Askofu Ruwaichi amuunga mkono Rais Ruto kupinga Ushoga hadharani!

Askofu Ruwaichi amuunga mkono Rais Ruto kupinga Ushoga hadharani!

MTAZAMO

JF-Expert Member
Joined
Feb 8, 2011
Posts
19,675
Reaction score
33,583
Wakuu,

Askofu mkuu Jimbo Katoliki la Dar es Salaam anaongea na waandishi wa habari juu ya Pugu Marathoni lakini pia amegusia swala la maadili ya jamii. Amesema amefurahishwa na kauli dhabiti ya Rais Ruto wa Kenya juu ya kulinda maadili ya nchi hiyo na kupinga hadharani mambo ya ushoga.

Lakini pia Askofu Ruwaichi amesema Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alitoa kauli dhabiti juu ya maadili lakini kiongozi mwenzake wa serikali akasema hiyo si kauli ya serikali! Ameuliza hapo kauli ya serikali ni ipi?

My take; Kwa nguvu na kasi ya msukumo juu ya ushoga unaoendelea duniani bila sisi kuchora mstari wa wazi na jamii ya kimataifa kuelewa msimamo wetu huko mbele tutapata shida kubwa hizo haki zitapoanza kudaiwa na watu potential bila woga hapa kwetu.

Mama yetu Mh Rais Samia pia aligusia umuhimu wa kulinda maadili yetu na kwa msimamo wake na dini yake nafahamu hawezi kuyumba kwenye hili na mfano mzuri ni serikali kupiga marufuku vitabu vya shule vinavyochochea hayo.

Nchi za wenzetu haya mambo yalianza kama mchezo na pengine hakuna aliyeamini itafikia hatua ya kuhalalishwa kisheria na hata kufundishwa mashuleni! Sasa tusisubiri tufike huko maana kijamii tunaanza kuzoeshwa tuone kawaida! Tunaona watangazaji maarufu, mastaa na hata shughuli mbalimbali za burudani jamii ya mashoga wanajitokeza wazi bila woga.

Tusipoziba ufa tutajenga ukuta! Tuanze kuchukua hatua sasa, tusifanye mzaha na maadili ya msingi yanayolinda utu wetu.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Huwezi kuwa na uchumi tegemezi kisha uanze kupiga hesabu za kuyavimbia mataifa ya ulaya na marekani, hao viongozi wa serikali watakuwa wanasema tu chini chini, lakini hawawezi kuweka msimamo wa wazi utambulike mbele ya jumuia ya kimaifa, wanajua jeuri hiyo kama nchi hatuna.

Kila siku tunajinadi hatufungamani na upande wowote, naamini huu msimamo tunauendeleza hata kwenye masuala mengine kama hayo ya ushoga, hata kama ikiwa ni kimya kimya.
 
Huwezi kuwa na uchumi tegemezi kisha uanze kupiga hesabu za kuyavimbia mataifa ya ulaya na marekani, hao viongozi wa serikali watakuwa wanasema tu chini chini, lakini hawawezi kuweka msimamo wa wazi utambulike mbele ya jumuia ya kimaifa, wanajua jeuri hiyo kama nchi hatuna.
Ruto ameweka wazi, Museven amesaini kabisa sheria. Tunapaswa kuifanya hii iwe ajenda Afrika kama tulivyoweza kwenye vita nyingine. Wakiona viongozi wetu wanaweka msimamo hawawezi kutugawa kirahisi.

Hivi kama akina Nyerere wangekuwa na woga wa kiwango hiki wangepigania uhuru hadi nchi zingine zilizokuwa chini ya hao hao wazungu? Tena hali yetu ya uchumi haikuwa bora.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Bosi hanuniwi.

Wakizuia arv na mafuta kwa mwezi mmoja tu, mawaziri wote wanageuka kuwa mabalozi wa ushoga.
Ruto atamke lakin asitekeleze tamko, akianza kuwanyanyasa al shabab wanaanza kukinukisha.

Familia zimesahau majukumu.
Kwanza zipo nchi washirika wasiounga mkono huu ujinga ikiwemo Russia, Iran, China n.k Hata vita vya uhuru hatukuwa peke yetu! Kila jambo unaunganisha nguvu na yule mnayekubaliana.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Kwahyo ameenda kinyume na Papa?

 
Wakizuia arv na mafuta kwa mwezi mmoja tu, mawaziri wote wanageuka kuwa mabalozi wa ushoga

[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Vibaraka hawa wanaojiita serikali hawana uwezo wa kupinga ushoga!

Mabeberu yakidinda kule ulaya unashangaa samia anawapa ruksa watu wakatafunane.

HILI NALO TUTALITIZAMA.
 
Kwahyo ameenda kinyume na Papa
Kwani Papa anaunga mkono ushoga? Alafu Papa hata kama akiunga mkono ni yeye sio mafundisho ya Kanisa ambayo tunapaswa kufuata.

Papa kauli yake kukubalika kama kauli ya Kanisa lazima iwe na vigezo yaani isiwe kinyume na maandiko wala mapokeo.

Hata hivyo Papa Francis amekuwa kwenye kitimoto cha kupingwa waziwazi na maaskofu kwa jinsi anavyofafanua mambo, badala ya clarity inakuwa confusion!

Kwasababu vita ni kupinga ushoga tubakie kwenye kupinga ushoga bila kuangaliana usoni, dini, wala Utaifa.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom