni za Fulani Kasema basi usitupotezee muda kuanzisha Shutuma nyingine. Umeshindwa la udini, ukabila, 1.5t na ukanda, sasa unaleta la Mayanga. Usitufanye watoto.
Nimeeleza! zaidi ya hapo ushahidi kautoa Rais SSH siku ya maadhimisho ya Mwl Nyerere
Rais SSH ni msaidizi namba 1 wa JPM, sasa anaposema '' Ukabila, udini na ukanda tumerudi nyuma'' kama hiyo si fact nani msaidizi mwingine umjuaye?
*UTU:
Usisemee Kitu usichokijua wala usichopenda kukitafakari. UTU haupikiki chungu kimoja na huo upuuzi ulioitaja wa Haki na Demokrasia. UTU si zao la Mihemko ya watu.
Rekodi ya JPM haitetewi na flyover si kumtendea haki

Iangaliwe rekodi kwa ujumla katika Utu, ubinadamu , haki , demokrasia, uchumi , mahusiano na mataifa n.k.
Kuwa kifupi huwa natilia shaka uwezo wa kufikiri kila mtu anayejaribu kutetea Demokrasia na Haki za Binadamu. Mbaya zaidi ninapoona anajivunia uzamivu wake katika hivyo Viini Macho. Pole sana.
Una haki hiyo , haki usiyo nayo ni ya kudhani kuwa mawazo yako ni facts

Mheshimiwa huu ni mjadala, punguza jazba! pata funda la maji. Ukweli ni kama sindano itaingia tu hata kama huuitaki, utaipenda kwasababu ni dawa!
 
JPM ni kiongozi aliyewahi kutamka hadharani 'Kanda ya kasakazini itusubiri''
Kwamba Rais wa nchi anaeleza umma kuhusu kanda moja ya nchi anayotawala.

Rais JPM alikuwa na mamlaka ya kuinyima kanda hiyo anachodhani anataka bila kutangaza
Kutangaza ililenga kujenga chuki kati ya wananchi wa kanda nyingine na ile ya kaskazini

Wakati huo huo Magufuli

Well said, Magufuli kama aliona hilo hakutaka kulirekebisha. Watu wanaodai katiba mpya hoja yao ni hiyo uliyoitoa, kwamba, katiba iliyopo inashindwa kulinda masilahi ya Umma kutokana na udhaifu wake. Pamoja na udhaifu wa katiba ya 1977 JPM haikuiheshimu hata pale ilipokuwa takwa.

Hakuna mtu akiwemo JPM aliyewahi kukataa uwepo wake. Maana yake ni moja uwepo wake upo kama alivyosema CAG lakini haijulikani upo wapi. Alichokataa JPM ni kuibwa!
Kwahiyo dhima ya ushahidi si yangu ni ya wanaotuhumiwa

Alimstaafisha kwasababu hakuweza kufanya jingine lolote lakini huenda alifikiri hata kumfunga. Kuna wakati CAG alielezwa kuwa katika wakati usio wa kawaida, hilo linabaki kitendawili.
Ikiwa Assad alitumika kumchafua ni jukumu la mhusika kuonyesha hilo si wewe kuja na nadharia
Wananchi wanauliza 1.5T ipo wapi? Wanataka jibu wala hawasemi imeibwa !

OK tuangalie tuhuma

1. Akiwa Iringa, na imesemwa Bungeni na hadi leo kuna magazeti yana nukuu yake, JPM alisema ''Watu wa kasakazini watusubiri''. Kwamba anajenga chuki ya eneo moja la nchi dhidi ya jingine. Kulikuwa na sababu yoyote?

2. Ubaguzi: JPM alisema hatapeleka maendeleo walipochagua Wapinzani
Kwamba anakusanya kodi za Wananchi halafu anaamua matumizi kwa njia ya ubaguzi
Hili nalo unalionaje mheshimiwa!

3. Ukanda: Ni neno wakati wa utawala wa JPM na watu husema ni zamu ya kanda..
Hatujawahi kuzungumzia ukanda kama wakati wa wa JPM , teuzi zake tu zinatueleza
Ukisikia wanaosema ''gang' kuna hoja ! Unakumbuka tumbua majipu? Ilianzaje na iliishaje?

Kwanini Tumbua majipu ilikwenda kasi mwanzoni mwa utawala wake kisha kufa kabisa?

3. Udini : Aliyendekeza udini akipita maeneo ya ibada kueleza siasa.
Kuna mtu aliweka ushahidi wa teuzi zake na hilo halikupingwa na yoyote.

Aliifanya nchi kuwa na'' imani'' na kuwatenga wasioamini, wasio na imani, dini nyingine zilizopo nchini. Abadilisha salamu na kuzifanya katika misingi ya dini kitu kilichochoea udini.
Salamu za Waislam na Wakristi akitenga makundi mengine ya jamii

Akatumia imani yake kupambana na COVID-19 akilazimisha Taifa kuamini, kazi isiyo ya Rais

Akawanyima wenye dini , wasio na dini au imani fursa ya ''kupambana' na COVID kwa kukataa chanjo na kulazamisha watu watumie majani na MAOMBI. Kazi ya Rais si kusimamia IMANI

3.Ufisadi: Matumizi ya pesa nje ya bajeti!
Ndege ziliidhinishwa kununuliwa bajeti gani kwa cash?
Kwanini kuna mafungu yalipitishiwa Ikulu?

