Asilimia kubwa ya WanaCCM wanataka Mbowe abaki Mwenyekiti CHADEMA. Hawamtaki Lissu

Asilimia kubwa ya WanaCCM wanataka Mbowe abaki Mwenyekiti CHADEMA. Hawamtaki Lissu

Wanamjua atawasumbua. Wanatakiwa nao wabuni mbinu mpya za kukabiliana naye. Walishagundua mbinu za Mbowe ndo maana wanamtaka.
Wanajifanya wajanja hawa akina Mwashambwa, wanajidai kumtaka Mbowe ili CDM wamkatae Mbowe.

Hiyo maana yake ni kutaka Mbowe akose kura na kujificha wasijulikane wako na Lisu.
 
Lissu ni Mwiba kwa CCM!
Kimsingi siyo kwamba wanampenda Mbowe! Tangu zamani hawakumpenda isipokuwa mrithi wa Kiti ni Mbaya wao zaidi.
Kama angerithi mwingine asiye Lissu!
Mfano angegombea Kigaila,Mnyika,nk
wasingepika kelele kutamani Mbowe aendelee!
Lissu hawezi kuwa Mwiba kwa CCM hata kidogo.Mbona aligombea Urais na akaambulia aibu ya Mwaka?
 
Kwani si anachaguliwaga na wana CHADEMA wenyewe? Sasa anang'ang'ania vipi ikiwa anachaguliwa na wana CHADEMA?
Kwani na wewe ni mwana Chadema? Wana Chadema ndo wanahitaji mabadiliko ya kiuongozi lakini wewe unawaponda kuwa " watu wenye akili timamu" hawawezi kumchagua TAL. Wewe ndo standard International unit ( SI unit) ya kutambua watu wenye utimamu wa akili??
 
Kwani na wewe ni mwana Chadema? Wana Chadema ndo wanahitaji mabadiliko ya kiuongozi lakini wewe unawaponda kuwa " watu wenye akili timamu" hawawezi kumchagua TAL. Wewe ndo standard International unit ( SI unit) ya kutambua watu wenye utimamu wa akili??
Kwani wewe ukiwa na akili Timamu unaweza kushindwa kumtambua mtu mwenye utimamu wa akili na yule ambaye siyo.
 
Kwa kweli nimefarijika sana. Mbowe anapendwa sana. Anapendwa hadi na wana CCM. Akina Mshamba na tilalila wanampigia upatu Mbowe abaki Mwenyekiti. Hawamtaki Lissu.

Hii inaonesha udugu ambao umeanza wa CCM na CDM kwa namna ambayo ni nzuri kabisa. Yaani ukute siku Simba wanataka Kocha wa Yanga asiondolewe abaki. Unagundua mpira wetu umekua sana.

Kwa sasa Lissu anapigwa vita sana na CCM hawataki awe Mwenyekiti wa CDM. WANASEMA MWAMBA ANATOSHA. MIAKA KADHAA ILIYOPITA WALIKUWA WANASEMA AONDOKE AMEKAA MUDA MREFU SANA. CDM wakasema haondoki. Lakini naona maridhiano kwa sasa yamefana.

Wanasema wamegundua anafaa so aendelee kuwa Mwenyekiti wa CDM. lakini wanapingana na kundi la wana CDM ambao wanataka mabadiliko wanasema Mwamba sasa mwachie Mwamba mwingine naye atuongoze. Hapo kameibuka kakundi ka wenye njaa Yericko Nyerere huyu sasa anakuja na sera ya Mwamba abaki maana anafaidika na mabaki mabaki yanayobaki mezani au chakula kinachodondoka miguuni pa Mbowe.

Huyu Yericko alikuwa akipinga Magufuli kutaka badilisha katiba aongeze muda wa kutawala. Ila leo anataka mtu aliyeongoza miaka 20 aendelee. Sababu? Ana pesa. So wao wataokota okota pesa toka kwake.

Chadema inapoteza uaminifu. Kama Lissu aliteuliwa agombee Urais 2020 na sasa wanasema hafai kumbe walikuwa wanaingiza watanzania chaka.so hata sasa wanaposema Mbowe anafaa tusiwaamini. Sababu ni uongo ule ule kama wa mwaka 2020.

Mbowe amejenga urafiki mkubwa na wa kupendeza na wana CCM ni jambo zuri sana. Na wanampenda. Wanatamani aendelee kuongoza CDM. Hawataki msikia Lissu sababu Lissu atakiua Chama cha CDM. Wanaonesha namna gani wana upendo na CDM.

Akina Yericko vijana wadogo wameshindwa kuthibiti njaa na uchawa wanashinda kila siku kumponda Lissu wa chama chao hicho hicho sababu kwake hawapati kitu. Angalau Mbowe anawafanya mkono uende kinywani. Ukimwona Mbwa juu ya Mti Ujue kapandishwa.
Tilatila ndio yupi huyu😀😀😃
 
Back
Top Bottom