Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

Kwanza vinasanabisha wake zetu wagongwegongwe ovyo Ili tu kupata Hela ya rejesho
 
Sasa vicoba kwani ni fahari? Mtakuja kusifia hata kamari kisatu imepondwa na msiemtaka
Hivyo vicoba nikwaajili ya maskini. Hakuna waziri,RC,DC,DED, anaecheza vicoba.

Vicoba havijawahi kumkwamua mtu kutoka kwenye lindi la umaskini
 
Ajira ya bodaboda ni laana ya nchi yetu. Laana hutokea pale mtu au nchi in this case inapotawaliwa na viongozi wavivu, wezi na wazembe.

😂😂😂
Ndio maana nikakuambia hujui maana ya Laana.
Ajali inatokana na sababu nyingi, Ila kubwa ni Uzembe, ukosefu WA Elimu, kuvunja sheria za Barabara, kutojali nafasi za wengine uwapo Barabarani n.k.
Na sio kazi ya ubodaboda
 
Sasa vicoba kwani ni fahari? Mtakuja kusifia hata kamari kisatu imepondwa na msiemtaka
Hivyo vicoba nikwaajili ya maskini. Hakuna waziri,RC,DC,DED, anaecheza vicoba.

Vicoba havijawahi kumkwamua mtu kutoka kwenye lindi la umaskini
Eti mwisho wa mwaka wanapokea hela nyingi wanapo vunja kikoba,ndo wanasijikia ufahari 😁
 

Kama ni Mtazamo na Maoni yako basi uko sahihi.
Ila katika uhalisia Sio Laana.

Ni Sawa na kina Mpwayungu wanaosema kazi ya ualimu ni laana, ni mitazamo Yao binafsi Ila kiuhalisia sio.
 
Vyote ni vibaya. Na hapa ndipo tunaposhindwa kuelewena. Wewe hutaki kukubali kuwa tumefikia hapa i.e. ujira wa 140,000 kwa mwezi au 10,000 kwa siku kwa sababu tulikosea huko nyuma. Mimi najaribu kuonyesha kuwa siku za nyuma tumekosea sana na ndiyo maana tumejikuta hapa tulipo. Jaribu kuangalia basi in a pig picture. Bodaboda au machinga atafanya hiyo kazi mpaka lini? Unajua kila uchao vijana wengi tu wanazidi kujiingiza kwenye hii biashara? Ni nini mipango ya uzeeni kwa hao waendesha bodaboda na familia zao? Bado narudia: Bodaboda siyo solution ya hapa tulipofikia.
 
UNGETUNGA KITABU UNAICHOSHA SERVER
 
😂😂😂
Ndio maana nikakuambia hujui maana ya Laana.
Ajali inatokana na sababu nyingi, Ila kubwa ni Uzembe, ukosefu WA Elimu, kuvunja sheria za Barabara, kutojali nafasi za wengine uwapo Barabarani n.k.
Na sio kazi ya ubodaboda
Jaribu kusoma tena kwa ufahamu. Mimi sikuzungumzia suala la ajali hata kidogo. Nimeandika ''AJIRA'' na siyo ''AJALI''
 
Haya ni maandalizi ya Zama mpya na upinzani mpya HATA ikiwezekana na chama kipya tawala kabisa kutokana na aina za siasa wanazofanya wapinzani!

Ukichunguza KWA MAKINI utagundua wanapewa script ya kile wakisemacho kabla ya kukisema,Bado haijaeleweka wanafanya KWA maslahi ya Nani hasa!je ni system,je ni mtu,je ni chama Tawala au ni faida yao wenyewe!

Ni rasmi Sasa upinzani wa miaka mingi ulikuwa na baba yao anaoulea Ndio huyo anaetajwa kuwa aliwashauri nini cha kufanya waje au wasije nchini!matamshi ya lema yanapigia mstari dhana hii!!

Katika Zama hizi za katiba mpya kutajwa tajwa ni RASMI sasa kuwa katiba hii iliyopo inakufa na siasa zake na kuzaliwa mpya!

Wote KWA pamoja tukiri kwamba nchi yetu ni ya thamani kuliko chama CHOCHOTE wala upinzani wowote!

Wote tuseme Mungu ibariki Tanzania nchi yetu tuipendayo sana!
 
Vikoba havina msaada,

Ni hela yako inakatwa sijui, akiba sijui nini, wa kufaidi ni wachache.

Vikoba lazima mgombane mpaka mtishiane kurogana.

Kosa la Lema anasema ila hatoi option B, bila vikoba au bodaboda watu wapateje hela?
 
Mimi pia sioni faida,yaan pesa zako unaweka halafu unakuja kurudishiwa mwisho wa mwaka..then what? Kwamba umeshindwa kuhifadhi wewe mwenyewe? Kama hyo ndo logic
Wajanja wanafanyia hela za maskini kazi maskini anashangaatu
 
Huwezi kubeba tractor ukaliweka barabarani liwe linasafirisha abiria, kila kukitokea ajali maafa ni makubwa, halafu useme eti dereva wa tractor apewe mafunzo ya namna salama ya kusafirisha abiria. Tractor kwake ni huko mashambani, halijatengenezwa kwaajili ya kusafirisha abiria.

Pikipiki hazijatengenezwa kwaajili ya public transport. Kuna baadhi ya nchi, pikipiki hutumika zaidi mashambani tu ambako hakuna msongamano wa magari. Kule Australia, pikipiki zinatumika zaidi na wachunga kondoo. Pikipiki haijatengenezwa kwaajili ya kutembea kwenye highway, ndiyo maana kama ilivyo baiskeli, ina gurudumu moja mbele moja nyuma ili iweze kupita kwenye tracks (vinjia vyembamba). Kuziweka kama chombo cha usafiri wa umma ni makosa makubwa. Pikipiki kutokyluwa salama, hakusababishwi tu na uendeshaji mbaya wa pikipiki, mwenye gari anaweza kumgonga mwenye pikipiki. Kila wakati barabarani magari yanakwanguana lakini athari inakuwa ni ndogo sana kwa sababu yanakwanguana magari, abiria ndani wakiwa salama. Gari likiikwangua pikipiki, inamkwangua mwendesha pikipiki.
 
Vikoba havina msaada,

Ni hela yako inakatwa sijui, akiba sijui nini, wa kufaidi ni wachache.

Vikoba lazima mgombane mpaka mtishiane kurogana.

Kosa la Lema anasema ila hatoi option B, bila vikoba au bodaboda watu wapateje hela?
Tupatie uzoefu wako Mama mdenyi kuhusu vikoba.
 
Hizi boda boda biashara yake haijafikisha miaka 20, wakifikisha miaka 30 ndipo tutajua athari za hiyo kazi.
Kwa sababu za kisiasa tuendelee ziweka kwenye kundi la ajira
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…