Arusha: Wananchi walia na kituo cha mabasi makubwa ya abiria ya kwenda mikoani

Arusha: Wananchi walia na kituo cha mabasi makubwa ya abiria ya kwenda mikoani

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Wananchi jijini Arusha pamoja na abiria wanaotumia stand kubwa ya mabasi wamailalamikia uongozi wa jiji la Arusha kuwa wameshindwa kuwaletea mabadiliko kwa kuwajengea stand nyingine mpya ya kisasa tofauti na iliyopo sasa ambayo ipo tangu kabla ya uhuru hadi sasa.

Kutokana na udogo wa kituo hicho cha Mabasi umefanya baadhi ya makampuni kushusha na Kupakia abiria katika sehemu mbalimbali na wengine katika ofisi zao zilizopo sehemu tofauti tofauti jijini hapo na hivyo kuleta usumbufu kwa abiria na wageni kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Mfano gari za kwenda Namanga kuna ambazo zinapaki stand kubwa na. Nyingine nje ya uwanja wa mpira wa. Abeid karume.

Magari ya Kwenda Dar es Salaam kuna machache yanapaki ndani ya kituo hicho, mengine stand ndogo na. Mengine yamekuwa yakipakiza na kushusha abiria katika ofisi zao

Za kwenda karatu nazo kuna ambazo zinapaki ndani ya kituo na nyingine mbali na kituo hicho maeneo ya Sabena

Kituo hicho kikubwa cha mabasi hakina sehemu ya kusubiri abiria wala Wasindikizaji.

Hakuna sehemu ya kuwakinga na Mvua wala jua.

Na. Pia Usalama ni mdogo usiku na. Mchana kutokana na miundombinu ya kituo hicho cha mabasi na hivyo Kuwa na. Idadi kubwa ya vibaka, wezi, wavutaji wa madawa yote na vijana wa mitaani ambao ni tishio kwa wageni na abiria.

Wananchi wa jiji la Arusha wamekuwa wakilalamika miaka Nenda miaka rudi lakini hawaoni mabadiliko yoyote hadi sasa,kituo cha mabasi kilichopo hakiendani na hadhi ya jiji kwani jiji hili limekuwa likipokea wageni wengi ndani Na Nje ya nchi hivyo kituo hicho ambacho hakina uwezo hata wa kupaki mabasi (10)kumi kwa wakati mmoja, kinaharibu taswira ya jiji.
 
Ili mji wa Arusha upanuke na ukue kwa haraka wahusika wazingatie yafuatayo:
1. Ondoa stendi na masoko yale pale mjini kati.
2. Stendi mabasi ya kutoka Dodoma road inatakiwa iwe Kisongo. Weka soko huko.
3. Stendi mabasi kutoka Moshi road iwe USA au Chekereni. Weka soko huko.
4. Stendi magari kutoka Nairobi iwe Ngaramtoni ya Juu. Weka soko huko.
5. Stendi magari kutoka Simanjiro/Kiteto iwe Oljoro. Weka soko huko.

NB: Lakini msije mkalalamika kuwa stendi na masoko yako mbali!
 
Ili mji wa Arusha upanuke na ukue kwa haraka wahusika wazingatie yafuatayo:
1. Ondoa stendi na masoko yale pale mjini kati.
2. Stendi mabasi ya kutoka Dodoma road inatakiwa iwe Kisongo. Weka soko huko.
3. Stendi mabasi kutoka Moshi road iwe USA au Chekereni. Weka soko huko.
4. Stendi magari kutoka Nairobi iwe Ngaramtoni ya Juu. Weka soko huko.
5. Stendi magari kutoka Simanjiro/Kiteto iwe Oljoro. Weka soko huko.

NB: Lakini msije mkalalamika kuwa stendi na masoko yako mbali!
Safi sana mkuu nadhani wamesikia.
 
