Asiyoyajua Yericko Nyerere katika utafiti wa historia ya Mapinduzi ya Zanzibar

Asiyoyajua Yericko Nyerere katika utafiti wa historia ya Mapinduzi ya Zanzibar

Mkuu hiki ulichonunua kilikuwa majaribio tu ya soko, kitabu halisi kinakura 715.
Aina shida nikija December ntanunua jifunze kauli kwa wazee bado kijana unaitaji watu sna umenikela sna kwa matusi juu ya mzee Mohamed Said fanya halaka umbe radhi kwa kauli zako za kishenzi...
 
Mzee wangu inaonesha unapenda sana wazungusha vijana vijiwe vya kahawa na kuwapa utam wa historia nusunusu.(utani )..nadhan ungekua kwe sehemu mzuri zaidi kama ungetupa link tusome hiyo historia unayoijua kwani kwa jinsi unavyojitanabaisha ni kama weye ulishushiwa hiyo historia toka mbinguni...kama ulipata bahati ya kusimuliwa kujisifu tu bila kuiweka kama ilivyo unatuchanganya sis vijana ambao hatukupata bahati ya kuiona no bora basi hata huyo yericko nyerere alijaribu kutuonjesha hata kama haikuiva kisawasawa kama unavyojaribu kutuaminisha...nawasilisha

kaka naona una jibu la kumjibu mzee kumbe una jikwaa kuonekana ume jibu kubali kua iyu mzee ka kuzdi c hanga zajo acha ubishi wa kuonesha kusto jifahamu
 
Mjadala wa mapinduzi ya Zanzibar kwa muktadha wa Mohamed Said unaacha maswali

Kwa muda mrefu nimemuuliza Mohamed, maandiko yake yanaonyesha mapinduzi kuchagizwa kutoka nje ya Zanzibar na si kwa ridhaa ya Wazanzibar. Kwa mantiki hiyo mapinduzi yana 'Uharamu'

Januari 12 Wznz wanasherehekea Mapinduzi wanayotaita 'matukufu'
Kwa jicho la Mohamed hayakuwa na 'uhalali' achilia mbali damu iliyomwagika

Je, Mohamed anawaeleza nini Wazanzibar inapofika Januari 12?
Wanasherehekea 'haramu' au 'halali' yenye Uharamu?

unacho kiuliza kwa mzee mkuu ni siasa na si uandishi,na jibu lake ni segerea-muache mzee afahamishe kuusu mapinduzi wanao sherekea awaache wafate walio wapangia au wanao wafata-
 
Naona umeonyesha ulivyofanya kazi ktk ushauribwangu wa pili ilioutumia kama hitimisho langu..
Lkn nimepitia moja baada ya nyingine nimeona bado hujajitendea haki ww mwenyewe na sisi wasomaji.
Ulichofanya ni kidogo kuliko uwezo wako..
Kubwa ulilofanya ni hili la kumshambulia Yericko na kitabu chake kwa kumwita majina yote.

Ushauri na maneno mengine niliyoyaeleza hapo tafadhali yafanyie kazi.
Tuone Tamthilia ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa filam au kwa Audio au kitabu au kwa mashairi n.k

Aufwidersehen!

warum hast du schliesslich auf deutsch geschrieben
 
Ridhwani Mbaraka
Ridhwani,
Umerudi mtu mwingine kabisa.
Nimefurahi.

Unaandika katika lugha ya kistaarabu na kwa adabu.
Ahsante sana.

