Asante sana Bernard Kammilius Membe, Una kichwa kikali na ni mzalendo wa kweli

Asante sana Bernard Kammilius Membe, Una kichwa kikali na ni mzalendo wa kweli

Membe sio lazima kuvifuata vyama vya ACT,Chadema au CUF.
Kama atakuja na wimbi la watu wengi maarufu anaweza akatengeneza CCM B.tokana na vyama ambavyo havina mbunge hata mmoja.
Aende nccr
 
Kama umekula pesa za Membe ili umuuze uzirudishe hauziki kabisa, niweke historia sawa, Membe katimuliwa hajajitoa ccm
 
Hivi nyie wenzetu huwa mnapata wapi hela za kina Membe? Maana hela ya Lowassa sikuipata, na hii ya Membe pia sijaipata. Naona nyie wenzetu mnaopata hela za hawa wazee wa ccm, mna nguvu za kuandika makala za kuwapamba, lakini matokeo yote yanafahamika. Ila somo la Lowassa liko vizuri kwenye kichwa cha kila mpinzani wa kweli, asiye na maslahi binafsi na hao wazee wasaka madaraka toka ccm. Mleta uzi angalia pesa za Membe zisikufanye uchafue taswira ya upinzani, kwa sababu ya maslahi yako binafsi.
Mkuu tindo mpaka sasa sijasikia membe anasimamia nini, Ana falsafa gani ya kuongoza saiasa na uchumi ulioharibika?

Hajawahi andika makala kwenye gazeti, Wala journal, hajawahi kuhonjiwa na media za kitaifa na kimataifa, hajawahi andika kitabu, amezidiwa na jericho nyerere,
Hajawahi jitambulisha humu jf Kama ,.verified Member tumuhoji maswali magumu,

Huyu membe msomi anakosea wapi?
Ajitokeze tumuhoji tumpime kwanza

Ukiangali video clips za mwalimu nyerere na maachapisho yake wakati anapigania Uhuru ndo utajua ninacho maanisha
 
Hivi nyie wenzetu huwa mnapata wapi hela za kina Membe? Maana hela ya Lowassa sikuipata, na hii ya Membe pia sijaipata. Naona nyie wenzetu mnaopata hela za hawa wazee wa ccm, mna nguvu za kuandika makala za kuwapamba, lakini matokeo yote yanafahamika. Ila somo la Lowassa liko vizuri kwenye kichwa cha kila mpinzani wa kweli, asiye na maslahi binafsi na hao wazee wasaka madaraka toka ccm. Mleta uzi angalia pesa za Membe zisikufanye uchafue taswira ya upinzani, kwa sababu ya maslahi yako binafsi.
Mkuu tindo nilikasirika Sana Dr slaa alipoondoka CDM , nilishamsamehe lakini nimejifunza vitu vingi toka kwake,

sasa huyu membe anakuja opposition ili iweje?
 
Mkuu tindo nilikasirika Sana Dr slaa alipoondoka CDM , nilishamsamehe lakini nimejifunza vitu vingi toka kwake,

sasa huyu membe anakuja opposition ili iweje?

Sijui hata Membe katuonaje wapinzani. Nashangaa sana wapinzani wenzetu wanapompigia Membe debe, kana kwamba hatuna uwezo wowote wa kuelewa mambo. ACT wazalendo wakimchukua wao ni sawa, ila cdm wakithubutu ndio watatupoteza wafuasi wao. Wasitegemee sisi kumuunga mkono msaka madaraka kama Lowassa. Akipokelewa na kuwa mwanachama wa kawaida sawa, ila sio apewe nafasi ya kugombea urais.
 
...nakubaliana na wewe kwa kila kitu kuhusu huyu mwamba -Member,.ila wampokee kama member asipewe nafasi ya kugombea urais.
Lissu akipeperusha bendera ya urais -kina Membe &co.wawe benchi la ufundi na fitina za kumtoa jiwe.

...otherwise-naunga mkono hoja

Umewakilisha vizuri mno mawazo niliyokuwa nayo kuhusu Membe. Thanks to you mheshimiwa.
 
Sijui hata Membe katuonaje wapinzani. Nashangaa sana wapinzani wenzetu wanapompigia Membe debe, kana kwamba hatuna uwezo wowote wa kuelewa mambo. ACT wazalendo wakimchukua wao ni sawa, ila cdm wakithubutu ndio watatupoteza wafuasi wao. Wasitegemee sisi kumuunga mkono msaka madaraka kama Lowassa. Akipokelewa na kuwa mwanachama wa kawaida sawa, ila sio apewe nafasi ya kugombea urais.
Mbowe atapoteza support kiduchu tunayompa
 
Sijui hata Membe katuonaje wapinzani. Nashangaa sana wapinzani wenzetu wanapompigia Membe debe, kana kwamba hatuna uwezo wowote wa kuelewa mambo. ACT wazalendo wakimchukua wao ni sawa, ila cdm wakithubutu ndio watatupoteza wafuasi wao. Wasitegemee sisi kumuunga mkono msaka madaraka kama Lowassa. Akipokelewa na kuwa mwanachama wa kawaida sawa, ila sio apewe nafasi ya kugombea urais.

