Askofu Mwamakula: Mpendwa Mama Samia Suluhu Hassan, mambo yafuatayo ni muhimu

Askofu Mwamakula: Mpendwa Mama Samia Suluhu Hassan, mambo yafuatayo ni muhimu

Baada ya msiba wa mzee Mkapa rais Magufuli aliumia sana hakuwahi kuwa sawa.

Vifo vya Balozi Mahiga na wengine hapo kati hadi kuja kufikia Maalim Seif Sharif Hamad na balozi KIJAZI vilikua pigo kubwa sana kwake.

Hakika alijikaza kama rais na mwanaume mbele ya watu ila nafsi yake iliumia na moyo wake uliumia zaidi

Kila mwanadamu ana njia yake atayopita, ameumaliza mwendo apumzike kwa amani kipenzi cha watanzania[emoji120]
We Ni mke wake ulijuaje Kama aliumia
 
Hili ni kati ya mawazo ya hovyo sana katika uongozi wa taifa kiuchumi. Kupandisha mishahara kunasababisha gharama za maisha pia zipande na inflation kuongezekaa nathamani ya shillingi kutelemka; ndiyo mambo yaliyovuruga thamani ya shilingi kutoka dola 1 kwa shilling 5 hadi kufikia leo dola 1 kwa shilingi ~2300+. Kenya wana curreny stable sana kwa sababu hawapandishipandishi mishahara yao kufurahisha wapiga debe.

Hata Marekani mishahara yao imekuwa hivi ilivyo kwa zaidi ya miaka 15; ile 1% -3.5% adjustement ya inflation inategemea sana na namba za iflation mwaka huo, siyo wanasiasa kusema tu kuwa wamepandisha mishahara ya watumishi wote.

Wakati wa Magufuli mishahara haikupanda, lakini pia inflation haikupanda, na hivyo thamani ya shillingi ikabaki pale pale kwa muda wote wa utawala wake hadi anatangulia mbele ya haki.
Una umri gani?
Jakaya anaingia madarakani 2005 alikuta mshahara wa JWT kima cha chini ni 73,000/= mpaka anaondoka 2015 JWTZ mshaara kapandisha wakawa wanapokea si chini ya 700,000.Hayati Magufuli anaingia madarakani 2015 sukari kaiukuta inauzwa 1000-1500 kwa kg.Muda mfupi sana wa utawala wa hayati magufuli bei ya sukari ikapanda kufikia 2500-3000.Usiongee jambo wakati hujui chochote.

Jakaya kaacha Cement tunanunua 13000-13500 huyu unaemsifia cement kaisukuma 15500.

Nondo 12mm jakaya kaicha 12000 leo ni zaidi ya 15000 vivyohivyo kwenye bati nako ni majanga matupu,jakaya kaacha bati ya alafu 30g ikiuzwa kati ya 22000-25000 leo bati ya 30g ni zaidi ya 35000.

Hapo utagundua Jakaya aliboresha Maisha ya watu lakini hayati magufuli ameumiza Sana watu kwani wakati bei za bidhaa zinapanda lakini hakuna maboresho yoyote ya mishahara.Ajira mpya hakuna,Biashara nazo zinakufa,Bei za nafaka nazo zimekufa,ukweli ni kwamba awamu ya tano imeleta majanga Sana uraiani.

Nakushauri kama umesoma sanaa usichambue uchumi kwani uchumi ni taaluma,hio hoja kwamba usipandishe mishahara ili uzuie inflation jifunze hapo juu.
 
Katika maaskofu waongo huyo Mwamakula na ka nusu baraghashia kake yumo

Angalia anachoandika kila sehemu "Tunashauri" wanashauri na nani wakati yeye peke yake ndie anashauri

Na mwishoni anaandike yeye kama yeye majina ya wengine hayamo

Asome nyaraka za Katoliki zinavyoandikwa
Wakusema tunashauri toka mwanzo wanajitaja na mwishoni wanaandika majina na vyeo vyao
 
Back
Top Bottom