Pesa za EU kwa ajili ya COVID-19 hazikutmika ilipokusudiwa!

Zitto wa ACT kauliza Bilioni 70 zilizokuwa zinakwenda Mwanza bila maelezo ni za nini?

Uwanja wa Chato ulikuwa katika bajeti ya mwaka gani na unaletea nchi faida gani?

Mayanga construction ni kampuni ya nani?

Tanroad wanajenga vipi viwanda vya sukari?

Labda tuangalie rekodi ya ripoti ya CAG Kichere kwa undani
1. Nenda Kaskazi kawahoji watu wa huko walinyimwa nini na Magufuli walichostahili na kikapelewakwa Kanda ya Ziwa labda.

2. Mtwara Mjini 2015-2020, jimbo lilikuwa chini ya Cuf. Ukarabati wa Bandari, Ujenzi wa Soko, Hospitali ya Kanda, barabara, Vyuo, nk....
Huo ni mfano mmoja. Nawe unaweza kuleta mfano wa Jimbo LA Upinzani ambalo halikuwa na mradi wowote.

3. Unawezaje kuiona hoja katika Sukuma Gang na kushindwa kuona Hoja ya TimuMsoga? Huu ni unafiki.

4. Kila Kiongozi atafanya kazi na watu ambao ataona wanamfaa. Habari za kitotototo za sijui kubalance dini, kabila mara gender ni upuuzi wa Demokrasia. So hoja za werevu. Tunahitaji Ufanisi katika Ofisi ya Umma.

5. Juu ya Covid unatia aibu, siwezi hata kukujibu chochote. Unajichafua mbele za watu. Baki na Utumwa wako wa Usasa.

6. Urasimi wenu ulitufanya kuwa na Viongozi wa Ajabu huko nyuma, na wakafanya ya ajabu. Ukiukaji wa Magufuli umefanya tushuhudie yaliyo Makuu katika Taifa. Hilo linahalalisha MENGI sana kwake.
 
Nimeeleza! zaidi ya hapo ushahidi kautoa Rais SSH siku ya maadhimisho ya Mwl Nyerere
Rais SSH ni msaidizi namba 1 wa JPM, sasa anaposema '' Ukabila, udini na ukanda tumerudi nyuma'' kama hiyo si fact nani msaidizi mwingine umjuaye?

Rekodi ya JPM haitetewi na flyover si kumtendea haki

Iangaliwe rekodi kwa ujumla katika Utu, ubinadamu , haki , demokrasia, uchumi , mahusiano na mataifa n.k.
Nikisema unatia aibu sijui utasemaje....

Samia ametoa TUHUMA, SIO USHAHIDI WA TUHUMA. Kwa umri wako unashindwaje kutofautisha kati ya TUHUMA na Ushahidi wa Tuhuma?

CHUTAMA.

UTU si Msamaha, wala huruma, wala Upendo, wala heshima, si utii, si nidhamu wala unyenyekevu.
UTU ni namna vile MTU anavyoiWAJIBIKIA nafasi yake vema katika jamii yake.

Rudi darasani hata kama umri umeenda. Hekima za mvi hazipo tena Sikh hizi. Zihangaikie.
 
Nikisema unatia aibu sijui utasemaje....

Samia ametoa TUHUMA, SIO USHAHIDI WA TUHUMA. Kwa umri wako unashindwaje kutofautisha kati ya TUHUMA na Ushahidi wa Tuhuma?
Msaidizi namba 1 wa Rais ni witness 1 tuhuma zake ni ushahidi, ni shahidi !
UTU si Msamaha, wala huruma, wala Upendo, wala heshima, si utii, si nidhamu wala unyenyekevu.
UTU ni namna vile MTU anavyoiWAJIBIKIA nafasi yake vema katika jamii yake.
Rudi darasani hata kama umri umeenda. Hekima za mvi hazipo tena Sikh hizi. Zihangaikie.
Wanasema hivi ''UTU ni kitu kinachomfanya binadamu awe binadamu kwa maana ya kuwa na upendo , huruma na unenyekevu kikimtofautisha na vitu visivyokuwa na utu''

Unapojali nafsi ya mtu umeujali utu na una utu. Unapojali nafasi ya wenzako katika jamii unautekeleza utu na una utu. Unapopenda wenzako katika jamii unatenda utu na una utu.
Unapopenda na kuonyesha huruma na unyenyekevu unatenda utu na una utu.

Ukiliona jambo linalokera na kuudhi likakuchukiza huo ni utu na awaye ana utu
Ukithamini roho na nafsi za wenzako kama nafsi yako, awaye ana utu

Kama huna hayo huna utu!

