Askofu Ikongo: Walioniteka, kunivalisha kitambaa cha sumu nawafahamu

Askofu Ikongo: Walioniteka, kunivalisha kitambaa cha sumu nawafahamu

Waambieni hao viongozi wa kanisa waachane na siasa.

Biblia gani hizo wanasoma?

Mi nimesoma Bible ya king James, nimesoma lost books from the bible, ninasoma wisdom of Solomon (apocrapha) sijaona vikimchanganya Mungu na politics.
Kwa hiyo alichotendewa ni sahihi kabisa kwako kwa sababu tu yeye ni Askofu?
Pumbavu sana
 
Kwahiyo mmeona huyo askofu katekwa kwasababu za kisiasa?au ndo watanzania wa jamii forum katika ubora wenu
Hapa tuna watu ambao ufahamu wao ni CCM na CHADEMA basi! Huwezi hata kuelewa walimaliza darasa la ngapi!
 
Waambieni hao viongozi wa kanisa waachane na siasa.

Biblia gani hizo wanasoma?

Mi nimesoma Bible ya king James, nimesoma lost books from the bible, ninasoma wisdom of Solomon (apocrapha) sijaona vikimchanganya Mungu na politics.
Kama ni hivyo mbona kuapishwa wanatumia vitabu vya dini?au yale ni majalada yake labda mle ndani hakuna mistari
 
SASA NMEGUNDUA TATIZO ULILO NALO NI KUBWA KULIKO NLIVYODHANIA. HILO HALIKUTOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGANA KUOMBA.

Unaelewa nini kuhusu THEOCRATIC GOVERNMENT? Uache kusoma biblia kwa kukurupuka, tafakari kupata ujumbe.

Sauli ni zao la waisraeli kukataa mfumo wa UFALME wa MUNGU na kutaka kufanana na mataifa mengine. Lakini kumbuka pia Mungu alikuwa ni mfalme wao na alikuwa akiwapangia katiba. Sasa lete katiba ya Mungu wako kwenye taifa lenye imani milioni uone!! Acheni tabia ya kumsingizia Mungu enyi vipofu.

Kristo alikuja kuandaa taifa lake, taifa jipya, taifa la watu walioitwa kwa jina lake. Hawa ndio waliaminio jina lake. Hawa wameitwa UFALME WA MUNGU, wameifia dunia na sasa wanaishi kwa ajili ya Kristo. Sio wenye kujiinua kwenye mfumo wa dunia kwa sababu wa sio wa ulimwengu huu. SOMA BIBLIA KWA KUTAFAKARI
 
Nyenyere Crimea hii mnadhani siyo siasa? Au kwa kuwa hamjaona chadema,act na ccm? Au hamjaona neno Mbunge,waziri,mkuu wa mkoa,mkuu wa wilaya n.k? Jaman why hampendi kutumia akili?

Wewe unarumia akili yako sisi tunatumia hekima ya Mungu. Kwako hekima hii inaonekana ni upumbavu kea sababu unapotea.

15 Wakawaamuru kutoka katika baraza,wakafanya shauri wao kwa wao,
16 wakisema, Tuwafanyie nini watu hawa? Maana ni dhahiri kwa watu wote wakaao Yerusalemu ya kwamba ishara mashuhuri imefanywa nao, wala hatuwezi kuikana.
17 Lakini neno hili lisije likaenea katika watu, na tuwatishe wasiseme tena na mtu awaye yote kwa jina hili.
18 Wakawaita, wakawaamuru wasiseme kabisa wala kufundisha kwa jina la Yesu.

Hakina siasa

19 Petro na Yohana wakawajibu wakawaambia, Kwamba ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe;
20 maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia.
21 Nao walipokwisha kuwatisha tena wakawafungua, wasione njia ya kuwaadhibu, kwa sababu ya watu; kwa kuwa watu wote walikuwa wakimtukuza Mungu kwa hayo yaliyotendeka;
26 Wafalme wa dunia wamejipanga, Na wakuu wamefanya shauri pamoja Juu ya Bwana na juu ya Kristo wake.
27 Maana ni kweli, Herode na Pontio Pilato pamoja na Mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika katika mji huu juu ya Mtumishi wako mtakatifu Yesu, uliyemtia mafuta,
28 ili wafanye yote ambayo mkono wako na mashauri yako yamekusudia tangu zamani yatokee.
29 Basi sasa, Bwana, yaangalie matisho yao; ukawajalie watumwa wako kunena neno lako kwa ujasiri wote,
30 ukinyosha mkono wako kuponya; ishara na maajabu vifanyike kwa jina la Mtumishi wako mtakatifu Yesu.
31 Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.

