Arusha: Makada 5 wa CHADEMA wakamatwa wakidaiwa kuingilia mifumo ya mawasiliano ya kibenki ili kuiba fedha kwa ajili ya Uchaguzi

Arusha: Makada 5 wa CHADEMA wakamatwa wakidaiwa kuingilia mifumo ya mawasiliano ya kibenki ili kuiba fedha kwa ajili ya Uchaguzi

Wale waangalia series tushazoea haya mambo ya kubanbikiwa kesi afu baadae unatishiwa useme ni mtu fulani kakutuma
 
Sarakasi mpya imeanza. Kesho utasikia wana kosa tofauti kabisa. Usije ukakuta kinachotafutwa ni CDM wamejipanga vipi kwenye uchaguzi huu huko Arusha (Simu, computers na nyaraka). Kwenye hiyo list sioni mbobezi hata mmoja wa Compuer science au IT au kitu kama hicho. Tusubiri.
Eti mpiga debe mzoefu adukue taarifa za kibenk, tunaustahiri umaskini tunaouishi
 
Wewe
Uwezekano wa Mwana CHADEMA Kuwa Muhalifu Ni Mkubwa Sana
Wewe unaweza kujituhumu kuiba penzi kwa Mme wako, au mke wako?
Lakini ukiona mtu anamnyemelea si lazima umuchunguze?
Chadema ndi wanafanya kila njia kuingia madarakani, lakini CCM wao wana hayo madaraka tayari,
Sasa wajikague kwa lipi?
 
Yaani tayari Polisi wameshagundua lengo la kuiba pesa ni kwa ajili ya kampeni?
 
Kamanda Hamduni upo duni kweli, unakubali kuharibu image ya jeshi la polisi kubambika watu kesi ya jinai!? Kuingilia mifumo ya kibenki ni kosa la uhujumu uchumi.
Kwanini unakataa siyo uhujumu uchumi? Tusaidie wewe mwanasheria nguri?
 
Marehemu Sitta aliziita siasa za maji taka. Kule Singida mgombea wa ubunge wa CHADEMA alivamiwa usiku nyumbani kwake na kupigwa eti kwa vile kulikuwa na silaha nnyumbani kwake. Alipopekuliwa, wakamkuta na kisu na panga nyumbani kwake. Wakamkata na kumpeleka kituoni kwa kukutwa na kisu na panga nyumbani kwake! bi siasa za maji taka kweli kweli.
Umenikumbusha aisee,hiyo ishu ya Dada rehema wa singida niliifungulia Uzi hapa modes wakauzuia hadi leo
 
Eti mpiga debe mzoefu adukue taarifa za kibenk, tunaustahiri umaskini tunaouishi
Inaweza ikawa kweli kijana kasoma IT hawataki kumwajiri,basi mchana anaenda kupiga debe ,usiku anaingia mtandaoni kupiga freelancer,
Ila hapo mlengwa ni mdogo ake Lema
 

1602280845122.png


Michango imekwama!


1602280970476.png
 
Polisi wa arusha mtakuwa pia mlihusika kuchoma moto zile ofisi za chadema arusha.
 
Hiyo ni sehemu ya kazi ya jeshi la police - hata hivyo police inabidi wajiepushe na uwezekano wa kutafsiriwa vibaya hasa kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi

Aidha, wananchi endeleeni kuwa watulivu sababu Tanzania ni moja tu na Mungu alitukirimia nchi hii kwa sababu maalum
 
Makada watano CHADEMA mbaroni kwa tuhuma za makosa mtandaoni

Katika taarifa yake, RPC Kamanda Hamduni, alisema Jeshi la Polisi halijihusishi na siasa na kwamba wajibu wa jeshi hilo umeelezwa kwenye katiba.
Chanzo: IPP Media
Huyu Kamanda Hamduni ni RPC na wakati anadai hivyo angalia huyu OCD wake anavyomfokea Mh. Mbowe...

Huku ni kuchanganyikiwa...​
 
Vilevile, wanatuhumiwa kuendesha mafunzo batili yanayolenga kutenda uhalifu wa kijinai katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 28 mwaka

Hii plot wanayodai Polisi inafaa iingie Hollywood na ktk novel za dizaini ya Carlos the Jackal Muere “el maestro de los espías” francés que arrestó al terrorista Carlos na The Day of the Jackal. Ni makundi ya kigaidi tu ndiyo yanayoweza kupanga mpango kama huu unaodai wa kuvunja au kuingilia mifumo ya kibenki ili kuweza kufadhili operesheni maalum. Chama cha kisiasa kama CHADEMA hakina uwezo, utaalamu wala rasilimali watu wakuweza kufikia hata kuwaza kutafuta fedha namna hiyo.
day-of-the-jackal-lead.jpg


It is cold at 6:40 in the morning of a March day in Paris, and seems even colder when a man is about to be executed by firing
 
Duuh jamaa haachi asili yake aisee, ila kaadvance toka kwenye magari mpaka kwenye benki.
 
Back
Top Bottom