Uchaguzi 2020 Asante sana Tundu Lissu kwa kutetea Waislamu walioko jela kwa uonevu, Mungu akulipe kheri nyingi sana

Uchaguzi 2020 Asante sana Tundu Lissu kwa kutetea Waislamu walioko jela kwa uonevu, Mungu akulipe kheri nyingi sana

Ni bora akachaguliwa mwakilishi wa mabeberu walau tutendelea kuishuhudia demokrasia ila siyo mwakilishi wa BAHIMA EMPIRE, halafu mwaka 2025 tukaishia kutawaliwa kidikteta kama ilivyo Rwanda na Uganda.
marekani kwenyewe hakuna demokrasia sasa sijui unazungumzia demokrasia gani
 
Kama mahakama ya juu imeshaamuru mtu aachiliwe. Mahakama ya chini inaona kigugumizi gani ?!

Je mahakimu hawapo huru kufanya kazi zao ?! Au nini !!

Maelekezo kutoka juu!

Watawala wanaweza kuingilia mahakama ngazi zote, ila mahakimu wa chini wanawamudu zaidi kwa sababu zinaongozwa na mahakimu ambao hawana kinga ya kazi zao!

Kule mahakama za juu zenye majaji huwa wanapenyeza misimamo yao lakini wakati mwingine majaji husimamia haki bila hofu kwa sababu wana kinga za ajira na pia kulinda heshima ya kazi zao kwa sababu hukumu zao husomwa na majaji wengine duniani!
 
Muache ugaidi
_.m.u.k.u.n.a._-20200908-0001.jpg
 
Kama JPM ameweza kuwaachia akina babu Seya ambao walikutwa na hatia ya kulawiti na kubaka vitoto,iweje masheikh ambao hakuna ushahidi dhidi yao wanaendelea kusota rumande!!!!?
Waislam mchagueni Lissu akatende haki kwa waumini na viongozi wenzenu!
KWa mujibu wa sheria zetu, rais hana uwezo wa kumuachilia mtu aliyeko rumande, yule aliyefungwa hata maisha, yaani maadamu kahukumiwa na mahakama, rais anayo HAKI ya either kumpunguzia makosa au hata kumuachilia. KWa case ya ma sheikh, rais angeweza kushurutisha vyombo vyake hivyo vinavyo fanya uchunguzi, vifanye haraka ili viongozi wale wa dini wapewe HAKI yao kwa mujibu wa sheria zetu na hapa ndio Tundu anapopaongelea. In fact hata mimi nina amini wale masheikh hawana makosa au kama wanayo makosa basi USHAHIDI serikali HAINA na ndio maana haiwapeleki mahakamani, sawa tu na kina Rugemalulila; tukachague kiongozi anae penda HAKI ili AMANI idumu
 
Kwako Ndugu Lissu

Amani ya Mwenyezi Mungu iwe nawe
Napenda kuchukua fursa hii kukushukuru kwa dhati ya moyo wangu kwa kitendo chako cha Utu na kupenda haki kwako kwa namna unavyotetea Viongozi wa dini ya Kiislamu walioko Jela kiuonevu.

Umekuwa consistent sana kuhusu uonevu huu, umezungumzia kuhusu Masheikh zaidi ya 70 huko Arusha walioko jela, si kwa sababu wana makosa bali eti wanaipinga BAKWATA ambayo umma umeshatambua kuwa siyo chombo chenye kulinda au kutetea maslahi ya waislamu, bali ni mkono wa system kwa ajili ya kuwathibiti waislamu, Hao viongozi wa BAKWATA wakipewa maslahi machache machache ya hapa na pale kutoka serikali ya CCM basi hufanya bidding kwa ajili ya manufaa ya serikali hiyo, hawana mpango kabisa na mustakbali mkubwa wa Waislamu wenzao nchini! .

Lakini pia umezungumzia Masheikh wa Zanzibar ambao kwa uonevu mkubwa, na ukatili mkubwa kutoka kwa serikali ya CCM na viongozi wake wameendelea kusota magerezani kwa miaka zaidi ya Sita sasa bila kuwepo kwa ushahidi wa kutosha wa kuwatia hatiani, na pia wakiwa wametekwa kutoka Zanzibar walipokuwepo na kwenye sheria zenye kutoa dhamana kwa makosa waliyoshitaiwa nayo na kisha kuletwa huku bara kwenye sheria ambayo haitoi dhamana kwa makosa yale ili kuwatesa na kuwaumiza.

Tatu umezungumzia kuhusu Masheikh walioko huko mikoa ya kusini, huko Mtwara ambao nao wako ndani kiuonevu.

Kwa hiyo inavyoonekana serikali ya CCM inatesa Watu wa Mungu, kama haiwatesi kwa nini Inaweka Masheikh wake Jela bila haki?. Je serikali hii ya kidhalimu ina utofauti gani na serikali tunazozisoma kwenye maandiko matakatifu ziliziokuwa zinaonea na kutesa watu wa Mungu?

