mguu ndama
JF-Expert Member
- Mar 29, 2017
- 263
- 121
Acha utoto umri huu utakuwa lini?Acha anyooshwe maana wakiambiwa kwa maneno hawasikii
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Acha utoto umri huu utakuwa lini?Acha anyooshwe maana wakiambiwa kwa maneno hawasikii
Umeishia kidato gani umesoma kweli wewe au ni kilaza?Kama ndo waandishi hawa hawa wachochezi inatakiwa wapigwe na viboko kabisa...alafu walale central wiki mbili wakila pumba na maji...hakuna kulemba hapa kazi tuuuuuuuuuuuuuuuuu
Nakumbuka kipindi Maghuful amemaliza kuwapisha Wakuu wa mikoa na Wilaya,alisema 'mna uwezo wa kumuweka yeyote ndani',hii kauli ilinishtua na kubaki najiuliza kulikuwa na muhimu gani? kulisema hil,sasa ndiyo nimeanza kuona kusudio lake
BOTTOMLINE NI KUWA BASHITE DAUDI NA MRISHO GAMBO WALIWEKWA WALIPO MAKUSUDI KUVURUGA AMANI, VYAMA VYA WAPINZANI. THERE IS NO DOUBT ALIYEWAWEKA ANAWAJIBIKA NAO, FULLY INFORMED WANACHOKIFANYA, KWA BARAKA ZAKE.
A daylight robbery. Pesa zitolewe uraiani ambako ni salama halafu zipelekwe kwa mGambo? Haikubaliki kabisa hata ukitumia MAGAZIJUTO [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]Hawajachiwa.Dhamana ilikuwa wazi kama pale pesa zingepelekwa kwa Gambo.
Kule hawana siasa za kitoto kama za lema ulishawasikia wakitukana mkuu wa wilaya au mkoa kule wanajielewa.Lema ni tatizoArusha wanapelekwa pelekwa kama watoto na huyo boya.....huo upuuzi aupeleke mwanza au mbeya akaone moto.
Ndiyo, sii umeona kwa Nape? Pamoja na yote aliyowafanyia katolewa bastola hadharani. Malima kataka kucharazwa shaba SAA sita mchana! Bado tutasikia mengi tuu, Mwigulu atwangwa rungu la kichwa na Green guard, yule aliyechapwa fimbo na Ndugai alipa kisasi, Makonda achapwa makonde na Wassira Lumumba nk nk.Utawala wa chuki na visasi wakimaliza na Upinzani itaendelea na wanaccm wenzake.Alisema JKN ubaguzi ni kama kula nyama ya mtu haiishi.
Wamesahau Chuki hujenga utengamano.Kesho sijui watamlaumu nani.
Ungesema hawana siasa za kitoto kama za Gambo, kwani lema ndio kawakamata watoa rambi rambi we bata maji?Kule hawana siasa za kitoto kama za lema ulishawasikia wakitukana mkuu wa wilaya au mkoa kule wanajielewa.Lema ni tatizo
Hapana siamini kwamba Mh. Rais hua anamtuma kiongozi kila kitu anachotakiwa kufanya.
Mh. Rais hawezi kufuatilia mambo Madogo kama misiba na nani atoe rambi rambi na amkabidhi nani?
Kwa kumwangalia tu yule mkuu wa mkoa kisaikolojia na hata maumbile ya sura yake tu sio mtu mwenye busara wala hekima.
Ni aina fulani ya watu wenye wivu ,chuki na roho mbaya.
Ndio maana Mwenyezi Mungu aliweka sheria na hukumu zake. Alijua wazi kuwa akimwachia Mtu kazi ya kutoa hukumu ya haki bila kumwekea sheria na utaratibu wa kufuata patakua na kuonewa , chuki ,ubinafsi, majivuno ,kujikweza na upendeleo.
Ifikie mahali viongozi wa dini na watu waliolitumikia taifa hili kwa Muda Mrefu kwa uadilifu waseme jambo. Hawa vijana wanaoparamia madaraka kwa kutumia nguvu na kuwadhalilisha wengine ili kujijenga kisiasa hawafai kabisa kutuunganiasha na kutuletea maendeleo.
