Askofu Mwamakula kuongoza matembezi ya hiyari kuhamasisha Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi

Askofu Mwamakula kuongoza matembezi ya hiyari kuhamasisha Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi

Huyu mzee atulie asitafute matatizo na sirikali hauji kama hizo ndiyo silaha kubwa za sirikali kuwachapia wanyonge..
Vuta picha katiba mpya ikaondoa ukomo wa uongozi wa mihula kwa rais
 
kwani hata kama katiba ikibadilishwa watz wanajua kufuata na kutumia katiba?
mbona katiba ya sasa ina mambo mengi ya kumjali na kumtetea mtz lakini mtz hajui kitu kuhusu hilo?

kwa maana hiyo basi katiba itakuwa ina manufaa gani kama mtz ameshindwa kuitumia na kuitambua hasa kukosa uthubutu wa kudai haki zake za msingi za kikatiba zilizopo kwenye katiba?

NB; wtz acheni propaganda msizokuwa na uelewa nazo, nakuhakikishieni hata kama katiba ikibadilishwa hamna kitu mtafanya kwasababu ni wazembe wa kufuatilia na kuzijua haki zenu za kikatiba na hata mkizifuatilia na kuzijua bado wtz hamna uthubutu wa kuthubutu kupambania haki zenu.

All in all msitake kuiingizia serikali gharama zisizo na maana za kuandaa na kutengeneza katiba ambayo hamjui kuitumia na hamna uthubutu nayo, acheni kufuata mikumbo na propaganda za kishenzi, KATIBA ILIYOPO INATOSHA.
 
Haya maandamano yasijekuwa kama yale ya uchaguzi. Lissu aliitisha maandamano b8la kukoma akaandamana mwenyewe.
Askofu asijejikuta anatembea peke yake
 
Hatuna tume huru ya Uchaguzi matokeo yake sasa hivi tuna mtu Ikulu ambaye ni haramu, Bunge haramu na Serikali haramu kutokana na uhuni na udhalimu uliofanywa October 28 uhuni na udhalimu ambao tume huru ya Uchaguzi haitaruhusu.

Matokeo yake Rais halali atakayechaguliwa na Bunge watabidi wajitume sana ili kuweza kuchaguliwa tena kwani uhuni kwenye uchaguzi hautakuwepo tena.

Bunge litakuwa na uwezo wa kumuondoa Rais madarakani kama halina imani naye na Wananchi wa majimboni watakuwa na uhuru wa kumuondoa Mbunge kama hawaridhiki na utendaji wake. Hayo yatakuwa ni mabadiliko makubwa sana Nchini.
kwani hata kama katiba ikibadilishwa watz wanajua kufuata na kutumia katiba?....
 
Bandekile Maana yake Wamemuachaaaaaa kutokana na kuwa na tabia Amvayohaiendani nao. Kanisa la Moravian Tanzania walimtenga kutokana na ugombanishi wake Kanisani, Anajiita Askofu lakini hana hadhi ya uaskofu n.k.
Hapo anatafuta Kiki ya kutafuta waumini kwa nguvu ila hana mvuto wala upako
Kheri ya huyu kuliko wale wanaovuta posho kwa kuongozana na viongozi wa CCM.
 
Huyu ndio kiongozi wa dini sio mapengo na snich mwenzie alhad
 
Mkuu nielimishe...
Unadai Katiba Mpya ili iweje?
1.Iwepo tuuu
2.itekelezwe?
3.Au yote kwa pamoja?
Ambayo haitakubali mtu yoyote awe juu yake! Yani aogope kuivunja maana atawajibishwa kwa mujibu wake.
 
Anayafanya hayo kwa kutumia andiko gani kwenye biblia
Acha undezi man, unataka rejea ya kwenye bible juu ya hili??? Embu tueleze basi, Job Ndugai anarejea kipengele gani cha katiba kuwakumbatia akina Mzee Halima na wenzake huko bungeni?

Hili ni jambo jema, linahitaj kuungwa mkono na wapenda AMANI na demokrasia wote nchini
 
KWA NINI ASKOFU AONGOZE KAMPENI YA KUUNDA TUME HURU YA UCHAGUZI NA KUANDIKWA KWA KATIBA MPYA?

Usiku wa Tarehe 3 Desemba 2020, niliwatangazia umma wa Watanzania na ulimwengu kwa ujumla kuhusu adhma yangu ya kuongoza Kampeni ya Kuunda Tume Huru ya Uchaguzi na Kuandikwa kwa Katiba Mpya ya Tanzania. Kampeni hiyo ambayo itaanza Januari 2021 itafanywa kwa njia ya Matembezi ya Hiali katika nchi nzima ambapo nitasafiri katika kila Mkoa na Wilaya za Tanzania (Bara na Visiwani). Pia, nitaweza kusafiri kwenda nje katika baadhi ya nchi kuonana na Watanzania wanaoishi nje ya nchi (Diaspora).