Uko sahihi kabisa kiongozi.
 
Chama kilichounda Mwamuzi, Mfadhili na Msimamizi wa Shughuli ya Kiserikali, ya kampeni na upigaji kura, usimamizi wa matokeo, na utangazaji matokeo, ndio kitashinda.
 
View attachment 1499858

Tukio lililotokea jana la Mheshimiwa Membe Kutangaza Kujitoa "RASMI" ndani ya chama cha CCM sisi wapenzi wa Demokrasia tumelipokea kwa furaha kubwa, na kwa hakika limethibitisha jambo moja kuhusu Mheshimiwa Membe, nalo ni kwamba Brother Bernard Kammilius Membe hatanii, habeep, Anapiga!. Sisi wapenda demokrasia tunachambua kitendo hicho cha Membe kama ifuatavyo:

1. Membe ameukwepa mtego aliokuwa amewekewa na Jiwe
Sote tunajua wazi, Kufukuzwa kwa uananchama wa Ndugu Membe kulitokana na hofu tu ya Jiwe asipate ushindani ndani ya Chama katika kinyang'anyiro cha kugombea uchaguzi kupitia CCM. Maamuzi ya kumfukuza uanachama hayakuwa halali kwa mujibu wa katiba ya chama chao kwa hiyo kikanuni Membe alikuwa bado ni mwanachama halali kabisa ila kwa mujibu wa Udikteta wa mtu fulani hakuwa mwanachama.

Kikao kinachopaswa kuthibitisha kufukuzwa uanachama wa Membe ni halmashauri kuu ya chama, kwa hiyo ni dhahiri kikao hicho kingeitishwa baada ya zoezi la kuchukua fomu ndani ya chama hicho kufungwa na hivyo kama maamuzi ya kumfukuza yangekubaliwa au kukataliwa na kikao hicho tayari Membe angekuwa ameshapitwa na deadline ndani ya chama ya kuchukua fomu, na pia kwa muda huo tayari angekuwa amechelewa basi la upinzani ambalo by that time lingekuwa limeshaweka tayari options zake!

Kitendo cha Membe kuamua kuchomoka mwenyewe RASMI sasa ni timing nzuri sana, na hii inathibitisha uwezo mkubwa wa Mheshimiwa Membe wa kupiga mahesabu ya kisiasa!. Sasa hivi yupo kwenye better position kisiasa kuliko kama angeendelea kung'ang'ania kusubiri maamuzi ya kikao cha Halmashauri kuu Taifa ya CCM juu ya hatma yake.

2. Membe ana uchungu na nchi hii na ni mzalendo wa kweli
Kitendo cha kupambana akiwa ndani ya chama, wakati kila mtu ndani ya CCM akiwa ameufyata, kuogopa au kujipendekeza kwa Jiwe, hata hivyo Membe aligoma katakata kulamba viatu vya Jiwe. Membe alisimama na kusema ukweli juu ya namna nchi inavyoendeshwa. Membe anakumbukwa kwa kukemea siasa za hofu, siasa za kuumiza wapinzani, siasa za maguvu badala ya kupambana kwa hoja. Wakati Membe anasimama na kuyazungumza haya, hakuna key figure ndani ya CCM aliyekuwa akisimama waziwazi na kuyasemea haya. Kwa muktadha huu namuona Membe kama mtu ambaye enzi za ujana wake alifanya kazi Ikulu ya mwalimu nyerere kwa muda mrefu, Ni dhahiri ameathiriwa sana na falsafa za bosi wake huyo wa zamani katika kusimama bila woga kutetea haki na kupinga na kuchukizwa na vitendo vya uonevu dhidi ya watu wengine. Kwa muktadha huu ni dhahiri Membe ni mzalendo wa kweli sana.

3. Upinzani hauna haja ya kumhofia mheshimiwa Membe
Kuna wale ambao walikuwa dissapointed na Ujio wa Lowasa na kitendo ambacho Lowasa aliwafanyia wapinzani. Kiukweli kabisa siyo sahihi kumlinganisha mheshimiwa Membe na Lowasa. Kwanza Malengo ya kugombea urais kati ya Lowasa na Membe ni tofauti. Drive mojawapo kubwa ya Lowasa ya kugombea uraisi kwa udi na uvumba ilikuwa ni Kusettle score na akina JK. Lowasa alitaka kuwaonyesha kuwa naye anaweza kukalia hicho kiti akawanyoosha kama walivyomnyoosha yeye kwenye Richmond.

Lowasa hajawahi kuwa na Ajenda ya kupanua demokrasia zaidi au kutetea utawala wa sheria na ndiyo maana hajawahi tangu akiwa ndani ya CCM au nje ya CCM kutetea demokrasia pana isipokuwa tu pale maslahi yake yalipoguswa (mfano kutohojiwa kwenye ishu ya richmond, au alipokatwa ndani ya CCM). Tofauti na Membe ambaye kwenye utawala huu, kaonyesha wazi hapendi mambo ya kidiktetadikteta. Kwa muktadha huu, values za Membe zinaalign zaidi na msimamo wa upinzani kuliko Lowasa, hivyo ni sahihi wapinzani kumpokea na kushirikiana naye kulichomoa Jiwe kwenye uchaguzi unaokuja.


