ANUNNAKI: Nadharia za Mungu, miungu, fumbo la sciencenscience na Teknolojia kubwa katika Dunia ya kale, kuanguka Kwa civilization na kuinuka Tena

Kumwabudu Mungu maana yake nini?
 
Jamaa wamesoma hizo ngano na hekaya za sumeria wamekuwa brainwashed ile mbaya hakuna kitu wameelewa kwenye hizo story bado wadogo sana wanao muda wa kutafiti na kutafakari ipo hatua watajua ukweli na nuru ya Mungu muumbaji wataiona.
Hawajaelewa vizuri hizo kazi za sumeria na wala hawajaelewa vizuri historia nzima ya biblia na hata dini zingine.

Hawajui chanzo cha maisha ni nini? Ni wamejipata tu kuwa wana akili saana kuliko binaadamu wote wanaoamini uwepo wa Mungu walikuwepo kina mtume Paul walikuwa wabishi tena wasomi na wenye kufikiria kwa kina kuliko,lakini mwisho wake walikiri tu uwepo wa Mungu.

Muda ni mwalimu mzuri.

Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
 
Kumwabudu Mungu maana yake nini?
Ipo hivii; Kumpenda Mungu, kumuabudu Mungu kunapatikanaje? ''Mkinipenda mtazishika amri zangu''; kumuabudu Mungu kwa kweli ni kuyatenda mapenzi yake, mapenzi yake ni sisi tupendane na kutumikiana tukitambuana kama ndugu na tukimtambua kama Baba Yetu.

Ndiyo maana hata hiyo juu ikaitwa ni amri/kanuni kuu, na kimsingi ni hiyo ni moja hata kama unaona wamesema ya kwanza ni hii na ya pili ni hii usibabaike.
 
Hahaaahhaahah pale akili ndogo inapojudge mambo magumu,nilitegemea utakuja na fact kukanusha madai ya Accient civilization kupitia maandiko ya Sumeria ila umeshindwa unaishia kubabaika tu nikikuuliza tablet Gani ya Wasumeria ambayo haijaelezea the begging of life Katika Dunia hasa kumhusu Mwanadamu na Mtu wa kwanza?
Hizo Sumerian tablets umewahi zisoma kamanda au unabisha kitu ambacho hata huna idea nacho kama ilivyo kawaida ya Waafrika wengi wa dizaini Yako?

Kingine Broo ngoja nikuchane Hiyo Elimu tu ya kuhusu hizi Dini za Abrahamic naijua nje ndani,na Tena nilikua muumini kindaki ndaki yaani kiufupi theolojia hainipigi chenga kiasi kwamba hata nikikutana na askofu wako tutashare glass ya champagne vizuri tu,
Halafu kingine watu kama nyie hua ni watetea Dini msiokua na ufahamu wowote zaidi ya kukariri bible verses mkijiona mnajua sana kuliko wengine,
Trust me Broo Kwa Elimu na ufahamu nilionao kuhusu Dini hasa ya ukristo nauwezo wa kujiita mtume na Nabii na nikakufanyia ushawishi ukaja nikupige sadaka,

Usione tunatoa hizi Elimu ukadhani tumepagawa na mapepo la hasha tunaujua ukweli mchungu ambao hampendi kuusikia ila Kwa maslahi na agenda ya kikundi Cha watu wachache endelea kuhadaiwa!

Karibu!
 
Hahaaahhaahah pale akili ndogo inapojudge mambo magumu,nilitegemea utakuja na fact kukanusha madai ya Accient civilization kupitia maandiko ya Sumeria ila umeshindwa unaishia kubabaika tu nikikuuliza tablet Gani ya Wasumeria ambayo haijaelezea the begging of life Katika Dunia hasa kumhusu Mwanadamu na Mtu wa kwanza?
Hizo Sumerian tablets umewahi zisoma kamanda au unabisha kitu ambacho hata huna idea nacho kama ilivyo kawaida ya Waafrika wengi wa dizaini Yako?

