Askari Polisi wa Dar aliyetajwa na Rais Samia arejeshwe ili kudhibiti ujambazi ni nani?

Dawa ya Majambazi ni Kula Vyuma tu Msitu wa Mabwepande........Ukikamata mmoja anapigwa pinchi anataja mtandao wake wote kisha wanakula vyuma wote...Hii ndio iliyochangia KOVA kumaliza ujambazi DIZZIM.
Hakuna jambo la hatari kama kuua watuhumiwa bila kuwafikisha mahakamani. Ni lazima kutatokea makosa na watauawa watu wasiyo na hatia. Pia polisi na wanasiasa wasio waaminifu watatumia hiyo loophole kufanya unyama kwa watu wasio na hatia.
 
ukweli unaujua. Nenda kafanye tafiti kitaa. JPM was a revered leader. Hata mmpake matope vipi hachafuki. Mkumbuke ndiye rais wa Kwanza TZ kuwa na makamu Mwanamke, ambaye ni mama Samia ambaye ni rais sasa. Legacy ya JPM haifutiki mioyoni mwa watu kona zote za nchi.
 
Ningekuwa mkuu wa Chuo fulani ningekupa Phd uitwe Dr. Victor Solomon. Unaongea point sana. "Napigia mstari neno wenye utimamu wa akili". Watu wanaleta ushabiki badala ya hoja za kuisaidia nchi.
 
Je Akifa itakuwaje
 
Mbona JPM na zile kauli za kaa na mavi yako hamkumshauri.
 
Ningekuwa mkuu wa Chuo fulani ningekupa Phd uitwe Dr. Victor Solomon. Unaongea point sana. "Napigia mstari neno wenye utimamu wa akili". Watu wanaleta ushabiki badala ya hoja za kuisaidia nchi.
Mtaumia hadi 2025
 
Mama anaongoza nchi kwa kutumia mitandao, yani et kaona huko mitandaoni wamemtaja huyo Askari hata jina halikumbuki.
Ulitaka awe anapiga ramli kujua matatizo ya wananchi wa kawaida?
Mitandao Kwa dunia ya sasa ni chanzo kizuri kama sio kikuu cha habari ndio maana na wewe uko hapa.
Kiongozi makini Lazima utafute Mawazo/maoni/malalamiko,ambayo kimsingi wasaidizi wake hawawezi kukufikishia kwasababu yanawashtaki wao.

Ulitegemea IGP Katika briefing za kawaida angejichomea kwamba Dar ujambazi umeongezeka?
Mataga na yule Kiongozi wenu hayati ndio mlikuwa mnatanani malaika azime mitandao ajabu na nyie mko mtandaoni.Akili zenu giza tupu
 
Mm naona hapo anataka tu IGP amtoe mambosasa na kumleta mtu mwingine
Akimtoa mambosasa na kumweka mwingine haitasaidia kitu ujambazi upo hata mikoani. Mbona Mambosasa kamaliza majambazi mengi tu. Awasisitizie alichosema jpm jambazi alazwe chini.
 
Mimi sijasema kujua matatizo kupitia mitandao bali nimezungumzia kuongoza nchi kwa kutumia mitandao, kuna tofauti kubwa hapo.
 
Mtaumia hadi 2025
Mimi siumii namtakia Mema Mama kwasababu mimi ni muumini wa Falsafa si watu ila natamani mama akaze buti na akifanikiwa Imefanikiwa Nchi yangu Tanzania, watu wanamchukulia poa mama naona. Pia mitandaoni kila siku kuna nini? Kwamba mama hana vyombo, "utasikia nimesikia mitandaoni" Idara zetu zile za juu ziko wapi kumpa mama Taarifa? Mitandao ni mizuri kwamba inaweza toa taarifa ambayo si biasi but kuna muda mitandao inatoa taarifa ambazo ni biasi. Narudia tena, Molali ya Askari na hasa wa Juu inategemea sana Mama wanamsoma vipi? Naona kama bado anachukuliwa poa au bado hajaeleweka hasa dira yake kuhusu mambo ya kukomesha ujambazi. Nchi hii inahitaji ushujaa kidogo, kuna watu (baadhi) ni wagumu kuelewa.

Sitapenda Mazuri waliyoyafanya na Hayati akiwa top yapotee yaani arudi nyuma halafu watanzania waanze sema ona tumerudi nyuma. Natamani Watanzania waseme, ona tumesonga mbele zaidi ya tulipokuwa. Itakuwa Raha kwa nchi yetu Tanzania.
 
Kwanza tutambue kua kila mwanadamu ameumbwa kwa jinsi yake. Hatuwezi lazimisha Samiah akawa kama JPM ni kuingilia uumbaji wa mungu. Jambo la msingi tumuombee mama afanikiwe maana nchi Hii ni yetu sote. Vijembe na matusi havisaidii
 
Ume mnukuu vibaya hakutoa maelekezo yoyote ya askari fulani kurudishwa Dar ila aliongea kiutu uzima kuwa mitandaoni watu hadi wanasema afande nani.....arudishwe maana alisaidia kukomesha Ujambazi.Usipoelewa kauli hiyo lazima uje na scenario ya afande mmoja lakini kauli hii inawaamsha maafande wa Jiji la DAR ES SALAAM kuwa wamelala.
 
Rais anayesema ujambazi umeongezeka Dsm kwa sababu ya askari mmoja amehamishwa, bila kuwa hata na taarifa za ndani za huyo askari, hapa hatuna Rais, tuna mzigo tu Ikulu.
Hujafuatilia hotuba unaandika kulingana na post.Mtoa post kakosea na wewe unakosea
 
Ukiona RPC anatumia sana media ,ujue hakuna kitu hapo ni sawa na mbwa kubweka bweka hovyo.Watu wa kazi wanafanyaga mambo yao kimya kimya kwa utulivu kabisa,ndiyo utaona matolea halisi. Sasa wewe jambo dogo tuu RPC anakimbilia kwa media
 
legacy ipi kwa mfano ?
 
Rais anayesema ujambazi umeongezeka Dsm kwa sababu ya askari mmoja amehamishwa, bila kuwa hata na taarifa za ndani za huyo askari, hapa hatuna Rais, tuna mzigo tu Ikulu.
Lakini mama alikuwa ananukuu tu maneno ya waja mitandaoni.
 
Mkuu nakushauri usipende sana kuamini stori za vijiweni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…