Nyerere alichukizwa na mauaji ya vikongwe Shinyanga! alijitokeza akaalaani mambo yanayofanywa na serikali yake. Ali Hassan Mwinyi akajiuzulu ili kuwajibika na kuonyesha huruma, upendo na unyenyekevu. Wote wawili wakawa ni viongozi wenye Utu hata kama walikuwa na mapungufu ya kibinadamu

Sifa ya kwanza ya kiongozi katika jamii ni UTU wake. Ombwe la UTU linautweza ubinadamu

Utu si kuwajibika ni sehemu ya UTU lakini UTU una ukuu ukiutangulia uwajibikaji kwa mbali

Kuwajibika hakuna maana yoyote bila kuutanguliza UTU.
Tumejifunza thamani ya UTU kwa ushuhuda, tuutukuze !
 
1. Nenda Kaskazi kawahoji watu wa huko walinyimwa nini na Magufuli walichostahili na kikapelewakwa Kanda ya Ziwa labda.

2. Mtwara Mjini 2015-2020, jimbo lilikuwa chini ya Cuf. Ukarabati wa Bandari, Ujenzi wa Soko, Hospitali ya Kanda, barabara, Vyuo, nk....
Huo ni mfano mmoja. Nawe unaweza kuleta mfano wa Jimbo LA Upinzani ambalo halikuwa na mradi wowote.
Dhamira ''intent'' ina maana kubwa sana.

Kitendo cha kusema ''Watu wa kaskazini wasubiri'' hakikuwa na nia njema.

Ni kitendo kilichoonyesha CHUKI moyoni , kwa bahati nzuri au mbaya neno likatoka mdomoni.

Kwa dhamira yake nani anayejua ametenda maamuzi yapi akiwa na dhamira hiyo?

Kazi ya kiongozi wa nchi ni kuunganisha Taifa liwe kitu kimoja si kuwagawa kikanda.

Ni kiongozi gani nchini aliyewahi kutoa kauli kama hiyo?
4. Kila Kiongozi atafanya kazi na watu ambao ataona wanamfaa. Habari za kitotototo za sijui kubalance dini, kabila mara gender ni upuuzi wa Demokrasia. So hoja za werevu. Tunahitaji Ufanisi katika Ofisi ya Umma.
Katika kitabu chake, Rais Mkapa anasema Nyerere alimwambia hatamshauri nani awe katika baraza lake la mawaziri, akifanya hivyo litakuwa baraza lake. Nyerere akamshuri Mkapa kwamba azingatie ukweli kuwa nchi hii ina makabila na watu wa dini mbali mbali.

Viongozi wanaofikiri , wenye maono na akili nzuri ndivyo wanavyoona mambo

5. Juu ya Covid unatia aibu, siwezi hata kukujibu chochote. Unajichafua mbele za watu. Baki na Utumwa wako wa Usasa.
Hapa ndipo wala usizungumzie nadhani hata wewe huna jibu !

Ni eneo JPM alivurunda kitaifa na kimataifa.

Huwezi kuchukua specification za kipimo fulani ukaweka mafenesi halafu utegemee majibu.
Mtu aliyesoma sayansi atashangaa kusikia achilia mbali aliyefanya ni mwana sayansi.

JPM akaaminisha ulimwengu masks (Barakoa) zinaletwa ili kuua Watanzania kwa vita ya uchumi.
Hivi unaamini wazungu wanaleta COVID kwa barakoa! katika vita ya'' uchumi''

Tukajengewa banda la kufukiza Muhimbili, hivi lile banda liliishia wapi?
Tukaambiwa tufukize nyasi kwasababu zinatibu

Wananchi wakaambiwa hakuna COVID nchini kuna changamoto ya kupumua.
Ni kosa la jina kusema COVID wakati dunia nzima inazizima

Maruku ya kutoa takwimu ili wananchi na dunia wasijue nini kinaendelea!

Well well, akawadhihaki waliovaa barakoa! aliwaona wendawazimu akisifia wasiovaa

Akahimiza maombi na sala , Mecca na Vatican wana social distancing wanavaa barakoa.
Tukawa dunia na mungu wetu tukitumia misahafu na Bibilia zao.

Alituma ndege kuchukua mchachai Madagascar, mwezi mmoja baadaye Madagascar wakaomba kuokolewa na WHO.

Akapiga marufuku chanjo tujiridhishe kwanza! Yeye akiwa amepewa chanjo utotoni na kila asubuhi Watoto wa Tanzania wanapata chanjo, ya COVID alitaka kujiridhisha maana watatuua!
si ya polio, tetanus, TB! n.k.

Tuachie hapa! inatosha

6. Urasimi wenu ulitufanya kuwa na Viongozi wa Ajabu huko nyuma, na wakafanya ya ajabu. Ukiukaji wa Magufuli umefanya tushuhudie yaliyo Makuu katika Taifa. Hilo linahalalisha MENGI sana kwake.
Twambie kipi alichofanya ambacho hakikuwahi kufanywa na viongozi huko nyuma
 
Msaidizi namba 1 wa Rais ni witness 1 tuhuma zake ni ushahidi, ni shahidi !

