Ansbert Gurumo ahoji kwa nini Lissu atumie kibwagizo cha CCM wakati akitangaza kugimbea uenyekiti "tuna imaniii.... na Lissu... Oyaa... "

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Ansbert Ngurumo, moja ya magwiji wa habari na uchambuzi ameonyesha kuwa na mashaka kwamba kwa nini Lissu ameibuka na wimbo wa CCM katika kutangaza nia.

Mwandishi huyo amesema kwamba inawezekana mkutano wa Lissu ulijaa wana CCM waliovalishwa nguo za Chadema, hivyo wakajisahau na kujikuta wanaimba wimbo waliouzoea.

Ansbert Ngurumo amesema ukumbi ulijaa watu ambao sio wana chadema, wala wapiga kura.

Mwenye uwezo wa kupandisha hiyo link tafadhali, ina madini mengi
 
Mengi yatajulikana. Mkutano ule uliandaliwa na Msigwa, kwa hivyo elements za ccm zilijitokeza
 
Huo wimbo ushakuwa common to everyone.
Isiwe mada kuwa ni pro-ccm.
#CRITICAL THINKER.
 
Ni Mpumbavu tu anayeamini Lisu anafadhiliwa na CCM

Freeman Mbowe hajawahi kurudisha KADI ya CCM kama ambavyo Dr Slaa na Mzee Marando hawajawahi kurudisha KADI za CCM

Kinembe wewe bado mtoto mdogo 😄
Yatajulikana tu, ni suala la muda
 
Hiyo kauli ilianza zamani sana kabla ya hata ccm, sema wakaja ku popularize kwa kuitumia wenyewe kwenye mikutano yao kama ilivyo kawaida yao nzuri ya kurithi vitu vizuri tulivyoachiwa na waasisi wa taifa hili

Ni kama upinde tu, chimbuko lake ni zama za kale kutokakwa Mungu mwenyewe tena inamaanisha jambo zuri sana kabla ya mapunga kuiteka na kuifanya yao
 
Nilifuatilia hiyo speech ya Lissu mwanzo hadi mwisho,Walionzisha kuimba huo wimbo ni Wanachama na sio Lissu,Sasa kosa la Lissu ni lipi hapo?
 
Hivi ni kwanini siasa za ki Africa tuna kasumba ya kumuabudu mtu kwamba wenzake au wengine hawawezi kuongoza au taasisi haiwezi kuwepo bila mtu flani ala cha kushangaza huyu mwandishi naye anajiita msomi!!! upuuzi
 
Ni Mpumbavu tu anayeamini Lisu anafadhiliwa na CCM

Freeman Mbowe hajawahi kurudisha KADI ya CCM kama ambavyo Dr Slaa na Mzee Marando hawajawahi kurudisha KADI za CCM

Kinembe wewe bado mtoto mdogo 😄
Maigwa anamuendesha Lissu kama vile drone inavyoendeshwa
 
Kwa mtizamo wangu kuna mmoja hapo anahitaji kugombea urais kwa mara ya pili, na kuna mwingine yeye haitaji kugombea urais bali anataka alete mgombea uraisi atakaye kuwa na mvuto kwa wapiga kura na atakayesaidia chama kupata wabunge wengi maana kwenye nafasi ya urais ni ngumu kwa upinzani kushinda. Yupo mmoja hapo ameshagundua ya kuwa nafasi ya kumbea urasi ni ndogo mno hivyo anaweza kuondoka endapo atakatwa sasa hataki kuondoka kizembe.
 
Nilifuatilia hiyo speech ya Lissu mwanzo hadi mwisho,Walionzisha kuimba huo wimbo ni Wanachama na sio Lissu,Sasa kosa la Lissu ni lipi hapo?
Ukumbi ulijaa wana CCM, na kila jambo halikutokea kwa bahati mbaya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…