Hivi huu mkoa wa Arusha hakuna kazi ya kufanya kwa nafasi ya mkuu wa mkoa zaidi ya siasa ?
Hivi mkoa wa Arusha ni pale mjini tu kwenye jimbo la Mh. Lema?
Mbona huko Longido,Loliondo na kwingineko wananchi wanaishi kama wanyama wa porini kwa umaskini na kukosa maji, miundo mbinu duni n.k?
Kwa nini mkuu wa mkoa anaonekana kukimbizana na viongozi wenzake waliochaguliwa na wananchi Kikatiba?
Hivi Meya wa jiji hawezi kumtembelea mfiwa na kutoa rambi rambi?
Nawashangaa wanaosema Eti suala la msiba lisiwe la kisiasa!!
Aibu kubwa kwa anayesema hivyo mana msiba ule ulishaitwa wa kitaifa na tuliona walioendesha shughuli ya kuwaaga marehemu walikua ni wanasiasa. Wanasiasa pia ni sehemu ya watu wa Taifa hili tena kwa mfano Meya na mbunge ni wanasiasa na wawakilishi wa wananchi. Mkuu wa mkoa ni mwanasiasa na meya ni mwanasiasa.Wote kwa pamoja ndio wanaofanya msiba uitwe wa kitaifa mana unawaunganisha watu wa itikadi mbali mbali.
Kwenye msiba akienda mwanasiasa atazungumza kisiasa na akienda mtu wa dini anazungumza kidini.
Mkuu wa mkoa na Meya wote wana majukumu kikatiba na kisheria. Hakuna haja ya kuvutana wakati hakuna hatari yoyote au uvunjifu wa amani au uasi uliofanyika.
Hilo walilofanya viongozi na Meya wao haikua ni kazi ya kiserikali bali ni ya watu binafsi.Pia shughuli ya ule msiba uliisha siku walipoaga na makamu wa rais akiwemo baada ya hapo kila mtu anawatembelea wafiwa kwa wakati wake na kwa namna anavyoona inafaa au aambatane na nani!!
Mbona wakuu wa mikoa nchi hii wapo wengi lakini hatuoni wakifanya mambo ya ajabu ajabu?
Mbona wengine wanasimamia Mikoa yao bila kugombana na wabunge wa vyama vya upinzani?
Kwa nini vyombo vya dola vinatumika kwenye mambo ya kujitafutia umaarufu na sifa za mtu binafsi?
Hivi viongozi wetu hawajui kuwa Wanasiasa siku zote shughuli zao zinaenda kisiasa siasa? Kwa nini katiba isiheshimiwe inayotambua uhuru wa kisiasa na uwepo wa vyama vingi?
Kuna haja gani ya dola kulazimishwa kuingilia Mambo ya misiba kwa kuchagua nani atoe rambi rambi na nani asitoe?
Nani apokee na kukabidhi na nini asipokee ?
Ni sheria ipi inayosema kuwa mkuu wa mkoa apokee rambirambi kwa niaba ya familia za watu?
Kwa kweli nimemshangaa sana huyo mkuu wa mkoa kwa kushindwa kuwaelewa watu wa Arusha na kujua kuwa wanataka maendeleo na wanafuatilia mambo yanayotokea na ndivyo wanavyozidi kukikataa chama chake. Tatizo viongozi wetu wanashindwa kucheza na wenyeji wa maeneo tofauti ; mila zao ,desturi zao,dini zao na itikadi zao za kisiasa!
Watu wa Arusha wengi ni watu wanaopenda kuona haki inatendeka . Huwezi ukawashinda kwa ubaya.
Huyo mkuu wa mkoa ajifunze kwa wakuu wa Mikoa wa Kagera, Katavi, Mtwara, Mwanza, Singida, Iringa Mbeya,Tanga n.k ambao wanazunguka huko Vijijini kuhamasisha maendeleo ya watu bila kujenga chuki na uhasama wa kisiasa?
Huwa najiuliza Mbona Mkoa wa Arusha ni kati ya mikoa yenye watu maskini na wenye matatizo makubwa sana huko vijijini?
