Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

Kwahiyo Lema anataka kusema vijana wasijipambanie wakae majumbani?

Huyu mzee wa canada amekula maharagwe ya wapi?

Akwende zake canada huko akauze mali kwa mabeberu. Shenzi type!
vijana wa kitila mkumbo na madelu wanaendesha bodaboda au wako BOT na TRA.
 
Mtungi wa gesi kg 13 huko Kenya huuzwa kwa Ksh 403 sawa na shilingi za kitanzania 7366
Mtungi wa gesi Kg 14.5 Tanzania huuzwa shilingi za kitanzania Tsh 55,000 sawa na Ksh3012

Tofauti:

Kenya mtungi wa kg 13 ni shilingi za kitanzania Tsh 7316
Tanzania mtungi wa kg 14.5 shilingi za kitanzania Tsh 55,000

Swali : Kenya wanachota gesi baharini?

Erythrocyte
 
Lema Ni mpuuzi mno ,vijana wakishika mapanga wanasema serekalin ya ccm haiwezeshi vijana wakifanya biashara ya bodaboda hyo Kaz Ni laaanaa jmn watu wajeukie wapi

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Kijana anapowaza na kuchukua hatua ya kufanya shughuli isiyo ya kihalifu ili kujipatia kipato halali anakuwa kafanya uamuzi bora kabisa, kuliko kukaa bila kazi au kuwa mwizi/jambazi/kibaka/panya road.
 
Mpe mwanao bodaboda Kama ni kazi nzuri u can never appreciate suffering of others if ur smart upstairs period , Lema is hating fucking life made by Ccm regime
Wewe mhaya na wewe ni bwege tu! Hivi hapa duniani watu wote wanaanzaga maisha na mafanikio? Hata vitabu vya dini vinasema mtu afanye kazi na Mungu atabariki kazi za mikono yake! Acheni ujinga tena nyinyi wahaya siku hizi ni maskini wa kutupwa!
 
Hamna ambaye hataki kijana wake apigwe kiyoyozi na kulipwa atleast million 5 kwa mwezi. Shida hizo kazi za maslahi hayo zina wenyewe.

Makapuku tunapigana vikumbo kwenye mishahara ya laki na nusu hadi laki 4. Hapo unahaso kweli ukiipata kazi ya laki 3 unashukuru Mungu unakubaliana na muhindi tu.

Kwa sasa kazi za kulipwa million 1 tu unaweza ukaota mvi hujawahi kukanyaga ofisi yeyote ile. Ni huzuni af unakuta kuna shogar mmoja anaongea mavi!
Hawa wanasiasa wetu wasiishie tu aina tu ya shughuli wanazofanya vijana wengi siku hizi kujikimu, wageukie na hizi ajira na ujira unaopatikana katika uhalisia.

Hawa wasajili line waliofikiwa leo, ni wafanyakazi katika makampuni makubwa tu ya mawasiliano, leo wamefikiwa na naamini ni kwa sababu ya kiasi cha ujira wanaolipwa. Ni kujiuliza tu, alipokua bungeni alifanya jitihada zozote kuweka msukumo bunge kutunga sheria/kufanya maboresho ya sheria kuweza kuongeza kiwango cha ujira kwa "hawa" waajiriwa hasa sekta binafsi?
 
Namsikiliza Mbunge wa zamani Nndg Lema Jembe FM, anahojiwa alipokeaje suala la yeye kufutiwa kesi zake.

Lema anadai moja ya vitu anavyompongeza Mama ni pamoja na yeye kufutiwa mashtaka pia mikutano ya kisiasa.

Amesema kitu pekee CCM walichoshindwa kufanya ni kutengeneza ajira za maana zaidi kwa Watanzania kujiajiri kwenye kazi duni kama bodaboda na kusajili laini.

"Nikisikia mwanangu ni bodaboda au anasajili laini inabidi atafute sehemu ya kukaa, kwangu simtaki tena," alisema Lema.

Mwamba kaamua sasa.

