ARUSHA: Meya, wamiliki wa shule, paroko na Waandishi, wakamatwa na Polisi Shuleni, wanyimwa dhamana

hawa wakina gambosh walitaka pesa wawe wanapelekewa wao tu ili wazipige, sasa watu wamechoka wanapeleka moja kwa moja kwa wahusika...
matokeo yake wanakamatwa kwa kusingiziwa upuuzi... Nchi hii kazi ipo, utafika wakati tena si mbali tutapangiwa na serikali hadi muda wa kupumzika na wake zetu..
 
hivi bado wanapewa rambirambi tu? mimi nashauri pesa zilizobaki zifanyiwe matumizi mengine kwani wazazi wa hao watoto wanajiweza 100%
 
Sasa cocochanel, mumetangaza kuwa mumewapa wafiwa pesa ya rambi rambi mil3.8 kumbe mumewapa 1 na kuwaahidi nyingine mtalipa baadae, kuna pesa ya chakula mumetumia m4, watu wanauliza hivyo vyakula wamekula wapi, haya kwa msaada wa mama samia, hawa vijana wasingepelekwa nje kutibiwa kwani serikali ilishasema ingewatibu hapa hapa, hebu kuweni na huruma jamani, mnakuwa kama hamna watoto, nchi sio ya kijani, nchi ni yote sote, hamna hati miliki inapotokea maafa kama haya watu siasa muache ili tuwahudumie wahanga, nyie kweli mpaka rambi rambi mnameza kweli?

Daah, na yatajulikana mengi tu, hizi pesa tutaziacha hapa hapa na hakuna atakayezikwa nazo, mie kwangu nasema kuweni na utu, litakuja kutokea jambo kubwa sana na watu, mashirika yatagoma kutoa kwa huu ukiritimba wenu, mnajitahidi sana kujenga chuki katika jamii tuonane wabaya, lakini sie tumeshikamana na hatutachukiana kamwe upendo aliotuachia Nyerere tutazidi kuuenzi,

Katu hatutatengamana, ila tu chuki itatengenezwa kati ya viongozi na wananchi na sio wananchi kwa wananchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…