Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

Lema ameendeleza dharau Kwa watu maskini akisema vikoba ni umaskini.

Ikumbukwe Vicoba ni ubunifu wa wamama katika kujikwamua ila kama kawaida kwa kuwa amefanywa kipofu Ili aumbuke amewatukana tena wamama.

Watu maskini eleweni kwamba huyo sio mtu wenu na kama hamuamini endeleeni kimshabikia.

 
Watu wote wanafiki wanaoshabikia kazi inayoua vijana wetu kwa idadi kubwa wamelaanika maana hawathamani maisha ya vijana wengi wanaoangamia na kupata ulemavu wa kudumu kila siku.

Serikali ithamini maisha ya vijana wetu. Itengeneze mazingira mazuri yatakayoeawezesha watu wafanye kazi halali, zinazowapatia kipato, hata kama ni vipato vidogo, lakini wawe salama.

Tuachane na wanafiki wanaishabikia vijana waendelee kuwa bodaboda, huku kazi yenyewe inawaua na kuwapa ulemavu kwa idafi kubwa, ilihali watoto wao hawawafanyi wawe bodaboda.

Amelaanika mtu yule anayemtumia binadamu mwenzake kufanya matendo ya hatari huku yeye akijinufaisha ama kwa mapato ama kwa umaarufu, wakati mtendakazi akipoteza maisha au kuwa kilema.

Tunafahamu, wapo wengi humu wanaitetea kazi ya bodaboda kwa sababu wamenunua pikipiki na kuwapa vijana wazitumie, huku wao wakiletewa pesa kila siku. Kama kweli ni kazi yenye baraka na salama, kwa nini hawanunui na kuwapa watoto wao wakatafutie pesa ili wawaletee?

Pikipiki ni usafiri wa mtu mmoja mmoja, tena kwa mazingira fulani tu, haustahili kuwa usafiri wa umma. Uendeshaji wa pikipiki una risk kubwa ya kiusalama kwa sababu tatizo dogo la barabarani, mwendesha pikipiki anakuwa victim wa kifo au ulemavu.

Uhalali wa kazi hautokani na ukweli tu kuwa kwa sababu unapata kipato. Leo boda boda mpaka wanatengewa wodi zao mahospitalini, halafu mtu mjinga na mnafiki anatetea kuwa ni ajira inayostahili kuendelezwa! Tusiwe wanafiki, tujali maisha ya vijana hawa kama tunavyoyajali maisha yetu na ya watoto wetu. Vijana hawa wapo tayari kuhatarisha hata maisha yao kwa sababu jamii imeshindwa kuwapa hifadhi. Hili siyo tatizo la waendesha bodaboda bali ni tatizo la jamii yetu nzima.

Watu Kufa au Kupata ulemavu Kwa sababu ya bodaboda ni Kutokana na ukosefu WA Elimu katika kazi hiyo na kutofuata sheria za udereva na usalama Barabarani, Na sio kuwa kazi hiyo ni Laana.

Ni jukumu la serikali kuandaa Mpango na utaratibu na kuupa nguvu kuhakikisha ili uwe bodaboda na uendeshe MTU lazima upate mafunzo na upewe Leseni,
Kisha iundwe sheria kuwa endapo utakuwa hauna Leseni na hauna cheti cha mafunzo utapewa adhabu ya kifungo cha muda Fulani.
Pia endapo utasababisha ajali na hauna Leseni wala mafunzo itahesabika kama umefanya mauaji ya kukusudia

Ni Sawa na MTU ajenge nyumba alafu Hana gani ya uhandisi majengo, nyumba ikianguka anapaswa kupewa adhabu Kali. Lakini huwezi sema ujenzi wa nyumba au ufundi Washi ni Laana.

Ndio maana Elimu ni muhimu.
Lakini sio Elimu ya kupotosha Watu kuwa kuna kazi ni Laana ilhali sio Laana.
Ndivyo wasomi wengi WA siku hizi mlivyo,
 
Kwako kipi Bora?
Kufanya uzalishaji ulipwe 140,000 Kwa mwezi
Au kufanya bodaboda upate Kwa Siku 10,000/=

Sijasema hao wazalishaji WA viwandani wanafanya vibaya, Nop! Kila mmoja afanye anachoona kipo Mbele yake na anachoweza kufanya.

Kufanya kazi sio tatizo, hakuna serikali duniani inayotaka Vijana wake wateseke, ni kwamba Serikali na taifa lenu na mataifa ya Afrika tayari yameshazidiwa Step na washidani wao wazungu.

Wewe hata ungepewa Urais Kwa miaka 100 huna ambalo utafanya,
Ni vigumu kuelewa mambo haya
Umekosa uelewa. Suala siyo kiwango cha mapato ndicho kinachoifanya kazi fulani kuwa ya baraka au ya laana.

