Askari wa JWTZ aliyemuita Polisi 'paka' wakati akitimiza majukumu yake afutwe kazi

Hata kama...ndio amuite mlinda amani mwenzie PAKA!!
 
Hiyo ni kweli trafiki alikosea pakubwa kutamka "nakuonya" hilo neno kwenda kwa askari wa jwtz tena mbele za watu alipo sawa kabisa sidhani kama kuna mwanajeshi atayeweza vumilia neno hilo toka kwa trafiki,

Hapo ndipo linapokuja lile swala la kujuwa unazungumza na nani na wapi na utumie maneno gani.
 
Ukifanya general overview basing on experience utaweza kusema traffic huenda alifanya makosa in the first place!

Traffic wakati mwingine anaamua kuvuta foleni magari ya upande mmoja Kwa muda mrefu kupita kiasi takriban lisaa zima?!
Imagine!
 
Ilikuwa zamani hiyo mkuu. Polis siku hizi wengi ni degree holders. Lkn jeshini Kuna mijtu imejiunga juzi tu hapa eti kisa ina nguvu za kunyanyua vyuma
Kinachotakiwa ni Askari wetu wafanye kazi kwa kuheshimiana na uweledi Wawapo kazini, na nje ya kazi wajitambue. Alafu degree holders, hawezi kukaa barabarani, au kakaa lindo

Wenye elimu hizo, hupelekwa kwenye vitengo maalumu, vinavyohitaji elimu zaidi.

Na hata upande wa majeshi mengine, wasomi hutumika maeneo maalumu, yanayo hitaji elimu kubwa zaidi.
 
Yule mtoto wa Simbachawene alifanywa nini?

Si yuko mtaani mpaka leo?

Na aliwatukana Polisi tena kituoni kwao!

Acheni kuziona ajira za wenzenu kama njugu mawe,guyo unataka afukuzwe kazi kwa tusi moja.
Akiingia mtaani akaamua kuwa jambazi ghafla unayajua madhara yake?

Hao Polisi wao wanakula Rushwa mchana kutwa Barabarani, mbona wasianze kwa kufukuzwa wao kwanza?

Madhara ya Rushwa ni makubwa kuliko madhara ya Tusi!

Watanzania punguzeni Roho mbaya,shida zenu binafsi zisiwatowe ubinadamu.

Mleta mada una Roho ya Fisi!
 
Alafu hili tukio, kama lililoambatana na hiyo video ndilo, basi siyo la hivi karibu ni tukio la miaka mitatu nyuma kama siyo minne, hili lishaletwa hapa wenye kurudisha kumbukumbu nyuma, watalikumbuka hili.
 
Kama hakuna ushahid Basi tuendelee kunywa bia tu..na modes futen huu uzi
 
Mbona inaonekana huyo jwtz ni sergeant na huyo polisi ni constable...sasa huoni nani mtovu wa nidhamu hapo?, kubishana na senior wake hadharani
 
Baeleze...
 
Mwaka Jana police walitoa tangazo la kazi wanahitaji watu wenye ufaulu wa division 4
... hao ni purposely kwa ajili ya kwenda kulinda makazi na familia za viongozi usiku wakiwa wamepumzika! Wewe na first class yako ukipewa hiyo kazi utaweza? Tuheshimu kazi za watu.
 
Kwa mujibu wao JWTZ kua wao ndio askari waliobaki woote ni raia wa kawaida.. hajalishi ni polisi askari magereza wala askari wa barabaran hao woote ni raia kwao
 
Bro! unalinganisha kibanda cha udongo na ghorofa halafu unauliza kipi chenye thamani!
Huwajui police uyo mjeda atawekewa ata risasi zilizompiga Akwilina kikosi kizima kimkatae
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…