Annunaki created Man: Binadamu tunaoishi sasa tulitengenezwa (tuliumbwa) na Annunaki

Annunaki created Man: Binadamu tunaoishi sasa tulitengenezwa (tuliumbwa) na Annunaki

Hoja yao kubwa ni kwamba hayo maandiko yapo toka zamani kabla ya hivi vitabu vya dini na kwamba hata Biblia imecopy huko na Qur'an imekopi kwenye biblia.
Ukifatilia kwa undani na ukifanya utafiti utaona wazi ya kuwa habari za Annunak zimekuta habari za Adamu tangu zamani ndiyo maana nawauliza wamuanishie mtu wa kwanza kuelezea habari hizo. Suala la Annunaki ni nadharia iliyo pandikizwa ili kuwatoa watu katika dini, sababu habari hizo zimewakuta wanadamu wapo tayari.
 
KUTOKANA NA MAELEZO HAYO APO JUU NI DHAHIRI KUWA WANADAMU/WATU WANA ASILI TOFAUTI
Kabla swali lako halijajibiwa tayari umeshajipa majibu kwa swali ambalo mwenyewe umeuliza,hii inaonesha hata uambiwe nini huwezi kuelewa kwa sababu yatari una misimamo yako.
Kama wote wana wanadamu tumotokana na Adam na Hawa, kwanini tuwe na utofauti mkubwa katika makundi ya dam
Kama ulimsoma vizuri mtoa mada,nimesahau sehemu ya ngapi.

Mtoa mada alisema kwamba mazingira anayoishi mtu na mabadiliko anayopitia yanaweza kubebwa na DNA na mabadiliko hayo yakapita mpaka kwa mtoto.

Akatolea mfano wa mtu anayeogelea kwamba akifanya mazoezi sana kuna mambo atabadilika na mambo hayo yanaweza kupita mpaka kwa watoto.

Hivyo mazingira yanavyotuathiri yanaweza kubadilisha hata maumbile yetu na tukawa watu tofauti.

Hivyo kwa hoja hii ni wazi kwamba kutoka katika asili moja sio hoja kwwmba tusitofautiane.

Kwa sababu tumetoka katika asili moja lakini tumetawanyika na kuishi maeneo tofauti,na kula vitu tofauti kabisa.

Na hivyo vitu vinaweza kubadilisha physiology ya mtu akawa tofauti na wengine.

Kwa hivyo kuwa na rhesus tofauti baina ya mama na baba ni jambo la kawaida kwa sababu tulishaathiriwa na mazingira tofauti.


Kwanini mama mwenye kundi la Damu lenye Rh negative akibeba mimba ya kwanza mtoto akawa na kundi damu lenye Rh positive, mama anatengeneza antibodies/Kinga dhidi ya mimba zinazofuata, endapo mimba zinazofuata mtoto akiwa na Rh positive na damu zao zikaingiliana pindi mtoto akiwa tumboni mtoto anadhurika, kama kweli wote chanzo chetu ni kimoja, Adam na Hawa
Mkuu kuna uwezekano mkubwa wa sisi kuwa tofauti kwa sababu tumeishj mazingira tofauti.

Kwa sababu hiyo mwili unaadapt mabadiliko ya mazingira.

Na mabadiliko hayo ambayo yanatokea katika miili yetu inapita moja kwa moja kwa vizazi vyetu.

Ikiwa utakataa majibu haya maana yake pia ukatae k2amba hata annunaki hajamuumba mtu kwa sababu ingelikuwa tumeumbww na annunaki sisi wote tusingekuwa na utofauti.

Haiwezekani mimi niwe mfupi alafu hashim thabiti awe mrefu wakati sote tumeumbwa na annunaki.

Haiwezekani mimi niwe na macho makubwa alafu jirani yangu awe na macho maduuchu wakati tumeumbwa na annunaki.

Kwa msingi huo mkuu hoja uliyoitumia mkuu unapaswa kuitetea katika hadhra hii.
 
Ukifatilia kwa undani na ukifanya utafiti utaona wazi ya kuwa habari za Annunak zimekuta habari za Adamu tangu zamani ndiyo maana nawauliza wamuanishie mtu wa kwanza kuelezea habari hizo. Suala la Annunaki ni nadharia iliyo pandikizwa ili kuwatoa watu katika dini, sababu habari hizo zimewakuta wanadamu wapo tayari.
Mkuu huu mjadala ni mtamu sana ila kuna watu wanataka kuuharibu kwa kusingizia kwamba sisi wafia dini tumekuja kuleta fujo.