Kingine Broo ngoja nikuchane Hiyo Elimu tu ya kuhusu hizi Dini za Abrahamic naijua nje ndani,na Tena nilikua muumini kindaki ndaki yaani kiufupi theolojia hainipigi chenga kiasi kwamba hata nikikutana na askofu wako tutashare glass ya champagne vizuri tu,
Halafu kingine watu kama nyie hua ni watetea Dini msiokua na ufahamu wowote zaidi ya kukariri bible verses mkijiona mnajua sana kuliko wengine,
Trust me Broo Kwa Elimu na ufahamu nilionao kuhusu Dini hasa ya ukristo nauwezo wa kujiita mtume na Nabii na nikakufanyia ushawishi ukaja nikupige sadaka,

Usione tunatoa hizi Elimu ukadhani tumepagawa na mapepo la hasha tunaujua ukweli mchungu ambao hampendi kuusikia ila Kwa maslahi ya kikundi Cha
Inaonesha una upeo mdogo wa akili na kuchanganua mambo na Tatizo nilionalo kwako ni Mtu ambaye hutumii mantiki kureson baadhi ya mambo,
Kitu ambacho nilisisitiza Toka mwanzo ni kwamba Habari za Annunaki na Accient civilization hayahusiani na Imani na hata wao ANNUNAK hawakujiona ni Miungu ila Hiyo ilichangiwa na binadamu waliowafanya kuwaona na kuwapa title ya MUNGU/Miungu na ndio nadharia za Dini zikazaliwa,
Upo too imational kuhusu hii mada sababu Toka Mwanzo nakuambia Maswala hayo waanzilishi ni wao na wao sio MUNGU Kwa nadharia za watu wa Dini Bali Kwa nadharia tofauti Sana na mnavyochukulia
Mpaka hapa Sina msaada na wewe mwenye kuelewa na aelewe!
 
unazidi nichanganya Aisee baba wa mbinguni ndie nani?
Kutoka 3:15
15 Tena Mungu akamwambia Musa:
“Hivi ndivyo unavyopaswa kuwaambia Waisraeli, ‘Yehova Mungu wa mababu zenu, Mungu wa Abrahamu,a Mungu wa Isaka,b na Mungu wa Yakobo,amenituma kwenu.’ Hilo ndilo jina langu milele,d na hivyo ndivyo ninavyopaswa kukumbukwa kizazi baada ya kizazi.
 
Asante sana Dumas the terrible, kiukweli many facts & theories kuhusu Annunaki tumejadili sana humu, lakini kwa muendelezo huu watizidi kujifunza zaidi.


Tatizo linalotukumba sisi katika suala la kuamini ni Imani katika dini, Unapotaka kuelewa dini na imani yake inakuhitaji uende extra miles kwa kufuatilia historia yake(encyclopedia of religions) hapa utaelewa dhima nzima ya dini na imani yake katika ulimwengu, hii itakufanya usione ugumu wowote kuamini habari kama hizi za Annunaki.

 
Akuna kitu kama hicho watu
Mnapaswa kuwa Na fikiria kwanza
Mnaposema mwanadamu aliumbwa Na anunaki kwasababu ya kuchimba zahabu
Duniani
Hizo zahabu zilitengenezwa Nanani au ziliumbwa Nanani? Au dunia kipindi icho iliumbwa Nanani ?

Acheni Zarau bwana anunaki sio kitu ni michoro tu
 
ANNUNAK hawakujiona ni Miungu ila Hiyo ilichangiwa na binadamu waliowafanya kuwaona na kuwapa title ya MUNGU/Miungu na ndio nadharia za Dini zikazaliwa,
Upo too imational kuhusu hii mada
Nikisema binadamu waliwapa tittle ya umungu Kwa sababu tangu mwanzo walikuwa na notion za mungu vichwani mwao?. Kwa maana ya kwamba idea ya mungu ilikuwepo kabla hata ya kuja kwa anunaki utakubali? Hata kama ilikuwepo ilikuwa katika sura tofauti.

Nipo too emotional😂🤣🤣, duuh!. Binafsi natamani tuliapproach jambo hili logically ndio maana nikakuomba unitajie lengo la sisi kuwepo ili tuifuatilie logic yake. Nikajua hata utaniambia 'furaha' wewe ukasema kuchimba dhahabu!! Tukaifuata hiyo logic hadi kutafuta pesa/mali ukaonesha mwenyewe how ridiculous that idea is🤦‍♂️

Sasa naomba jibu la lengo la kuwepo kwetu huku duniani, au basi niambie kuwa hujui nikuache unatafuta lengo kwanza ndio tuje tujenge logic kutokana na utakachokichagua. Tafsiri kwanza [a worthy] lengo au kusudi halafu tujadili
 
Je, siwezi nikafanya hayo huku nikiwa atheist?
 