Wanasema hivi ''UTU ni kitu kinachomfanya binadamu awe binadamu kwa maana ya kuwa na upendo , huruma na unenyekevu kikimtofautisha na vitu visivyokuwa na utu''

Unapojali nafsi ya mtu umeujali utu na una utu. Unapojali nafasi ya wenzako katika jamii unautekeleza utu na una utu. Unapopenda wenzako katika jamii unatenda utu na una utu.
Unapopenda na kuonyesha huruma na unyenyekevu unatenda utu na una utu.

Ukiliona jambo linalokera na kuudhi likakuchukiza huo ni utu na awaye ana utu
Ukithamini roho na nafsi za wenzako kama nafsi yako, awaye ana utu

Kama huna hayo huna utu!

Nyerere alichukizwa na mauaji ya vikongwe Shinyanga! alijitokeza akaalaani mambo yanayofanywa na serikali yake. Ali Hassan Mwinyi akajiuzulu ili kuwajibika na kuonyesha huruma, upendo na unyenyekevu. Wote wawili wakawa ni viongozi wenye Utu hata kama walikuwa na mapungufu ya kibinadamu

Sifa ya kwanza ya kiongozi katika jamii ni UTU wake. Ombwe la UTU linautweza ubinadamu

Utu si kuwajibika ni sehemu ya UTU lakini UTU una ukuu ukiutangulia uwajibikaji kwa mbali

Kuwajibika hakuna maana yoyote bila kuutanguliza UTU.
Tumejifunza thamani ya UTU kwa ushuhuda, tuutukuze !
1. Ndugu, baki na Fikra zako kwamba Tuhuma za Rais ni Uthibitisho. Ila kwangu inanifanya nijisikie aibu kuona ni wewe unayetamka hivyo. Najiuliza, KWANINI UNAKUBALI KUJICHAFUA KIASI HICHO?

2. UTU.
Kujali nafsi za wengine hakupimwi kwa Uzito wa Hisia/Hulka/Mahaba yako kwao. KUJALI wengine kunapimwa na namna vile Unavyowajibikia mahusiano sahihi yaliyopo baina yenu.
Huruma tu pasipo sababu ya kuhurumia, au unyenyekevu, iwe msamaha, au Upendo, SI UTU bali ni UTUMWA NA UJINGA.

3. Ni sahihi kuwa sifa ya kwanza ya kiongozi ni UTU, yaani KUTAMBUA WAJIBU WAKE KWA WATU WAKE KULINGANA NA NAFASI YAKE. Sio kuhurumia wapumbavu, sio kuchekea waovu, sio kusamehe wahalifu, au kuwapenda waendao kinyume na wajibu wao.

4. Ni Nyerere aliyepeleka jeshi Uganda, na wakafa hata wenye mimba changa. ALIUA. Lakini hilo halibatilishi wala kuhalalisha UTU wake, mpaka pale tutakapotathimini UPI ni WAJIBU wake kulingana na nafasi yake katika alichokitenda.
UWE UNATOKA NJE YA BOKSI LA HISIA KUELEWA MAMBO.

Ni MWINYI mwenye rekodi ya kuhidhinisha Kunyongwa kwa watu. Lakini bado haikengeushi UTU wake.

UTU hautambulishwi kwa HISIA za mtu. UTU uko nje ya Mihemko yetu.

UTU ni MANTIKI.

Mkuu, shida umekaririshwa viini macho vingi vya kiimani (msikitini au kanisani) ndivyo vinavyokufunga kutoona Thamani Halisi ya Utu. Utu si Utofauti ukiopo baina ya binadamu na wanyama. Hata mbwa anaeza kuwa mkamilifu katika Utu kuliko binadamu anayependa Ubatili.

Jipe muda kutafakari vizuri juu ya Utu.
 
Dhamira ''intent'' ina maana kubwa sana.

Kitendo cha kusema ''Watu wa kaskazini wasubiri'' hakikuwa na nia njema.

Ni kitendo kilichoonyesha CHUKI moyoni , kwa bahati nzuri au mbaya neno likatoka mdomoni.

Kwa dhamira yake nani anayejua ametenda maamuzi yapi akiwa na dhamira hiyo?

Kazi ya kiongozi wa nchi ni kuunganisha Taifa liwe kitu kimoja si kuwagawa kikanda.

Ni kiongozi gani nchini aliyewahi kutoa kauli kama hiyo?
Maneno tupu hayatoshi kutambua Dhamira ya mtu(ila hili ni kwa walio huru tu)

Dhamira ya mtu IPO ndani ya DHATI yake. Na hakuna mtu anayeweza kusemea Dhati ya mtu mwingine, ila matendo yake mtu husemea kidogo juu ya Dhati yake mtu.

Ni watu dhaifu pekee wanaohukumu watu kwa kauli zao tu pasipo kujali matendo yao.

Mimi nimekupa matendo yaliyoenda kinyume na kauli zake, ulipaswa uoneshe vitendo vilivyoendana na kauli zake, sio kusemea Dhati za watu, utakuwa unatudanganya.

*Ni wewe unayesema ametenda udini, ukabila na ukanda, halafu hapa unatuambia tena kuwa 'Hakuna anayejua ametenda yepi akiwa na dhamira hiyo'
Wewe ni muongomuongo. Tunza kumbukumbu vizuri, itakusaidia.
 