Swali zuri mkuu naomba wakijibu unitag maana nina utitiri wa maswali kuhusu mada hii ila naenda kwa vipengele ili tusiondoe laddha ya mjadala
 
Hii inaonekana ni jamii, kwayo inahitaji maelezo ya kina baadae,swali langu bado hujalijibu. Swali lina taka uanishe ni nani wa kwanza kuelezea habari za Annunaki. Hapo ni sawa na useme Watanzania ni wa kwanza kuelezea jambo fulani, jibu si sahihi sababu haiwezekani kwa wote kuelezea jambo fulani pasi na wa kwanza, kwahiyo swali langu linataka uanishe ni nani wa kwanza kuelezea habari hizo.

Kisha tutarudi kuwajadili hao Sumerians.
Sumerians ni watu kama huyo mtume Muhammed wako, hawa walikuwa wanatunza rekodi na matukio mbali mbali katika lugha yao kwenye tablets, lugha hizo ndizo zinafanyiwa utafiti na kutafsiriwa kwa sababu ndiyo watu wa kwanza kuanzisha civilization. Civilization imeanzia kwao, utaratibu wa maisha tunaoishi leo umeanzia kwao, kwa sababu hizo lazima niwaamini kwa sababu jamii nzima haiwezi kurekodi uongo tofauti na wewe unayeamini masimulizi ya mtu mmoja tu Muhammed. Ni sawa sawa ulinganishe sample ya mtu mmoja kwa samples za watu kumi, sample kubwa itakupa accuracy nzuri, sample moja tu haiwezi kukupa accurate nzuri ya matokeo. Kwa muktadha huo mimi naamini kile kilichosemwa na wengi kwa records, hicho cha Muhammed sikiamini kabisa.
 
Nimecheka sana, mnaposhindwa kujibu maswali mnaanza kurauka. Shida yenu hamna elimu ya uhakiki wa habari.

Alichokiandika mtoa mada kinaingia katika visa vya kubuni ndiyo maana maswali ya msingi ameshindwa kujibu. Laiti kama mngekuwa mna hoji hakuna hata mjinga mmoja angekubali juu ya hizi habari.

Mimi nakuuliza swali hili, katika hao ambao wanatoa habari za Annunaki yupo aliye washuhudia kwa macho ? Hili la kwanza, swali lingine la msingi nimemuuliza mwenzako alichojibu ni kituko, nimemuuliza hivi ni nani wa kwanza kuelezea hizi habari za Annunaki ? Akajibu ni "Sumerians" hapa ameitaja jamii yenye ustaarabu fulani na swali langu hajalijibu, alitakiwa amuanishe aliye eleza habari hizi wa kwanza. Hapa ndipo ukweli ulipo. Mkishindwa kujibu swali hili, ni kuwa habari hizi ni za kutunga.

Sasa kama nyinyi mnafikiria kitoto na amuhoni ni nyinyi sisi tumeshatoka zamani sana katika kubeba beba mambo kishabiki bila kuhoni wala kufanya utafiti.
Unaposema hivyo, basi hata habari zenu za dini ni visa vya kubuni, wewe uliwahi kumuona mtume Muhammed/Yesu?
 
Hii inaonekana ni jamii, kwayo inahitaji maelezo ya kina baadae,swali langu bado hujalijibu. Swali lina taka uanishe ni nani wa kwanza kuelezea habari za Annunaki. Hapo ni sawa na useme Watanzania ni wa kwanza kuelezea jambo fulani, jibu si sahihi sababu haiwezekani kwa wote kuelezea jambo fulani pasi na wa kwanza, kwahiyo swali langu linataka uanishe ni nani wa kwanza kuelezea habari hizo.

Kisha tutarudi kuwajadili hao Sumerians.
hii haina tofauti na mtu akuulize ukristo aliuanzisha Nani, ukategemea atajwe mtu mmoja tu, haiwezekani. Lazima Kuna kamati ilikaa chini
 
Swali langu limeuliza ni nani wa kwanza kuelezea habari hizi. Ukijibu kuwa zimetoka "Babilonia" bado hujajibu swali sababu unazua maswali mengi kuhusu hicho ulichokijibu. Nitakuuliza huko babilonia hizo habari zimekutwa wapi na ushahidi wake ni upi kuonyesha Annunaki ndiyo amewaumba Wanadamu.