Nakuwekea baadhi ya niliyoandika:
  1. PUBLICATIONS/RESEARCH PAPERS/ARTICLES
  2. The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 –1968 The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press London, 1998 translated into Kiswahili as Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes 1924-1968 Historia Iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza, Phoenix Publishers, Nairobi, 2002.
  3. The Torch on Kilimanjaro, Oxford University Press, Nairobi, 2006
  4. Contributing author for an African anthology: The Mermaid of Msambweni and Other Stories, Oxford University Press 2007, Nairobi.
  5. Contributing author Dictionary of African Biography (DAB), Oxford University Press 2011, New York.
  6. Uchaguzi wa Busara, Abantu Publications 2008, Dar es Salaam.
  7. In Praise of Ancestors (1987) Africa Events (London).
  8. Abdulwahid Sykes: Founder of Political Movement (1988) Africa Events (London).
  9. Islam and Politics in Tanzania (1989) Al Haq International (Karachi)
  10. The Plight of Tanzanian Muslim (1993) Change (Dar es Salaam).
  11. Tanzania - The "Secular" Unsecular State (1995) Change (Dar es Salaam).
  12. The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003).
  13. Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000’ (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15th – 17th 2003).
  14. Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004).
  15. Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro 11th April 2004).
  16. Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience (Paper Presented at the Conference on Islam, Terrorism and African Development University of Ibadan, Nigeria 8th - 10th February 2006).
  17. Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the Pork Riots of 1993. (Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21st Century 1st - 3rd August 2006, Kenyatta University, Nairobi.
  18. 14. Muslim Bible Scholars of Tanzania – The Legacy of Sheikh Ahmed Deedat (1918 – 2005) Paper Presented at the International Symposium on Islamic Civilisation in Southern Africa Organised by The Organisation of Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA) The National AWQAF Foundation of South Africa (AWQAF SA 1 – 3 September 2006 University of Johannesburg.
  19. Tanzania: A Nation Without Heroes Seminar Organised by IFRA French Institute for Research in Africa and BIEA British Institute in East Africa 23rd and 24th September 2013 at IFRA Nairobi.
Ridhwani,
Mimi ni mhariri, mfasiri na pia ni ''publisher.''
Kusoma na kuandika ndiyo maisha yangu.

Nimejifunza kusoma labda nina miaka sita na bado sijakwenda shule.
Nakueleza haya ili tuelewane na tuende vyema.

asante mzee wangu tena mwaambie yericko swala la kutusi na kukashfu imani pia aliache
 
Ridhwani...
Una jina zuri sana na naamini unajua maana yake.

Huba sababu ya kunitishia kutukana.

Ikiwa hiyo ndiyo hulka yako usijuzuie fanya lile linalokupendeza
usijali uzee wangu.

Ikiwa umelelewa katika nyumba isiyo na adabu nani wa kukubadili
katika umri huo uliofika?

Mimi sijaandika historia ya Mapinduzi ya Zanzibar lakini nilikuwa
Mtafiti msaidizi wa Dr. Harith Ghassany wakati anatafiti kitabu
chake maarufu, ''Kwaheri Uhuru Ukoloni Kwaheri Uhuru.''

Inaelekea hukijui kitabu hiki kutokana na jinsi ulivyotoa fikra zako
hapa Majlis na kusema unaiamini historia iliyoandikwa na Mihangwa.

Kwa taarifa yako Mihangwa anaandika makala kuhusu Zanzibar hana
kitabu alichoandika kuhusu Zanzibar.

Kuandika kitabu hili ni jambo lingine kabisa.

Hiyo mosi.

Pili nimeandika na kuzungumza kuhusu historia ya Mapinduzi na
naweza kukuwekea link hapa zikusaidie.

Tatu sina khiyana dhidi ya Yericko ila naandika kusahihisha yake
ambayo mimi naona yamekosewa na hii ni kawaida katika duru
za uandishi na duru za kisomi.

Nne nakushauri tufanya mjadala wenye adabu na ustaarabu hizi
lugha za ''povu,'' zitumie kwa watu wengine kwangu si mahali pake.

Kwa kuhitimisha nakuomba urejee tena katika post yangu na angalia
zile picha za Mzee Mkwawa na Victor Mkello.

Katika vitabu ulivyosoma vya historia ya Zanzibar umepatapo kuona
mahali popote wametajwa?

Wale na wengine sikuwaeleza ndiyo waliokuwana funguo za mapinduzi
ya Zanzibar ya mwaka wa 1964.

Hata Mihangwa hakuwa anawajua hawa.
Kwa mara ya kwanza kawasikia kwa Dr. Harith Ghassany.
Wacha kujimilikisha historia as if wewe ni pekee uliyoyaona na kushiriki mapinduzi ya 1964.Historia ni amali ya jamii kwanini unataka wewe tu ndo mwenye vyanzo sahihi,lazima unamatatizo sehemu.Historia haiwezi kutaja kila mtu bali key figures.Unataka ulete historia yako ile huyu ndo alikuwa anampa kitoweo mwl.nonsense.
 
