ARUSHA: Polisi hawara aua mume wa ndoa kwa risasi

ARUSHA: Polisi hawara aua mume wa ndoa kwa risasi

Polisi wa kituo cha Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha wanadaiwa kumpiga risasi raia aliyetambuliwa kwa jina la Yohana Nasieli kwa kile kilichoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi kati ya mke wa marehemu na askari polisi.

Habari kutoka kwa ndugu na majirani wa marehemu zilisema kuwa tukio hilo limetokea aprill 12 mwaka huu majira ya saa 1.35 usiku katika mtaa wa sabasaba kata ya Monduli Tarafa ya Kisongo wilayani humo.

Vyanzo vilisema kuwa siku ya tukio ya marehemu alikuwana ugomvi na mke wake, Paulina Kiliani{37} na kumlalamikia mke wake kuwa sio mwaminifu katika ndoa akimtuhumu kuwa na mahusiano na askari polisi aliyefanya mauaji {jina linahifadhiwa} kuwa ndio mvunja ndoa yake.

Vyanzo vya habari viliendelea kusema kuwa siku ya mauaji marehemu na mke wake walikuwa na ugomvi mkubwa na kufikia hatua ya kupigana na mke alimpigia simu ya kiganjani askari polisi huyo na kumwelezea kupigwa kwake na mume wake na askari huyo akiwa na mwenza wakiwa na silaha walikwenda eneo la tukio.

Habari zilisema kuwa baada ya marehemu kumwona askari yule yule anayemtuhumu kufanya mapenzi na mke wake akiwa wa kwanza kufika eneo la tukio,marehemu kwa hasira huku akiongea kwa jazba kuwa wewe ndio niliyekuwa nakutafuta ghafla aliingia ndani ya nyumba yake na kuchukua panga kwa nia ya kumtishia askari huyo akiwa na mwenzake ili aondoke eneo la tukio.

Vyanzo vilisema kuwa kabla ya marehemu kufanya tukio la kutaka kumkata Askari huyo,ghafla askari huyo alifyatua risasi na kumpiga marehemu kifuani kushoto na mguuni na kufariki dunia papo hapo.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo alithibitisha tukio hilo kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari ambapo imesema kuwa NASIELI alijeruhiwa kwa risasi upande wa kushoto wa mguu na kwenye bega la mkono wa kushoto baada ya kukaidi amri halali ya askari Polisi ya kukamatwa na kutaka kumkata askari panga alilokuwa nalo mkononi mwake.

Kamanda aliendelea kueleza katika taarifa yake kuwa marehemu alikuwa amewafungia watoto wake na mtoto wa jirani yake ndani ya nyumba kwania ya kuwadhuru na baada ya kutoa taarifa askari waliamua kwenda eneo la tukio kwa nia ya kuwaokoa watoto lakini pia kumkamata mtuhumiwa.

Taarifa ilisema baada ya kufika eneo la tukio walianza kugonga mlango uliokuwa umefungwa ili kuokoa watoto waliokuwa hatarini wakati wanaokoa watoto hao nje ya nyumba hiyo walimwona mtuhumiwa huyo akiwa amejificha akiwa ameshika panga Mkononi huku akiwa fuata askari hao kwa lengo la kuwadhuru.

Alisema baada ya hali hiyo ndipo alipoamua kumpiga risasi kwenye bega lake la kushoto hali iliyosababisha kuvuja damu nyingi na kisha kupelekwa katika hospital ya wilaya ya Monduli na mtuhumiwa huyo alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu.

Ends...
Si mlishaambiwa MSIOE..

Kwanini hamsikii lakini?

#YNWA
 
Ndugu na majirani wanasemaje?
Marehemu alikuwa ana kichaa cha mapenzi.Mtu ambaye hukumtoa bikra,ulimkuta akiwa na meno 32 yameshaota,huna undugu naye hata kidogo;Akiamua kuchukua 50 zake kwanini usiachane naye?Wanawake mbona wako wengi na kila siku wazuri wanaendelea kuzaliwa?Angeachana naye kiroho safi,sasa hivi angekuwa bado yuko hai,sanasana maumivu ya moyo angeyapata siku za mwanzo mwanzo,baadae maisha yangiendelea.Ona sasa uhai wake umepotea na mwanamke amemuacha anaendelea kuvinjari na madume mengine!
 
Mhh hatari sana kwa kweli maisha haya yaani watoto wanasikia au kuona baba yao akipigwa risasi na kufa aisee dunia ishaharibika utadhani kwa wazulu kumbe Arusha...huyo polisi kazi anayo kesi hana ila Dunia itamhukumu...
 