Maneno tupu hayatoshi kutambua Dhamira ya mtu(ila hili ni kwa walio huru tu)
Dhamira ya mtu IPO ndani ya DHATI yake. Na hakuna mtu anayeweza kusemea Dhati ya mtu mwingine, ila matendo yake mtu husemea kidogo juu ya Dhati yake mtu.
Kabla ya tendo kuna nia au kusudio 'intent' hata mbele ya court of Justice kuna hukumu yake
Kwa watu wa psychology wanasema lazima uelewe aina za watu na tabia zao.
Hili ni somo zito na sitakutendea haki nikiingia katika mjadala nawe!
Mimi nimekupa matendo yaliyoenda kinyume na kauli zake, ulipaswa uoneshe vitendo vilivyoendana na kauli zake, sio kusemea Dhati za watu, utakuwa unatudanganya.
Aliwaambia wana habari '' ...don't think you have that much power'' , unataka kujua nini kiliendea katika media? Unakumbuka kuna waandishi wamekimbia na wengine hatujui walipo leo hii!
Unakumbuka alisema '' wanaosaliti vita ya uchumi wanafanywa nini'' the rest is history
Akatamka hataweka lockdown, haikutokea
Akaahidi kuufuta upinzani mwaka 2020, well sijui hili unasemaje

Jambo zuri sana kwake ni kuwa kila alichosema alitimiza! intent na action zake vilifuatana!

Sasa ndugu yangu mbona hoja za COVID hujagusa hata moja?
Nimeorodhesha hoja za kutosha tu alichokifanya
 
1. Ndugu, baki na Fikra zako kwamba Tuhuma za Rais ni Uthibitisho. Ila kwangu inanifanya nijisikie aibu kuona ni wewe unayetamka hivyo. Najiuliza, KWANINI UNAKUBALI KUJICHAFUA KIASI HICHO?
Kuna msemo usemao 'Beauty is in the eye of beholder'' . Sina shaka wasomaji wana macho
3. Ni sahihi kuwa sifa ya kwanza ya kiongozi ni UTU, yaani KUTAMBUA WAJIBU WAKE KWA WATU WAKE KULINGANA NA NAFASI YAKE.
Yes! lakini je, upi ni wajibu wa kiongozi kwa watu wake kulingana na nafasi ya JPM?
Kwa mujibu wa katiba yetu na kiapo cha Urais, ni kwamba, Rais atalinda watu na mali zao
Rejea hapo, atalinda WATU na MALI zao. Neno Watu limetangulia mali zao
Wajibu wa kwanza wa Rais ni kulinda Watu ! Kama hujaelewa uliza
4. Ni Nyerere aliyepeleka jeshi Uganda, na wakafa hata wenye mimba changa. ALIUA. Lakini hilo halibatilishi wala kuhalalisha UTU wake, mpaka pale tutakapotathimini UPI ni WAJIBU wake kulingana na nafasi yake katika alichokitenda.
Ni ipi dhamira ''intent yake' na upi ni wajibu wake kwa alichotenda.
Ni MWINYI mwenye rekodi ya kuhidhinisha Kunyongwa kwa watu. Lakini bado haikengeushi UTU wake.
Mwinyi hajaidhinisha kunyongwa watu! alisaini kama ilitokea.
Kama alifanya hivyo ni kwa mujibu wa mamlaka yake kisheria na hakufanya kosa.

Aliyeidhinisha kunyongwa watu ni Bunge la JMT, likatoa idhini kwa Mahakama kutafuta haki kwa mtuhumiwa.

Anayepatikana na hatia ananyongwa kwa mujibu wa sheria ya nchi iliyotungwa na Bunge na kusainiwa na Rais. Rais anatoa kibali cha tendo hilo kufanyika, haidhinishi kwani tendo kwani limeshaidhinishwa na kuthibitishwa na Mahakama imethibitisha hatia .

Lakini pia Katiba imempa Rais nguvu ya kusamehe
Msamaha wa Rais haubadilishi hukumu, ni '' prerogative power'' aliyopewa na katiba.

Rais anayesamehe wanaotaka kunyongwa hajavunja sheria yoyote ya nchi
Rais anayetoa kibali cha kunyongwa hajavunja sheria yoyote ya nchi.

Hoja yako juu ya Mwinyi ni 'null and void ab initio'
 
Ni eneo JPM alivurunda kitaifa na kimataifa.

Huwezi kuchukua specification za kipimo fulani ukaweka mafenesi halafu utegemee majibu.
Mtu aliyesoma sayansi atashangaa kusikia achilia mbali aliyefanya ni mwana sayansi.

JPM akaaminisha ulimwengu masks (Barakoa) zinaletwa ili kuua Watanzania kwa vita ya uchumi.
Hivi unaamini wazungu wanaleta COVID kwa barakoa! katika vita ya'' uchumi''

Tukajengewa banda la kufukiza Muhimbili, hivi lile banda liliishia wapi?
Tukaambiwa tufukize nyasi kwasababu zinatibu

Wananchi wakaambiwa hakuna COVID nchini kuna changamoto ya kupumua.
Ni kosa la jina kusema COVID wakati dunia nzima inazizima

Maruku ya kutoa takwimu ili wananchi na dunia wasijue nini kinaendelea!

