ATCL watolea ufafanuzi kuhusu hali ya tairi la ndege iliyosambaa Katika Mitandao ya Kijamii

ATCL watolea ufafanuzi kuhusu hali ya tairi la ndege iliyosambaa Katika Mitandao ya Kijamii

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Salaam,

Shirika la ndege Tanzania, ATCL watolea ufafanuzi kuhusu hali ya tairi ya ndege iliyosambaa Katika Mitandao ya Kijamii ambayo inaonesha tairi iliyoisha.

UFAFANUZI KUHUSU HALI YA TAIRI LA NDEGE YA KAMPUNI YA NDEGE TANZANIA (ATCL) ILIYOSAMBAA KATIKA MITANDAO YA JAMii


ATCL inapenda kutoa ufafanuzi kuhusiana na habari iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu hali ya matairi ya ndege zake. Tarehe 23 Aprili , 2022 katika mitandao mbalimbali ya kijamii zilisambaa picha zikionesha hali ya matairi ya ndege aina ya Dash 8 0400 ambayo ilikuwa inadaiwa kuwa hali yake inahatarisha usalama wa ndege na abiria .

ATCL inamshukuru kwa dhati abiria huyu kwa kuonesha umakini kwa usalama wa abiria na ndege. Umakini wake umesababisha kutolewa kwa ufafanuzi juu ya matumizi ya matairi ya ndege na usalama wake ambao utafafanua hali halisi na utawaondolea hofu abiria na wadau wote.

ATCL inapenda kutoa ufafanuzi kwa umma kuhusiana na madai hayo kama ifutavyo: Katika kuhakikisha usalama abiria na ndege yenyewe , ATCL hufanya ukaguzi wa lazima wa ndege zake zote katika maeneo yote ya ndege yakiwemo matairi kama ifutavyo:

Ukaguzi wa ndege baada ya safari zote za siku (Daily Check) ;

Ukaguzi wa ndege kabla ya kuanza safari zake za siku (Departure Check) ; na

Ukaguzi wa ndege baada ya kila safari (Transit Check).

Kuhusiana na madai yaliyotolewa kuhusu hali ya matairi, ATCL inapenda kutoa ufafanuzi ufuatao:

1. Miongozo ya ufuatiliaji wa hali ya matairi na ubadilishaji wake hutolewa na waundaji wa ndege husika. Ndege iliyofanya safari namba TC106 aina ya Dash 8 0400 kati ya Dar es salaam na Mbeya siku ya tarehe 22 Aprili, 2022 maelekezo na miongozo yake yametolewa na Kampuni ya De Havilland. Maelekezo na miongozo hiyo inabainisha kwamba, uchunguzi wa hali ya matairi utafanyika kila siku iii kubaini kama tabaka la juu limelika na kufikia nyuzi (reinforcement cord) kuonekana . Baada ya nyuzi hizo kuonekana kwa mara ya kwanza, miongozo inaagiza tairi hilo kutumika kwa miruko isiyozidi minane (08) kabla ya kubadilishwa (rejea kiambatisho cha muongozo kutoka kwa waundaji);

Kwa kufuata miongozo hiyo, ATCL hurekodi taarifa za miruko kwa tairi hilo tangu lilipo bainika kulika kwa mara ya kwanza;

Kwa mujibu wa rekodi zilizowekwa na ATCL, tairi ya ndege tajwa lilikuwa na mruko mmoja (01) tangu kubainika kulika kwa tabaka la kwanza, hivyo kulikuwa na miruko saba (07) zaidi hadi kufikia ukomo wa matumizi yake kwa mujibu wa miongozo ya matumizi ya matairi;

Kwa msingi huo, tairi hilo lilikuwa bado ni salama kutumika kwa mujibu wa miongozo iliyowekwa na waundaji na kufuatwa na ATCL.

Kutokana na miongozo hiyo, hali ya tairi kuwa katika hali hatarishi haiwezi kubainika kwa kuangalia kulika kwa tabaka la juu la tairi bila kurejea kumbukumbu za matumizi ya tairi kufuatana na miongozo ya utumiaji.

