Askofu Bagonza: Lissu amekosea kueleza in details alichoongea na Rais, akiendeshwa na mashabiki

Askofu Bagonza: Lissu amekosea kueleza in details alichoongea na Rais, akiendeshwa na mashabiki

Fisiemu wameumia sana, lini Liongo ameshawahi mkosoa hata jiwe au kiongozo yoyote kipindi cha jiwe au kiongozi yeyote wa Chief Hangaya?
Anajua kukosoa wapinzani tuu.
 
hata mimi nililiona hili, nadhani hakupaswa kusema hayo yote..ingekuwepo na summary ya pande zote.

Rais ni rais tu..lazima apewe heshima yake
Nyie mnajuaje kasema yote? Mlikuwepo kwenye kikao au ni hisia zenu zinawatuma kuwa Lissu kaongea yote? Mnajuaje kazungumza kuwawin wazee wa kulisha maneno kaamua kuwawahi
 
Rroho na ikuume tu. Nchi imelipuka kwa shangwe.
Sioni kosa la Bagonza ni maoni yake tu.

Tundu hakukutana na Rais kuomba maji, barabra na umeme. Kaongea maswala mtambuka ya watanzania kama Taifa.

Ni mambo yale yale ya siku zote. Siri ya nini?
Inawezekana hujamuelewa askofu. Ni kweli Lissu hakutakiwa kutoa taarifa ya walichozungumza unless otherwise kama wamekubaliana.

Naona kama inajenga taswira kwamba hata yale aliyoyasema japo ni ya msingi lakini Rais hawezi kutekeleza au kufanya jambo kwasababu eti Lissu kasema.
 
Askofu Dkt. Bagonza ameeleza haya baada ya Rais Samia kukutana Tundu Lissu, naa baadaye Lissu kuongelea kile alichozungumza na Rais.

Lissu anaweza kuwa amekosea kwenda in detail ya mazungumzo na Rais, na wasaidizi wa rais wanaweza kuwa wamekosea kurusha picha za Lissu kukaguliwa, kusisitiza nani kaomba kukutana, usuluhishi unahitaji restraint, Rais anapotoshwa, Lissu akiendeshwa na mashabiki"

Pia soma
- BRUSSELS, UBELGIJI: Rais Samia akutana na Tundu Lissu na kufanya mazungumzo mafupi
- Summary ya Maongezi ya Rais Samia na Tundu Lissu yaliyofanyika Ubelgiji



Lissu kwa hali halisi alingeweza kunyamaza. Lakini wenye nia mbaya. Lakini vilevile hatujui kama kasema yote au kasema yake tu ambayo anataka watu wajue. Mfano hajasema Raisi kasema nini zaidi ya kusema ataenda kuifanyia kazi. Hajatoa siri za Rais zaidi ya kusema mwenyewe
 
Kwa hili napingana na Dkt Boganza. Lissu kafanya vema sana kusema ukweli & uwazi wa kilicho zungumzwa! La sivyo wachawi wasingekawia kumtungia stories za kusaliti au kusalimu amri!
Kasema kwa faida ya nani?? In protocol hii imekaaje ukutane na Rais halafu Rais asiseme mmezungumza nini na wewe ukaenda kubwabwaja? Sio sawa!
 
Lissu amefanya vile ili kusiwepo na aina yoyote ya kukasalitiana. Ikumbukwe leo Rais alitakiwa kukutana na uongozi wa EU hivyo kikao na Lissu ni turufu kwa serikali ya SSH kuliko kwa Lissu.

Kwa vyovyote, Rais alitaka kujenga hoja ya kuwa na nia njema ya kuanzisha mjadala na upinzani hususani Lissu ambaye yupo ukimbizini alikokwenda kupitisha bakuli.

Kwa Lissu kutoka hadharani na kusema yale, Rais anafungwa na hawezi kumgeuka Lissu kwenye zile hoja, labda atashindwa kutekeleza makubaliano kwa shinikizo la chama chake lakini dunia itajua hakuwa mkweli katika mjadala. Lissu asingetumia ile fursa, hoja zingepitishwa kinyemela katika meza ya mazungumzo na viongozi wa EU alafu rais akirudi nchini anaamua kupotezea, hapo tayari Lissu anakuwa ametumika.
Nakubaliana na wewe mia kwa mia ,wewe ndio mtu mwenye akili zaidi kuchangia mjadala huu.
Bila lisu kufanya hivyo kungetokea upotoshaji mkubwa na propaganda za hali ya juu kuhusu kikao hicho.
Lisu kichwa au waliomshauri afanye hivyo ni vichwa kwelikweli.
Asante kwa komenti hii.
 
Mimi binafsi sijaona kosa la Lisu , kulikuwa hakuna haja ya kuficha kitu, sote tulikua na hamu kubwa ya kujua kulikoni , kama asinge tuelezea tungebaki na kimuhemuhe, bora katutuliza mioyo, big up Lisu , bigup Mama Samia.
 
Sometimes Lissu ni wa kumsamehe tu, madhira aliyofanyiwa hata ingekuwa mimi au wewe tusingekuwa sawa kisaikolojia muda wote.

All in all, ilikuwa ni vyema wamekutana na kuwa na kikao, mengine yote ni yatokanayo tu
Hivyo ndivyo alivyo Lissu wala hata sio kwa sababu ya lile tukio alilofanyiwa.
 
Kasema kwa faida ya nani?? In protocol hii imekaaje ukutane na Rais halafu Rais asiseme mmezungumza nini na wewe ukaenda kubwabwaja? Sio sawa!
Ulitaka nani aseme?.Mwenye agenda zakumwambia rais alikua Lissu sasa ulitaka rais ndiye aje aseme kua niliongea na lissu na kaniambia kesi ya mbowe ni kesi ya mchongo..Rais hana sababu yoyote yakuelezea umma mazungumzo ya lisu yalivyokua maana yaye yuko kwenye upande wa kutekeleza hoja alizoletewa ila lissu ana sababu kwasababu mazungumzo yale yanafaida kwake,chama chake na hali ya kisiasa kwa ujumla.na amefanya vyema kueleza ili wananchi tujue na tumsubiri rais aamue atakalo amua.sasa sijui vichwa vyenu vinatakaje.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Ni kweli na hii inaonyesha hafai kuwa kiongozi mkubwa.

Rais kamheshimu amemfuata unless wangaitisha press ya pamoja.

Mh.Rais next time achana na Hawa wajinga wasio na adabu wala wasiojoelewa.
Rais hajaumizwa kwa lolote ila nyie kajamba nani na roho zenu za kutu ndio mnajifanya mmeumia.kwendeni uko.hopeles kabisa.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Katika mazingira ya Lissu kuwa ughaibuni na hana passport iwe imeibwa au ilipotea...ni lazima ujenge urafiki na serikali kwa udi na uvumba. Hizi vurugu zinatakaga uwe kwanza na passport
 
Back
Top Bottom