Hebu tuonyeshe wewe mwenye akili siasa iko wapi hapo? Watu wanazuiwa kuhubiri JINA LA YESU, ndio siasa hiyo? Fafanua tuone basi
 
@Mamdenyi uko sahihi kabisa. Huwa nawashangaa wanaokimbilia Agano la Kale kuhalalisha kanisa kujihusisha na siasa za dunia. Wanachukua mfumo wa taifa la Israeli ya kale wanajaribu kuuoanisha na serikali za sasa.

Yesu Kristo hakuwahi kuwa na ugonvi na "serikali" badala yake maadui zake namba moja walikuwa watu wa "dini." Pilato alijaribu kumfungua awe huru, watu wa dini walisema nini?

Sio sawa kuhubiri siasa badala ya habari za ufalme wa Mungu. Yohana Mbatizaji hakufungwa kwa sababu za kisiasa bali baki za binadamu. Sababu za haki za binadamu kwa kumkemea Herode kupora mke wa ndugu yake, hilo nalo ni siasa? Tafakari

Turudi kwenye agano jipya. Kikubwa kinachokemewa ni udhalimu, haijalishi ni mtu gani anatenda, Yesu aliukemea hadharani bila oga, Yohana alifanya hivyo, mfalme mmoja enzi za mitume alikufa kwa chango kwa ajili ya udhalimu na kumkufuru Mungu kupitia huo udhalimu.

Viongozi wa dini mchana kweupe bila kuogopa kemeeni maovu na udhalimu bila kuchagua sura.

Mchungaji mwema hawezi kuacha kondoo wakaliwa na mbwa mwitu au mbweha, ktk siasa za leo kuna mbweha wengi, tuwape ngumi za uso na makavu laivu bila oga.
 
Waambieni hao viongozi wa kanisa waachane na siasa.

Biblia gani hizo wanasoma?

Mi nimesoma Bible ya king James, nimesoma lost books from the bible, ninasoma wisdom of Solomon (apocrapha) sijaona vikimchanganya Mungu na politics.
Wewe ni takataka ibilisi tena wahed blalifuu
 
Basi unasoma halafu huelewi. Ungekuwa unaelewa ungeelewa kwa nini Yeremia alifungwa, nani alihusika kumchagua Saul na kumtengua, nani alimteua Daud... Ungefahamu Ugomvi wa Yesu na Utawala wa Kirumi, kwa nini Yohana mbatizaji alikatwa kichwa. Yapo mengi unafahamu Yohana Mbatizaji alikemea nini?

Siasa ipo sana katika Biblia labda kama huelewi. unamfaham Esther alifanya nini pale Harmani alipotaka kuwatowesha watu wake?

Wewe hufahamu Siasa ndo maana unaona kama hakuna Siasa. Biblia ina Siasa sana na ina watumishi wengi ambao wamehusika na siasa.

Nabii Isaya alienda kumwambia Sauli mwanasiasa kuwa Mungu amemkataa.. hiyo haikuwa Siasa?

Hao wanasiasa kwa nini wanaapishwa na viongozi wa Dini au wanatumia Biblia na Quran kuapa? Hiyo siyo kuchanganya Dini na Siasa?
Tukio la Askofu Pius Ikongo kutekwa na watu wenye silaha aina ya bastola wakiwa na magari mawili na kufunikwa na kitambaa chenye sumu na kupata madhara makubwa mwilini linasikitisha sana.

Kinachoumiza ni kutokamatwa wala kuhojiwa kwa watesi wake licha ya kuwatambua na kuwataja kwa majina katika maelezo yake polisi.

Kwa maelezo yake, ametumia zaidi ya milioni 170 kujitibu Afrika Kusini, Kenya, Muhimbili na KCMC kwa mwaka mmoja na nusu.

Take note: Askofu huyu ameoa kwenye familia ya Nyerere.