Kina nani wanasema au kuamini Mola alijiumba ? Mola yupo wala hajawahi kutokuwepo.

Hayo maandishi yameandikwa na nani ? Usiitaje jamii, katika elimu ya uhakiki wa habari inaonekana kabisa muandishi hajulikani na mtu wa kwanza hajulikani ? Habari yenye sifa hii inataka itiliwe nguvu na habari nyingine isiyo kuwa na shaka kabisa na itoke kwa mtu mwenye kuaminika na mkweli na mwenye kujulikana.

Wewe unaweza kututhibitishia ya kuwa hizo habari zimetoka huko ? Kingine unaijua Babiloni ?

Tafuteni vitabu vya Kamusi ya miji mjue habari za jamii na maeneo yao na sifa zao.

Hakuna kushindana hapa tunaangalia uhalisia, nikuulize tu swali la msingi, unahakiki vipi habari za kale ? Je kwa kuona michoro kwenye mapango ? Wanagapi kwenye mapango wanachora vitu ilimradi tu kufurahisha nafsi zao ?

Akili mmepewa bure ili mzitumie kuutafuta ukweli.

Nimecheka sana, huyi mtoa mada mimi mara ya kwanza nilimpuuza kwa sababu ya kutokujibu maswali, ila nilivyo pita nikaona anajitapa kwamba hawezi kurudia jambo ambalo ameshaliezea na mwingine akawa anamtuhumu kwamba hajibu maswali, nikaamua kutilia mkazo juu ya hili.

Shida yenu mnafikiri kwamba watu wote humu wanapenda stori kama mnavyopenda nyinyi, sisi wengine tuna hoji na kufikiri kwa usahihi.

Hakuna hoja ambayo mtoa mada ameiweka sababu mada yote imemili katka umashaka. Angalia namna ya usimuliaji wa mada yake, utaona "Inasemekana..." mara "Walishuka kutoka sauari nyingine..." ukimuuliza ushahidi uko wapi ? Hana ushahidi je nani aliwaona wakishuka au nani alielezea habari hizi wa kwanza na yeye alizitoa wapi ? Majibu hana.

Anatakiwa yeye kwanza ahakiki alichokiandika na ajibu maswali anayo ulizwa.
Sasa mkuu wewe kupuuza mada si sawa na kudondosha punje moja ya mchele kutoka kwenye gunia la mchele.

Hao hakini mitume unaowataja humu references yao ya kuanzisha hizo dini ni hizo hizo jamii, Hebrews, Jeweish n.k dini zao chimbuko lao ni huko. Kwahiyo mimi nikwambie kama ambavyo huyaamini haya, ila unayaamini ya mtume basi ushajiweka katika namna hiyo.
 
Wapi nimesema au nimeamini Mungu amejitengeza ?

Ninacho amini mimi ni kuwa Mola hajatanguliwa na wakati yeye yupo wala hakuwahi kutokuwepo.

Sasa hili la kujitengeneza unatakiwa utuambie umelitoa wapi ? Usitusemeze maneno.

Mimi swali langu liko pale pale ni nani wa kwanza kuelezea habari za Annunaki ? Je aliwaona hao Annunaki ?
Kwahiyo Mungu wako humjuhi?

Nakujibu tena kwamba ni watu wa kale kutoka sumerians kabla ya mtume Muhammed na Yesu hawajatokea katika huu ulimwengu.
 
Maswali yangu hujajibu kama umejibu maswali yangu, muanishe yule wa kwanza kuelezea habari za Annunaki ni nani ? Usitaje jamii sababu bado tutarudi pale pale kumsaka huyo wa kwanza katika hiyo jamii ni nani ?

Sasa usibishane kwenye hakuna. Muwe mnahakiki hizi habari na kuhoni kwanza kabla hamjaleta humu.

Mimi sina jibu langu ndiyo maana natumia lugha nyepesi sana kuuliza maswali ili lugha isiwe kikwazo, mfano mimi ungeniuliza ni nani wa kwanza kuleta habari za Uislamu mimi ningekujibu kuwa ni "Mtume Muhammad" wala nisingesema n "Waarabu au Maqureishi". Kisha kitokea hapo tunaenda hatua nyingine kwamba je ni kweli Mtume Muhammad ndiyo wa kwanza kuleta habari za Uislamu hivyo mpaka tunapata ukweli wa habari husika.
Ndiyo maana nasema huna majibu yako kichwani.
Eti nisitaje jamii ya watu, really? , yaani unamuamini mtu mmoja kuliko kilichosemwa na wengi?