3c76fab69f297d7a1053e3c760e87c70.jpg
yericko nyerere sijui unakumbuka ulikuja kuniuzia hicho kitabu ilala amana ofisini kwangu na nikampigia mzee Mohamed Said ukaongee nae nia yngu kubwa nilikuwa nataka uende kuongeza elimu hakika unaitaji kuivishwa zaidi na magwiji km mzee Mohamed Said sio kukalia ubishi km ndugu zetu wa lumumba jaribu kumsoma vizuri mzee wetu utamuelewa nia yke kujaribu kutaka kkujenga zaidi kijana wake lkn naona unataka kuleta ushindani sio na sababu hakika ww ni Kichochi uwezi kuingia kwenye kundi la ninga jaribu kkubari kukoselewa...

thanks bro kwani napenda watu wanao nena ukweli
 
Naendelea kushikilia msimamo wangu kuhusu yale niliyoandika mwanzo kabisa wa mjadala huu.
Wewe baba una shida zako na Yericko na wala sio makosa ya kimaudhui au kiufundi ya kitabu chake.

Yaani wewe una tatizo nae lingine kabisa.Haulali,hauogi,haundi chooni kisa kitabu cha Yericko na Yericko mwenyewe....IPO SHIDA KWAKO TENA SI NDOGO.

Ushauri wangu mwingine.
Fanya editing/hariri kitabu chote kwa kua ww ni mhariri andaa chapisho moja liweke kwenye soft copy na hard copy ili tununue tusome.
Itakua umemtendea haki yeye na wewe mwenyewe na jamii nzima ya wapenda historia.
Hii personal attack sio kitu cha maana ktk maisha yako na yake.

Jinsi unavyyojibiwa na jinsi unavyoendelea kuleta hoja zingine inaonekana moyo wako umevia,umumia,umejawa na hila kwamba kwanini sikuandika mm ninaejua kila kitu mpka aandike Yericko alieokotaokota hili na lile.

Umri wako mkubwa na utaalam ulio nao unatosha kuona kazi kubwa iliyofanywa na Yericko na kuithamini na kumtia moyo na si vinginevyo.

Aisee mwafrika mweusi na roho yake nyeusi tii!

acha maneno ya jikoni mkuu ,mbona maneno yako yanakosa sura kamili
 
Yericko,
Katika hayo yote uliyosema lililo la kweli moja tu kuwa mimi naipenda dini yangu Uislam kiasi nilipoona historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika imeandikwa lakini mchango wa wazalendo Waislam hawamo, nilinyanyua kalamu na kuandika kitabu kizima.

Hili kuwa wewe unanimudu mimi hapa unajitutumua hilo hawajaliweza wenye elimu kupita wewe utaliweza wewe?

Huwezi kupambana na mimi kwa kuandika "kitabu" kimoja ulichochapa mwenyewe bila "publisher."

ikibidi mtu muudhi kwa kumuambia ukweli
 
Heheee umemwambia vema mkuu, huyu mzee ana matatizo makubwa, nahisi ana matatizo ya kiakili japo anaweza kujidhania ni mzima... Ni mwaka wa tano sasa tunajadiliana mambo haya haya kwa mwendo huuhuu wa mzee Said

wewe ndo ujielewi mzee huyo tuna mfahamu sana kwa mapana uku ughaibuni vyuo vingi tuu,
 
Aina shida nikija December ntanunua jifunze kauli kwa wazee bado kijana unaitaji watu sna umenikela sna kwa matusi juu ya mzee Mohamed Said fanya halaka umbe radhi kwa kauli zako za kishenzi...

tena ambo radhi mzee huyo huku ughaibuni tuna mfahamu kama pesa,nilijarbu kutizama vipost vyake na maneno yake yasio mwelekeo tukaona hana jipyaa
 
Ndugu zangu,
Kipimo cha kitabu chochote ni kwanza reviews na zimechapwa wapi.

Hapa Afrika ya Mashariki kitabu cha Sykes kilifanyiwa serialization tatu katika gazeti la The East African December 1998.

John Iliffe na Jonathon Glassman walifanya review katika Cambridge Journal of African History na James Brennan alifanya review sikumbuki jina la journal.

Tanzania kitabu kilifanyiwa review na Business Times na baadhi ya magazeti.

Lakini kitabu kiliuzika sana katika tafsiri ya Kiswahili na hasa baada ya mijadala hapa JF.

Ukweli ni kuwa watu wengi waliumizwa na hii historia mpya na wengine walishangazwa kuwa iweje historia hii ilikuwa imefichwa kwa miaka yote ile.

Kilichofuata nilipata mialiko mingi ya kuzungumza ndani na nje ya Tanzania kilele ni siku nilipozungumza Northwestern University Evanston, Chicago kwani hawa ndiyo wanaongoza dunia katika historia ya Afrika na hii ilikuwa baada ya kufanya mhadhara University of Iowa.