Suala la Katiba Mpya na Tume Huru sio suala la vyama vya kisiasa pekee! Ni suala ambalo linamhusu kila Mtanzania. Huko nyuma, zoezi hili liliachiwa wanasiasa na tumeona madhara yake. Siku mwanasiasa mmoja aliposhika madaraka na kutamka kuwa Katiba Mpya sio kipaumbele chake, zoezi la kuandika Katiba Mpya likakoma mara moja pasipo kujali gharama zilizotumika huko nyuma.

Upinzani ambao ungelitegemewa kupiga kelele Bungeni kwa niaba ya wananchi sasa umeondolewa na hivyo Bunge limebaki la Chama kimoja ambacho Mwenyekiti wake ambaye pia ni Rais alitamka wazi kuwa Katiba Mpya sio kipaumbele kwake. Hii ina maana kuwa hata Tume Huru ya Uchaguzi ambayo kwa kiasi kikubwa ni zao la Katiba Mpya haiwezi kupatikana.

Tukikaa kimya sote, kuna hatari ya Bunge la Chama kimoja kufanya mabadiliko makubwa ya Katiba iliyopo kwa lengo la kuzidi kuongeza madaraka na mamlaka kwa watawala na hata kuoondoa zaidi mamlaka ya watu. Vyama vya Siasa ambavyo vimekatazwa kufanya Mikutano ya Hadhara na hata kufanya Maandamano, vimezidi kumalizwa nguvu kwa kuondolewa Bungeni kupitia Uchaguzi Mkuu ulioghubikwa na kila aina ya ubabe, nguvu za vyombo vya dola na ufisadi. Kwa sababu hiyo, sauti mbadala iliyokuwa itokee kupitia Vyama vya Upinzani sasa tusiitegemee kuwa itakuwa na nguvu ya kutosha! Tuna imani kuwa vyama vya Siasa vitatiwa nguvu kubwa baada ya kuona jitihada hizi za Kiaskofu. Bila shaka navyo vitaunga mkono juhudi hizi sambamba na asasi za kiraia!

Ni kwa sababu hiyo, mimi niliye Askofu, nimesikia msukumo mkubwa kutoka moyoni mwangu kuwa yanipasa kuchukua hatua ya kuwahamasisha na kuwaandaa Watanzania kwa ajili ya mabadiliko makubwa ya kijamii, kimwili, kiroho na kiuchumi yatakayotokana na Kuundwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi na Kuandikwa kwa Katiba Mpya (Isaya 6:8-10).

Ni wazi kuwa kila jambo lazima liwe na mahali pa kuanzia na lazima pawepo na mtu au watu wa kulisemea. Ni dhahiri kuwa Watanzania katika wingi wa mamilioni yao wanataka na wanapenda mabadiliko makubwa. Changamoto iliyopo sasa ni nani wajitokeze kuwaongoza watu hawa kuelekea katika kilele cha mabadiliko hayo.

Hata wanachama na viongozi walio wengi wanaotokana na CCM wanapenda mabadiliko hayo lakini wanakosa ujasiri wa kupingana na Mwenyekiti wao aliyetamka wazi mbele ya hadhara kuwa Katiba Mpya sio kipaumbele kwake. Viongozi wengi wakuu wastaafu wa CCM na Serikali wangelipenda kuona na kushuhudia Katiba Mpya ikiandikwa, lakini itifaki za kiuongozi zinawazuia kupingana hadharani na mtazamo wa Rais aliyepo madarakani. Kwa sababu hiyo wanabakia kunung'unika chinichini.

Ni kwa sababu hiyo, Kampeni hii kuongozwa na Askofu ina umuhimu wake. Itakuwa ni Kampeni ya aina yake itakayoungwa mkono na makundi mengi ndani na nje ya nchi. Hata Malawi, Vyama vya Siasa viliposhindwa kuleta mabadiliko ya kidemokrasia, shinikizo kutoka kwa Maaskofu liliwezesha nchi kuyabusu mabadiliko mwanzoni mwa miaka ya 1990.

Kwa neema ya Mungu mimi nipo tayari kwa ujasiri mkubwa. 'Nimeshamfunga paka kengele'! Maaskofu wengi pamoja na viongozi wengine wa dini wapo nyuma yangu katika hili. Lililo muhimu zaidi ni kuwa Mungu yupo nyuma na mbele yangu! Shime Watanzania! Tuungane wote pamoja pasipo kujali vyama, itikadi, dini, elimu, ukabila nk.

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki na Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Makanisa ya Moravian ya Uamsho Duniani
 
Naam, inabidi tuelewane tu. Huku vitisho dhidi ya mabeberu vya kuwekewa vikwazo na kunyimwa misaada vikiwa vimepamba moto, huu ndio muda sahihi pia wa kuanzisha vuguvugu la kudai Tume huru na katiba mpya.
 
Back
Top Bottom