Well well, akawadhihaki waliovaa barakoa! aliwaona wendawazimu akisifia wasiovaa

Akahimiza maombi na sala , Mecca na Vatican wana social distancing wanavaa barakoa.
Tukawa dunia na mungu wetu tukitumia misahafu na Bibilia zao.

Alituma ndege kuchukua mchachai Madagascar, mwezi mmoja baadaye Madagascar wakaomba kuokolewa na WHO.

Akapiga marufuku chanjo tujiridhishe kwanza! Yeye akiwa amepewa chanjo utotoni na kila asubuhi Watoto wa Tanzania wanapata chanjo, ya COVID alitaka kujiridhisha maana watatuua!
si ya polio, tetanus, TB! n.k.

Tuachie hapa! inatosha


Twambie kipi alichofanya ambacho hakikuwahi kufanywa na viongozi huko nyuma
Hili nilikua njiani kukujibu:
Tuhuma zako juu ya Corona zinakuweka wazi juu haya yafuatayo:-

1. Unaabudu wanasayansi na umekuwa kama mtumwa wao kwa kila wanachosema.

2. Una kaulimbukeni juu ya watu unaowaita Wasomi na usomi wao. Wamekuwa reference yako kwa kila kitu.

3. Ni mpotoshaji wa makusudi (ni kwa sababu najua unajua Magufuli aliposema Vita ya Uchumi juu ya Korona alimaanisha nini) Zaidi, inaonesha chuki zako tu.

4. Narudia tena, WEWE NI MUONGO NA MPOTOSHAJI(na hilo linadhihirisha chuki zako) Hakuna Mtanzania aliyeambiwa afukize nyasi, na hata wewe unalijua hilo.

5. Una kasumba ya Uduni, na hii inafunga Utumwa wa Fikra ulionao. Unatukuza mno Uzungu.

6. Mpaka sasa ni Watanzania milioni 2.8 waliopata Chanjo mliyoletewa. Na mbaya zaidi wengi kati ya hao mliwapata kwa ignorance yao na wengine MLIWALAZIMISHI(hasa wa mama waliohuhudhuria Kliniki-nimelishuhudia mwenyewe hili)
Wapo pia watumishi wa serikali waliochanja kwa vitisho vya nafasi zao serikali(hasa wale waliosimamia zoezi LA chanjo, Ushahidi upo)

Kati ya watu wazima 38 mil ni ni zaidi ya watu 35 mil walioamua KUGOMEA HUO UPUUZI WA CHANJO. Sasa uwe unapita mtaani kuwasema kwamba ni wajinga, walugaluga, primitive, kama hawajakupopoa mawe.

Dunia yako imesahau juu ya CORONA baada Vita ya Ukraine. Ilipaswa ikutafakarishe sana, kwa bahati mbaya hutaki.

Hoja zako nyingi juu ya Corona nilishakujibu, na wadau wengi walishakujibu, uliukimbia ule Uzi. Kama una chchote basi rudi kule.

Ukuu wa Magufuli ni huu
Ni uwezo wake wa Kuchagua Kundi LA Werevu(Japo ni wachache) na kutochagua kwake kundi LA wapumbavu(japo ndio kundi LA wengi)

Na kufanya hivyo imeamsha Tafakari za wengi kumuunga mkono.
 
Kuna msemo usemao 'Beauty is in the eye of beholder'' . Sina shaka wasomaji wana macho

Yes! lakini je, upi ni wajibu wa kiongozi kwa watu wake kulingana na nafasi ya JPM?
Kwa mujibu wa katiba yetu na kiapo cha Urais, ni kwamba, Rais atalinda watu na mali zao
Rejea hapo, atalinda WATU na MALI zao. Neno Watu limetangulia mali zao
Wajibu wa kwanza wa Rais ni kulinda Watu ! Kama hujaelewa uliza

Ni ipi dhamira ''intent yake' na upi ni wajibu wake kwa alichotenda.

Mwinyi hajaidhinisha kunyongwa watu! alisaini kama ilitokea.
Kama alifanya hivyo ni kwa mujibu wa mamlaka yake kisheria na hakufanya kosa.

Aliyeidhinisha kunyongwa watu ni Bunge la JMT, likatoa idhini kwa Mahakama kutafuta haki kwa mtuhumiwa.

Anayepatikana na hatia ananyongwa kwa mujibu wa sheria ya nchi iliyotungwa na Bunge na kusainiwa na Rais. Rais anatoa kibali cha tendo hilo kufanyika, haidhinishi kwani tendo kwani limeshaidhinishwa na kuthibitishwa na Mahakama imethibitisha hatia .

Lakini pia Katiba imempa Rais nguvu ya kusamehe
Msamaha wa Rais haubadilishi hukumu, ni '' prerogative power'' aliyopewa na katiba.

Rais anayesamehe wanaotaka kunyongwa hajavunja sheria yoyote ya nchi
Rais anayetoa kibali cha kunyongwa hajavunja sheria yoyote ya nchi.

