Arusha: Wakuu wa Shule ambao Shule zao zimefanya vibaya kitaifa wapewa vinyago vya sokwe

Arusha: Wakuu wa Shule ambao Shule zao zimefanya vibaya kitaifa wapewa vinyago vya sokwe

Camilo Cienfuegos

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2015
Posts
18,960
Reaction score
67,654
Kama kuna kada inajua kudharauliwa basi ni ualimu.

Wakuu wa Shule katika halmashauri ya Arusha Dc wamepewa vinyago vya nyani ili kuongeza kiwango cha ufaulu baada ya shule zao kufanya vibaya katika mitihani ya kitaifa ya kidato cha 2, cha 4 na cha 6 mwaka jana.

Hii imekaaje kitaalamu?

C1B1B144-2CAF-4C5E-BE5B-BB9A5C4273FC.jpeg
 
Kama kuna kada inajua kudharauliwa basi ni ualimu. Wakuu wa Shule katika halmashauri ya Arusha Dc wamepewa vinyago vya nyani ili kuongeza kiwango cha ufaulu baada ya shule zao kufanya vibaya katika mitihani ya kitaifa ya kidato cha 2, cha 4 na cha 6 mwaka jana.

Hii imekaaje kitaalamu?

Mtoa kinyago SI alikuwa Mafweza /mkuu wa neck aliyetangulia au namchanganya wajameni?
 
Pumbavuuu sana kwa REO na DEO wa Arusha kwa ubunifu wa KISOKWE.
[emoji35][emoji35][emoji35][emoji35][emoji35]
 
Hii nchi ina baadhi ya viongozi wenye uwezo mdogo sana wa kufikiri! Yaani kwa akili zao wanaamini wanafunzi walioshindwa kukariri masomo kuliko wanafunzi wengine, basi hawana akili! Jambo ambalo siyo sahihi hata kidogo.

Kwanza Serikali inatakiwa kuachana na mambo ya kuingiza siasa kwenye elimu! Hii sera yao ya kuruhusu wanafunzi wote kuhitimu kidato cha nne, halafu masomo yenyewe ni ya kukariri tu, na yasiyo na mchango wowote ule kwenye maisha yao! ni sera ya hovyo kupitiliza.


Serikali inatakiwa kuanzisha vyuo vya ufundi stadi kila Kata! Kama ilivyofanya kwenye shule za Kata. Halafu wanafunzi wote wanaopata alama za chini na za kati, wanapekekwa huko kwa ajili ya kusomea cheti katika fani mbalimbali kama vile ufundi, upambambaji, michezo, maigizo, nk. Na baadaye kupata sifa ya kujiendeleza katika ngazi ya stashahada, shahada, nk.

Na wale wanafunzi wenye uwezo wa kukariri masomo (wenye akili) ndiyo wangepata nafasi ya kuendelea na masomo ya Sekondari na Chuo katika mfumo uliopo sasa. Haya mambo ya kulazimisha watoto kukariri masomo, ndiyo huchangia sana kufeli kwao, na mwisho wa siku lawama zinapelekwa kwa walimu!

Serikali ingeboresha elimu ya VETA nchini (Mfano kunzisha vyuo hivyo katika ngazi ya kila kata), naamini kwa kiwango kikubwa tatizo la ajira kwa vijana lingepungua sana. Kuwadhalilisha watu kwa makosa ya watu wengine, siyo sawa hata kidogo.
 
Sisi hapa JF ngoja tuwakabidhi zawadi ya emoji ya Kima ili wajifunze kuiba mitihani kama wakuu wa shule nyingine zinazofanya vizuri🐒🐒🐒
 
Kama kuna kada inajua kudharauliwa basi ni ualimu.

Wakuu wa Shule katika halmashauri ya Arusha Dc wamepewa vinyago vya nyani ili kuongeza kiwango cha ufaulu baada ya shule zao kufanya vibaya katika mitihani ya kitaifa ya kidato cha 2, cha 4 na cha 6 mwaka jana.

Hii imekaaje kitaalamu?

Mbona huyo sokwe kafanana na huyo wa meza kuu?
 
Hizo fedha za kuchongea vinyago zimetoka kwenye mifuko yao binafsi ama ni Kodi zetu ndio zilizotumika kufanyia upupu huo.kiongozi alosimamia Hilo zoezi je alishawahi kaa chini na waalimu wakajadili Nini wafanye ili watoto wafaulu,mi nadhani naye kuna haja ya kuitwa na wakubwa zake akabidhiwe lingedere Tena lenye nyororo atembee nalo mpaka atatue changamoto zinazofanya ufaulu uwe duni
 
Kama kuna kada inajua kudharauliwa basi ni ualimu.

Wakuu wa Shule katika halmashauri ya Arusha Dc wamepewa vinyago vya nyani ili kuongeza kiwango cha ufaulu baada ya shule zao kufanya vibaya katika mitihani ya kitaifa ya kidato cha 2, cha 4 na cha 6 mwaka jana.

Hii imekaaje kitaalamu?

Nyani ama sokwe ni kivutio cha utalii, ni kinyago cha heshima.

Kama maana yao ndiyo hiyo, wangelichonga kinyago cha popo.

Popo ndiyo alama tangia zamani hutumika mashuleni kuelezea matokeo ya wanafunzi ma mbumbumbu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii nchi ina baadhi ya viongozi wenye uwezo mdogo sana wa kufikiri! Yaani kwa akili zao wanaamini wanafunzi walioshindwa kukariri masomo kuliko wanafunzi wengine, basi hawana akili! Jambo ambalo siyo sahihi hata kidogo.

Kwanza Serikali inatakiwa kuachana na mambo ya kuingiza siasa kwenye elimu! Hii sera yao ya kuruhusu wanafunzi wote kuhitimu kidato cha nne, halafu masomo yenyewe ni ya kukariri tu, na yasiyo na mchango wowote ule kwenye maisha yao! ni sera ya hovyo kupitiliza.


Serikali inatakiwa kuanzisha vyuo vya ufundi stadi kila Kata! Kama ilivyofanya kwenye shule za Kata. Halafu wanafunzi wote wanaopata alama za chini na za kati, wanapekekwa huko kwa ajili ya kusomea cheti katika fani mbalimbali kama vile ufundi, upambambaji, michezo, maigizo, nk. Na baadaye kupata sifa ya kujiendeleza katika ngazi ya stashahada, shahada, nk.

Na wale wanafunzi wenye uwezo wa kukariri masomo (wenye akili) ndiyo wangepata nafasi ya kuendelea na masomo ya Sekondari na Chuo katika mfumo uliopo sasa. Haya mambo ya kulazimisha watoto kukariri masomo, ndiyo huchangia sana kufeli kwao, na mwisho wa siku lawama zinapekekwa kwa walimu!

Serikali ingeboresha elimu ya VETA nchini (Mfano kunzisha vyuo hivyo katika ngazi ya kila kata), naamini kwa kiwango kikubwa tatizo la ajira kwa vijana lingepungua sana. Kuwadhalilisha watu kwa makosa ya watu wengine, siyo sawa hata kidogo.
Umenena vema kaka
 
Imagine mzungu angempa mtu mweusi hiyo zawad...hehehehee
 
upuuzi wa hali ya juu..

wala cyo ya kuchekewa..

ni udhalilishaji, na inapunguza ari ya kufanya kazi
 
Wakuu wa shule za secondary zilizofanya vibaya kidato cha 2,4,na 6 kwa mwaka 2020/2021 wamepewa tunzo za vinyago ili kuwapa motisha wafanye bidii kipindi kijacho.
Screenshot_20211118-202400.png
 
Back
Top Bottom