Msikilize hapa:




View attachment 1484754


Kwa hii story ya Askofu Ikongo inaonesha picha halisi ya jinsi nchi hii ilivo na TABIA ZA WATANZANIA!
Kama watu wamethubutu kupanga KUMWUA ASKOFU MTUMISHI WA MUNGU na tena KADA WA CCM wakishirikiana na Vyombo vya Ulinzi na Usalama.....!!
Hebu fikiria angelikuwa ni MPINZANI angelifanywaje?
 
Waambieni hao viongozi wa kanisa waachane na siasa.

Biblia gani hizo wanasoma?

Mi nimesoma Bible ya king James, nimesoma lost books from the bible, ninasoma wisdom of Solomon (apocrapha) sijaona vikimchanganya Mungu na politics.
Mwanamke atabaki kuwa mwanamke tu Idiots.
 
Turudi kwenye agano jipya. Kikubwa kinachokemewa ni udhalimu, haijalishi ni mtu gani anatenda, Yesu aliukemea hadharani bila oga, Yohana alifanya hivyo, mfalme mmoja enzi za mitume alikufa kwa chango kwa ajili ya udhalimu na kumkufuru Mungu kupitia huo udhalimu.

Viongozi wa dini mchana kweupe bila kuogopa kemeeni maovu na udhalimu bila kuchagua sura.

Mchungaji mwema hawezi kuacha kondoo wakaliwa na mbwa mwitu au mbweha, ktk siasa za leo kuna mbweha wengi, tuwape ngumi za uso na makavu laivu bila oga.

Kukemea udhalimu sio SIASA!! Jukumu la viongozi wa dini ni Kukemea DHAMBI, sio siasa za CHADEMA na CCM. Dhambi ni standard, haina chama. Kukemea maovu ni jukumu la kila mmoja, bali kujiingiza kwenye siasa sio wajibu wa viongozi wa kidini. Kama mkristo anavyoweza kuwa rais kwenye zama hizi, ndivyo ilivyo kwa mwislamu n.k. Tuache kumshusha Mungu kwa kumhusianisha na mifumo ya hovyo ya kidunia.
 
Waambieni hao viongozi wa kanisa waachane na siasa.

Biblia gani hizo wanasoma?

Mi nimesoma Bible ya king James, nimesoma lost books from the bible, ninasoma wisdom of Solomon (apocrapha) sijaona vikimchanganya Mungu na politics.
Mama, achana na propaganda za ajabu. Kama hujui Jambo usijifanye unajua
 
Basi unasoma halafu huelewi. Ungekuwa unaelewa ungeelewa kwa nini Yeremia alifungwa, nani alihusika kumchagua Saul na kumtengua, nani alimteua Daud... Ungefahamu Ugomvi wa Yesu na Utawala wa Kirumi, kwa nini Yohana mbatizaji alikatwa kichwa. Yapo mengi unafahamu Yohana Mbatizaji alikemea nini?

Siasa ipo sana katika Biblia labda kama huelewi. unamfaham Esther alifanya nini pale Harmani alipotaka kuwatowesha watu wake?

Wewe hufahamu Siasa ndo maana unaona kama hakuna Siasa. Biblia ina Siasa sana na ina watumishi wengi ambao wamehusika na siasa.

Nabii Isaya alienda kumwambia Sauli mwanasiasa kuwa Mungu amemkataa.. hiyo haikuwa Siasa?

Hao wanasiasa kwa nini wanaapishwa na viongozi wa Dini au wanatumia Biblia na Quran kuapa? Hiyo siyo kuchanganya Dini na Siasa?
Mkuu umeeleza vzr, ila aliyeenda kumjuza mfalme Sauli kuwa MUNGU amemkataa ni Nabii Samwel
 
Waambieni hao viongozi wa kanisa waachane na siasa.

Biblia gani hizo wanasoma?

Mi nimesoma Bible ya king James, nimesoma lost books from the bible, ninasoma wisdom of Solomon (apocrapha) sijaona vikimchanganya Mungu na politics.
Siku hizi siasa na dini imekuwa pete na kidole
Imefika wakati viongozi wa siasa wanaoenda kuabudu kwenye sehemu za ibada kutengewa muda maalum nakualikwa kwenye mimbali kutangaza kampeni na kupiga porojo za siasa kana kwamba wako kwenye majukwaa ya siasa.
 
Back
Top Bottom