Nilialikwa Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin ambako nilizungumza na nilikaa mwezi mzima kwa kuandika paper na kuwaachia.

Hii papers inaitwa "Tanzania A Nation Without Heroes."

Siwezi kutaja kote nilipoalikwa na kuzungumza maana kwingine ni mialiko private katika miji ambayo napita kwa mengine lakini jamaa wakisikia niko mjini hunialika kwa chakula na kuniomba nizungumze.

Niliingizwa katika mradi wa Oxford University Press Nairobi wa kuandikia historia kwa ajili ya shule za msingi wakati huo huo wakijifunza Kiingereza na niliandika kitabu kimoja na cha pili ni anthology na waandishi wengine kutoka nchi nyingine za Africa.

Niliingizwa pia katika mradi wa Harvard na Oxford University Press , New York uliojulikana kama Dictionary of African Biography (DAB) uliochapa volume 6 za maisha ya Waafrika mashuhuri.

Haya yote sikuyategemea ukiachia mbali jinsi nilivyovutia watu hapa Majlis.

Watu wakijua nimeingia jamvini wanajazana kwa kufanya "bashing" nami husimana kuwajibu.

Natoa shukurani nyingi kwa JF kwani kama si wao kitabu changu na mimi nisingefahamika na watu wengi kote duniani wanakosema Kiswahili kwa kiasi hiki.

Hii imepelekea pia blog yangu www.mohammedsaid.com kupata umaarufu mkubwa kwa "viposti" vyangu.

Nashauri ikiwa ndugu zangu mmeridhia na tuufunge sasa mjadala huu.

Ahsanteni sana.
 
Umepwaya mno. Usiumie kwa kuwa mtu fulani anakuwa maarufu juu ya usemaji fulani kuwa nawe mbunifu.
No one can survive by his own effort even those whom you are mentioning they reached where you saw them by applying external effort done by others.
Yeriko piga kazi kijana achana na kelele hizi.
 
Nimshauri kijana mwenzangu Yeriko kwamba anasafari ndefu ya kwenda katika huu ulimwengu wa uandishi na iliafanikiwe basi auchunge mdomo wake na majibizano yake katika uandishi.
Naamini kwamba kuna vitu kweli anavijua na kweli amevitafiti lkn bado hajafikia kikomo cha elimu ya uandishi mahiri wa vitabu historia. Wala Yerriko asivimbe kichwa kwakua mtu fulani kwautashi wake au kupendezwa kwake kaamua kusema eti kitabu chake kinahadhi ya PhD.
Yerriko yawezekana kabisa kwamba mzee wetu labda amekukosea ni vyema ungemwambia tuu kwa busara sio kuleta lugha za matusi.
Lakini pia sishangai sana maana huko bara muliowengi ni watoto wa nje ya ndoa kwahivyo hamna namna lazima tuu mtachomoza.
 
Kwa ss nipo njee ya nchi wakt nipo hapo nmenunua kitabu toka kwake maana ni moja ya sterehe zangu kusoma ww vp unacho japo kimoja...
5a28b183ec5e7279d608584153522319.jpg
Mkuu ngoja niwe mkweli tu.
Mimi ni mpezi mkubwa sana wa kusoma vitabu lakini nilikatishwa tamaa sana na vitabu kadhaa vya waandishi wa nyumbani nisingependa kuwataja.

Mfano kuna kitabu kinachofanana maudhui ya mambo ya usalama kama hicho ulichoshika mkononi kwenye picha. Kilitoka nadhani 2016. Ule ulikuwa mzaha kwa wasomaji hata kama kingesambazwa bure.

Kwa sasa ninasoma vitabu vya nje tu na vya nyumbani nilisoma vya zamani tena vichache.

Sasa nimepatwa na uoga wa kufadhaika nafsi yangu kwa kujenga matumaini makubwa kwa vitabu vyetu kisha nakutana na uandishi usio wa kina.

Unaweza kumdharau mchangiaji aliesema profesa wake alimwambia asiviamini vitabu vilivyo andikwa kwa kiswahili lakini kama wewe ni msomaji wa vitabu vingi na ukakutana na kitabu kama hicho nilichokilalamikia basi unaweza kukubaliana na huyo profesa.
 
Yawezekana bwana Said ana hoja ktk hilo alilolisemea kuhusu hicho kitabu; lakini hii haiondoi ukweli kuwa bwana Said ni msomi ambaye hakuelimika.
 
Back
Top Bottom