4. Kama CCM inanunua wapinzani, kuna ubaya gani upinzani ukachukua Majembe yanayoikacha CCM bure?
Siasa ni watu na mikakati. Kitendo chochote kinachochochea mgogoro au dissatisfaction kwenye kambi ya mwenzio basi kwako ni faida. Kitendo chochote kinachopelekea kuondoka kwa mwanachama au waunga mkono wa chama hicho na kuja kambi yako kisiasa ni jambo zuri cha msingi liwe managed vizuri!. Kama CCM inanunua wapinzani, kwa nini upinzani uone haya kuchukua watu potential waliomo ndani ya CCM?

Membe siyo mtu mdogo, ni mtu mzito, ana watu wengi mikoa ya kusini waliochoshwa na kuonewa kwao kwenye ishu nyingi ikiwemo korosho. Utamuachaje mtu kama huyu?, Yaani chance ya kupata kura za kusini uiachie hivi hivi wewe utakuwa mwanasiasa gani?. Najua hofu ni Lowasa, lakini kimsingi Namna issue ya Lowasa ilivyokuwa handled toka mwanzo ilikosewa. Lowasa alitakiwa apewe terms siyo yeye kudictate terms all tje time. Naamini Membe atakuwa teamworker zaidi kuliko kujiinua na kutaka chama na upinzani kumtumikia yeye badala ya yeye kushirikiana na wenzie as a team kuleta mabadiriko chanya ndani ya nchi.

5. Wananchi wanangoja kwa hamu maamuzi ya upinzani
Kiukweli kabisa kabisa kuna kundi la wana CCM wanaujuua ukweli kuwa upinzani kwa sasa ni kama volcano iliyodormant, wanajua kuwa upinzani upo na una nguvu isipokuwa kwa utaratibu wa kidikteta uliofanywa na utawala huu uko dormant temporarily. Nguvu hii ya Upinzani inahitaji Spark ili ilipuke, Spark kubwa ni kuonyesha Umoja, Mshikamano na kuwapa wananchi mtu aliyepikwa akapikika kiuongozi, mtu ambaye ana uwezo wa ushawishi na kujenga hoja, mtu ambaye akili yake ni inacharge.

Kwa hakika upinzani utanufaika sana na uwepo wa Membe katika rank za majemedari wao wa kulichomoa jiwe kwenye uchaguzi ujao. Hebu fikiria vichwa kama Lissu, Zitto, Mnyika, Mbowe, Maalim, Membe, Nyalandu vishirikiane kuzunguuka nchi nzima kupiga kampeni ya kulichomoa jiwe hali ya kisiasa nchini itakuwaje?. Mimi naona Patachimbika aisee, CCM watakuwa na wakati mgumu sana.

Hitimisho
Kitendo alichokifanya Membe cha kukataa kulamba viatu, na kusimama ndani ya chama kutaka mtawala anayekuwa amemaliza mhula wake wa kwanza awe challenged ni kitendo kizuri sana kwa mustakbali wa demokrasia na maendeleo yetu. Kitendo hicho kinasaidia mtawala asijione yuko entitled kutawala miaka kumi, bali aone kuwa kazi yake itakuwa evaluated kila baada ya miaka mitano na asipotosha chama kitamtoa.

Kwa muktadha huu Membe kapigania haki za wana CCM wengi kwenye suala la haki ya kuchagua au kuchaguliwa, haki ambayo pia inalindwa na katiba ya nchi. Kwa mitendo hiki tu ni dhahiri pia kuwa kama Membe atakuwa raisi, atatawala kwa mujibu wa sheria na katiba na hivyo hatokuwa dikteta!

Kwa maana hiyo kama ukinipa uchaguzi leo kati ya Membe na Magufuli, Membe anaweza kuwa booonge la raisi

Membe yuko vizuri
Membe anafaa!
Hapo namba 2 mkuu hueleweki kabisa, arudishe kwanza hela za Walibya, pia atuombe radhi watanzania kwa unafiki wake, tangu utoto wake ni sehemu ya serikari ya ccm, kazeeka eti leo haina Demokrasia! Akafie mbele huko kivyake
 
Membe akitaka kuitikisa ccm ni kuwashawishi hawa wafuatao waende upinzani!
1.Kinana
2.Nape
3.Makamba
4.January
5.Nchimbi
6.Sofia
7.Wote waliotumbuliwa waliokuwa katika madaraka ccm itaweweseka sema muda autoshi.
 
Mkia hauwezi kutikisa Ng'ombe
Membe akitaka kuitikisa ccm ni kuwashawishi hawa wafuatao waende upinzani!
1.Kinana
2.Nape
3.Makamba
4.January
5.Nchimbi
6.Sofia
7.Wote waliotumbuliwa waliokuwa katika madaraka ccm itaweweseka sema muda autoshi.
 
Back
Top Bottom