Ndugu Lissu, Unafanya kazi kubwa sana na nzuri kutetea waislamu nchini. Nakufananisha na Mfalme mmoja wa nchi ya Ethiopia aitwaye Najashi(King Negus kwa kiingereza) aliyekuwepo kipindi Mtume Muhammad alipoanza mafundisho yake huko Arabia, Wanafunzi wa mtume walikuwa wakionewa na serikali katili za Wapagani pale Makka, Mtume akawaagiza wanafunzi wake wakimbilie Ethiopia kwa yule Mfalme ili kujinusuru,mtume akawaambia kuwa waende ethiopia huko kuna mfalme, tena ni mkristo na ni muadilifu na atawatendeeni wema. Na kweli yule mfalme aliwapokea vizuri na kuwatendea wema sana, aligoma hata kuwarudisha Makka pindi ile serikali dhalimu ya Arabia ilipotuma ujumbe kwa huyo mfalme wa Ethiopia ili wale watu warudishwe huko Arabia wakateswe! .
Sasa wewe ndugu Lissu unafanya kazi kama ya mfalme Najashi, unawatetea hawa waislamu wanaonyanyasika katika serikali hii ya CCM.

Nakuomba ndugu Lissu uendelee na moyo huohuo, umeonyesha jinsi ulivyo binadamu, mwenye utu kwelikweli. Tofauti yako na watawala wa CCM ni kubwa sana ni kwamba wewe ni Mtu, wao ni makatili, wewe ni mpenda haki wao ni madhulumati, wewe ni hero wao ni cowards.

Mwisho kabisa, ningependa kukujulisha kuwa waislamu wanakerwa na teuzi za serikali ya awamu hii zinazonuka udini, Nakuomba hili suala ulisemee, ulizungumzie bila woga kwa sababu haiwezekani katika nchi hii kufanya teuzi zinazoonekana waziwazi kuwa zina mrengo wa kidini halafu nchi ikakaa kimya. Hii siyo dhana yangu, bali Masheikh wameshalalamika kuhusu hili, Sheikh Halifa amelisemea hili jambo, Sheikh Ponda na Shura ya maimamu wamelisemea hili jambo. Serikali ya Magufuli haijajibu hoja hii zaidi ya kuwatisha Masheikh hao. Nakuomba ndugu Lissu, mteta haki, msema kweli, na shujaa asiyeogopa madhalimu. Simama na ulizungumzie hili.

La Mwisho nakuomba ukiwa rais, uondoe ubaguzi huu wa Udini, utengeneze serikali shirikishi(inclusive) ambayo itawapa nafasi watu kwa fairness kabisa badala ya kuangalia dini zao au majina yao kama yanasound kizungu au Kiarabu

FREEDOM, JUSTICE AND PEOPLE CENTRED DEVELOPMENT.
[/QU Huyo lissu si awatoe sasa kama ana ubavu anabweka tu mitaani
 
Kwako Ndugu Lissu

Amani ya Mwenyezi Mungu iwe nawe
Napenda kuchukua fursa hii kukushukuru kwa dhati ya moyo wangu kwa kitendo chako cha Utu na kupenda haki kwako kwa namna unavyotetea Viongozi wa dini ya Kiislamu walioko Jela kiuonevu.

Umekuwa consistent sana kuhusu uonevu huu, umezungumzia kuhusu Masheikh zaidi ya 70 huko Arusha walioko jela, si kwa sababu wana makosa bali eti wanaipinga BAKWATA ambayo umma umeshatambua kuwa siyo chombo chenye kulinda au kutetea maslahi ya waislamu, bali ni mkono wa system kwa ajili ya kuwathibiti waislamu, Hao viongozi wa BAKWATA wakipewa maslahi machache machache ya hapa na pale kutoka serikali ya CCM basi hufanya bidding kwa ajili ya manufaa ya serikali hiyo, hawana mpango kabisa na mustakbali mkubwa wa Waislamu wenzao nchini! .

Lakini pia umezungumzia Masheikh wa Zanzibar ambao kwa uonevu mkubwa, na ukatili mkubwa kutoka kwa serikali ya CCM na viongozi wake wameendelea kusota magerezani kwa miaka zaidi ya Sita sasa bila kuwepo kwa ushahidi wa kutosha wa kuwatia hatiani, na pia wakiwa wametekwa kutoka Zanzibar walipokuwepo na kwenye sheria zenye kutoa dhamana kwa makosa waliyoshitaiwa nayo na kisha kuletwa huku bara kwenye sheria ambayo haitoi dhamana kwa makosa yale ili kuwatesa na kuwaumiza.

Tatu umezungumzia kuhusu Masheikh walioko huko mikoa ya kusini, huko Mtwara ambao nao wako ndani kiuonevu.

Kwa hiyo inavyoonekana serikali ya CCM inatesa Watu wa Mungu, kama haiwatesi kwa nini Inaweka Masheikh wake Jela bila haki?. Je serikali hii ya kidhalimu ina utofauti gani na serikali tunazozisoma kwenye maandiko matakatifu ziliziokuwa zinaonea na kutesa watu wa Mungu?