Kama kipato kikubwa ndiyo kipimo cha ubora wa kazi, basi ujambazi ungekuwa ni kazi bora sana kwa sababu jambazi, kwa mara moja anaweza kuiba milioni 50.

Panua mawazo yako ufanye argument sensibly.
 
Lema ameendeleza dharau Kwa watu maskini akisema vikoba ni umaskini..

Ikumbukwe Vicoba ni ubunifu wa wamama katika kujikwamua ila kama kawaida Kwa kuwa amefanywa kipofu Ili aumbuke amewatukana tena wamama..

Watu maskini eleweni kwamba huyo sio mtu wenu na kama hamuamini endeleeni kimshabikia.

Akili ndogo haiwezi kuelewa positively ilichoongea akili kubwa. Lema analenga kuwamsha msiridhike na maisha hayo bali mdai Serikali iwajengee mazingira ya kupata maisha bora zaidi.
 
Huyu jamaa hajui kuongea, ni wa kumpa taifa aongoze kweli? Ina maana aliokuwa anawatetea JPM wenye kipato cha jinsi hiyo wana laana? Hao hoa kwa kuwa ni wengi kidemokrasia ndio wanaokupa uongozi.
 
Anaandika, Robert Heriel

  • Kazi na kuwa kipato duni hakuifanyi kazi hiyo kuwa ya Laana.
  • Kazi kufanywa na watu wasio na Elimu hakuifanyi kazi hiyo iwe ya Laana.
  • Kazi kufanywa pasipo kufuata utaratibu hakuifanyi kazi hiyo kuwa na Laana.

Kazi ni ibada kwa wale waamini na waaminio. Kazi yoyote halali aifanyo mtu ni ibada. Lakini pia kufanya kazi kisheria ni kutimiza wajibu ndani ya taifa. Kusema kazi Fulani ni Laana kisa mapato ya Kazi hiyo ni duni, ni dharau na ujinga wa msemaji.

Kazi kuwa hatarishi haimaanishi kuwa ni kazi ya Laana. Bodaboda ni kazi kama kazi zingine, Umachinga ni kazi kama kazi zingine, Udalali ni kazi kama kazi zingine, Ukuli na upiga Debe ni kazi kama kazi zingine.

Ni mtu mpumbavu na mjinga asiyeelewa mambo hayo.

Lena anadharau sijui Vikoba kisa watu wanachanga bukubuku au elfu tatu, hizo pesa zinazochangwa sio pesa za wizi, ni pesa halali, hawajamuibia mtu. Ni jasho Lao, dharau na Kiburi sio Kizuri.

Kwa Watu waungwana, wasomi walioelimika, wenye maadili na hofu ya Mungu huwezi kuwasikia wakiongea mambo ya hovyo kama hayo.

Lema kama mtu ajionaye mwenye akili, exposure na aliyewahi kuwa kiongozi kwa nafasi ya Ubunge, pamoja na sisi wasomi na watu wa serikali pamoja na viongozi wa dini tulipaswa kufanya haya yafuatayo;

1. Kuzitambua kazi mpya zilizozuka hivi karibuni kutokana na mapinduzi ya Teknolojia na ujio wa Utandawazi. Kazi kama za bodaboda, umachinga, kazi za mitandaoni, kazi za udalali n.k, ni muhimu kuzitambua.

2. Kuziwekea Sera, Sheria na Kanuni ili kuwapa Haki na Fursa watakaojiingiza humo.

3. Kutunga na kuingiza mitaala ya kozi fupi na ndefu zitakazofundisha kazi hizo kwa gharama nafuu, ili kuzipa thamani kazi hizo. Kupitia Elimu na Sheria zitakazotungwa kutakuwa na maadili ya hizo kazi.

Utoaji wa Elimu utasaidia kazi hizo kutokufanywa kiholela. Kutawafanya wafanyaji wa kazi hiyo kuwa nadhifu kimavazi, pia utumiaji wa lugha fasaha na zenye nidhamu utazingatiwa kwani ni sehemu ya kazi.

4. Kuandaa mfumo wa Bima ya Afya kwa gharama nafuu inayolingana na kipato cha kazi hizo. Bahati nzuri siku hizi ipo ile Bima ya CHIF ya elfu 40.

5. Kuandaa mifumo ya ulipaji wa Kodi au Ushuru kulingana na eneo la kazi. Hii ni kumfanya kila mtu awajibike kuijenga nchi.
Kwa mfano bodaboda akilipa elfu hamsini kwa mwaka kama Kodi haiwezi kumshinda. Hata hivyo pesa hiyo lazima iingizwe moja kwa moja kwenye Leseni ili kuepusha usumbufu.

