Kipangaspecial
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 20,778
- 28,722
Nyinyi wananchi mlikubali vipi muongozwe na kichaa, au na nyinyi ni vichaa?Jeshi? Litafanya nini wakati huyo kichaa ndio alikuwa amiri jeshi mkuu?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nyinyi wananchi mlikubali vipi muongozwe na kichaa, au na nyinyi ni vichaa?Jeshi? Litafanya nini wakati huyo kichaa ndio alikuwa amiri jeshi mkuu?
IGP Mahita alikomaliwa na Wabunge aombe radhi akasema;Ni
Ni hadi uwe na akili Ili kumuelewa
Hiki ni kipindi cha kila mtu kutaka kujulikana kwamba ni shujaa, hata kama ni kwa sababu za kuipuuzi.
Naagalia maelezo ya Diallo, ni wazi kwamba hajitambui nafasi yake na hatambui matokeo na maelezo yake.
Kwa kiasi kikubwa ni elimu ndogo aliyonayo ambayo haikuongezeka kwa miaka yote aliyoacha kazi yake ya RMA na kujiita daktari.
Kama kweli alijitoa muhanga bila kujali nafasi yake, iweje siku moja tu unaomba radhi? Hii ni kutaka kujinyonga, kitendo ambacho ni cha kipuuzi, halafu pia ukashindwa kuchagua tawi zuri au kamba imara ya kukamata shingo yako, ambao ni upuuzi wa juu zaidi.
Kwa mtindo huu CCM bado muna mbumbumbu wengi tu!
Diallo asiye na tatizo la akili ameifanyia nini nchi hii?Kilicho muhimu ni kwamba Diallo ameuelezea utawala wa awamu iliyopita katika uhalisia wake.
Tatizo la afya ya akili ya marehemu ni dhahiri, na wengi walikuwa wanajua. Juu ya yeye kutibiwa Mirembe na Ujerumani, inafahamika. Lakini kwaajili ya heshima ya mgonjwa, miiko ya kitabibu inasema ugonjwa ni siri ya mgonjwa. Hata hivyo illikuwa siyo sahihi mtu mnayefahamu ana tatizo linaloweza kuleta madhara makubwa kwa Taifa na wananchi, mkampa nafasi ya uongozi wa juu kabisa.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza, bwana Anthony Diallo amewaomba radhi watanzania kwa kauli zake alizozitoa kuwa viongozi wa Serikali waliopita walikuwa na mafaili mirembe.
View attachment 1849688
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Mwanza, Dk. Anthony Diallo ameomba radhi ‘kiaina’ baada ya kauli yake kuzua mjadala ndani na nje ya chama chake.
Dk. Diallo amesema, ametafasiriwa vibaya na baadhi ya watu huku akiwataka wanachama wa chama hicho tawala nchini Tanzania kuwa makini kwani wapo wasiowatakia mema wanatumia mwanya huo kuwachonganisha.
Ni baada ya jana Jumamosi, tarehe 10 Julai 2021, kuzungumza masuala mbalimbali yaliyojitokeza katika utawala wa awamu ya tano akigusia suala la nchi kuongozwa kwa matamko.
Dk. Diallo aliyewahi kuwa waziri, alizungumza hayo katika kipindi cha Ajenda, kinachorushwa na kituo chake cha televisheni cha Star TV, jijini Mwanza.
Akijibu swali la mwandishi wa habari aliyetaka kupata maoni yake juu ya nchi kuongozwa kwa matamko bila kufuata Katiba na sheria, Dk. Diallo alisema, kuna umuhimu wa kuangalia historia ya mtu kabla ya kupewa dhamana ya kuongoza.
Mimi nafikiri tuwe waangalifu tu katika kuchagua tuwe tuna ‘track record’ kwani huko nyuma tuliwahi kuchagua watu walikwisha kwenda hospitali za vichaa ‘milembe’ harafu unamwachia aongoze nchi, kwa hiyo tuwe makini,” alisema.
Kauli hiyo ilizua mjadala na leo Jumapili, tarehe 11 Julai 2021, akizungumza na waandishi wa habari amesema “nilifanya kosa kwa kutolea mfano wa wakati uliopita badala ya wakati ujao kuwa tusipokuwa waangalifu tunaweza kuchagua viongozi wenye matatizo ya akili.”
