At their peaks,nani alikuwa mkali zaidi...Marlaw Vs Mb Dogg?

At their peaks,nani alikuwa mkali zaidi...Marlaw Vs Mb Dogg?

dah, Mb mbwa alipendwa sana na ma sista du,huwa naona wanacomment youtube huko ila ni ajabu akapigwa chini😂
Tale,bwana fela na ndugu suka huu umoja ulipoteza vipaji vingi sana so sad,
Ukipishana nao t huna lako
 
Nikiweka Ushabiki wangu kwa marlaw pembeni. Mb dog anatakiwa kuwekwa na G.O.A.T wenzake maana alikuja na sound yake ambayo nadhani ndio foundation ya hizi nyimbo za mapenzi unazosikia leo,

hata Ukiiweka bongo flava katika Major Eras ,

1. (Kabla ya 2005)
Era ya Different tunes yaani kila mmoja aliimba kwa tune yake Dully sykes, Lady jay dee,TID, Q chief, Ray C , Juma nature, Stara thomas etc (Bongo flava halisi, Zouk, Rhumba, Rnb).. hili ndo kundi la waasisi "Era ya passion na muziki mzuri"

2. (2004 - mwanzoni mwa 2010)
Era ya Mb dog maana watu wote waliofuatia kama kama Kassim, Z anto, Ali kiba, Rich mavoko, Diamond (wa mwanzoni) walipita katika njia zake. Hata tune nyingi za leo ni kama zimetokea kwake

3. (Mwanzoni mwa 2010 hadi 2015)
Era ya T.H.T ama Ruge mutahaba, huyu hakuwa msanii ila alikuja na wasanii kama Barnaba, Ditto, Mwasiti, Amini, Marlaw, Maunda Zorro, Vumilia.. Ambao walikuja na muziki ambao ni rafiki zaidi kwa live band tofauti na ala ya Mb Dog

4. (2015 hadi sasa)
Tupo Kwenye Era Ya Commercial music ikiongozwa na Diamond platnumz.. Kinaimbwa kinachouza, haiangaliwi ladha ya muziki inaangaliwa investment and return. Watu wanatengeneza makundi na labels ili wasurvive maana muziki umekuwa expensive.. Watu kama marioo wenye multiple talents kubwa na back up ndio wanaweza kusurvive

Kwa kuangalia hili, Mb Dog anahitaji competition na watu walioleta impact kwenye muziki kwa ujumla kwa hiyo marlaw sio fit kwake.. Anahitaji Hall of fame
Umemaliza kila kitu mkuu mb dog ndo godfather wa mziki wa kuimba kulia lia bongo hii,,
 
ingawaje Marlaw alikuwa ni msanii mkali na mwenye sauti nzuri na mashairi makali, ila hii thread ilipaswa kumlinganisha Mb-dog na Matonya kwa kipindi kile
Ni kweli,
Mb Dog vs Matonya hapo wengi tungekuna vichwa,
Wote nawapenda tho Matonya ningempa kura yangu.
 
Mb Dog afananishwe na Matonya au Z. Anto, huyo Marlaw ni kumuonea. Mb dog aliimba sana enzi zake, kwamim naweza kumuweka top 10 ya wasanii bora wa muda wote Bongo
 
MB Dogg na Marlaw, kuwashindanisha sio kivile kwani Dogg alikuwa ni habari nyingine labda Matonya itamake sense sababu kipindi kile alitoa albamu yake ile yenye vaileth na akahit sana

ila bado MB Dogganafunika wote hao, hata kiuandishi nilipata kusikia Fayher G anasema aliiandika albamu yote ya Matonya ukiacha wimno wa Vaileth ambao inasadikiwa kauandika Tundaman
 
Back
Top Bottom