Huyo marehemu alijua ni mapolisi na wana silaha yet, akanuia kumpiga panga??
Sasa kawaachia gepu full kujivinjari.
Apumzike alikojiandalia
Wanawake ni wengi duniani unaweza kuwapata hata kwa mafungu ukitaka.

Everyday is Saturday................................😎
 
Lipi ni lipi? Tuamini majirani au kamanda wa mkoa?
Kama shida ni wivu kama walivyosema majirani, mke tayari amekosa mme, amebaki mjane, na huyo askari hatomuoa. Yani amekosa bara na Pwani na hii dhambi itamtafuna maisha yake yote.
Sure atavuna alichopanda kwa kipindi alichobaki nacho duniani, karma inamhusu sana neno furaha kwenye mahusiano litakuwa kitendawili.
 
Dah, huyo Askari lazima alogwe na ndugu wa mwanamume.

Kama sio kufa kwa kulogwa basi dhambi itamtafuna aone bora kufa.

Ningekuwa mimi ndo huyo mwanamume, ningemuacha kiroho safi, ningetafuta kabinti kabichi kabisa naoa ndan ya siku tatu.!
 
Polisi wa kituo cha Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha wanadaiwa kumpiga risasi raia aliyetambuliwa kwa jina la Yohana Nasieli kwa kile kilichoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi kati ya mke wa marehemu na askari polisi.

Habari kutoka kwa ndugu na majirani wa marehemu zilisema kuwa tukio hilo limetokea aprill 12 mwaka huu majira ya saa 1.35 usiku katika mtaa wa sabasaba kata ya Monduli Tarafa ya Kisongo wilayani humo.

Vyanzo vilisema kuwa siku ya tukio ya marehemu alikuwana ugomvi na mke wake, Paulina Kiliani{37} na kumlalamikia mke wake kuwa sio mwaminifu katika ndoa akimtuhumu kuwa na mahusiano na askari polisi aliyefanya mauaji {jina linahifadhiwa} kuwa ndio mvunja ndoa yake.

Vyanzo vya habari viliendelea kusema kuwa siku ya mauaji marehemu na mke wake walikuwa na ugomvi mkubwa na kufikia hatua ya kupigana na mke alimpigia simu ya kiganjani askari polisi huyo na kumwelezea kupigwa kwake na mume wake na askari huyo akiwa na mwenza wakiwa na silaha walikwenda eneo la tukio.

Habari zilisema kuwa baada ya marehemu kumwona askari yule yule anayemtuhumu kufanya mapenzi na mke wake akiwa wa kwanza kufika eneo la tukio,marehemu kwa hasira huku akiongea kwa jazba kuwa wewe ndio niliyekuwa nakutafuta ghafla aliingia ndani ya nyumba yake na kuchukua panga kwa nia ya kumtishia askari huyo akiwa na mwenzake ili aondoke eneo la tukio.

Vyanzo vilisema kuwa kabla ya marehemu kufanya tukio la kutaka kumkata Askari huyo,ghafla askari huyo alifyatua risasi na kumpiga marehemu kifuani kushoto na mguuni na kufariki dunia papo hapo.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo alithibitisha tukio hilo kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari ambapo imesema kuwa NASIELI alijeruhiwa kwa risasi upande wa kushoto wa mguu na kwenye bega la mkono wa kushoto baada ya kukaidi amri halali ya askari Polisi ya kukamatwa na kutaka kumkata askari panga alilokuwa nalo mkononi mwake.

Kamanda aliendelea kueleza katika taarifa yake kuwa marehemu alikuwa amewafungia watoto wake na mtoto wa jirani yake ndani ya nyumba kwania ya kuwadhuru na baada ya kutoa taarifa askari waliamua kwenda eneo la tukio kwa nia ya kuwaokoa watoto lakini pia kumkamata mtuhumiwa.

Taarifa ilisema baada ya kufika eneo la tukio walianza kugonga mlango uliokuwa umefungwa ili kuokoa watoto waliokuwa hatarini wakati wanaokoa watoto hao nje ya nyumba hiyo walimwona mtuhumiwa huyo akiwa amejificha akiwa ameshika panga Mkononi huku akiwa fuata askari hao kwa lengo la kuwadhuru.

Alisema baada ya hali hiyo ndipo alipoamua kumpiga risasi kwenye bega lake la kushoto hali iliyosababisha kuvuja damu nyingi na kisha kupelekwa katika hospital ya wilaya ya Monduli na mtuhumiwa huyo alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu.

Ends...
Habari imeanza kwa kumtuhumu askari... Mwishoni mwa habari... Mtuhumiwa anatetewa na kupewa kesi Marehemu
 
Polisi wanateteana sana, unaona huyu kamanda wa Mkoa wa Arusha majibu yake, anatetea mauaji kabisa aisee, Serikali lazima hapa iingilie kati.
 
Back
Top Bottom