Assad kawatesa Sana Wasyria kwenye gereza la Sednaya

Assad kawatesa Sana Wasyria kwenye gereza la Sednaya

econonist

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
20,189
Reaction score
29,663
Nina fuatilia hapa Al Jazeera kuhusu yaliyokuwa yanafanyika kwenye gereza la Sednaya nadhani Assad alikuwa mtu katili Sana. Ndio maana wasyria wameshangilia Sana. Leo halaiki ya watu walifika kwenye gereza la Sednaya kuona kama ndugu zao bado wapo. Ila kwa masikitiko wengi hawapo aidha walikufa kwa mateso au waliuawa na askari wa Assad. Nimejiuliza kwa Nini waarabu wanachukiana hivi?. Unabadilisha gereza kuwa machinjio ya raia wako. Kweli Assad hafai kabisa.

Ukisikiliza shuhuda za hapo utashangaa Sana. Watu walikatwa miguu na wengine kuuawa. Kuna wengine wamepotea kabisa . Inadaiwa wafungwa karibia 1000 waliuawa kwenye kipindi Cha Assad. Huyu hakuwa binadamu wa kawaida .
 
Nilipita huko miaka ya nyuma yaani Syria na Jordan nchi mbili tofauti kabisa
Syria ni wakomunist ukiingia kutoka ni kazi maana hata $ hupati ni mwendo wa kuruka tu
Ubabe mwingi hata Iraq ina unafuu sana enzi hizo
Kote nimeishi
Familia ya Assad imeiharibu hiyo nchi kwa miongo mingi
 
Umetumia neno waarabu kuwauwa wenzao ila unasahau mauaji yetu ambayo sisi sio waarabu ila unapotea miaka huku ndugu wakijua ipo siku utaonekana
Ukatili ni ukatili tu haujalishi wewe ni Mexican au mchina wote wakiwa madarakani ni makatili tu
Ila wanachagua sadaka mbaya sana...kuua watu
 
Nina fuatilia hapa Al Jazeera kuhusu yaliyokuwa yanafanyika kwenye gereza la Sednaya nadhani Assad alikuwa mtu katili Sana. Ndio maana wasyria wameshangilia Sana. Leo halaiki ya watu walifika kwenye gereza la Sednaya kuona kama ndugu zao bado wapo. Ila kwa masikitiko wengi hawapo aidha walikufa kwa mateso au waliuawa na askari wa Assad. Nimejiuliza kwa Nini waarabu wanachukiana hivi?. Unabadilisha gereza kuwa machinjio ya raia wako. Kweli Assad hafai kabisa.

Ukisikiliza shuhuda za hapo utashangaa Sana. Watu walikatwa miguu na wengine kuuawa. Kuna wengine wamepotea kabisa . Inadaiwa wafungwa karibia 1000 waliuawa kwenye kipindi Cha Assad. Huyu hakuwa binadamu wa kawaida .
Umesahau hao wafungwa unaowaona ni zaidi ya 30,000.karibu wote walikuwa kwenye makundi ya kigaidi hasa Isis na alqaida/alnusra front. Umesahau wao walivyokuwa wanachinja watu kikatili, walikuwa wakiwaua wengine kinyama sana, ingia youtube kuanzia 2012 hadi 2016 ndio utawajua hao ni kina nani? Bila Russia kuingilia kati kuna vizazi vingekuwa vimeshafutwa na hao unaowaona.
Kumbuka kule kwa Yazid Irak waliua wanaume na watoto wa kiume wote nasema wote lengo ni kufuta kizazi cha wayazidi ambao wanasemekana ndio watu wenye muonekano mzuri kuliko wote Duniani.
Pia ndio kizazi pekee cha kikristo kilicho survive kwa zaidi ya miaka 2000.Wakawateka wanawake wote na kuwabaka ili wazae kizazi kipya kisicho cha wayazidi na mpaka sasa ipo hivyo. Kila mwanamke au binti wa kiyazidi amezalishwa kwa nguvu mbegu mpya.
Marekani inayokuonyesha hao wafungwa wa Syria yenyewe kwa kuwatumia Wakurdi kule kaskazini inashikiria wafungwa wa ISiS 50,000 hapo hapo ndani ya Syria. Can you imagine hali zao zipoje? Uturuki imeuteka jana mji wa Wakurdi wa Manbij marekani inahofu endapo uturuki ikiendeleza oparesheni zake watawaachia hao wafungwa wote zaidi ya 50,000 ambao Marekani imewafunga kwa kuwatumia Wakurdi.
Kwa hiyo Serikali ya Assad iliwafunga 30,000 lakini Marekani huyo huyo anayejifanya mwema anawashikiria kwenye magereza yake yaliyopo Syria hiyo hiyo more than 50,000 kule kaskazini ambako ameng'ang'ania hataki kuachia kwe visima vya mafuta anakojichotea tuu kama yake.
Hii Dunia ni ya kinafiki kinafiki kinafiki hasa western zaidi ya unayoyajua au kuyaona.
 
Hata USA inatesa huko Guantamo
Kule si huwa kunapelekwa wale magaidi

Kwa mfano kale kagaidi ka kitanzania kalikoshiriki kulipua ubalozi wao hapa Bongo, si kako huko?

Halafu na kenyewe kana jina la dini yetu,

Hivi, dini yetu na ugaidi vinauhusiano gani?

Ki ukweli, nipo kwenye njia panda, sielewi iwapo siku za usoni nitakuwa tena wa dini hii
 
Ila kwa masikitiko wengi hawapo aidha walikufa kwa mateso au waliuawa na askari wa Assad. Nimejiuliza kwa Nini waarabu wanachukiana hivi?. Unabadilisha gereza kuwa machinjio ya raia wako. Kweli Assad hafai kabisa.
Unaambiwa alijaza wasiojulikana kila kona ya Nchi.

Wenye uwezo maelfu wakimbia Nchi. Wanyonge walibaki wakisubjri kuchinjwa kama kuku
 
Sana sana
Tamaa za madaraka hizo

Kuna rais alikuwa anaitwa Mujica alikuwa ni humblest President in the world alikuwa anatoa 90% ya mshahara wake kwa wasiojiweza
Dunia mapito hii tuishi kwa huruma
Tukiwa hai hatujui hilo...
Na ndiyo maana mwenye Mali akifa ndugu kwa hasira huzitumia kwa mwezi mmoja.Lakini kama mtu aliishi nao vizuri hata kwa kiasi bas watawaangalia mpaka watoto wa marehemu
 
Back
Top Bottom