ARUSHA: Meya, wamiliki wa shule, paroko na Waandishi, wakamatwa na Polisi Shuleni, wanyimwa dhamana

Ccm ni janga la Tanzania
 
Mkuu wa mkoa ameamuru polisi kuwakamata kwa kuwa wameenda kutoa rambirambi moja kwa moja kwa wafiwa bila kumfikishia yeye, hii aibu kubwa, msiba Gambo anaugeuza siasa? Yaani wafiwa wasitembelewe bila kibali cha polisi? Amekula rambirambi sasa ana haha aibu kweli.
 
Kuna vitu vinafanyika unashindwa kuelewa logic behind nani katuloga kiasi tunafanya mambo hata ambayo mtoto wa primary school hafanyi
 
Kuna haja ya sheria zetu kufanyiwa marekebisho, police wawe wanapewa amri na baadhi ya maofisa tu tena wenye weredi, tutakua tunawalaumu bure police kwa kutumiwa na baadhi ya viongozi ili kulinda maslahi yao lakini sheria zetu ndio zenye tatizo, police anachotakiwa ni kutii tu hata kama hakubaliani na hilo jambo.
 
Wanaotoa hizo rambi rambi wanataka rambi rambi zao ziwafikie walengwa, wamechoka na upigaji unaofanywa na magamba,... Unamlazimishaje mtu rambi rambi kwa kuzipeleka! Aibu sana..
 
Ni kweli mkuu,lakini nadhani wenye uwezo wa kushawishi mabadiriko hayo ni polisi wenyewe,kwasababu ndio wanachonganishwa na raia kila mara.
 
Hapo umemlenga nani? Kama ni waliokamatwa umefanya makosa kwani idadi kubwa ya waliokwenda ni wazazi,viongozi wa dini,wanahabari na katika taarifa meya amealikwa hivyo acha ukali kwa kuona rambirambi zimepita kushoto.
 
Na hawa polisi waache kutumika vibaya, ndio maana wanatengeneza tabaka na wananchi,...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…