Arusha: Watuhumiwa wa ugaidi waliosota gerezani kwa miaka 10 waachiwa huru

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Mahakama kuu kanda ya Arusha leo 16/06/2023 imewaachia huru watu 12 wakiwemo Mashehe waliosingiwa kesi ya Uongo ya Ugaidi.

Walifunguliwa kesi No. 65 ya 2022 na kunyimwa dhamana, ambako wamewekwa selo kwa zaidi ya miaka 10.

Tunamuomba Mwenyezi Mungu atoe haki kwa wote waliotunga unyama huu, Amina.

---
MAHAKAMA Kuu kanda ya Arusha imewaachia huru Mashekhe tisa waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya jinai namba 63 ya Mwaka 2022. Kwa kudaiwa kujihusisha na matukio ya kigaidi mwaka 2014.

Washtakiwa hao waliodaiwa kurusha Mabomu katika Bar ya Arusha Night Park na kusabisha kifo cha Mtu Mmoja mnamo April 13, 2014 ni pamoja na Abdalla Athumani, Ally Hamisi, Abdalla Wambura, Rajabu Ahamed, Hassan saidi, Ally Jumanne, Yasin sanga, Shambani Abdallah, na Ibrahim Herman,

Mbali na Mashekhe hawa tisa walioachiwa huru Mashekhe wengine kumi n wawili wenye kesi za ugaidi wamesalia Magereza wakisubiri hatma yao.


 
Miaka yote hiyo 10 na kuachiwa bila ya kukutwa na hatia! Je! Wana haki ya kisheria kulipwa fidia yoyote ile?
 
Unaomba mwenyezi Mungu atoe kisasi au awasamehe...
 
Hadi leo ni miaka mingapi mleta madaaa?
PUnguza jazba kwanza sheheee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…