Kwa maelezo haya, ATCL inapenda kuutoa wasiwasi umma wa watanzania na abiria wote kwa ujumla kwamba ndege zetu zipo salama kabisa na kwamba suala la usalama wa abiria na ndege kwetu ni namba moja. Hivyo, tunaomba wateja wetu waendelee kutumia ndege za ATCL kwa safari zao bila hofu.

Msemaji wa Kampuni ya Ndege Tanzania.​


Screenshot_20220425-165248.png
Screenshot_20220425-165306.png
Screenshot_20220425-165322.png
Screenshot_20220425-165435.png
 

Attachments

Serikali ikitokea habari JF inayowahusu huwa wanapata SANA kigugumizi kutamka JF.
Ni sawa na kipindi kile cha kutetea serikali 2 kwenye bunge la katiba.
walikuwa wanaonesha mikono miwili kuashiria serikali 2 kwa sababu wakinyosha vidolf viwili wanakuwa wanaisapoti CHADEMA.
 
Hawa wanahatarisha maisha ya wasafiri ili waendelee kupata fedha zaidi. Tairi linaonekana lipo kipara lakini kwa vile watengenezaji walisema basi wanashindwa kuchukua hatua. Siku zote tunaambiwa akili za hao mbayuwayu changanya na zako lakini hatusikii hadi yatukute. Je, wajua kiwango cha njia ya kurukua ndege huko kwao kikoje ukilinganisha na hiki cha kwetu?
 
Hawa wanahatarisha maisha ya wasafiri ili waendelee kupata fedha zaidi. Tairi linaonekana lipo kipara lakini kwa vile watengenezaji walisema basi wanashindwa kuchukua hatua. Siku zote tunaambiwa akili za hao mbayuwayu changanya na zako lakini hatusikii hadi yatukute. Je, wajua kiwango cha njia ya kurukua ndege huko kwao kikoje ukilinganisha na hiki cha kwetu?
Asiye sikia la mkuu huvunjika guu, ngoja tuone kama kweli watabadili tairi baada ya miruko nane (8)
 
Hiyo ndege TC106 a.k.a KITULO, karibia kila siku inaenda Mbeya, me nilipanda tarehe 19 kwenda Mbeya na tairi lilikuwa kipara hivyo hivyo nadhani wamefunika kombe tu mwanaharamu apite maana hiyo miruko 8 wanayodai itakuwa imeshapita na kiukweli linatakiwa kubadilishwa kabisa.
 
Yani wanatuona mabwege, nani ana uthibitisho kwamba ule ni mruko wa kwanza?
Najiuliza ingekuwa ndege ya kiongozi wangetembelea hiyo tairi? au wanaona common citizens ni ng'ombe.
Kwenye huo muongozo iko wazi kwenye # 2 (hakikisha nyuzi hazionekani) hilo ndio la msingi
Hiyo note imewekwa kwa emergency, ni sawa na kubeti.
Waziri wa uchukuzi au huyo mkuu wa ATCL anatembelea V8 lenye tairi kipara?
 
Kama hilo lingekuwa tairi la gari lisingeruhusiwa kuwa barabarani sembuse tairi la ndege ambayo inakuwa na mgandamizo mkubwa wakati wa kutua. Tairi limeishia limepita kidogo kwenye level ya nyuzi kuonekana. Zile zimepitiliza kuonekana, au mpaka twende Twitter tuwaulize De Havilland, Bombardier, Airbus na Goodyear waseme kama hilo tairi ni salama?
 
Salaam,

Shirika la ndege Tanzania, ATCL watolea ufafanuzi kuhusu hali ya tairi ya ndege iliyosambaa Katika Mitandao ya Kijamii ambayo inaonesha tairi iliyoisha.

UFAFANUZI KUHUSU HALI YA TAIRI LA NDEGE YA KAMPUNI YA NDEGE TANZANIA (ATCL) ILIYOSAMBAA KATIKA MITANDAO YA JAMii


ATCL inapenda kutoa ufafanuzi kuhusiana na habari iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu hali ya matairi ya ndege zake. Tarehe 23 Aprili , 2022 katika mitandao mbalimbali ya kijamii zilisambaa picha zikionesha hali ya matairi ya ndege aina ya Dash 8 0400 ambayo ilikuwa inadaiwa kuwa hali yake inahatarisha usalama wa ndege na abiria .