Mkuu hapa safuher kasema kua hoja ya kua sumeria ni watu wa zamani ama maandishi yao ni ya muda mrefu sio hoja kua ni lazima yawe ya kweli 100%.

Ujue hata sie kuna vizazi vitakuja miaka maelfu ijayo, je kisa kuna bible & quran basi wategemee hayo tu kua ni maandishi ya kweli ya kizazi hiki kisa tu ni ya zamani??
Vipi kama hao Sumeria pia walikua na migongano kimawazo kama sasa?? Na hayo mawazo ya sumeria baadhi yakawa si sahihi.?
 
Je, siwezi nikafanya hayo huku nikiwa atheist?
Swali zuri mno, limekuja kama sapraizi asee! kimsingi naona kama unaweza. Inawezekana. Huwa sipingagi ukweli eti kisa nipinge tu. Naona uwezekano wa kufanya hivyo ukiwa atheist upo. Sema utahitaji uujue uzuri na ubaya ili kuweza, utenganishe ukweli na uongo, sense na not sense.

Sema swali labda linakuwa ni nini kitakusukuma kufanya hivyo. Nini kitakuwa kipimo cha huo wema kwa ndugu/jirani. Nisaidie kuelewa hapo
 
kumbuka Sumeria waliabudu miungu inayoonekana Kwa macho Yao
Hata leo wabo baadhi ya watu wanaabudu ng'ombe ambao wanawaona kwa macho.

Wapo watu wanaabudu masanamu ambayo wanayaona kwa macho.

So sumerian kuabudu vitu wanavyoviona kwa macho sio hoja ya msingi.
Wasumeria sio wendawazimu kiasi hicho watunge uongo na kuandika kwenye clay
Je Annunaki waliwaagiza au kuwaamrisha wasumeria wawaabudie wao annunaki ?

Ama sumeria waliamua tu wenyewe kuwafanya hao majitu kuwa ndio miungu iliyotoka juu na wala annunaki hawakuagiza wafanywe miungu ?

Dumas the terrible
 
Karibu mkuu wangu Artificial intelligence katika makala hii tuendeleze mjadala nimefurahi Sana ujio wako hapa!
 
life code alisepaga kwa mijitu mijinga kuja na maubishi ivi ivii hivi kwann mtu unakuwa mbishi kujifunza mpka ubishanee??!!!!
 
Wewe Ndie umetaja Hilo jina la Mungu wa Israelites Kuna member humu wakuitwa Uhakika Broo alidai Mungu Hana jina na wewe Hapo umemtaja Yehova Na ndio maana nikamuuliza hilo swali!
 
Dogo tena wewe dogo sana jipe moyo kuwa unajua Sanaa hizo tablets uje juzi tu hapa duniani alafu unadai kuwa unajua teolojia kuliko askofu wangu,unaweza kuchukua sadaka yangu au pesa yangu.

Kweli utandawazi na uhuru wa kufikiria,nakupa tu pole nenda kajifunze tena dogo hujaelewa chochote cha msingi ndani ya hizo hekaya za sumeria na hujui chochote kuhusu dini yoyote.
By the way huna uwezo wa kufikiria,nilichoona kwako unaweza tu kuhifadhi data nyingi ulizosoma kutoka vitabu mbalimbali ila uwezo wa kufikiria huna na sikia dogo nina uhakika hayo umeyameza kama yalivyo na utakaa nayo kama yalivyo hayana maana kwako wala kwa jamii yako.

Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
 
Dogo wewe ndio hutumii akili nadhani unakurupuka sana ukishasema Mungu tu maana yake ni imani tayari,basi jaribu hata kuwa na akili hata za kuvukia barabara.
Ndio maana hapo mwanzo nishakuambia hii mada unaleta unajichanganya wewe mwenyewe ni kama jambo unalolijua wewe mwenyewe umejiaminisha ni kweli basi akili yako ndogo imelinasa kama sumaku unashindwa kutetea hoja zako.

Anza mwanzo nenda mpaka kwenye lengo lako unazunguka zunguka sana,mara haihusu watu wa dini kama haihusu watu wa dini Abraham na dini yake wanaingiaje hapa.

Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…