Mimi ntendelea kutaja hizo jamii kama ndiyo watu wa kwanza kuelezea hizo habari, kabla hata ya mtume Muhammed, yaani huyo kaziliwa kakuta hao wameisha ishi duniani. Kwahiyo kama unataka jina la mtu mmoja, hilo hutalipata kwangu.
 
Nilipoiona hii mada mara ya kwanza nikasema huyu mleta mada naye ni msikiliza ngano na masimulizi yasiyokuwa na uhakika. Kwetu sisi Mungu amejifunua bayana anaishi kwenye maisha yetu vizuri sana. Tunasubiri hadithi zingine za bwana AI
Mungu amejifunua bayana😂😂😂
 
Safi Mkuu. "Nakujibu kwa ufupi sana kwamba hayupo", kwa quote yako hii umenijibu vizuri sana kwamba hakuna kiumbe ambae yupo physical in shape anayeweza kujiunda/kujiumba mwenyewe.

Sasa turudi kwa kiumbe (ANNUNAKI)
Tumeshakubaliana kwamba Annunaki ni kiumbe ambe ni:-
(i) MTU -Anafanana vina saba na binadamu(mimi, wewe na wengine)

(ii) WANAZALIANA- Viumbe hao Annunaki wanaongezeka kwa kualiana.

(iii) WAPO (PHYSICAL IN SHAPE)- Viumbe hao Annunaki wana mwili yaan wapo physical in shape na kwamba unaweza kumuona kwa macho na kumgusa kama binadamu.

(iv) HAWAWEZI KUJIUNDA/KUJIUMBA -Viumbe hao Annunaki hawawezi kujiunda au kujiumbwa wenyewe, kwa sababu ni viumbe kama viumbe wengine walio physical in shape lazima waundwe na muundaji.

Kwa muktadha huo, sasa nakuuliza swali UNAWEZA KUNIAMBIA CHANZO/ MUUNDAJI WA HAO VIUMBE ANNUNAKI? (yaan walitokeaje tokeaje, maana hawawezi kujiunda wenyewe kama ulivyosema)
Wametoka sayari nyingine, Kwahiyo haijulikani ni walijiumba/wamejiumba na hakuna sehemu palipoandikwa wameumbwa na huyo Mungu wenu wa kwenye vitabu vya dini.

Na mimi nikuulize kama una amini hakuna kiumbe anayeweza kujitengeneza, je Mungu ni kiumbe/siyo kiumbe? . Mungu alijiumba mwenyewe au hakujiumba mwenyewe?
 
Mkuu mimi

Mungu mmoja mkuu ni mungu mwenyewe.

Ni sawa na kuulizq magufuli raisi ni nani ?
Jawabu itakuwa magufuli raisi ni magufuli raisi.

Labda useme unataka sifa za ziada ya huyo mhusika,na sifa ziko nyingi sana tu.

Bainisha vizuri swala lako mkuu ili tujue tunajibu unachotaka
Mungu mwenyewe ndiyo nini?, sijakielewa ulichojibu.
 
Ukifatilia kwa undani na ukifanya utafiti utaona wazi ya kuwa habari za Annunak zimekuta habari za Adamu tangu zamani ndiyo maana nawauliza wamuanishie mtu wa kwanza kuelezea habari hizo. Suala la Annunaki ni nadharia iliyo pandikizwa ili kuwatoa watu katika dini, sababu habari hizo zimewakuta wanadamu wapo tayari.
Zimekuta habari za Adam kwa uzibitisho hupi. Unawwza kuniambia imepita miaka mingapi tangia Adam awepo duniani?
 
Kwa hivyo tjkubaliane kwamba habari za annunaki na adamu zote hazina uthibitisho na kila mtu aamini maandiko anayotaka ?
Za Annunaki na Adam zinauzibitisho, ila za Mungu hazina uthibitisho. Hakuna kitu chochote chenye force of manifestation alafu kisi exist katika physical form.

Na nimekuuliza yapita miaka mingapi tangu uwepo wa adam hapa duniani?
 
Back
Top Bottom