Tetesi: Ansbert Ngurumo: Makonda anatafutiwa ubalozi

Tetesi: Ansbert Ngurumo: Makonda anatafutiwa ubalozi

Ni kweli nchi wanaweza kumkataa mtu lakini kuna kigezo gani cha kumkataa Makonda hasa nchi za Africa?
 
Hivi Nchi inaweza mkataa balozi wa Nchi nyingine ambae ni mpya?
Yap. Balozi anaweza kukataliwa na nchi mwenyeji. Sababu mbali mbali hutolewa. Kuna kipindi mkwere alimteua balozi wetu kwenda Rwanda lakini Rwanda wakamkataa. Nasikia mr slim alihisi yule balozi wetu mteule alikuwa ntu wa system!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
C ampeleke Iraq, Syria au Afghanistan???.. Akikosa huko ampeleke hapo kwa ndugu zetu Somalia... Very simple
hahaaa unataka awe kiziwi ". maana masikio lazima yataathirika tu " kutokana na kusikiliza milipuko ya mabomu daily "
 
UBALOZI umegeuzwa jalala Tanzania? JPM anataka kuachana na Makonda, lakini anaogopa kumtumbua ili siri zao zisivuje. Sasa anatafuta pa kumficha nje. Kikwazo ni lugha na rekodi yake mbaya. Nchi 5 zimemkataa. Bado wanabahatisha katika nchi 2 za Afrika zitumiazo Kireno na Kifaransa

Hii itakuwa kutoa/kuanika aibu yako kwa watu wengine. Ataenda kutoa matamko ya ajabu ajabu huko.
 
===
Mmm! unachosema ni moja ya njia lakini si hiyo pekee.
Wewe ulipoteuliwa, haikutangazwa kwanza. Jina lako likapelekwa katika nchi ulikokuwa unapangwa kupelekwa. Nchi hiyo baada ya kufanya vetting ikatoa green light. Ukatangazwa na kuapishwa. Ukaenda na sasa uko huko.

Kuna wanaotangazwa kuwa wameteuliwa lakini wanakaa muda mrefu mpaka nchi husika ziridhie ndipo mabalozi waende. Hata waambata wanakataliwa kama rekodi zao zina matege.
Narudia tena, kuna Sheria na taratibu za Kidiplomasia. Diplomasia sio Siasa.
Wengi wenu humu mnahemka na fukuto la uanaharakati bila kuwa na uelewa wa masuala mengine ya msingi.
Ingekuwa ni rahisi kiasi hicho nina hakika kwa Utukutu na utovu wa nidhamu wa baadhi ya hao "Wakimbizi Uchwara" nina hakika Dr. Slaa angekuwa ni mmoja wa wahanga wa mwanzo kabisa.
 
Huyo jamaa alionyeshwa kwenye news ya TV ya Sweden anaitwa Hashil Seif anafanya kazi kwenye human rights, Aliyeteuliwa nimemsahau jina lakini alikuwa katika Usalama wa Taifa na akitesa watu. Waswedish walimkataa baada ya huyu Hashil kuprotest na kutoa ushahidi wà aliyoyafanya huyo jamaa
Ulisema hili tukio lilitokea enzi za utawala wa Mzee Mwinyi, ndio Maana nikahoji mwaka wa tukio na jina sahihi la huyo Balozi(Usalama wa Taifa mtesa watu) aliyekataliwa kwa shutuma za Utesaji.
Unamjua/kumfahamu Balozi wa Tanzania aliyemaliza muda wake hivi karibuni nchini Canada!? Naomba jibu tafadhali ili tuendelee.
 
Hivi Nchi inaweza mkataa balozi wa Nchi nyingine ambae ni mpya?
Inaweza kulingana na recorde za huyo balozi hata rwanda iliwahi kumkataa balozi wakati wa Jk sababu alikuwa ni mpelelezi nguli na wakati ule hatukuwa poa kimahusiano
 
Mmmh apo Ngurumo kafeli,bashite na ubalozi wapi na wapi.

Huyu tutabananae apa apa mpaka jiwe aondoke
Hawezi kuachwa uraiani apuyange kama sie huyo mkuu,amevuruga watu wengi sana hivyo ni lazima apelekwe sehemu ya mbali ambako bado atakuwa na ulinzi akiwa kama balozi.

Kijana mdogo kabisa alikuwa na nafasi nzuri ya kuwa kiongozi mzuri mbeleni lakini misifa na ulimbukeni wa balehe ya pili plus washauri kina Le Mutuz,Muro,Musiba duh!mbombo ngafu
 
UBALOZI umegeuzwa jalala Tanzania? JPM anataka kuachana na Makonda, lakini anaogopa kumtumbua ili siri zao zisivuje. Sasa anatafuta pa kumficha nje. Kikwazo ni lugha na rekodi yake mbaya. Nchi 5 zimemkataa. Bado wanabahatisha katika nchi 2 za Afrika zitumiazo Kireno na Kifaransa
Zitaje hizo nchi,lugha sio kikwazo acha uongo,kwani kuna lugha ya mabalozi,kuna mabalozi kibao wanaongea lugha za kwao tu
 
UBALOZI umegeuzwa jalala Tanzania? JPM anataka kuachana na Makonda, lakini anaogopa kumtumbua ili siri zao zisivuje. Sasa anatafuta pa kumficha nje. Kikwazo ni lugha na rekodi yake mbaya. Nchi 5 zimemkataa. Bado wanabahatisha katika nchi 2 za Afrika zitumiazo Kireno na Kifaransa
Apelekwe Korea Kaskazini kwa mzee Mapanki.
Kwa Makonda huko ni ithibati tosha.
 
Back
Top Bottom