blogger
JF-Expert Member
- Mar 13, 2012
- 12,112
- 15,060
Mungu anawaumbua.. wanajikuta wamesema bila kujielewa..Haya yanayotokea sasa hivi ni Kwa bahati mbaya, mazoea au ni planned? Polisi mwenye cheo kikubwa kama huyu anawezaje kutamka maneno mazito kama haya? Huku akifanya demonstration?
Pia soma:
~ Kuelekea 2025 - Nape Nnauye: Matokeo ya kura inategemea nani anahesabu na nani anatangaza, ili mradi ukimaliza unasema Mungu nisamehe!
~ DC Longido: Mazingira ya 2020 na yale yaliyofanyika kwenye mapori yalitengenezwa na serikali ili tupite bila kupingwa!
~ Mwenyekiti UVCCM Kagera, Faris Buruhan: Tukiwapoteza wanaomtukana Rais Samia mitandaoni, Polisi msiwatafute
Je, tuamini Yale magari ya kisasa kwa ajili ya Polisi ambayo yataingia nchini hivi karibuni ni hongo kwa Jeshi la Polisi kutoka Serikali ya CCM?
Unawezaje kusema "Mama ni Rais wa nchi hii si kwa SABABU mlipiga kura na sisi (Jeshi la Polisi) tumo"!
Hii ni kauli ya kijinga na kifedhuli Sana, kwa MTU yoyote yule anayejielewa hawezi kushabikia hili
Mungu yupo aisee.