Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

Vicoba sio kuhifadhi pesa. Wanakopeshana na riba inakuwepo, kuna faini ndogo ndogo pia. Ni kanuni ya Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu. Kama vicoba havina kazi, basi mfumo wa kukopa pesa nyingi benki na kurudisha nyingi kuliko uliyokopa haina maana pia.
Inaonesha Godiblesi yeye haheshimu complexity ya maisha.
 
Asilimia zote nakubal. Angalia wenzetu wanzungu kama wana vikoba. Wenzetu mshaara unapangwa na serkar unajikimu na kuweza ku save. Shida ya sisi uwez save
 
Kwani ajali za barabarani hasa mabasi ya mikoani huwa haziui? mbona kuna wakati zinafululiza mpaka watu wanashtuka?

Kwa hiyo tuseme na kuendesha mabasi ya mikoani pia ni kazi ya laana?

Bodaboda wana umuhimu wao kwenye jamii yetu, hawa kinachohitajika kwao ni kupewa elimu ya kujikinga na ajali, na wazingatie sheria za usalama barabarani.

Jitahidi kupunguza hisia kwenye maandishi yako, tafakari kwa kina.
Nenda jeshi la Polisi ukapate takwimu za ajali za bodaboda. Hakuna hata siku moja inayopita bila ya vifo vilivyosababishwa na ajali za bodaboda.

Ajali zipo kwenye shughuli zote, za usafirishaji, uzalishaji, hata kwenye starehe. Lakini ajali kugeuka kuwa janga ni pale idadi yake inapokuwa ya kupindukia.

Uliwahi kusikia kuna hospitali imetenga wodi maalum kwaajili ya waliopata ajali za mabasi? Lakini kwa bodaboda, zipo. Mpaka hapo, hupati tu ujumbe, hata kama huna access ya takwimu za ajali nchini?
 
Vicoba ni dalili ya umasikini kwenye jamii, baadala yake watu wafundishwe namna yakuwa productive popote walipo, familia zifundishwe uwekezaji wa viwanda vidogovidogo hata majumbani ziwe zinafanya production ya quality products kwa ajili ya viwanda vinavyofanya mass production...
Huko Vicoba Wana source vitu gani? Hayo unayosema kwani hayafanyiki Veta na sido?
 
Asilimia zote nakubal. Angalia wenzetu wanzungu kama wana vikoba. Wenzetu mshaara unapangwa na serkar unajikimu na kuweza ku save. Shida ya sisi uwez save

Hata Tanzania mbona watu wanasave tu pesa
 
Vicoba sio kuhifadhi pesa. Wanakopeshana na riba inakuwepo, kuna faini ndogo ndogo pia. Ni kanuni ya Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu. Kama vicoba havina kazi, basi mfumo wa kukopa pesa nyingi benki na kurudisha nyingi kuliko uliyokopa haina maana pia.
Inaonesha Godiblesi yeye haheshimu complexity ya maisha.
Ni mropokaji haelewi chochote,eti huyu ndio anataka Kugombea na Kuna watu watamchagua 🤪🤪
 
Kama Lema aliita bodaboda ni kazi ya laana kwa sababu ina kipato kidogo, hapo alikosea. Kipato kidogo siyo kigezo cha kazi kuwa ya laana.

Lakini jambo moja lililodhahiri bodaboda ni tatizo kubwa linalohitaji ufumbuzi wa haraka ili kuwapa matumaini vijana hawa wanaoangamia kila siku.

Ndivyo ilivyokuwa mantiki ya kile alichokuwa anakiongea kuanzia mwanzo mpaka mwisho hasa alipogusa hoja ya Hali duni ya Maisha ya mtanzania,

Lema Adili na serikali na CCM, wananchi kwao atake uungwaji mkono.
Nilifurahi aliposema kuwa Wananchi wamelala, wanatetewa lakini wao wapo kimya, akatoa mfano Lissu mpaka anapigwa RISASI wananchi wapo kimya. Badala ya ku-react.
Angesema kuwa Lisuau au yeye alikimbia Nchi akiwa anawatetea wapate Haki zao ikiwemo Haki ya kufanya kile wakipenacho, sio ajabu wapo wanaopendahuo ubodaboda, Ila angewawekea mazingira mazuri wafanye bila Kupata madhara ya ajali za Uzembe, Haki za Kupata bima na kuweka Akiba katika mifuko ya hifadhi n.k
 
Lema ameendeleza dharau Kwa watu maskini akisema vikoba ni umaskini.

Ikumbukwe Vicoba ni ubunifu wa wamama katika kujikwamua ila kama kawaida kwa kuwa amefanywa kipofu Ili aumbuke amewatukana tena wamama.

Watu maskini eleweni kwamba huyo sio mtu wenu na kama hamuamini endeleeni kimshabikia.


Vikoba ni umasikini.
Vimevunja ndoa nyingi.

Mashamba yameuzwa.
NYumba zimeuzwa.
Fanicha ndio usiseme.
 
tunahitaji nguvu ya moja kwa moja kwenye kujenga nchi hasa kutoka kwa vijana.. Kijana wa boda boda anachotafuta ni hela ya kula yeye na kwa risk kubwa sana...

tungeweza kumpa ajira jeshini na kumpa mafunzo akawa hata operator wa tractor kwenye miradi mikubwa ya mashamba makubwa ya serikali chini ya JWTZ..
Kijana huyu akiwa jeshini tunampa mafunzo yatakayomfanya awe skilled labor force, lakini wakati huo huo anakuwa modern trained soldier ambaye ikitokea vita anakuja kama askari wa akiba.. Akiwa jeshini anazalisha, tunamlipa mshahara mzuri, tunampa bima ya afya na familia yake nk, anapewa mikopo nafuu kudevelop familia yake.

Hawa vijana wote tukiwatumia kwenye mlengo huo, in 5yrs taifa litakuwa na mashamba makubwa ya chakula na biashara, kwa mwaka tunaweza kuwa na kipato kikubwa sana kama Taifa...
Kwa hiyo hapa Tanzania Kuna upungufu wa ma operator wa matrekta si ndio? Hiyo unayoita kazi ya kula imewawezesha kuanzisha miradi Mingi tuu
 
Lema muongo kama alikuwa anakwenda kukagua migodi yake kwa kuvaa baibui, ukafikiri Serikali aina watu wake huko kwenye migodi? Serikali ikikutaka hata uchimbe shimo inakukuta huko kwenye shimo, Serikali kama ilikuwa inamwitaji hatawakati wa kuvuka mpaka angelikamatwa tu, mbona Nyarandu alirudishwa na akuna kilichompata!na mpaka Sasahivi yuko ccm anakula bata; Chadema uongo wanaotunga kuaribu sifa za Magufuli utawarudia tu, hauwezi kupanda kwa kukanyaga mtu au kimchafua ukadhani wewe utakuwa salama.Akuna jipya ambalo Magufuli alitenda ambalo watangulizi wake hawakuwai kulitenda.
Ni kweli
 
Lema ameendeleza dharau Kwa watu maskini akisema vikoba ni umaskini.

Ikumbukwe Vicoba ni ubunifu wa wamama katika kujikwamua ila kama kawaida kwa kuwa amefanywa kipofu Ili aumbuke amewatukana tena wamama.

Watu maskini eleweni kwamba huyo sio mtu wenu na kama hamuamini endeleeni kimshabikia.

Kukosoa na kupinga mambo pasipo kupendekeza njia mbadala wa nini kifanyike ni tatizo sana.
 
Back
Top Bottom