Asante mkuu kwa nyongeza hiyoKwa kifupi, jikumbushe pia na mbinu waliyotumia wakoloni kudhalilisha tamaduni zetu na kubadili kabisa 'mind set' za watawaliwa.
Dini, tamaduni, mila na desturi za waAfrika wazawa zikatwezwa na kuonekana kila cha mzungu ni cha maana hata kama alikosea.
Na huo ukoloni wa kifikra unaendelea hadi leo vichwani mwa waAfrika walio wengi, kuona kila cha mzungu iwe dini, lugha, tamaduni nk nk hata kama kimekosewa, kuwa ndivyo vilivyo bora na mahususi hata kama ni vibaya na havitufai!
Asante studioMi naona sawa tu Mlima Mrefu upendezao
Ngoja tusubiri wajuzi waje.Ukweli sijawahi jua hilo.
Nyongise.
Huenda ikawa na ukweli ndani yake.hii nadharia ya kwanza kwenye maarifa ya jamii sikumbuki darasa la ngapi nilishawahi isomaa
Ipo wapi mkuu? Ila itakuwa karibu na mkoa huoLukuledi haipo Ruvuma
Shukurani mkuu hapo nilimanisha wajerumani wenyewe.Mjerumani hawezi kuipa project yake jina la kiingereza. Namba 1 inakataa labda kama ulimaanisha uingereza
Nini tena
Kweli ngoja tuwategemee tu.Wazungu si ndio wamewaweka kwenye ramani [emoji23][emoji23]
AiseeWakuu bila shaka uzima upo. Basi nashukuru pia poleni kwa wale uzima unapelea.
Leo nimeamua kuja mbele yenu kuuliza kwa nini Wazungu tu? Naamu hii inamaana ya kuomba msaada wa majibu kwenu.
Ukifuatilia Asili au Maana ya Maneno ya majina ya maeneo mengi hapa nchini utakuta na majina hayo asili yake au maana mzungu kuhusika ndani yake.
Mifano;
1- Asili ya Neno Geita.
Geita imetokana na neno la kisubwa(kwa nadharia moja) yenye maana ya neno Keita yaani kuuwa (kwa kisubwa). Hivyo hapo zamani watu waliokuwa wakipita milimani kuingia Geita walikuwa wakifia njiani hivyo wenyeji wakawa wanasema Akabanga Keita Abhantu yenye maana Mlima unauwa wafu (kwa kisubwa). Hivyo Neno Keita wazungu walishindwa kuita wakaita Geita na ndiyo ikawa mwanzo wa neno Geita.
2- Asili ya neno Kilimanjaro
Zamani ilikuwa ikiitwa (kilima kyar'yu)kwa kabila la kichaga yaani kilima chetu. Wazungu wakashindwa kutamka (kyar'yu)yaani chetu ndo wakaanza kuita kilimanjaro mpaka likazoeleka hivyo na hapo ikawa mwanzo wa neno Kilimanjaro.
3- Asili ya neno Lukuledi mkoani Ruvuma
Lukuledi ni moja ya eneo lililopo mkoani Ruvuma asili yake ni kwamba maeneo hayo kulikuwa na mto hivyo wanawake walipenda kuoga maeneo ya mto, sasa wazungu wakipita pale wanaanza kuongea Look Ladies hivyo na sisi Wabongo tukajua Hilo eneo bila shaka ni Look Ladies hivyo kwa vile kizungu hakikueleweka wao walijua ni Lukuladi sawa na Look Ladies na hapo ikawa mwanzo wa jina hilo.
4- Asili ya Jina kolomije- Mkoani Mwanza
Kuna mzungu alikuwa anaitwa J. Hivyo kwa jinsi alivyokuwa alijitambulisha akawa anawambia call me J akimaanisha niite J(kw kiswahili), basi hilo eneo likaitwa kolomije na wenyeji walio Kuwa wakijua mzungu huyo anasema eneo hilo ni Kolomije yaani call me J.
Pia kuna maeneo mengine ambayo uwepo wake ni chanzo cha wazungu.
Je, bila wazungu tusingekuwa na majina ya maeneo yetu au kabla ya mzungu sisi hatukutambua umuhimu wa majina ya maeneo.
Wenu Kasomi naomba majibu pia unaweza share stori ya chanzo cha eneo.
Aisee!Nadhani tuliwaamini sana hata Mbeya,sehemu moja kule Chunya mzungu alisema making a loss!wao wakasema amesema Makongolosi!Ndo jina mpaka sasa!Wakuu bila shaka uzima upo. Basi nashukuru pia poleni kwa wale uzima unapelea.
