Yule baba Prophet katoa pesa zake milioni 100 kusaidia wananchi ambapo si mbunge wala kiongozi yoyote wa serikali, inatokea tu kajamaa ambako kalikuwa kakilipwa mamilioni ya fedha na posho kibao, na hakakuchangia chochote kwa wananchi, halafu kanatoa kashifa mbele ya haohao wananchi ambao kaliwafanya mgongo wa kupandia eti mmelaaniwa kwa sababu ya biashara zenu za kufukuza upepo?
Siasa zingine za kijinga tu!
Tamko la Lema kuwahusu bodaboda, ni msimamo wa Chadema? Na kama siyo, Lema akemewe mara moja!
Mtu amekuwa mbunge zaidi ya miaka 15, bodaboda alizikuta na akaziacha, lakini hakufanya lolote ili tu kuwatoa hao bodaboda kwenye biashara hiyo ya laana kama anavyodai, isitoshe, bodaboda zimekuwa zikitumika sana kwenye mikutano ya Chadema na zimekuwa zikikiheshimisha chama na Viongozi wake
Sisi tukuiteje?
Ni ujingaa au Canada anataka kuihamishia Tanzania kwa maneno tupu?
Bodaboda zimesomesha watoto na wengine wapo vyuoni wazazi wao wakiwasomesha kwa hizo boda, halafu mtu mmoja tu kutoka Kanada tena kwa ukimbizi wa kuhongwa ili tu aitwe mkimbizi aje kutukana kazi zetu?
Lema, ulilpaswa kuwasimanga boda baada ya kuainisha ulichowafanyia wana Arusha miaka 15 ukiwa mbunge na au ungeshuka na mbadala wa kazi hiyo kutokea huko Canada
Lema, Licha ya kukaa ughaibuni miaka zaidi ya miwili bado haikutosha kuondoa upuuzi wa kufikiri?