LGE2024 Arusha: Vurugu zaibuka, wafuasi CHADEMA wataka kunyukana

LGE2024 Arusha: Vurugu zaibuka, wafuasi CHADEMA wataka kunyukana

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
..

..Chadema wako imara, na wana uchungu na chama chao, ndio maana ngumu zinatembea.

..Na siku Polisi wakiacha kuwalinda Ccm lazima watachezea kichapo toka kwa Chadema.
Mimi kwa kiasi nawaelewa Chadema. Nahisi experience yao inawafanya kwenda overboard kuhakikisha hawaingii watu ambao ni mamluki.
Ni kama nguvu waliotumia kuhakikisha kuwa Msigwa hashindi na haikuchukua muda tukamuona yuko kwenye jukwaa akikinanga chama chake cha awali!

Haipendezi lakini wanajiona wako kwenye vita.

Amandla...
 

Attachments

  • IMG-20241113-WA0060.jpg
    IMG-20241113-WA0060.jpg
    416.8 KB · Views: 3
Lemma anamwaga rushwa za hatari, ni mwendelezo wa vita baridi dhidi ya Mbowe ili asiteuliwe kuwa mgombea Urais wa chadema
 
Mpo salama wanajukwaa?

Baadhi ya wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Arusha wamejikuta wakiingia kwenye mgogoro mkubwa uliosababisha kurushiana maneno makali na hata ngumi, muda mfupi baada ya mkutano kati ya Naibu Katibu Mkuu Bara wa chama hicho Benson Kigaila na waandishi wa habari uliofanyika katika Ukumbi wa Golden Rose, Novemba 13, 2024.

Mashuhuda wameripoti kuwa vurugu hizo zilianza majira ya saa 12:30 jioni na ziliendelea kwa takribani saa moja. Wanachama hao walionekana wakirushiana lawama huku wakidai kuwa walishambuliwa na vijana wa hamasa wa chama hicho.

"Tumeshambuliwa na vijana wa hamasa bila sababu yoyote ya msingi," ameeleza mmoja wa wanachama, ambaye alisisitiza kuwa tukio hilo limeleta mgawanyiko ndani ya chama.

Mbali na malalamiko ya kupigwa, baadhi ya wanachama hao walimtupia lawama nyingi Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Kaskazini, Godbless Lema, wakimtuhumu kuwa na mienendo inayowakatisha tamaa ndani ya chama. Wamesema kuwa mienendo hiyo imekuwa chanzo cha migogoro na kutokuelewana miongoni mwa wanachama.

View attachment 3151765

Chanzo: Jambo TV
Polisi wasaidieni hao pimbi watauwana
 
Kichapo cha kung fu au kichapo kwenye sanduku la kura?

..kote kote.

..polisi wakikaa pembeni Ccm hawawezi kuwakabili Cdm.

..unakumbuka vikao vya halmashauri ya Dsm jinsi madiwani wa Cdm walivyokuwa wanatembeza makonde kwa madiwani wa Ccm?
 
unakumbuka vikao vya halmashauri ya Dsm jinsi madiwani wa Cdm walivyokuwa wanatembeza makonde kwa madiwani wa Ccm?
Haha ninachojua kuchapana makonde ni dalili ya kukosekana kwa busara...

Mtu akizidiwa nguvu ya hoja, hukunja ngumi.
 
Haha ninachojua kuchapana makonde ni dalili ya kukosekana kwa busara...

Mtu akizidiwa nguvu ya hoja, hukunja ngumi.

..ni lini Ccm wamekuwa na hoja?

..Cdm walikuwa wanawabutua madiwani wa Ccm kwasababu walikuwa weziwezi, wajanjawajanja.
 
Back
Top Bottom