Leseni na Kodi isizidi 100,000/= kwa upande wa madereva bodaboda. Kama dereva bodaboda ni wa kuajiriwa basi watashare yeye na bosi wake gharama ya Kodi, huku Leseni ikibaki kuwa wajibu wa dereva mwenyewe. Mfano kama Kodi ni 50,000 kwa mwaka basi mmiliki wa bodaboda atalipia 25,000/= na dereva bodaboda atalipia 25,000/= Kwa Mwaka. Huku gharama za Leseni ikibaki kuwa ya dereva.

6. Angalau kila mwaka itolewe semina ya madereva bodaboda, na mafunzo kwa Madereva bodaboda kwa ngazi ya Kata.
Kazi Hii waifanye Polisi Kata wakipewa Posho kwa kazi hiyo watakayoifanya.

7. Iundwe Programu ya kuhamasisha watu kupenda kazi zao bila kujali wanapata kiwango gani cha fedha na iundwe sheria ni marufuku kwa mtu kutoa maneno ya kashfa kwa kazi zingine; yaani maneno ya kutusi, kudharau na kujeli kazi zingine, ili kukifanya kizazi kinachokuja kisije lukua na kasumba mbaya kuhusu baadhi ya Kazi. Kudharau kazi za wengine ni chanzo kikuu cha janga la ajira.

8. Kutokana na nchi yetu bado ni Maskini, kazi za umachinga haziepukiki, utaratibu maalumu hasa katika ngazi ya Serikali za Mitaa uundwe ili kuhakikisha unasimamia machinga katika maeneo waliyomo nje ya katikati ya jiji.

Wawekewe muda maalumu wa kuendesha shughuli hizo kwa kupanga pembeni ya barabara sehemu ambazo ni salama (nasisitiza sehemu ambazo ni salama). Kwa mfano kuwaruhusu wafanya shughuli hizo kuanzia saa 11:00 jioni mpaka saa 4:00 usiku chini ya masharti yafuatayo;

  • Kuhakikisha eneo hilo ni Safi kabla na baada ya biashara.
  • Kutokupanga biashara kwa wapita njia.
  • Kutoa Ushuru kila siku labda ni buku, au kiwango chochote kulingana na eneo bila kutoa excuse yoyote ya sijui sijauza au nimeuza.
  • Kutokujenga kibanda chochote eneo hilo.
  • Kufanya biashara kwa muda uliopangwa na Serikali.
  • Kuuza bidhaa halali.
  • Kuuza bidhaa zenye thamani itakayowekwa na Serikali kama itakavyoona inafaa, labda tuseme bidhaa zitakazopangwa barabarani ziwe bidhaa ndogondogo mfano nguo, matunda, maji n.k na sio mtu aweke biashara yenye mtaji wa mamilioni ya pesa.
  • Kulipa Faini ya kiwango kitakachowekwa na Serikali au kufukuzwa eneo hilo na kutopewa eneo jingine ikiwa atavunja kwa makusudi taratibu zilizowekwa n.k.

Kitu kikubwa ambacho Lema angekisema ni kuiambia, au kuilaumu serikali kwa kushindwa kuwasaidia hao wenye hizo kazi anazoziita ni za laana. Na sio kuwaponda watu walioamua kujishughulisha kwa shughuli halali.

Au anafikiri kuwa mwanasiasa kwa kupiga mdomo na kubwabwaja kwenye majukwaa ndio kazi ya baraka au kazi bora kuliko kazi nyingine? Kila kazi ni bora itategemea na mtazamo wa anayeifanya.

Wapo Watu ambao hata uwaambie wawe wabunge hawatotaka kuwa wanasiasa. Kudharau kazi ya mtu mwingine au kipato cha mtu mwingine ni dalili ya kutokuwa muadilifu, dalili ya kiburi na ushamba fulani hivi.

Unadharau kazi ambayo kuna watu wanaendeshea familia zao, wanatoa Sadaka kwa Miungu yao, Wanahudumia watu katika maeneo yao. Wewe kwa akili yako ndogo unawakejeli.

Watu wanatafuta Maisha mazuri lakini kupata pesa nyingi haimaanishi ndio maisha mazuri. Maisha mazuri ni kupata kipato halali kwa kazi halali, kwa jasho lako. Tuache kudharau Watu na kazi zao.

Ujumbe huu umemtumia Lema kama mwakilishi wa watu wote wenye dharau na kejeli na Kiburi, sio kwa Lema peke yake.

Nawatakia Sabato njema.

Ni yule Mtibeli,

Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
Sikudhani nawe unaweza kuwa na akili ndogo! Na kwa hakika akili ndogo haiwezi kuelewa positively ilichoongea akili kubwa. Lema analenga kuwamsha msiridhike na maisha hayo bali mdai Serikali iwajengee mazingira ya kupata maisha bora zaidi.
 
Lema ameendeleza dharau Kwa watu maskini akisema vikoba ni umaskini.