Ili mji wa Arusha upanuke na ukue kwa haraka wahusika wazingatie yafuatayo:
1. Ondoa stendi na masoko yale pale mjini kati.
2. Stendi mabasi ya kutoka Dodoma road inatakiwa iwe Kisongo. Weka soko huko.
3. Stendi mabasi kutoka Moshi road iwe USA au Chekereni. Weka soko huko.
4. Stendi magari kutoka Nairobi iwe Ngaramtoni ya Juu. Weka soko huko.
5. Stendi magari kutoka Simanjiro/Kiteto iwe Oljoro. Weka soko huko.

NB: Lakini msije mkalalamika kuwa stendi na masoko yako mbali!
Wazo zuri
 
Eneo la stendi lilishatengwa pale Kiserian mahali pazuri kabisa. Mrisho Gambo akiwa mkuu wa mkoa akawapa rushwa madiwani wakapinga ili wapeleke kule Oljoro Bondeni city kwenye shamba la rafiki yake muhindi aliempa rushwa ili alipwe fidia baada ya shamba kumshinda. Hapafai Na ni kushoto Kwa kila kitu.
CCM 2025 toa Mrisho Gambo weka Binamu Bananga.
 
Ili mji wa Arusha upanuke na ukue kwa haraka wahusika wazingatie yafuatayo:
1. Ondoa stendi na masoko yale pale mjini kati.
2. Stendi mabasi ya kutoka Dodoma road inatakiwa iwe Kisongo. Weka soko huko.
3. Stendi mabasi kutoka Moshi road iwe USA au Chekereni. Weka soko huko.
4. Stendi magari kutoka Nairobi iwe Ngaramtoni ya Juu. Weka soko huko.
5. Stendi magari kutoka Simanjiro/Kiteto iwe Oljoro. Weka soko huko.

NB: Lakini msije mkalalamika kuwa stendi na masoko yako mbali!
Ushauri mbovu sana huu. Kwa hiyo mtu anayetoka moshi kwrnda karatu, ashukie USA apande dala dala mbili hadi kisongo ili apande gari la kwenda karatu? Maana kubwa ya kuwa na stand kuu ni kurahisisha pia connection.
 
Arusha ndio mnataka kuifananisha na Mwanza kweli?

Arusha inapambana na miji kama Musoma, Geita, Katoro, nk. Kahama sasa sio level za Arusha tena.

Soon senta kama Kagongwa ama Runzewe zinaipita Arusha.
 
Eneo la stendi lilishatengwa pale Kiserian mahali pazuri kabisa. Mrisho Gambo akiwa mkuu wa mkoa akawapa rushwa madiwani wakapinga ili wapeleke kule Oljoro Bondeni city kwenye shamba la rafiki yake muhindi aliempa rushwa ili alipwe fidia baada ya shamba kumshinda. Hapafai Na ni kushoto Kwa kila kitu.
CCM 2025 toa Mrisho Gambo weka Binamu Bananga.
Swala la stand kubwa hadi leo imekuwa ni dana dana isioisha
 
Ili mji wa Arusha upanuke na ukue kwa haraka wahusika wazingatie yafuatayo:
1. Ondoa stendi na masoko yale pale mjini kati.
2. Stendi mabasi ya kutoka Dodoma road inatakiwa iwe Kisongo. Weka soko huko.
3. Stendi mabasi kutoka Moshi road iwe USA au Chekereni. Weka soko huko.
4. Stendi magari kutoka Nairobi iwe Ngaramtoni ya Juu. Weka soko huko.
5. Stendi magari kutoka Simanjiro/Kiteto iwe Oljoro. Weka soko huko.

NB: Lakini msije mkalalamika kuwa stendi na masoko yako mbali!
Sasa hapa ndio itakuwa umetesa wananchi mpaka wataonja joto ya uwezi tawanya tawanya stend namna hiyo kwani uhalisisia utakuwa umeuondoa. Stend inatakiwa ikae sehem ambaya ni centre. Yaan ukienda stend unakuwa gari za kila Mahali. Wewe ulizosema hapo stend zaid ya tatu na zote hayo maeneo uliotaja yako zaidi ya umbali wa kilometer tano.
 
Back
Top Bottom