Yana mkuu wa mkoa wa Arusha amekua kama yeye ndiye mkuu wa Wilaya ya Arusha mjini.Muda wote ni pale mjini na kamera za waandishi tu.Huko vijijini anamwachia nani?
Hana uwezo wa kusimamia mkoa! Apewe uDC. Maendeleo hayaji kwa kuweka wadau wa maendeleo ndani na kuharasi watu.
Huko Longido watu hawana maji lakini mkuu wa mkoa anahangaika na mambo madogo kabisa ambayo hayana tija kabisa kwa taifa la leo wala la kesho.
Kwani Meya kwenda kuwafariji wapiga kura wake inazua vipi mipango ya serikali ya maendeleo kwa mkoa wa Arusha?
Mh. Rais alitoa ahadi nyingi sana kwenye kampeni zake. Na sasa muda uliobakia ni miaka miwili na nusu tu kumaliza awamu ya kwanza.
Watu wanataka kuona kuona ahadi zake zinatimizwa kwenye mikoa na wilaya na vijiji vyote.
Je ,kufikia 2020 ahadi zitakua zimetimia kwa 50%?
Na kati ya hiyo miaka miwili kuna kipindi kigumu cha uchaguzi wa ndani wa chama cha mapinduzi na uchaguzi wa serikali za mitaa. Kampeni na dira itakua ni kuongezeka kwa uchumi na maendeleo na maisha bora ya watanzania!
Mkuu wa mkoa Kuendelea kuhangaika na masuala ya rambi rambi ni kuzidi kuwapa watu kiki za kisiasa.
Tukubali tu kuwa Siasa haijawahi kuachwa tangu binadamu alipoanza kustarabika.
Ni hatari zaidi watu wakikaa kimya kuliko wakiongea.
Watu wakisema wanapunguza jazba zao na kufikia muafaka.
Libya,Iraki,Siria, Misri, zimesambaratika baada ya watu kukaa kimya kwa muda mrefu bila kupewa nafasi ya kusemea maisha yao.
Hili suala la kukamata kamata viongozi kwa makosa mdogo madogo sio jambo jema sana.
Ni bora tungeamua kukamata wale wanasiasa walioliibia taifa letu na kunufaisha familia zao kuliko kuhangaika na wakina Mh. Lema na mh.Kalisti ambao hawana tatizo na rasilimali za nchi yetu. Watu watu walilihujumu taifa hili wao ndio wanapaswa wakae gerezani na sio Tundu Lisu au Lema.
Yote hayo yana mwisho ni muda tuTAIFA LENYE AMANI NA UTULIVU!!!
HIVI MKUU WA MKOA ANAWEZA KUWA YUPO NYUMBANI KWAKE KALEWA POMBE ANAPIGA SIM POLISI ANAWAAGIZA POLISI WAMKAMATE MTU FULANI NA AWEKWE NDANI.....UNAKAMATWA KWELI.
KUNA UMUHIM WA KILA MTU KUJILINDA MWENYEWE.
Kwa kuwa ni mamlaka hata kama ni manyang'anyi, wauwaji, watekaji na wenye tamaa tuwahshim mpumbavu siku zote hujitambua ya kuwa ni mwenye akili kumbe ni pumbavu yawezekana na ww ulizaliwa hivyo toka tumboni kwa mamayo lkn amini wajinga ni sehem ya tatizo ktk nchi hii.Acha chuki za kinafki na viongozi kisa ni wana CCM...lazima muheshimu mamlaka...
Tatizo kubwa la arusha ni lema arusha hata ilipokuwa Na mkuu wa mkoa ambaye si mwongeaji mjifungia ofisini lema hakuisha vituko kutwa alikuwa akiitisha maandamano yasiyo na kichwa wala miguu Arusha mjini . Akikosa kisa ataanza kutukana raisi kuwa atakufa nk. Lema ana mapepo sio bure. Anahitaji watoa mapepo wamsaidieUngesema hawana siasa za kitoto kama za Gambo, kwani lema ndio kawakamata watoa rambi rambi we bata maji?