Inawezekana ana hoja, lakini atoe muongozo nini kifanyike ile hao boda boda waweze kuendesha maisha yao!!!! Sizani kama wao wanapenda izo shughuli ila wengi wao elimu ni duni, wenye elimu pia ajira hakuna, boda boda bajaji ni kazi raisi isiyohitaji mtaji, ukiwa na boss tu anakupa unazungusha unaleta pesa na wewe unabaki naya kula!!! Lakini nini kifanyike vijana ni wengi wapo mtaani na life ni ngumu ile mbaya, waganyaje wakae tu na kama wakiamua kukaa tu bila kazi si ndo makundi yataibuka nchi nzima ya panya road?

Hakuna amani kwenye njaa, yeye aseme nini kifanyike
 
kwa mazingira ninayoishi na pasingukuwepo na hawa bodaboda bas ata uchumi wangu huu nilionao japo kidogo ningeusikia tu kwawenzangu, maana inaturahisishia sana safari, unapenyapenya vichocho kwa TVS mara town hii apa.

mbarikiwe sana bodaboda ila muwe na nidhamu ktk chombo
 
Mtungi wa gesi kg 13 huko Kenya huuzwa kwa Ksh 403 sawa na shilingi za kitanzania 7366
Mtungi wa gesi Kg 14.5 Tanzania huuzwa shilingi za kitanzania Tsh 55,000 sawa na Ksh3012

Tofauti:

Kenya mtungi wa kg 13 ni shilingi za kitanzania Tsh 7316
Tanzania mtungi wa kg 14.5 shilingi za kitanzania Tsh 55,000

Swali : Kenya wanachota gesi baharini?

Erythrocyte
Hili sio kweli mkuu fanya uchunguzi zaidi, sio kenya nao jua mimi.
 
Ameiambia ccm ifanye kitu msianze kumshambulia.

Tatizo la maskini akiambiwa ukweli anachukia badala ya kutafakari
Serikali haiwezi kufanya kitu kuhusu suala la Ajira, huelewi?

Serikali inachokijua ni kukusanya Kodi na tozo na kubomoa vibanda kuhusu Ajira Serikali anajifanya ahusiku huku wazazi wakigoma kuwapeleka watoto shule wanapomaliza darasa la 7 wafanye issue zingine za MIKONO na kusaidia familia zao km kulima majaruba na kuuza mabumunda Serikali hio hio inawafuata nyumbani wazazi kwa vitisho eti waende shule kwa lazima na wakimaliza kusoma muda wamepoteza shuleni Ajira Serikali haiwapi so what do you expect? Watoto wamepoteza muda mwingi shuleni wanamaliza shule Ajira hakuna,

Ningeona Serikali ina akili wangesema mwanafunzi ukimaliza la 7 usilazimishwe kwenda Sekondari amua mwenyewe unataka uende wapi mradi ushaondoa ujinga kichwani basi pambana na maisha mengine usingeona vijana wanataabika hivi wengi wangekua na mishe zingine kitambo huko muaroni na kwenye majaruba ya mpunga
 
Hivi wewe na Lema mnajua kwamba kuna watu wanalipwa elf 4 kwa siku na wengine elfu 6 katika viwanda vya the so called matajiri wa kibongo bongo hawa?

Lema anatambua kuwa kuna graduates wanalipwa laki 2 kwa mwezi katika situation hii ambayo nauli zinakaribia buku na bei ya nafaka kwa kilo ni zaidi ya dollar 1?

Mngeanza na kutatua hizi changamoto nadhani hio option mnayoifikiria ingekuwa na maana zaidi!
Tatizo la jamii yetu tunaonaga tatizo tu pasipo kujua chanzo cha tatizo, maana Leo hii role model wa vijana wengi ni wale waliopata mafanikio kwa zari Yani njia zilizofanya wakafanikiwa hamuwezi fanikiwa Kundi kubwa mfano mziki, uigizaji, mpira, at the end vijana wanashindwa komaa na njia sahihi mfano shule, au kujifunza ujuzi njia ambayo imefanikisha Kundi kubwa la watu matokeo yake vijana wanataka Short cut, udereva boda boda, akabet, sijui awe muigizaji au msanii vitu ambavuo vinawapotezea mda tu

Boda boda haiwezi kufanya ukawa na kipato imala Cha kubadilisha maisha zaidi ya kupata pesa ya kula tu, kununua sabufa za mchina, frat screen za mchina, sofa za magumashi, ukala wali maharage usiku ukajiona umeyaweza maisha ila ukiumwa week mbili tu upo ndani unaanza kuuza vitu vyako

My take
Shughuli ambayo utaugua ukalala ndani wiki moja familia ikaanza. Kupata shida ya pesa za matumizi siyo ajira hiyo acha
 
Shida ni kwamba na wanaoleta taarifa za Lema humu wanadokoa statement tata wanaleta hivyohivyo bila maelezo ya ziada au source of information,watu wanaanza kujadili kila mtu na fikra zake.

