Askofu Mkuu Mwandamizi Protase Rugambwa ateuliwa kuwa Kardinali

Askofu Mkuu Mwandamizi Protase Rugambwa ateuliwa kuwa Kardinali

Nitaanzia mbali sana bro!. Cardinal ni "Prince of Rome"...na limezaliwa kutoka, katika historia ya watu amba walikua wakichaguliwa kumsaidia Askofu wa Roma katika ushauri na uongozi katika utendaji wake. Na baadaye kundi hili likagawanywa katika vitengo mbali mbali...na hasa baadaye yakazaliwa makundi manne yaliyosimamia makanisa makuu manne ya Roma- yaani Kanisa la Kipapa ya Mt. Yohane wa Lateran ( Cathedral of Rome), Mt. Petro, Mt. Paulo na Maria Mkuu ( Mary Major)...haya makundi yakawa kama Cardinal Points, points of reference, na muongozo katika kumsaidia Askofu wa Rome ambaye ndio Baba Mtakatifu. Hivyo ndivyo likazaliwa neno "Cardinal"...ila maana halisi, anaye chaguliwa anakua "Prince of Rome" na anapata hadhi ya Ukasisi wa Jimbo la Roma, na hapo ndipo anapatiwa moja ya Kanisa Roma ama Parokia. Hawa Cardinals wanakua katika hadhi tatu; Cardinal Bishop, Cardinal Priest na Cardinal Deacon...ambazo ni hatua cardinal anapitia kulingana na muda, na kuundwa/ kufanywa kwake ( to be created ).

Hivyo basi, kardinali ni Tuzo anayopewa Askofu, Padre au Shemasi. Askofu Mkuu ni Askofu wa Jimbo Kuu, mathalani Tz yapo nane.

Nchi inaweza kuwa na makardinali hata wanne. Ukardinali ni tuzo sio cheo ktk mfumo wa ngazi ktk vyeo vya kanisa.
Makardinali ni wajumbe wa baraza(conclave) inayomchagua Papa kiti kikiwa wazi. Wao pia ni wagombea kwa maana Papa anachaguliwa miongoni mwa Makardinali.
Hawagombei kama kwenye siasa bali hufungiwa kila mmoja kwenye chumba chake bila kuonana na mwingine na kupigiana kura. Mshindi lazima apate theluthi mbili ya kura zote.... Askofu Mkuu au Askofu mwingine hana nafasi hiyo....Nchi kama Italy wanao 28, USA wako 11, German 5 wakati Rwanda hawakuwahi kuwa na cardinal mpaka walipompata last year.

Pia tuwekane sawa kuwa Kadinali siyo mkuu wa Kanisa KATOLIKI NCHINI, Lahasha, bali Rais/Mwenyekiti wa TEC ambaye kwasasa ni Askofu Gervas Nyaisongwa wa Jimbo Kuu la Mbeya. Hivyo Fr Kitima ni mtu mkubwa sana kwasasa kikanisa kama Katibu wa TEC. Mara kadhaa idara ya habari nchini imekuwa ikifanya haya makosa kwa kudhani Kadinali ni mkubwa kuliko maaskofu wengine. Big NO.
Tusilaumu vyombo vya habari

Hata wanasiasa na Makardinali wenyewe hujidhihirisha kuwa wao ni Wakubwa sana kuliko Rais wa TEC...hasa Mzee Pengo, kazingua sana wakati wake
 
Wewe fala sana,kumbe unamhukumu mtu kwa kuangalia sura yake,sasa una utofauti gani na Wasukuma wa Shinyanga waliokuwa wanaua Vikongwe wenye macho mekundu kwa kuwatuhumu kuwa ni wachawi?.
Ni ngumu sana kunielewa bwashee
 
Mheshimiwa, Askofu mkuu Mwandamizi Protase Rugambwa, na sasa Kadinali,

Bwana Mungu akubarikie na kukulinda,

Bwana Mungu akuangazie Nuru za Uso wake na kukufadhili,

Bwana Mungu akuinue uso wake na kukupa Amani. [emoji120][emoji120][emoji120]
 
Inakuhusu nini? Ni majibu ya Mwafrika, hata alipoletewa hii Imani hakuhoji, aliacha jadi yake na kudandia jadi za kizungu. Ni lazima nihoji kuhusu hivyo vyeo, Ni kulingana na mafundisho ya Yesu?
 
Nataka kutunga wimbo wa kumpa heko Mheshimiwa Askofu Mkuu, Protase Rugambwa,

Nisaidieni mistari iendane na huu wito wake mpya wa Kadinali.

Naona safari ya Vatican hii hapa.
 
Boss mkuu wa RC Tanzania ni nani?
Tupe hierarch kidogo atleast top three nchini hapa
Hakuna boss mkuu wa RC Tanzania. Hayupo.

Kuna maaskofu yenye mandate kwenye majimbo yao bila kuingiliwa na yeyote isipokuwa anaewateua yaani POPE.

Kuna TEC wajumbe wa TEC ni maaskofu wote wa majimbo including cardinal.

Kuna RAIS wa TEC na KATIBU wake.

Kwenye mambo yakufanyia maamuzi, misimamo ya pamoja kikanisa ndio utawasikia hao TEC.

RAIS wa TEC nae ni ASKOFU somewhere Hana uwezo kuingilia maamuzi ya askofu Fulani ndani ya jimbo Fulani.

Mapadre wako chini ya maaskofu wao wa jimbo.


