ARUSHA: Polisi hawara aua mume wa ndoa kwa risasi

ARUSHA: Polisi hawara aua mume wa ndoa kwa risasi

Wewe tayari ni motiveshini spika.
Kwani mapenzi lazima niwe na wewe?

Hii kauli niliwahi kutamkiwa na mpenzi wangu miaka 15 iliyopita.

Lakini imenifanya niikumbuke hadi leo,, na kunifanya nisilazimishe mapenzi kwa mwanamke yeyote.
 
Polisi mbwa wana akili sana kuliko polisi mtu.
Tayari wameua mume halali, na bosi wa polisi kamfutia makosa muuaji.
Halafu bado hamjajua laana zenu zinatokea wapi?
Hao Wana laana ndy maana wakushastaafu wanaishi maisha magumu sana na hawachukui muda hufariki dunia
 
Polisi wa kituo cha Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha wanadaiwa kumpiga risasi raia aliyetambuliwa kwa jina la Yohana Nasieli kwa kile kilichoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi kati ya mke wa marehemu na askari polisi.

Habari kutoka kwa ndugu na majirani wa marehemu zilisema kuwa tukio hilo limetokea aprill 12 mwaka huu majira ya saa 1.35 usiku katika mtaa wa sabasaba kata ya Monduli Tarafa ya Kisongo wilayani humo.

Vyanzo vilisema kuwa siku ya tukio ya marehemu alikuwana ugomvi na mke wake, Paulina Kiliani{37} na kumlalamikia mke wake kuwa sio mwaminifu katika ndoa akimtuhumu kuwa na mahusiano na askari polisi aliyefanya mauaji {jina linahifadhiwa} kuwa ndio mvunja ndoa yake.

Vyanzo vya habari viliendelea kusema kuwa siku ya mauaji marehemu na mke wake walikuwa na ugomvi mkubwa na kufikia hatua ya kupigana na mke alimpigia simu ya kiganjani askari polisi huyo na kumwelezea kupigwa kwake na mume wake na askari huyo akiwa na mwenza wakiwa na silaha walikwenda eneo la tukio.

Habari zilisema kuwa baada ya marehemu kumwona askari yule yule anayemtuhumu kufanya mapenzi na mke wake akiwa wa kwanza kufika eneo la tukio,marehemu kwa hasira huku akiongea kwa jazba kuwa wewe ndio niliyekuwa nakutafuta ghafla aliingia ndani ya nyumba yake na kuchukua panga kwa nia ya kumtishia askari huyo akiwa na mwenzake ili aondoke eneo la tukio.

Vyanzo vilisema kuwa kabla ya marehemu kufanya tukio la kutaka kumkata Askari huyo,ghafla askari huyo alifyatua risasi na kumpiga marehemu kifuani kushoto na mguuni na kufariki dunia papo hapo.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo alithibitisha tukio hilo kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari ambapo imesema kuwa NASIELI alijeruhiwa kwa risasi upande wa kushoto wa mguu na kwenye bega la mkono wa kushoto baada ya kukaidi amri halali ya askari Polisi ya kukamatwa na kutaka kumkata askari panga alilokuwa nalo mkononi mwake.

Kamanda aliendelea kueleza katika taarifa yake kuwa marehemu alikuwa amewafungia watoto wake na mtoto wa jirani yake ndani ya nyumba kwania ya kuwadhuru na baada ya kutoa taarifa askari waliamua kwenda eneo la tukio kwa nia ya kuwaokoa watoto lakini pia kumkamata mtuhumiwa.

Taarifa ilisema baada ya kufika eneo la tukio walianza kugonga mlango uliokuwa umefungwa ili kuokoa watoto waliokuwa hatarini wakati wanaokoa watoto hao nje ya nyumba hiyo walimwona mtuhumiwa huyo akiwa amejificha akiwa ameshika panga Mkononi huku akiwa fuata askari hao kwa lengo la kuwadhuru.

Alisema baada ya hali hiyo ndipo alipoamua kumpiga risasi kwenye bega lake la kushoto hali iliyosababisha kuvuja damu nyingi na kisha kupelekwa katika hospital ya wilaya ya Monduli na mtuhumiwa huyo alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu.

Ends...
Dah wanaume wanahanga mia kwa kukosa michepuko.
 
Haya mambo ni mepesi kujibu ukiwa nyuma ya keyboard lakini usiombe yakukute.....ni watu wachache sana wanaovuka salama kwenye mitihani ya mapenzi......kwenye mambo yanayohusu mapenzi huwa simlaumu mtu kwa jambo lolote au hatua yoyote atakayoifanya maana mtu anapozama penzi anapoteza sehemu kubwa ya utendaji kazi wa ubongo wake...........

USIOMBE YAKUKUTE......
 
Askari yupo sahihi hata kama alikuwa anatembea na huyo Paulina.
Askari angefuata ethics za kazi yake. Tukio hilo lilikuwa linamhusu personally kwa kupigiwa simu ya mkononi na marehemu,angetuma askari wengine kukwepa kuwa emotional involved.Inawezekana emotions ziliathiri maamuzi yake.
 
Huyo mwanamke amethibitisha kwamba ana mahusiano ya kimapenzi na askari polisi maana hadi kumpigia simu ya kiganjani huyo askari ni ushahidi tosha kwamba namba yake alikuwa nayo kwa madhumuni hayo.
 