Ndugu Lissu, Unafanya kazi kubwa sana na nzuri kutetea waislamu nchini. Nakufananisha na Mfalme mmoja wa nchi ya Ethiopia aitwaye Najashi(King Negus kwa kiingereza) aliyekuwepo kipindi Mtume Muhammad alipoanza mafundisho yake huko Arabia, Wanafunzi wa mtume walikuwa wakionewa na serikali katili za Wapagani pale Makka, Mtume akawaagiza wanafunzi wake wakimbilie Ethiopia kwa yule Mfalme ili kujinusuru,mtume akawaambia kuwa waende ethiopia huko kuna mfalme, tena ni mkristo na ni muadilifu na atawatendeeni wema. Na kweli yule mfalme aliwapokea vizuri na kuwatendea wema sana, aligoma hata kuwarudisha Makka pindi ile serikali dhalimu ya Arabia ilipotuma ujumbe kwa huyo mfalme wa Ethiopia ili wale watu warudishwe huko Arabia wakateswe! .
Sasa wewe ndugu Lissu unafanya kazi kama ya mfalme Najashi, unawatetea hawa waislamu wanaonyanyasika katika serikali hii ya CCM.

Nakuomba ndugu Lissu uendelee na moyo huohuo, umeonyesha jinsi ulivyo binadamu, mwenye utu kwelikweli. Tofauti yako na watawala wa CCM ni kubwa sana ni kwamba wewe ni Mtu, wao ni makatili, wewe ni mpenda haki wao ni madhulumati, wewe ni hero wao ni cowards.

Mwisho kabisa, ningependa kukujulisha kuwa waislamu wanakerwa na teuzi za serikali ya awamu hii zinazonuka udini, Nakuomba hili suala ulisemee, ulizungumzie bila woga kwa sababu haiwezekani katika nchi hii kufanya teuzi zinazoonekana waziwazi kuwa zina mrengo wa kidini halafu nchi ikakaa kimya. Hii siyo dhana yangu, bali Masheikh wameshalalamika kuhusu hili, Sheikh Halifa amelisemea hili jambo, Sheikh Ponda na Shura ya maimamu wamelisemea hili jambo. Serikali ya Magufuli haijajibu hoja hii zaidi ya kuwatisha Masheikh hao. Nakuomba ndugu Lissu, mteta haki, msema kweli, na shujaa asiyeogopa madhalimu. Simama na ulizungumzie hili.

La Mwisho nakuomba ukiwa rais, uondoe ubaguzi huu wa Udini, utengeneze serikali shirikishi(inclusive) ambayo itawapa nafasi watu kwa fairness kabisa badala ya kuangalia dini zao au majina yao kama yanasound kizungu au Kiarabu

FREEDOM, JUSTICE AND PEOPLE CENTRED DEVELOPMENT.
Ubaguzi wa kidini unaousema kwanza haupo huku bara bali upo Zanzibar. Pili nionyeshe mgombea ubunge au uwakilishi huko Zanzibar ambaye ni mkristo. Je Zanzibar hakuna wakristo hata kama wachache?
Hao masheikh, Lissu anaowatumia kama chambo ili kupata kura za waislamu hawana tuhuma za makosa ya jinai? Kumbuka kule zanzibar padre amewahi kuuawa mlangoni kanisani, watalii kumwagiwa tindikali yote hiyo kutokana na mahubiri ya chuki katika nyumba za ibada, kanda zilizorekodiwa.

Huku bara kuna wakati makanisa yalichomwa, mengine mipango ya kuyashambulia iliwahiwa ndio ikawa salama. Ugaidi wa Kibiti yeye Lissu aliufurahia.

Serikali yeyote makini haiwezi kukaa kimya wakati kuna watu wanapanga na kutekeleza ugaidi ndani ya nchi. Lissu anaweza kuwa na uchungu na waislamu kuliko waislamu wenyewe ea Zanzibar walioamua kuwachukulia hatua baada ya kuona vitendo vyao vya kigaidi vimezidi licha ya kuonywa mara kadhaa? Hivi yaliyokuwa yakiendelea kule Zanzibar na Kibiti wakati ule kabla hawajawekwa ndani yeye Lissu alikuwa hayaoni au ndio cheap politics?

Kama kuna mtu anataka nafasi za uteuzi ziwe nusu kwa nusu baina ya ukristo na uislamu basi kwanza aanzie Zanzibar kabla hajazungumzia bara .
 
Ni bora akachaguliwa mwakilishi wa mabeberu walau tutendelea kuishuhudia demokrasia ila siyo mwakilishi wa BAHIMA EMPIRE, halafu mwaka 2025 tukaishia kutawaliwa kidikteta kama ilivyo Rwanda na Uganda.
Saudi Arabia demokrasia hakuna ila ana urafiki mzuri tu na hao mabeberu(wapenda demokrasia).
 
Ila usisahau hao Masheikh walishikiliwa tangu enzi za Kikwete! Hivyo ni vyema na yeye akatajwa kuhusika kwa namna fulani kama Rais wa wakati huo.
Mbona babu Seya alishikiliwa tangu enzi za Kikwete ameachiwa na Magufuli.
 
Back
Top Bottom