Hoja yako juu ya Mwinyi ni 'null and void ab initio'
1. Yes, hiyo ni Katiba inavyosema. Na hata isiposema huo ndio Utu/Wajibu wa Kiongozi.

Kulinda Watu na Mali zao lakini usifunge macho yako hapo tu, unatakiwa kujua ni KULINDA WATU NA MALI ZAO DHIDI YA WATU.

2. Sikuwa natafuta makosa ya Mwinyi wala Nyerere. Militia mifano tu ili uelewe Utu ni nini, bahati mbaya umekuwa mzito kuelewa. Nilishakuambia Huruma, Kusamehe, Kupenda, Unyenyekevu, Utii, sio KIPIMO CHA UTU.

Ukaukimbia mfano wa Nyerere.

Nikuambie tu labda... Hata kuua kunaweza kuwa UTU. USIPENDE FIKRA RAHISIRAHISI.
 
Hapa ndipo wala usizungumzie nadhani hata wewe huna jibu !

Ni eneo JPM alivurunda kitaifa na kimataifa.

Huwezi kuchukua specification za kipimo fulani ukaweka mafenesi halafu utegemee majibu.
Mtu aliyesoma sayansi atashangaa kusikia achilia mbali aliyefanya ni mwana sayansi.

JPM akaaminisha ulimwengu masks (Barakoa) zinaletwa ili kuua Watanzania kwa vita ya uchumi.
Hivi unaamini wazungu wanaleta COVID kwa barakoa! katika vita ya'' uchumi''

Tukajengewa banda la kufukiza Muhimbili, hivi lile banda liliishia wapi?
Tukaambiwa tufukize nyasi kwasababu zinatibu

Wananchi wakaambiwa hakuna COVID nchini kuna changamoto ya kupumua.
Ni kosa la jina kusema COVID wakati dunia nzima inazizima

Maruku ya kutoa takwimu ili wananchi na dunia wasijue nini kinaendelea!

Well well, akawadhihaki waliovaa barakoa! aliwaona wendawazimu akisifia wasiovaa

Akahimiza maombi na sala , Mecca na Vatican wana social distancing wanavaa barakoa.
Tukawa dunia na mungu wetu tukitumia misahafu na Bibilia zao.

Alituma ndege kuchukua mchachai Madagascar, mwezi mmoja baadaye Madagascar wakaomba kuokolewa na WHO.

Akapiga marufuku chanjo tujiridhishe kwanza! Yeye akiwa amepewa chanjo utotoni na kila asubuhi Watoto wa Tanzania wanapata chanjo, ya COVID alitaka kujiridhisha maana watatuua!
si ya polio, tetanus, TB! n.k.

Tuachie hapa! inatosha
Soma hoja hapo juu kisha uonyeshe moja tu ambayo ni tuhuma na si ukweli
Hili nilikua njiani kukujibu:
Tuhuma zako juu ya Corona zinakuweka wazi juu haya yafuatayo:-
 
1. Yes, hiyo ni Katiba inavyosema. Na hata isiposema huo ndio Utu/Wajibu wa Kiongozi

Ukaukimbia mfano wa Nyerere.

Nikuambie tu labda... Hata kuua kunaweza kuwa UTU. USIPENDE FIKRA RAHISIRAHISI.
Mfano wa Nyerere ni mzuri sana, alipoingiza nchi katika vita alifanya hivyo ili kulinda WATU na MALI zao dhidi ya Idd Amin. Nyerere alikwenda Diamond Jubilee akawaeleza Watanzania chanzo cha vita, tupo wapi na tulidhamiria nini. Unakumbuka '' Nia ya kumpiga, sababu za kumpiga na uwezo wa kumpiga tunao''

Nyerere hakuvumbua vita isiyokuwepo! unaelewa? Vita tu ya kichwani mwa mtu!
 
Hili nilikua njiani kukujibu:
Tuhuma zako juu ya Corona zinakuweka wazi juu haya yafuatayo:-
Hakuna tuhuma kuna facts. Je, Magufuli hakuhimiza kujifukiza ? Lini Magufuli alivaa Barakoa?
Je, hakusema Barakoa zinavitu anajua siri za nchi? Je, hakuhimiza maombi, je hakukutaza chanjo, je hakuagiza banda la kujifukiza Muhimbili, je, hakutuma ndege na Profesa Kabudi kwenda Madagascar, Je hakuzogoa wavaa barakoa kanisani?
1. Unaabudu wanasayansi na umekuwa kama mtumwa wao kwa kila wanachosema.
Yes kwasababu tunawasiliana kwa sayansi pasi kujuana. Kila unachotumia wewe ni zao la kazi za sayansi. Ninaikubali sayansi na matokeo yake pasi na shaka!
2. Una kaulimbukeni juu ya watu unaowaita Wasomi na usomi wao. Wamekuwa reference yako kwa kila kitu.
Hujajibu hoja, hayo yanayonihusu yasikusghulishe