ATCL inamshukuru kwa dhati abiria huyu kwa kuonesha umakini kwa usalama wa abiria na ndege. Umakini wake umesababisha kutolewa kwa ufafanuzi juu ya matumizi ya matairi ya ndege na usalama wake ambao utafafanua hali halisi na utawaondolea hofu abiria na wadau wote.

ATCL inapenda kutoa ufafanuzi kwa umma kuhusiana na madai hayo kama ifutavyo: Katika kuhakikisha usalama abiria na ndege yenyewe , ATCL hufanya ukaguzi wa lazima wa ndege zake zote katika maeneo yote ya ndege yakiwemo matairi kama ifutavyo:

Ukaguzi wa ndege baada ya safari zote za siku (Daily Check) ;

Ukaguzi wa ndege kabla ya kuanza safari zake za siku (Departure Check) ; na

Ukaguzi wa ndege baada ya kila safari (Transit Check).

Kuhusiana na madai yaliyotolewa kuhusu hali ya matairi, ATCL inapenda kutoa ufafanuzi ufuatao:

1. Miongozo ya ufuatiliaji wa hali ya matairi na ubadilishaji wake hutolewa na waundaji wa ndege husika. Ndege iliyofanya safari namba TC106 aina ya Dash 8 0400 kati ya Dar es salaam na Mbeya siku ya tarehe 22 Aprili, 2022 maelekezo na miongozo yake yametolewa na Kampuni ya De Havilland. Maelekezo na miongozo hiyo inabainisha kwamba, uchunguzi wa hali ya matairi utafanyika kila siku iii kubaini kama tabaka la juu limelika na kufikia nyuzi (reinforcement cord) kuonekana . Baada ya nyuzi hizo kuonekana kwa mara ya kwanza, miongozo inaagiza tairi hilo kutumika kwa miruko isiyozidi minane (08) kabla ya kubadilishwa (rejea kiambatisho cha muongozo kutoka kwa waundaji);

Kwa kufuata miongozo hiyo, ATCL hurekodi taarifa za miruko kwa tairi hilo tangu lilipo bainika kulika kwa mara ya kwanza;

Kwa mujibu wa rekodi zilizowekwa na ATCL, tairi ya ndege tajwa lilikuwa na mruko mmoja (01) tangu kubainika kulika kwa tabaka la kwanza, hivyo kulikuwa na miruko saba (07) zaidi hadi kufikia ukomo wa matumizi yake kwa mujibu wa miongozo ya matumizi ya matairi;

Kwa msingi huo, tairi hilo lilikuwa bado ni salama kutumika kwa mujibu wa miongozo iliyowekwa na waundaji na kufuatwa na ATCL.

Kutokana na miongozo hiyo, hali ya tairi kuwa katika hali hatarishi haiwezi kubainika kwa kuangalia kulika kwa tabaka la juu la tairi bila kurejea kumbukumbu za matumizi ya tairi kufuatana na miongozo ya utumiaji.

Kwa maelezo haya, ATCL inapenda kuutoa wasiwasi umma wa watanzania na abiria wote kwa ujumla kwamba ndege zetu zipo salama kabisa na kwamba suala la usalama wa abiria na ndege kwetu ni namba moja. Hivyo, tunaomba wateja wetu waendelee kutumia ndege za ATCL kwa safari zao bila hofu.

Msemaji wa Kampuni ya Ndege Tanzania.​


View attachment 2200136View attachment 2200137View attachment 2200138View attachment 2200139
Tatizo la wataalamu wetu hawana aibu wakikamatwa wanaeleza na kitu ambacho kinaonekana kwa macho, lengo lao ni ku-confuse ummah lay men, lini tayari ilio isha au kipara kuhesabiwa kwa miruko......ajari kutokea haisubiri miruko kuisha wana hatarisha maisha ya watu badili tayari plz acheni uswahili.
 
Back
Top Bottom