Leo nimeamua kuja mbele yenu kuuliza kwa nini Wazungu tu? Naamu hii inamaana ya kuomba msaada wa majibu kwenu.
Ukifuatilia Asili au Maana ya Maneno ya majina ya maeneo mengi hapa nchini utakuta na majina hayo asili yake au maana mzungu kuhusika ndani yake.
Mifano;
1- Asili ya Neno Geita.
Geita imetokana na neno la kisubwa(kwa nadharia moja) yenye maana ya neno Keita yaani kuuwa (kwa kisubwa). Hivyo hapo zamani watu waliokuwa wakipita milimani kuingia Geita walikuwa wakifia njiani hivyo wenyeji wakawa wanasema Akabanga Keita Abhantu yenye maana Mlima unauwa wafu (kwa kisubwa). Hivyo Neno Keita wazungu walishindwa kuita wakaita Geita na ndiyo ikawa mwanzo wa neno Geita.
2- Asili ya neno Kilimanjaro
Zamani ilikuwa ikiitwa (kilima kyar'yu)kwa kabila la kichaga yaani kilima chetu. Wazungu wakashindwa kutamka (kyar'yu)yaani chetu ndo wakaanza kuita kilimanjaro mpaka likazoeleka hivyo na hapo ikawa mwanzo wa neno Kilimanjaro.
3- Asili ya neno Lukuledi mkoani Ruvuma
Lukuledi ni moja ya eneo lililopo mkoani Ruvuma asili yake ni kwamba maeneo hayo kulikuwa na mto hivyo wanawake walipenda kuoga maeneo ya mto, sasa wazungu wakipita pale wanaanza kuongea Look Ladies hivyo na sisi Wabongo tukajua Hilo eneo bila shaka ni Look Ladies hivyo kwa vile kizungu hakikueleweka wao walijua ni Lukuladi sawa na Look Ladies na hapo ikawa mwanzo wa jina hilo.
4- Asili ya Jina kolomije- Mkoani Mwanza
Kuna mzungu alikuwa anaitwa J. Hivyo kwa jinsi alivyokuwa alijitambulisha akawa anawambia call me J akimaanisha niite J(kw kiswahili), basi hilo eneo likaitwa kolomije na wenyeji walio Kuwa wakijua mzungu huyo anasema eneo hilo ni Kolomije yaani call me J.
Pia kuna maeneo mengine ambayo uwepo wake ni chanzo cha wazungu.
Je, bila wazungu tusingekuwa na majina ya maeneo yetu au kabla ya mzungu sisi hatukutambua umuhimu wa majina ya maeneo.
Wenu Kasomi naomba majibu pia unaweza share stori ya chanzo cha eneo.
Hivi umepata kujiuliza unapopita katika mitaa mbalimbali ya mjini Dar au mji mwingine wowote Tanzania, jina la mtaa au eneo husika limetokana na nini?
Kwa mfano, Kijito Nyama limetokana na nini? Au Mlalakuwa, Au Mtoni kwa Aziz Ali n.k, n.k. Labda utadhani imetokea tu ... just ipo ipo, hapana! Baadhi ya majina ya mitaa yana historia ndefu na yenye kukumbukwa hata kwa vizazi vijavyo.
Hapa napenda kuwahabarisha maana ya mtaa au eneo la nje kidogo ya jiji la Dar liitwalo Gongo la Mboto.Jina hili limetokana na nini? Nakumbuka nilipata kusimuliwa na mwalimu wangu mmoja miaka ile pale Tambaza Sekondari nikiwa kidato cha pili.
Alisema palikuwa na mzee mmoja mashuhuri ambaye alipata kuishi katika eneo hilo.Huyu jamaa alikuwa mkulima. Jina lake aliitwa Mboto. Siku moja alijilawa kwenda katika konde lake kwa ajili ya kujipatia riziki.
Wakati ule, maeneo yale yalikuwa na giza la mapori na vichaka kadhaa. Jioni yake asirudi nyumbani. Kesho yake hadi mchana Mboto haonekani.
Mbiu ikapigwa watu wakakusanyika,kilichofuata ni msako mkali wa kumtafuta mzee huyu.Baada ya siku kadhaa wakakuta nyayo za mnyama mkubwa mithili ya Simba na ishara ya purukushani kadhaa.
Walipochunguza zaidi wakafanikiwa kukuta Gongo ambalo alipenda kutembea nalo mzee huyu.Wakahisi kuwa Mboto huenda amekutwa na maafa ya kuliwa na Simba. Walichokiona pale ni Gongo lake,Ndipo hilo eneo hadi leo lajulikana kama Gongo la Mboto.
Tuhabarishane maana ya maneno mengine kama Msasani, Mikocheni,Mto wa Mbu n.k.