Hoja ni hii, taja jambo moja ambalo Magufuli amelifanya na ambalo halijawaji kufanywa na kiongozi mwingine yoyote kwa mujibu wako
3. Ni mpotoshaji wa makusudi (ni kwa sababu najua unajua Magufuli aliposema Vita ya Uchumi juu ya Korona alimaanisha nini) Zaidi, inaonesha chuki zako tu.
Hakuna chuki, hebu tujadili kuna vita ya uchumi kuhusu Corona kwa lipi.
Nani anapigana vita ya uchumi na Tanzania, na vita hiyo imeshaije maana hatusikii tena
4. Narudia tena, WEWE NI MUONGO NA MPOTOSHAJI(na hilo linadhihirisha chuki zako) Hakuna Mtanzania aliyeambiwa afukize nyasi, na hata wewe unalijua hilo.
Yes zipo hotuba za Magufuli akihimiza kujifukiza. Waziri wake Jafo akatekeleza maagizo ya boss na wengine wakiwemo wabunge na mawaziri wakaunga tela.
Tuna ushahidi pale Muhimbili wa banda la kujifukiza
5. Una kasumba ya Uduni, na hii inafunga Utumwa wa Fikra ulionao. Unatukuza mno Uzungu.
Jibu hoja usijadili mtu, sisi ni wanadamu tuna udhaifu tu kama viumbe wengine.
Majadala usiwe juu ya madhaifu yetu bali juu ya matokeo ya madhaifu yetu hasa kwa truliowapa dhamana. Tafadhali Jibu hoja, na hapa ni moja tu, je ilikuwa sahihi Rais JPM kusema '' watu wa kaskazini wasubiri''?
6. Mpaka sasa ni Watanzania milioni 2.8 waliopata Chanjo mliyoletewa. Na mbaya zaidi wengi kati ya hao mliwapata kwa ignorance yao na wengine MLIWALAZIMISHI(hasa wa mama waliohuhudhuria Kliniki-nimelishuhudia mwenyewe hili)
Wapo pia watumishi wa serikali waliochanja kwa vitisho vya nafasi zao serikali(hasa wale waliosimamia zoezi LA chanjo, Ushahidi upo)

Kati ya watu wazima 38 mil ni ni zaidi ya watu 35 mil walioamua KUGOMEA HUO UPUUZI WA CHANJO. Sasa uwe unapita mtaani kuwasema kwamba ni wajinga, walugaluga, primitive, kama hawajakupopoa mawe.
Muhimu hapa ni kuwa kila mtu ana uhuru wa kuchagua. Nipo katika rekodi hapa JF nikisema chanjo iruhusiwe asiyetaka asisumbuliwe. Mauti ni tukio la mtu binafsi.
Kisichotakiwa ni kuingiza imani za watu kwa wengine na kuwanyima haki ya wanachotaka

Waliokufa wakitamani chanjo hawakutendewa haki.
Kuzuia chanjo kwa imani ya mtu binafsi ima kidini au kutoamini sayansi au kutoamini mabeberu haukuwa uungwana. Kuzuia takwimu watu wasijue nini kinatoke haikuwa sahihi. Kuzuia watu wasitamke ugonjwa ilikuwa collective imbecilisation ya hali ya juu. Haikuwa sahihi ! period
Ukuu wa Magufuli ni huu
Ni uwezo wake wa Kuchagua Kundi LA Werevu(Japo ni wachache) na kutochagua kwake kundi LA wapumbavu(japo ndio kundi LA wengi)
Ni maoni yako yaheshimiwe, lakini pia wanaopinga yako hawawezi kuwa wapumbavu kwasababu huna hati miliki ya maoni!
Na kufanya hivyo imeamsha Tafakari za wengi kumuunga mkono.
Wengi kwa takwimu zipi? Kumbuka kuna Quantity and Quality
 
Soma hoja hapo juu kisha uonyeshe moja tu ambayo ni tuhuma na si ukweli
Hizo ni Tuhuma za Kwamba kilichofanyika ni Ubatili.

Lakini pia unadai NYASI, ubadai imani, mbali zaidi unadai Magufuli alitaja Vita ya uchumi kati ya Tz na Nchi gani sijui.

Juu ya hilo nikuache, hope umeshachanjwa tayari. Subiri na ya watoto itakapofika uipeleke familia nzima.
 
N
Mfano wa Nyerere ni mzuri sana, alipoingiza nchi katika vita alifanya hivyo ili kulinda WATU na MALI zao dhidi ya Idd Amin. Nyerere alikwenda Diamond Jubilee akawaeleza Watanzania chanzo cha vita, tupo wapi na tulidhamiria nini. Unakumbuka '' Nia ya kumpiga, sababu za kumpiga na uwezo wa kumpiga tunao''

Nyerere hakuvumbua vita isiyokuwepo! unaelewa? Vita tu ya kichwani mwa mtu!
Ndio maana nilikuambia UTU ni Wajibu. Sio kusamehe tu, kuhurumia tu, kujali tu, au kunyenyekea Ubatili.

Hivyo nani amekufa, ameteswa, amepotea, nk si kigezo cha kumtuhumu mtu kukosa UTU, ila tu kama haikuwa sehemu ya Wajibu wake.

Vita ya Nyerere iliua mpaka watoto wadogo, lakini haikufanya umkoseshe Utu. Muhimu ni justification tu.
 
Back
Top Bottom