Na sijasema mtu kuwa aliyekuwa na tatizo ila nilikosea tu kwenye maelezo. Nawataka radhi wale ambao walinielewa vibaya kwani wapo waliotafasiri wanavyojua wao,” amesema Dk. Diallo.
Mwanasiasa huyo mkongwe nchini amsema “mimi nadhani tuwe waangalifu sana hasa wana CCM, tumeanza kuingiliwa sana.”
Dk. Diallo amekosoa kitendo cha baadhi ya viongozi wa chama hicho kuanza kutoa matamko kabla ya kumsikiliza au kumuuliza alikuwa ana maanisha nini.
“Unakuta ni kiongozi wa chama anatoa tamko na kunituhumu kama vile nimefanya kosa, bila hata kuniuliza. Lazima tuwe waangalifu sana wana CCM,” amesema Dk. Diallo.
Miongoni mwa viongozi waliomshtumu ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM), Kenani Kihongosi alisema, viongozi walioaminiwa na “chama chetu, na wanakaa katika vikao vya maamuzi, tunawaomba wawe na nidhamu na chama hiki.”
“Chama hiki ni kikubwa kuliko mtu, kwa hiyo mwenyekiti na katibu mkuu wetu, niwaombe sisi kama UVCCM, kauli ile imetuudhi sana, mwenyekiti wa CCM anapozungumza hivyo hapaswi kuungwa mkono.”
Kihongosi aliongeza kwa kusema “kama yeye aliona wanapaswa kwenda milembe hapa anafanya nini, kama ni vikao vya maamuzi yeye ni miongoni na kauli zile kama sisi vijana zinatuvunja moyo.”
Mwanahalisi
Diallo na watu wa aina yake ni WANAFIKI, hizi kelele ni baada ya maslahi yake kuguswa, na kwa hakika hautasikia akisema lolote baya likifanywa na chama chake na Serikali inayoongozwa na chama chake.Ujumbe wa Dr. Diallo umenyooka kama rula. Ni nadra sana kwa wana CCM kuziishi ahadi zao za nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko kama alivyofanya Dr. Diallo. Tumpongeze kwa hili.
Nimeona hapo juu mmoja kaandika kuwa ni RMA lkn akajiita daktari.Hivi ni doctor wa kitu gani huyu shujaa wetu mpya aliyeuzungumza ukweli wa lile sanamu la chato kuwa na valid certificate ya uwendawazimu
Hata mrembe vipi sisi tunajua message sent and delivered! Hata chizi Magufuli alikuwa anasema hivi hivi message sent and delivered!MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Mwanza, Dk. Anthony Diallo ameomba radhi ‘kiaina’ baada ya kauli yake kuzua mjadala ndani na nje ya chama chake.
Dk. Diallo amesema, ametafasiriwa vibaya na baadhi ya watu huku akiwataka wanachama wa chama hicho tawala nchini Tanzania kuwa makini kwani wapo wasiowatakia mema wanatumia mwanya huo kuwachonganisha.
Ni baada ya jana Jumamosi, tarehe 10 Julai 2021, kuzungumza masuala mbalimbali yaliyojitokeza katika utawala wa awamu ya tano akigusia suala la nchi kuongozwa kwa matamko.
Dk. Diallo aliyewahi kuwa waziri, alizungumza hayo katika kipindi cha Ajenda, kinachorushwa na kituo chake cha televisheni cha Star TV, jijini Mwanza.
Akijibu swali la mwandishi wa habari aliyetaka kupata maoni yake juu ya nchi kuongozwa kwa matamko bila kufuata Katiba na sheria, Dk. Diallo alisema, kuna umuhimu wa kuangalia historia ya mtu kabla ya kupewa dhamana ya kuongoza.
“Mimi nafikiri tuwe waangalifu tu katika kuchagua tuwe tuna ‘track record’ kwani huko nyuma tuliwahi kuchagua watu walikwisha kwenda hospitali za vichaa ‘milembe’ harafu unamwachia aongoze nchi, kwa hiyo tuwe makini,” alisema.