Mfano kuna Uziuliwekwa humu,Lema kasema kujenga ukuta Mererani ni ushamba(hio ilikuwa heading)ila source haikuwekwa,nilipofualitilia ni kweli alisema hivyo ila kuna maelezo mengi alitoa kuhusu hilo na alitoa ushauri mzuri tu,na akasema kwa kuwa viongozi wote wapo Arusha(semina) atawashauri mawazo yake.

Nadhani tunahitaji media serious imualike kwa mahojiano atoe ufafanuzi juu ya kauli zake hizi,tujue hasa anamaanisha nini.

Leo East Africa radio walikuwa na uongozi wa Bodaboda Dar,wale viongozi nao walilaumu hio kauli wakisema kwamba watu wanasomesha wanajenga na kwa siku boda hakosi 30,000(Siku mbaya) kwamba kwa mwezi hakosi 800,000 na kwamba wanawazidi hata kada fulani ya waajiriwa serikalini.

Baadae mtangazaji akaanza kuwadadisi,kama mna kipato hicho inakuwaje mnakosa bima ya afya ya 600,000 kwa mwaka?wakaanza bla bla kwamba hio tumetaja ni kama ukiweka akiba,wakaambiwa kwa takwimu za muhimbili kila siku wanapokea majeruhi 6 wa bodaboda pale,wakadai eti hao sio bodaboda ila ni vijana wa mikoani wameletwa kubeba mayai kusambaza kitu ambacho ni uongo.

Je unaweza kufanya kazi ya Bodaboda kuanzia ujana hadi uzee?Je utapenda mtoto wako arithi kazi yako? hawakuwa na majibu ya maana.

Ukweli ni kwamba kauli ya Lema kwa juu juuu inakera ila ukiingia ndani ukweli upo,Ilikuwa wamtafute Lema bahati mbaya naona hawakufanikiwa mpaka kipindi kinaisha.
Haya mambo ya kuweka heading za kimtego zilianzishwa na Millardayo na sasa kila mtu ambaye ana followers kuanzia 200k anatafuta template kwa ajili ya kupost habari kwa heading tata kama hizo

Wana habari hawaamini katika habari kuweza kuwavutia wasomaji kuchukua muda wao kuisoma.

Wanaamini mpaka kifanyike kitu cha ziada kuteka attention za watu ndio watu wanaweza kusoma au ku view habari zao.

Sasa sio wote wanaosoma au ku view habari yote kusikiliza the whole speech, wengi wakisoma heading inawatosha kuanza kujaji contents ya ndani (ambayo hawajaisoma wala kui view)
 
Tatizo la jamii yetu tunaonaga tatizo tu pasipo kujua chanzo cha tatizo, maana Leo hii role model wa vijana wengi ni wale waliopata mafanikio kwa zari Yani njia zilizofanya wakafanikiwa hamuwezi fanikiwa Kundi kubwa mfano mziki, uigizaji, mpira, at the end vijana wanashindwa komaa na njia sahihi mfano shule, au kujifunza ujuzi njia ambayo imefanikisha Kundi kubwa la watu matokeo yake vijana wanataka Short cut, udereva boda boda, akabet, sijui awe muigizaji au msanii vitu ambavuo vinawapotezea mda tu

Boda boda haiwezi kufanya ukawa na kipato imala Cha kubadilisha maisha zaidi ya kupata pesa ya kula tu, kununua sabufa za mchina, frat screen za mchina, sofa za magumashi, ukala wali maharage usiku ukajiona umeyaweza maisha ila ukiumwa week mbili tu upo ndani unaanza kuuza vitu vyako

My take
Shughuli ambayo utaugua ukalala ndani wiki moja familia ikaanza. Kupata shida ya pesa za matumizi siyo ajira hiyo acha
Hapo mambo yako bayana kabisa, yani kazi hizo ni hand to mouth.
 
Back
Top Bottom