Askari Polisi asakwa kwa mauaji ya mtuhumiwa wa Wizi wa Simu

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Jeshi la polisi mkoani Iringa linamsaka Askari wa Jeshi hilo aliyefahamika kwa jina la Sajenti Rogers wa Kituo cha Polisi Ipogolo na Askari wa jeshi la Akiba aitwaye Thomas Mkembela kwa tuhuma za kumuua Nashon Kiyeyeu mwenye umri wa miaka 23, Mkazi wa Nyamuhanga, Manispaa ya Iringa aliyekuwa anatuhumiwa kwa wizi wa simu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa SACP Alan Bukumbi amesema Disemba 14, Sajenti Rogers alipokea taarifa kutoka kwa mwananchi ambaye hakumtaja jina kuwa mtuhumiwa Nashon alimwibia simu yake.

Ameeleza kuwa bila kutoa taarifa kituoni, Sajenti Rogers kwa kushirikiana na Mgambo huyo walimkamata mtuhumiwa na inadaiwa walimpiga na walipoona amepoteza fahamu, walimpeleka hospitali moja binafsi na baadaye kumhamishia, hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa ambako ilibainika mtuhumiwa, Nashon Kiyeyeu alikuwa ameshafariki.
Your browser is not able to display this video.
 
Jeshi la Polisi mkoani Iringa linawatafuta askari Polisi mmoja na Mgambo mmoja waliomuua mwananchi mmoja na kumtelekeza hospital kisha Wao kupotelea Kusikojulikana

Askari hao ni Sajenti Rogers na Mgambo Thomas ambao wamemuuwa Kijana aitwae Nashon Kiyeyeu

Source: Mwananchi
 
Ukishafikia sgt kwenye level ya uaskari you suppose kuwa mfano wa wa chini yako na pia unakuwa na experience na kazi
But then wapo wanaojisahau, exeptional ni jwtz
 
wakuu hawa wanaoitwa polisi sio watu wa mchezo, ilikua hivi, polisi alipewa taarifa kua Kuna jamaa ameiba simu. ndipo polisi aliamua kuongozana na mgambo na kumsaka jamaa.

walipompata wakaanza kumchezeshea kichapo. gafla jamaa hali ikawa mbaya wakampeleka kituo cha afya cha private, walipoona hali imekua mbaya wakampeleka hospital ya rufaa ya mkoa wa iringa, kwa bahati mbaya jamaa akawa tayari amekwisha fariki.

polisi ameingia mitini na kikosi cha jeshi la polisi linamsaka afande wa kituo cha ipogolo kwa mauaji ya kijana.

my take hawa polisi wanaharibu sana maisha yetu.
 
hii taarifa ilisharipotiwa kama uhalifu na polisi wamechukua hatua.Kwa nini hujasema ukweli wa tukio na kilichofanyika?
kwa nini unataka kuipotosha jamii??
kwa nini unataka kujenga muendekezo wa chuki dhidi ya polisi??
kuwa mzalendo!!
Polisi inapaswa kukuhoji kwa upotoshaji huu
 
ukweli ni kua polisi kaua kijana muibaji wa simu
 
Mbona Mkali Mkuu!
 
Polisi, mkitaka kujisafisha na uchafu huu, toeni hadharani picha za watuhumiwa, wekeni na dau, muone kama hawajakamatwa kesho asubuhi.

Kinyume na hapo ni kuuhadaa umma wa Watanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…