Askari mwenye mafunzo kuokoa watoto kwa kumpiga risasi mtekaji mpaka kufa(risasi mbili) kwa hili kunahitajika kuangalia na kurekebisha mafunzo wanayopewa askari wetu wawapo chuoni,zamani mimi nilikuwa najua angalau mtuhumiwa ameshindikana sana(amejizatiti) na hakuna namna basi ikilazimu atulizwe kwa risasi ya mguu tena ni kwa nyuma sio "face 2 face"
kisa hichi kinasikitisha sana wahusika wafatilie na hatua za haraka zichukuliwe
 
Mwambieni huyo kamanda wa polisi mama kapata hii kesi tayari ajiandae.
 
Polisi wa kituo cha Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha wanadaiwa kumpiga risasi raia aliyetambuliwa kwa jina la Yohana Nasieli kwa kile kilichoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi kati ya mke wa marehemu na askari polisi.

Habari kutoka kwa ndugu na majirani wa marehemu zilisema kuwa tukio hilo limetokea aprill 12 mwaka huu majira ya saa 1.35 usiku katika mtaa wa sabasaba kata ya Monduli Tarafa ya Kisongo wilayani humo.

Vyanzo vilisema kuwa siku ya tukio ya marehemu alikuwana ugomvi na mke wake, Paulina Kiliani{37} na kumlalamikia mke wake kuwa sio mwaminifu katika ndoa akimtuhumu kuwa na mahusiano na askari polisi aliyefanya mauaji {jina linahifadhiwa} kuwa ndio mvunja ndoa yake.

Vyanzo vya habari viliendelea kusema kuwa siku ya mauaji marehemu na mke wake walikuwa na ugomvi mkubwa na kufikia hatua ya kupigana na mke alimpigia simu ya kiganjani askari polisi huyo na kumwelezea kupigwa kwake na mume wake na askari huyo akiwa na mwenza wakiwa na silaha walikwenda eneo la tukio.

Habari zilisema kuwa baada ya marehemu kumwona askari yule yule anayemtuhumu kufanya mapenzi na mke wake akiwa wa kwanza kufika eneo la tukio,marehemu kwa hasira huku akiongea kwa jazba kuwa wewe ndio niliyekuwa nakutafuta ghafla aliingia ndani ya nyumba yake na kuchukua panga kwa nia ya kumtishia askari huyo akiwa na mwenzake ili aondoke eneo la tukio.

Vyanzo vilisema kuwa kabla ya marehemu kufanya tukio la kutaka kumkata Askari huyo,ghafla askari huyo alifyatua risasi na kumpiga marehemu kifuani kushoto na mguuni na kufariki dunia papo hapo.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo alithibitisha tukio hilo kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari ambapo imesema kuwa NASIELI alijeruhiwa kwa risasi upande wa kushoto wa mguu na kwenye bega la mkono wa kushoto baada ya kukaidi amri halali ya askari Polisi ya kukamatwa na kutaka kumkata askari panga alilokuwa nalo mkononi mwake.

Kamanda aliendelea kueleza katika taarifa yake kuwa marehemu alikuwa amewafungia watoto wake na mtoto wa jirani yake ndani ya nyumba kwania ya kuwadhuru na baada ya kutoa taarifa askari waliamua kwenda eneo la tukio kwa nia ya kuwaokoa watoto lakini pia kumkamata mtuhumiwa.

Taarifa ilisema baada ya kufika eneo la tukio walianza kugonga mlango uliokuwa umefungwa ili kuokoa watoto waliokuwa hatarini wakati wanaokoa watoto hao nje ya nyumba hiyo walimwona mtuhumiwa huyo akiwa amejificha akiwa ameshika panga Mkononi huku akiwa fuata askari hao kwa lengo la kuwadhuru.

Alisema baada ya hali hiyo ndipo alipoamua kumpiga risasi kwenye bega lake la kushoto hali iliyosababisha kuvuja damu nyingi na kisha kupelekwa katika hospital ya wilaya ya Monduli na mtuhumiwa huyo alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu.

Ends...
Baada ya kutokea ugomvi mke wa marehemu alimpigia simu "hawara" polisi akafika na mwenzake askari polisi?. Marehemu akakimbia kuleta panga askari akajihami kwa kumshambulia marehemu kwa risasi?
Msemaji wa jeshi la polisi naye katoa sintofahamu marehemu hakutii sheria bila shuruti?
Na watoto walikuwa wamefungiwa?

Somo:
Kuna muda ukiwa na matatizo hata kivuli chako kinakumbia.
 
Lipi ni lipi? Tuamini majirani au kamanda wa mkoa?
Kama shida ni wivu kama walivyosema majirani, mke tayari amekosa mme, amebaki mjane, na huyo askari hatomuoa. Yani amekosa bara na Pwani na hii dhambi itamtafuna maisha yake yote.
Kamanda aeleze ilikuwaje huyo askari akaenda na silaha eneo la tukio. Yaani askari wawili huku wana silaha kwenda kumkamata mhalifu mmoja ambaye taarifa za uhalifu wake (malalamiko) haijaelezwa zilifikaje kituoni. Ilipigwa 112 au simu binafsi ya askari nk

Kamanda atoe taarifa kwa kina.
 
Back
Top Bottom