Askofu Gwajima: Nchi imekosa maono, kila Rais anakuja na lake, ipo siku tutajuta

Askofu Gwajima: Nchi imekosa maono, kila Rais anakuja na lake, ipo siku tutajuta

Johnny Sack

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2017
Posts
8,984
Reaction score
19,288
Askofu Gwajima ambaye ni Mbunge wa Kawe kasema nchi imekosa maono kwa kuwa kila Rais akiingia madarakani anaachana na ya mtangulizi wake, kuongeza hilo kamwe halitaweza kutuletea maendeleo

Gwajima amesema nchi inatakiwa kuwa na mikakati yake ya muda mrefu na kila rais anayeingia madarakani anaongozwa na mikakati na maono hayo na sio kuleta vitu vyake vipya, ama sivyo anaweza akaja Rais wa ajabu ambaye atavuruga kila kitu na hakuna atakeyeweza kumbana kwa kuwa hakuna maono.



Mbunge wa Kawe, Josephat Gwajima amesema ni muhimu Tanzania kuwa na Dira ya Taifa ili kila Rais anayeingia Madarakani asimamie maono ya Nchi na si yake binafsi

Akiwa Bungeni amezungumzia kila Rais anayeingia Madarakani kuanza na lake akisisitiza hakuna Nchi inayoweza kuendelea ndani ya Utawala mmoja

Ameeleza, "Alipoishia Nyerere, Mwinyi hajaendelea pale. Alipoishia Mwinyi, Mkapa hajaendelea. Alipoishia Mkapa, Kikwete hajaendelea pale na Magufuli naye hajaendelea. Kila Rais anayeingia Madarakani anaanza chake"
 
Ila ana point, acheni ushabiki, ikiwa kila Rais akija anafanya yake, au anaacha ya mtangulizi wake na kuponda na kufanya mengine mapya, na akiingia Rais mwingine tena anaanza upya tena mambo yake, ni hatari sana sana, sbb kuna mambo ni uti wa mgongo wa nchi, sasa ukikuta labda haijakamilika na kuiacha njiani, ni kukosa mipango ya maendeleo endelevu, nchi haijengwi hivyo.

Hata Mungu alivyoona mnara wa Babeli unajengwa haraka ili kuharibu au kusimamisha ujenzi, aliwapa lugha kila mmoja tofauti ili wasielewane na ili kazi ya ujenzi wa mnara wa Babeli ife, na kweli ikafa. Hivyo ikiwa kila Rais akija na lake na kuacha la mtangulizi wake yote, hatutafika hata kidogo, huko ni kukosa maono au lugha tofauti na in simple words, maendeleo ni kama mbio za vijiti.
 
Hivi kwanini hawa marais wanaoongozwa na ilani ya chama chao lakini bado kila mmoja wao huja na lake na kuacha la mwenzake?

Ina maana hawaifuati ilani ya chama chao?

Kama jibu ni ndio, basi ile kauli ya Kinana kwamba CCM ndio wanaiagiza serikali na sio serikali kuiagiza CCM itakuwa ni batili.
 
Mbona aliyepita aliacha yamtangulizi wake akaanzisha mapya na hakusema?
Tulieni nyie sukuma Gang zamu yenu ilishapita.
Ukiangalia PLANNING SYSTEM ya Tanzania ipo vizuri sana.
.
Yaani haimtaki kila RAIS aje na mipango yake au mambo yake.
.
Kila Planning kuna kitu kinaitwa INCREMENTAL PLANNING
.
Shida ya kuingiza siasa kwenye maendeleo ndio hii.
.
SHIDA YA KUIPA SIASA NAFASI KUBWA KULIKO UTENDAJI.
 
Mbunge wa Kawe, Josephat Gwajima ni muhimu Tanzania kuwa na Dira ya Taifa ili kila Rais anayeingia Madarakani asimamie maono ya Nchi na si yake binafsi

Akiwa Bungeni amezungumzia kila Rais anayeingia Madarakani kuanza na lake akisisitiza hakuna Nchi inayoweza kuendelea ndani ya Utawala mmoja

Ameeleza, "Alipoishia Nyerere, Mwinyi hajaendelea pale. Alipoishia Mwinyi, Mkapa hajaendelea. Alipoishia Mkapa, Kikwete hajaendelea pale na Magufuli naye hajaendelea. Kila Rais anayeingia Madarakani anaanza chake"
 
Mbona aliyepita aliacha yamtangulizi wake akaanzisha mapya na hakusema?
Tulieni nyie sukuma Gang zamu yenu ilishapita.
Gwajima ana hoja

Umemwelewa alichoongea ?
Kila Raisi akija anakuja na yake na kuponda ya mtangulizi wake

Nyerere aliponda ya wakoloni taifisha viwanda,Majumba,biashara mashule ya private nk na kufanya ya umma,Mwinyi akaponda ya Nyerere ,Mkapa akaponda ya Mwinyi,Kikwete akaponda ya Mkapa ,Magufuli akaponda ya Kikwete na Mama Samia anaponda ya Magufuli

Nchi utafikiri kichwa cha mwendawazimu kila Raisi ajaye anajifunzia kunyoa
 
..Ni mambo yapi yaliyoachwa? Maana kama ni miradi Mama Samia kwa kiasi kikubwa anajitahidi kumalizia miradi mikubwa iliyoachwa na marehemu huku pia akianzisha na mengine.
 
Ameshindwa kusema kwamba tatizo ni katiba mpya. Ameona akisema hvyo wenzie watamnanga lkn alimaanisha tatizo ni katiba itakayo tengeneza taasisi imara ambayo ndio itamuongoza mtu na siyo mtu kui guide taasisi
Ngoja leo tuweke siasa za katiba pembeni, tuongee kitaalamu then tutajua katiba inaingia vipi huko mbele.

Tupo kwenye hoja ya kwanini kila RAIS anakuja na maono yake.

HAPA KATIBA HAIMZUII KILA RAIS KUJA NA MAONO ANAYO YATAKA
 
Askofu Gwajima ambaye ni Mbunge wa Kawe kasema nchi imekosa maono kwa kuwa kila Rais akiingia madarakani anaachana na ya mtangulizi wake, kuongeza hilo kamwe halitaweza kutuletea maendeleo...
ccm ni chaka la mijizi tangu lini wakatuonea huruma watanganyika? wao ni mbele kwa mbele wanaangalia maslahi yao na watoto wao na wajukuu.
 
Back
Top Bottom