Kauli hiyo ilizua mjadala na leo Jumapili, tarehe 11 Julai 2021, akizungumza na waandishi wa habari amesema “nilifanya kosa kwa kutolea mfano wa wakati uliopita badala ya wakati ujao kuwa tusipokuwa waangalifu tunaweza kuchagua viongozi wenye matatizo ya akili.”
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM), Kenani Kihongosi
“Na sijasema mtu kuwa aliyekuwa na tatizo ila nilikosea tu kwenye maelezo. Nawataka radhi wale ambao walinielewa vibaya kwani wapo waliotafasiri wanavyojua wao,” amesema Dk. Diallo.
Mwanasiasa huyo mkongwe nchini amsema “mimi nadhani tuwe waangalifu sana hasa wana CCM, tumeanza kuingiliwa sana.”
Dk. Diallo amekosoa kitendo cha baadhi ya viongozi wa chama hicho kuanza kutoa matamko kabla ya kumsikiliza au kumuuliza alikuwa ana maanisha nini.
“Unakuta ni kiongozi wa chama anatoa tamko na kunituhumu kama vile nimefanya kosa, bila hata kuniuliza. Lazima tuwe waangalifu sana wana CCM,” amesema Dk. Diallo.
Miongoni mwa viongozi waliomshtumu ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM), Kenani Kihongosi alisema, viongozi walioaminiwa na “chama chetu, na wanakaa katika vikao vya maamuzi, tunawaomba wawe na nidhamu na chama hiki.”
“Chama hiki ni kikubwa kuliko mtu, kwa hiyo mwenyekiti na katibu mkuu wetu, niwaombe sisi kama UVCCM, kauli ile imetuudhi sana, mwenyekiti wa CCM anapozungumza hivyo hapaswi kuungwa mkono.”
Kihongosi aliongeza kwa kusema “kama yeye aliona wanapaswa kwenda milembe hapa anafanya nini, kama ni vikao vya maamuzi yeye ni miongoni na kauli zile kama sisi vijana zinatuvunja moyo.”
Chanzo: Mwanahalisi
---
Japokuwa ameomba msamaha, Dkt. Diallo asisamehewe na apewe adhabu kubwa ili iwe fundisho.
Amejua kuwa alifanya fyongo na kuongea pumba. Ili iwe fundisho kwa wanafiki kama Diallo apewe adhabu kali na kutimuliwa kabisa.
Hiki ni kipindi cha kila mtu kutaka kujulikana kwamba ni shujaa, hata kama ni kwa sababu za kuipuuzi.
Naagalia maelezo ya Diallo, ni wazi kwamba hajitambui nafasi yake na hatambui matokeo na maelezo yake...
Na Ndugai aliye na file Mirembe ajiuzulu pia!Ajiuzulu uenyekiti wa mkoa!
Hapo hajaomba radhi bali amesisitiza!
Hakuna jambo linanikera kama hili, CCM ndio wanapiga ngoma CDM wanacheza tena kwenye mambo ya kitoto sana, Mambo ya msingi yote yanakosa mwendelezo na kufa kimyakimya.Cdm mmebaki kuwa wacheza Ngoma za ccm tu kwa sasa, hakuna operation haki, maandamano Wala wabunge wa covid 19, kila sehemu mnaangukia pua.
Mchukueni sasa huyo Dialo wenu
Wanachofanya CCM ni damage control,kumlazimisha mwanaume aombe radhi,lakini jini limeishatoka kwenye chupa.😂 neno likisha chomoka halirudishiki mdomooni pinda mugongo pinda mugongo pinda muugongo🕺
Mkuu kwani CCM kuna anaye sema ukweli?Apewe adhabu kwa kuongea ukweli? Nchi ilitekwa na kichaa kwa muda wa miaka 5+
... Mahakama ya mafisadi si ipo? Mnasubiri ni kumfungulia mashtaka? Ufisadi wake umeonekana leo? Mwenyekiti wa CCM mkoa tena mkoa muhimu kiuchumi ujue. Mna ndimi elfu enyi wanafiki.Mkwepa Kodi aliyenyooka?
Kweli tatizo ni sisi