Asilimia kubwa ya Watanzania ni wapumbavu

Na mpumbavu mwingine badala ya kufanya anakuja JF analalamika baada ya hapo anakunywa kangala analala!
 
Kwa Makonda siyo kosa maana wanaona angalau anazungumzia shida zao
 
Kwenye halaiki ya watanzania mawazo yao kwa kiasi kikubwa yako kwenye:
1. Kupata pesa ya ziada bila kudhurumiwa.
2. Utani ulioambatana na ucheshi wa raha jipe mwenyewe.
3. Kupata mlo kamili na vinywaji vya kutosha bure bila kuingia gharama.
4. Kupata kazi nzuri inayolipa mapesa mengi bila kutoka jasho sana
5. Ngono ni kitu kisichoepukika kwenye mkusanyiko wowote na mbaya zaidi hakuna mahusiano kati ya mwanaume na mwanamke bila kujamiiana.
6. Watu wanaojali zaidi leo kuliko mambo ya kesho, masuala yanayohusu vizazi vijavyo sio issue.... watajua wenyewe, zaidi ni ponda raha kufa kwaja.
7. Watu wanaothamini ushabiki uliopotiliza kwenye michezo na siasa, yule anayeongea maneno mengi kwa sauti kubwa anaonekana mjanja na anakuwa mjanja zaidi hadi kustahili kusifiwa pale anapoliibia taifa kiasi kikubwa cha pesa.....Mungu tu ndie anaejua tunakoelekea kama nchi..... 😢 😭
 
Sasa kwanini ukubali elimu mbovu?
Huoni kwenye hiyo elimu mbovu kuna wanaotoboa vizuri na ubovu huo huo?
Mi naona shida ni wazazi
 
 
Umeona mbali sana Mkuu. Unfortunately pamoja na hiyo elimu, wenye division 1 wanaendesha bodaboda, wa div 0 anapeta. Niambie, ni waziri gani mwenye Div. 1 ya form 4 au 6 hapa nchini. Hao kina Bashit wanabebana na Bashits wenzao.
 
Umeona mbali sana Mkuu. Unfortunately pamoja na hiyo elimu, wenye division 1 wanaendesha bodaboda, wa div 0 anapeta. Niambie, ni waziri gani mwenye Div. 1 ya form 4 au 6 hapa nchini. Hao kina Bashit wanabebana na Bashits wenzao.
Ni mfumo wao huo wa kubebana huko ccm kuna mazero na ma four kama yote.
 
Kama ulivyoonesha upumbabu kuandika bila adabu na heshima
 
Hiyo ndio tanzania, wengi fuata upepo na huruma za kipuuzi mbele ya maslahi ya taifa na wengi. Rejea ishu ya sabaya kipindi anafanya maovu wengi walikuwa wakichukizwa na kulaani ila baada ya kukamatwa na kushtakiwa ikaibuka huruma eti bora asamehewe na wengine baada ya baadhi ya kesi kuisha wanadiriki kusema Mungu kamtetea, yani Tz tuna matabia ya ajabu ajabu mno. Ni kero.
 


Kwa upande wangu uko sahihi kwa asilimia 50 tu.


Kwamba mtoto wa miaka 15 kutokujua kusoma na kuandika serikali/CCM inahusika, sio kweli. Huyo mtoto huo ubongo umeshikwa na hiyo serikali/CCM kwa lazima na kuzuia hata juhudi zake binafsi na za wazazi na walezi wake kuhakikisha anajua angalau kusoma na kuandika?

Siasa zimeingizwa mashuleni na kuzuia waalimu kutenda wajibu wao Kama inavyostahiki? Kwamba serikali/CCM imepitisha amri ya kuzuia waalimu kuhakikisha wanafunzi wao wanajua japo kusoma na kuandika?

Serikali/CCM kutumia wajinga Kama mtaji wao kisiasa ndio inawapa sababu wanafunzi na wazazi kutokuwekeza kwenye elimu? Kwamba wamezuiwa kuhakikisha kwa gharama yoyote ile elimu inayotolewa mashuleni kwa watoto ni sahihi na hitajika?

Hiyo elimu inayotolewa kumuaminisha mtoto wa Kike kwamba akifeli anaweza kwenda kuuza mwili wake iko kwenye mtaala huu huu? Kwamba mitaala ya Tanzania inaelekeza pia mbinu za kudanga?

Mtoto wa kiume anafundishwa wapi betting Kama sio mtaani kwenye jamii yake alipotokea? Shule za Tanzania ziko na ofisi za betting siku hizi?

Kwamba serikali ilitakiwa ikemee kuhusu watoto kushiriki betting huku mitaani, hizo jamii ambazo ndio wazazi na walezi wa hao watoto zinafanya kazi gani?

Mbona elimu hiyo hiyo mbovu inawakomboa watoto wengine na wanafanikiwa katika malengo na mikakati yao ya kimaisha?


Tutabaki tunailaumu serikali/CCM huku tukiukwepa Ukweli kwamba hata SISI wananchi hatuwajibiki ipasavyo?

Sisi jamii tumekubali kuruhusu kazi ya ualimu kuwa ni sehemu ya biashara badala ya kuwa wito Kama ambavyo ilipaswa halafu lawama tunapeleka serikalini/CCM?

Sisi jamii ndio wanunuzi wa hao watoto wa Kike wanapokua wanadanga ama ni serikali/CCM?

Wamiliki wa hizo betting offices ni sisi wenyewe huku mitaani ama zinamilikiwa na serikali/CCM?


Sisi jamii tumeshindwa kujiongoza kwenye ngazi za family tutaweza vipi kusimama Kama taifa?
 

Dih! Tufanye 87% waliompigia kura Magu wote ni wapumbafu, na 13% wa tundulissu ndio werevu? Duh!
 
Ndiyo maana CCM watoto wao karibu wote wapo nje
 
Kama makonda. Aliwafanyia watu maovu basi tuamini kurejeshwa kwake...ni kuelekezwa kibla muda wowote tutasikia yaliyomtokea jiwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…