Cardinal anaweza kuwa na influence but wenzake wanaweza mpinga ikiwa maamuzi yake ni kinzani na hayana Tija refer Cardinal alipokuwa anaenda kinyume na wenzake wakati wa mZiLaNkeNdE.
 
Nataka kutunga wimbo wa kumpa heko Mheshimiwa Askofu Mkuu, Protase Rugambwa,

Nisaidieni mistari iendane na huu wito wake mpya wa Kadinali.

Naona safari ya Vatican hii hapa.
Ni kweli tupu. Aione espy na Nchumbiji yake. Time will tell
 
Hakuna boss mkuu wa RC Tanzania. Hayupo.

Kuna maaskofu yenye mandate kwenye majimbo yao bila kuingiliwa na yeyote isipokuwa anaewateua yaani POPE.

Kuna TEC wajumbe wa TEC ni maaskofu wote wa majimbo including cardinal.

Kuna RAIS wa TEC na KATIBU wake.

Kwenye mambo yakufanyia maamuzi, misimamo ya pamoja kikanisa ndio utawasikia hao TEC.

RAIS wa TEC nae ni ASKOFU somewhere Hana uwezo kuingilia maamuzi ya askofu Fulani ndani ya jimbo Fulani.

Mapadre wako chini ya maaskofu wao wa jimbo.


Cardinal anaweza kuwa na influence but wenzake wanaweza mpinga ikiwa maamuzi yake ni kinzani na hayana Tija refer Cardinal alipokuwa anaenda kinyume na wenzake wakati wa mZiLaNkeNdE.
Asante sana. Nimekuelewa sana.
Ila kama ni hivyo
Kwamba kila askofu na jimbo lake is like a sovereign state,
1. Wanalipwaje mishahara na marupurupu? Esp kama makusanyo/sadaka/offerings/biz ventures they lags from place to place territorial (methinks Dar is way richer than Tabora huko for example)
 
Asante sana. Nimekuelewa sana.
Ila kama ni hivyo
Kwamba kila askofu na jimbo lake is like a sovereign state,
1. Wanalipwaje mishahara na marupurupu? Esp kama makusanyo/sadaka/offerings/biz ventures they lags from place to place territorial (methinks Dar is way richer than Tabora huko for example)
Waumini ndio wanaohusika
 
View attachment 2682944
Askofu mkuu Mwandamizi Protase Rugambwa​


Mhashamu Protase Rugambwa sasa Mhadhama.

Baba Mtakatifu Fransisco amemteua Askofu mkuu Mwandamizi Protase Rugambwa kuwa Kadinali. Mhashamu Protase Rugambwa ni mwandamizi wa kiti cha uaskofu Jimbo kuu Katoliki la Tabora.

Hongera sana Mhashamu Rugambwa.

Taarifa toka Vatican
Sister Angela Rwekiza


-
Pia soma >
- Je, Protase Rugambwa ndiye Kardinali ajaye Tanzania?


--
KARDINALI MTEULE RUGAMBWA NI NANI?

▪︎Askofu Mkuu Rugambwa alizaliwa tarehe 31 Mei 1960 huko Bunena-Bukoba nchini Tanzania, akapata Daraja Takatifu ya Upadri kutoka mikononi mwa Mtakatifu Yohane wa Pili alipotembelea Tanzania tarehe 2 Septemba 1990 na kuwa Padri wa Jimbo Katoliki Rulenge-Ngara.

Kuanzia mwaka 2002 hadi mwaka 2008 alifanya utume wake kwenye Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa watu mjini Vatican. Baba Mtakatifu Benedikto XVI, tarehe 18 Januari 2008 akamteuwa kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki Kigoma, na tarehe 26 Juni 2012 akateuliwa kuwa Katibu Mwambata wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa Watu na Rais wa Mashirika ya Kipapa ya Kimisionari na wakati huo huo kumpandisha hadhi na kuwa ni Askofu mkuu.

Tarehe 9 Novemba 2017 Baba Mtakatifu Francisko akamteua kuwa Katibu mkuu wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa watu. Baada ya kulitumikia Baraza kwa vipindi viwili na muda wake ulipogota ukomo, kadiri ya Katiba mpya ya Kitume inayojulikana kama “Predicate evangelium” yaani “Hubirini Injili” Juu ya Sekretarieti kuu “Curia Romana” na Huduma Yake Kwa Kanisa na Kwa Ulimwengu”.

Tarehe 13 Aprili 2023, Baba Mtakatifu alimteua Askofu Mkuu Protase Rugambwa kuwa Askofu mkuu wenye haki ya kurithi Jimbo kuu la Tabora, Tanzania.

Bora tumepata Kadinali mpya. Cardinal Rugambwa the first was a humble man. Akaja mwingine baada ya kufariki. Kadinali ikawa ni kama cheo cha kisiasa.
Amechaguliwa mwingine wakati yeye akiona.
Sifa na utukufu kwa ukuu wake Mwenyezi Mungu.
Haya mengine yanakuja na kwenda. Kama vyeo tulivyonavyo.
Tujifunze kuwa wanyenyekevu. Mpaka kesho najiuliza nini kilitokea Cardinal wa Kwanza akazikwa nje ya jimbo lake alilofia. Labda yalikuwa matashi yake. Sijui....najiuliza tu
 
1696307004505.jpeg
 
Sikushangai ulikuwa bado hujazaliwa

Unajua shida ya mtu kama wewe ni kujaribu kulipaka matope kanisa katoliki kwa hila.
Unafikiri limefikisha zaidi ya miaka 2000 kwa bahati mbaya?
Kalagabaho! Unajidanganya sina namna ya kukusaidia
 
Back
Top Bottom