Ikumbukwe Vicoba ni ubunifu wa wamama katika kujikwamua ila kama kawaida kwa kuwa amefanywa kipofu Ili aumbuke amewatukana tena wamama.

Watu maskini eleweni kwamba huyo sio mtu wenu na kama hamuamini endeleeni kimshabikia.


HAo hightablers wengi vi vikoba
 
Hapo kwenye Laana ndio unashindwa kupaweka Sawa.
Laana maana yake ni nini?

Bodaboda sio tatizo, Hilo liko wazi.
Ni Ajira nzuri mno inayohitaji utaratibu tuu.
Kusema bodaboda ni Laana Wakati sio shughuli haramu ni dalili ya kutojua maana ya istilahi "Laana"

Ninarafiki zangu wanamiliki makampuni yanayohusiana na hizo bodaboda.
Wanafanya Free delivery na kusafirisha packaging Kutoka eneo moja kupeleka eneo jingine. Wanapata Pesa nzuri tuu(ingawaje Hii sio kipimo)
Kazi yoyote inahitaji Akili ya MTU na mtazamo chanya Kati kazi hiyo
Ajira ya bodaboda ni laana ya nchi yetu. Laana hutokea pale mtu au nchi in this case inapotawaliwa na viongozi wavivu, wezi na wazembe.
 
Umekosa uelewa. Suala siyo kiwango cha mapato ndicho kinachoifanya kazi fulani kuwa ya baraka au ya laana.

Kama kipato kikubwa ndiyo kipimo cha ubora wa kazi, basi ujambazi ungekuwa ni kazi bora sana kwa sababu jambazi, kwa mara moja anaweza kuiba milioni 50.

Panua mawazo yako ufanye argument sensibly.

Oooh!
Wenzako tumesomea mambo ya Lugha. Tunapomsikiliza MTU akiongea au akiandika tunachujua ujumbe na dhamira juu ya alichokiongea. Wewe ambaye hujaelewa ujumbe wa Lema basi itakupasa urudi shule ufundishwe namna ya Kupata ujumbe pale MTU anapozungumza au mtu anapoandika.

Kwa kukurahisishia,
Lema kajikita zaidi kuuzungumzia umaskini na watu wenye kipato duni, katika mifano yake akachomekea Ubodaboda, Kwa hiyo bodaboda haikuwa Hoja kuu isipokuwa ni ndani wa kile alichokuwa anakieleza kwenye hoja Ya Hali duni ya watanzania,
Akatoa mfano mwingine wa Serikali kugawa Gesi, bado hujapata ujumbe wa kile anachokizungumza?
Akatoa mfano WA Vikoba, akichomekea mfano mdogo wa Mke wake aliyecheza kikoba Mwaka mzima lakini kwenye kuvunja kikoba akashangaa kuna laki na busy.
Bado huelewi mantiki ya hotuba ya Lema?

Ili mtu awe na Hali duni bila Shaka lazima awe anafanya kazi yenye kipato DUNI. Hata hivyo sio Kwa wote.
Bado hujaelewa?
Hujui ni Kwa nini wanasiasa wanapenda Kutumia mifano ya machinga, bodaboda, na waalimu?
Bado hujaelewa mantiki ya Lema.

Nilichoandika ndicho ambacho kulikuwa ujumbe Katika hotuba ya Lema

Kama hukusoma Lugha omba usaidiwe
 
Labda kama unafikiri ulisikia na kuona mwenyewe lakini tulimsikia na kumuona akisema hivyo, kuwa bodaboda ni kazi ya Laana.
Mimi naweza kuiita ni kazi ya laana kwa context moja tu, siyo kazi salama. Inaua vijana wetu wengi wakiwa kwenye umri mdogo sana, na kuwaacha wengi wakiwa na ulemavu.

Kuna wakati, kwenye kampuni yetu, tuliamua kuwapa mikopo isiyo na riba wafanyakazi wetu. Vijana wengi kwa kutumia pesa hiyo wakaamua kununua pikipiki. Ndani ya wiki 3 tukawapoteza vijana 4 na mzee 1 mwenda kwa miguu kwa ajali za pikipiki (aliyegongwa na kijana wetu). Iliumiza sana. Tukasimamisha mikopo. Mwanzoni tukafikiria tutoe conditions za mkopo, kuwa hakuna atakayeruhusiwa kutumia hela ya mkopo kununulia pikipiki. Lakini tukaona kuna shida, maana mkopaji akinunua pikipiki, bado inakuwa ni vigumu kutambua kama ametumia hela ya mkopo au hela yake ya mshahara au mapato mengine. Tukaamua tuzidishe mafunzo, yaliyohusisha wataalam mbalimbali. Tukafanikiwa, mpaka leo hatujashuhudia kifo chochote cha ajali ya pikipiki kwa wafanyakazi wetu.
 
Back
Top Bottom